Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Ongea na Mwanao, Steve Mengele maarufu kama Steve Nyerere, ameonya kuhusu wimbi la vijana maarufu – hususan kutoka mitandao ya kijamii na burudani – kujitokeza kuchukua fomu za kugombea ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025, akisema si wote wenye nia ya dhati ya kuhudumia wananchi.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na Kishamba Media, Mengele amesema kuwa siyo kila kijana mwenye umaarufu anapaswa kuwa kiongozi, bali ni muhimu kila anayejitokeza kugombea kutafakari upya dhamira yake.
Mengele ambaye pia ni msanii na mwanaharakati wa kijamii, amesema kuwa katika kipindi hiki ambapo vijana wengi wanavutwa na mvuto wa siasa, kunahitajika busara na tafakari ya kina juu ya jukumu la mbunge katika jamii.
Akizungumza katika mahojiano maalumu na Kishamba Media, Mengele amesema kuwa siyo kila kijana mwenye umaarufu anapaswa kuwa kiongozi, bali ni muhimu kila anayejitokeza kugombea kutafakari upya dhamira yake.
Mengele ambaye pia ni msanii na mwanaharakati wa kijamii, amesema kuwa katika kipindi hiki ambapo vijana wengi wanavutwa na mvuto wa siasa, kunahitajika busara na tafakari ya kina juu ya jukumu la mbunge katika jamii.