Stendi ya mabasi Ubungo

Stendi ya mabasi Ubungo

Khantwe

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
59,468
Reaction score
119,622
Habari za Jumapili wakuu.

Kwa wale wanaoenda pale Ubungo watakubaliana na mimi. Kuna utaratibu huu ambao mimi binafsi nauchukia si kidogo.... Ni kuhusu wale wapiga debe wa pale stendi...kiukweli wamezidi na imekuwa kero kubwa kwa wasafiri.

Usikosee ukapita maeneo yale...utajuta usumbufu wake. Wale wapiga debe watakung'ang'ania mpaka basi hata ukiwaambia hausafiri.

Ifike wakati mamlaka zinazohusika ziliangalie hili kwa jicho la tatu...mimi naona kwa mji mkubwa kama Dar unaopokea wageni tofauti kutoka nchi tofauti haikutakiwa kuwe na uholela wa namna ile..ni aibu kwa taifa kiukweli.

Mimi nadhani kwa sababu mabasi haya ya mikoani yana ofisi zao wangekuwepo watu wachache tu pengine wasiozidi ishirini ambao watafanya kazi ya kuwaonesha watu kwenye ofisi husika ikitokea mtu hajui ofisi na utaratibu wa malipo upangwe na wenye ofisi au kila gari ikawa na mtu wake mmoja au wawili.

Najua kuna tatizo la ajira lakini ile kero ya ubungo imevuka mipaka aisee.

Naomba kuwasilisha.
 
Kungekua na utaratibu wa kununua ticket online au hata kwa mitandao ya simu wangeisha bila kuondoshwa.
 
Kungekua na utaratibu wa kununua ticket online au hata kwa mitandao ya simu wangeisha bila kuondoshwa.

Hii itakuwa ngum kidogo maana watanzania wachache wenye access ya mtandao....
 
Hii itakuwa ngum kidogo maana watanzania wachache wenye access ya mtandao....
Ndo maana akasema kwa mitandao. Aisee asiye na access hata ya airtel money mpesa tigo pesa huyo ni mfu kabisa. Maake hizi huduma zimekuwa msaada hadi vijijini. Na Iinaonyesha takribani kuna zaidi ya namba za simu million 14. Kwa haraka haraka pale ubungo sizani hata kuna wasafiri zaidi ya 20000 kila siku. Hili litawezekana. Katika hatua za maendeleo ukisema usubilie wote au usikie vilio vya wote hutopiga hatua yeyote. Tuliona malalamiko mengii kipindi serikali ilipoanza kuzima mitandao ya analog ila sasa hivi kimyaaa na maisha yanaenda
 
Kuna kipindi nilimsikia mwenyekiti wa chama cha wamiliki wa mabasi TABOA alisema walikuwa wapo kwenye hatua za mwisho za kuleta huo mfumo sasa sijui wamefikia wapi
 
Ndo maana akasema kwa mitandao. Aisee asiye na access hata ya airtel money mpesa tigo pesa huyo ni mfu kabisa. Maake hizi huduma zimekuwa msaada hadi vijijini. Na Iinaonyesha takribani kuna zaidi ya namba za simu million 14. Kwa haraka haraka pale ubungo sizani hata kuna wasafiri zaidi ya 20000 kila siku. Hili litawezekana. Katika hatua za maendeleo ukisema usubilie wote au usikie vilio vya wote hutopiga hatua yeyote. Tuliona malalamiko mengii kipindi serikali ilipoanza kuzima mitandao ya analog ila sasa hivi kimyaaa na maisha yanaenda

Okey nlikuwa sijaelewa kumbe.....itakuwa imekaa vema kumbe.
 
Kuna kipindi nilimsikia mwenyekiti wa chama cha wamiliki wa mabasi TABOA alisema walikuwa wapo kwenye hatua za mwisho za kuleta huo mfumo sasa sijui wamefikia wapi

Na wafanye hivyo upesi jamani....
 
Niwewe tu ukifika pale ukalegeza watakusumbua,wewe ukifika pale piga mwendo wacha kushangaa na anaye kufuata mpatie makavu,hawata kufuata.
 
Niwewe tu ukifika pale ukalegeza watakusumbua,wewe ukifika pale piga mwendo wacha kushangaa na anaye kufuata mpatie makavu,hawata kufuata.

Mkuu huwajui wewe wale....wanajifanya kukusalimia na kukuuliza vijimaswali.....ukiuchuna wanakutukana matusi wengine.....kifupi ni kero
 
Back
Top Bottom