Nimekuwa nikijiuliza ni nini kimewafanya SSRA kupitia serikali kupeleka sheria kandamizi bungeni huku wakijitetete ati kuwa wanataka kuwasaidia watu wastaafu vizuri. Huu wema umetoka wapi? Tokea lini serikali ya CCM ikawa na wema kwa wastaafu wake? Mbona wazee wastaafu wa ilokuwa Jumuia ya Africa Mashariki mpaka leo wanasota na si serikali iliyowasilisha msaada bungeni wala SSRA imeonekana kuwasaidia? Naona hela za wazee wa jumuia ya Africa Mashariki zilikuwa tamu sasa wanataka kutafuna na za vijana wanaofanya kazi kwa mikataba.
Nasema haiiingiii akilini hata kidogo. SSRA kama inasema ina nia njema, ituelezee imefanya nini kuibana serikali na mifuko husika kuhusu kurejeshwa fedha zilizochukuliwa kwenye mifuko na serikali hata bila ya mkataba kwa ajili ya kujenga UDOM na miradi mingine. SSRA inataka fedha zetu ziendelee kuchotwa na serikali halafu sisi tukae tukisota kama wale wazee wa Afrika Mashariki? CAG alishatoa riport kwamba serikali haijaanza kurejesha hizo fedha na ndiyo maana mifuko inaelekea kushindwa kuwalipa wanachama nando maana wanakuja na sheria ya kuzuia watu wasidai chao.
SSRA, acheni kuchukua solution za kijinga kama "mtaka cha uvunguni, kitanda nyanyua". Wabaneni serikali irudishe hela za wanachama. Pia tunapenda kusikia kuwa wakurugenzi na Bodi zilizotoa fedha za wanachama bila mikataba ya kueleweka wanatimuliwa.
Nasema haiiingiii akilini hata kidogo. SSRA kama inasema ina nia njema, ituelezee imefanya nini kuibana serikali na mifuko husika kuhusu kurejeshwa fedha zilizochukuliwa kwenye mifuko na serikali hata bila ya mkataba kwa ajili ya kujenga UDOM na miradi mingine. SSRA inataka fedha zetu ziendelee kuchotwa na serikali halafu sisi tukae tukisota kama wale wazee wa Afrika Mashariki? CAG alishatoa riport kwamba serikali haijaanza kurejesha hizo fedha na ndiyo maana mifuko inaelekea kushindwa kuwalipa wanachama nando maana wanakuja na sheria ya kuzuia watu wasidai chao.
SSRA, acheni kuchukua solution za kijinga kama "mtaka cha uvunguni, kitanda nyanyua". Wabaneni serikali irudishe hela za wanachama. Pia tunapenda kusikia kuwa wakurugenzi na Bodi zilizotoa fedha za wanachama bila mikataba ya kueleweka wanatimuliwa.