ok kaka. MSN wametoa aina tatu za Xbox (kuna ya nne ila bado haipiga hata mwezi sokoni na sijaigusa sositaiongelea). toleo ya kwanza inaitwa Phat version maana ilikuwa kubwa mno. utaijua maana ina HDD ndogo kama 20GB, 40GB au haina kabisa. toleo la pili ilikuwa inaitwa Elite. hii ni ndogo na huja na 120GB only. la tatu ni slim au Xbox S. hizi zinakuja aina mbili. ya 250 GB na 4GB. kati ya hizi tatu, Phat ni kimeo na rahisi kupata RROD yaani overheating na Slim ina posibility ndogo sana la kufanya hivyo. kuna fans zinauzwa za kusaidia kuprevent the overheating issue. Xbox zote zina uwezekano wa kuflash DVD (ila sio zote sawa, kuna zingine ngumu na zingine rahisi maana MSN wanatumia DVD Drives tofauti tofauti). kuna kitu kinaitwa JTAG au RGH. kuflash DVD Drive inaamanisha unaitoa region lock, yaani kama ilikuwa icheze NTSC games tu au PAL, unaweza kucheza any na hata za kuburn nyumbani. pia kuna JTAG na RGH hii ni jinsi ya kufanya Xbox yako ikubali kuweka games kwa HDD (yaani hamna haja ya DVD tena) na pia unaweza ongeza apps za washikaji (homebrew). lastly kuna ODDE (Optical Disc Drive Emulator). hii ni chip inawekwa kwa Xbox inafanya mashine ijue kuna CD ndani kila saa na hivi basi unaweka games zako kwa external HDD na kucheza. Xbox zote zinakubali method hizi tatu ila kuna Slims zinasumbua so the best ni Elite haswa Jasper. Jasper ni jina la code kueleza walitumia motherboard ipi kwa Xbox. kuna jinsi ya kujua Xbox ina motherboard ipi. na hii ni kwa kuangalia pale nyuma kwa power cable. nitakueleza vizuri hili nikiwa na net ya ukweli ili nikupachikie picha. kati ya methods tatu, flashing DVD Drive ndo the easiest, RGH ndo the best but hardest na ODDE ni ghali. nitaongeza mengine baadaye lakini jibu la haraka haraka mkuu ni kama unataka Xbox, tafuta elite Jasper