Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Wakuu!
Spika Dkt. Tulia Ackson amesema 'kutokumuona mtu haimaanishi ametekwa' wakati akijibu swali kuhusu utekaji ambao umekuwa ukiripotiwa hapa nchini
Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson ameeleza kuwa Bunge haliwezi kujadili kuhusu madai na tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa kwa Jeshi la Polisi kuwa wanahusika na masuala ya utekaji wa raia kutokana na kutokuwa na uhakika na uthibitisho wa Polisi kuhusika na matukio hayo.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Kulingana na Spika Tulia aliyekuwa akizungumza na Chombo Kimoja cha habari ameeleza pia kwamba matumizi ya neno Utekaji yamekuwa sio sahihi, akidai kuwa neno hilo limerahisishwa matumizi yake na wakati mwingine kuchanganywa na watu kupotea ama kutokuonekana kama ambavyo imekuwa kawaida ya watu fulani kuonekana kwenye maeneo fulani fulani.
"Sura inayoletwa Bungeni sio kwamba tujadili utekaji ni tujadili utekaji wa Polisi, Mimi sina taarifa kuwa Polisi ndio wanaoteka na yeye (Mbunge) alileta kwa sura kuwa Polisi ndio wanaoteka sasa Bunge haliwezi kujadili hoja kama hiyo. Kwanini? Bunge linapojadili hoja lazima litoe maazimio na tukitoa maazimio lazima tuiiagize serikali, haya tukishajadili polisi wanateka tunaiagiza nini Serikali? ivunje Jeshi la Polisi?" Amehoji Spika Tulia.
Video: UTV
Spika Dkt. Tulia Ackson amesema 'kutokumuona mtu haimaanishi ametekwa' wakati akijibu swali kuhusu utekaji ambao umekuwa ukiripotiwa hapa nchini
Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson ameeleza kuwa Bunge haliwezi kujadili kuhusu madai na tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa kwa Jeshi la Polisi kuwa wanahusika na masuala ya utekaji wa raia kutokana na kutokuwa na uhakika na uthibitisho wa Polisi kuhusika na matukio hayo.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Kulingana na Spika Tulia aliyekuwa akizungumza na Chombo Kimoja cha habari ameeleza pia kwamba matumizi ya neno Utekaji yamekuwa sio sahihi, akidai kuwa neno hilo limerahisishwa matumizi yake na wakati mwingine kuchanganywa na watu kupotea ama kutokuonekana kama ambavyo imekuwa kawaida ya watu fulani kuonekana kwenye maeneo fulani fulani.
"Sura inayoletwa Bungeni sio kwamba tujadili utekaji ni tujadili utekaji wa Polisi, Mimi sina taarifa kuwa Polisi ndio wanaoteka na yeye (Mbunge) alileta kwa sura kuwa Polisi ndio wanaoteka sasa Bunge haliwezi kujadili hoja kama hiyo. Kwanini? Bunge linapojadili hoja lazima litoe maazimio na tukitoa maazimio lazima tuiiagize serikali, haya tukishajadili polisi wanateka tunaiagiza nini Serikali? ivunje Jeshi la Polisi?" Amehoji Spika Tulia.
Video: UTV