Soka la Tanzania tangu miaka ya 80 mpaka leo

yutong

JF-Expert Member
Apr 15, 2011
1,601
338
Jamani wanajf hebu tujaribu kufikiria soka la tanzania wakati ule mapaka sasa, je unafikiri limepanda kiwango ama limeshuka? na unadhani nani kahusika ktk kulishusha ama kulipandisha kiwango? Nakumbuka enzi hizo kulikuwa na wachezaji kama akina Husein Masha, Athuman China, Idd Pazi, Rosta Ndunguru, Pita Tino, Nteze John nk. Kulikuwa na timu kali ambapo zilikuwa zinatowa upinzani sawa, timu hizo kwa kujikumbusha ni kama:-
1. Nyota nyekundu
2. Sigara
3. Pilsner
4. Simba
5. Yanga
6. Coastal Union
7. African Sports
8. Majimaji
9. RTC Kigoma
10. CDA Dodoma
11. Tukuyu Stars
12. Mecco
13. Pamba
14. Ndovu
15. Bandari Mtwara
16. Lipuri Iringa
17. Ushirika Moshi

Hebu angalia timu hizo wakati huo kisha linganisha na timu zetu za sasa. Wakati huo mabasi ya mikoa yalikuwa yanasafiri usiku tu
 
Umenikumbusha mbaali! Zile ndo zilikuwa enzi bwana! Matokeo unayapatia uwanjani siyo siku hizi unakwenda mpirani kuona idadi ya mabao tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom