Soka la bongo ni ubabaishaji mtupu

umelijua lini soka la bongo

Wewe ndio hujui mkuu, mimi nimefatilia soko tangia Pamba ilivyopanda daraja (Pamba ya Kina Joram Mwakatika) na Kocha Pius Nyamko..., Pamba (narudia) Pamba haijawahi kuchukua Kombe la Ligi Kuu Tanzania Bara
 
Tukuyu stars ya mwaka 1985 ilikuwa kama Barca!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums

Tukuyu Stars chini ya Ramlik Patel Kaka walichukua Ubingwa bila upinzani mkubwa 1985/86!First 11 yao hii hapa:

1.Mbwana Makata
2.Fred Chundu
3.Ally Kimwaga
4.Godwin Aswile
5.Suleiman Mathew Luhongo
6.Aston Pardon(RIP)
7.Peter Mwakibibi
8.Yusuf Kamba
9.Richard Lumumba(RIP)
10.Kais Mwalyoga
11.Justin Mtekele(RIP)/Karabi Mrisho
Kocha:Athuman Juma Mlimba(RIP)
Kikosi hiki hao Azam wangefungwa hata 10!!
 

Wachezaji wa Azam wakishangilia Jana Uwanja wa Sokoine. Kulia John Bocco amemkumbatia Mwaikimba

Bongo Darisalaaam , wafadhili wa ligi awa bingwa raha kweli kweli ! TFF watafanya nini hapo ngoja na TBL na Vodacom walete Timu zao tuone that tha nani zaidi !
 

na wewe ni mbabaishaji tu! hiyo azam unayoisema ilizifunga zote yanga na simba kwa hiyo na zenyewe zilipanga matokeo? jipange sawa sawa!
 

kijana umezaliwa mwaka gani? .unamjua george masatu hussein masha john makelele niko bambaga haoni baadhi ya wachezaji wa pamba

umelijua lini soka la bongo

Wakuu Pamba haijawahi kuwa Bingwa wa Ligi Tanzania Bara, ilikuwa Timu nzuri sana na uwezo wa kuwa Bingwa ilikuwa nao (kwa soka nzuri na ufadhili wa Bodi ya Pamba) lakini sadly haukuchukua Ubingwa..., Timu ambazo zimeshachukua Ubingwa ni:-

Tukuyu Stars (walipanda daraja mwaka huo huo wakachukua ubingwa na mwaka uliofuata wakashuka)
Coastal Union
Pan African
Mtibwa Sugar
Simba
Yanga na sasa
Azam

Sidhani kama nimeruka timu... (ila pamba haipo)
 
kama hayo yote unayoona ndo ubora wa Azam kushinda Simba na Yanga,mbona nao wajiingiza kwenye hizi fitna za kununua mechi?

ha ha ha ha! mliozoea vya kunyonga vya kuchinja hamviwezi! azam ni level nyingine hata kama hutaki!
 

hahahaaaaa, hivi yanga hawajasombwa na mafuriko mkuu
 
tatizo mshakariri simba na yanga ndo sababu na mwakani tynabeba tena mpaka muache ujinga wa kukalili..

Mwakani? Huu ni ubingwa wa kwanza kwa azam tangu ipande ligi kuu miaka nane iliyopita. Hivyo ubingwa wa pili utakuwa 2014 + 8 = 2022.
 

pia umesahau kuwaambia azam kawafunga wote wawili( cmba&yanga) msimu huu
 

Pamba: Bingwa wa Muungano: 1 time

Tanganyika: -
Yanga: 24 times
Simba: 18 times
Cosmopolitan: 1 time
Mseto: -ditto- Mtibwa: 2 times
Coastal: 1time
Pan Africans: -ditto-
Tukuyu: -ditto-
Azam: -ditto-

Wapenzi wote wa Yanga tukubli matokeo, Azam ni bingwa halali. Nawatakia kila la heri.
 
Wastani wa hoja za wacahngiaji unakubaliana bila ya kujijua na hoja ya mtoa mada. Walio wengi wanakubali kwamba 'Simba na Yanga' huwa zinahonga. Lakini timu hizo hazichezi ligi ya peke yao. Kama kuhonga, zitahonga timu nyingine kwenye ligi hiyohiyo, ikiwamo Azam yenyewe. Kwa hivyo kama ni hatia, mtoa na kupokea rushwa wote wana hatia. Sasa kama mchezo huo upo kweli. hata kama wahongaji ni timu hizo mbili, maana yake ni kwamba mwaka huu umefanyika pia. Hivyo kweli ligi hiyo ni ya ubabaishaji, hata kama bingwa angekuwa Ashanti. Aidha, hakuna mchangiaji yeyote aliyebisha madai ya mtoa mada kwamba refa aliboronga kwa faida ya Azam kwenye mechi na Mbeya City, iwe kwa makusudi au kwa bahati mbaya. Kwa asiye na upande kwenye hili, anashawishika kuamini kwamba mtoa mada yuko sahihi. Hasa ikitiliwa maanani mechi kadhaa zinazoihusu Azam ziliwahi kuchezeshwa namna hiyo misimu iliyotangulia. Mechi na Yanga iliyosababisha Cannavaro kufungiwa na Yanga kumpiga mwamuzi ilikuwa katika mazingira kama hao. Mwamuzi Ramadhan Ibada (Kibo) aliwahi kufungiwa kwa kuipendelea Azam kwenye mechi za Kimbe la Mapinduzi, iwe kwa makusudi au kwa bahati mbaya.Ndio maana kuna baadhi ya wachangiaji wamekuwa wakmtaka mwanzisha mada kuachana na wivu wakike. Bila ya kujijua, wachangiaji hao wanakusudia kwamba Azam iachwe ishinde kama ambavyo wanadhani Yanga na Simba zinashinda. Wastani wa hoja zote hizo ni kwamba kuna mushkeli mkubwa juu ya uungwana (fairness) wa matokeo ya mechi za Ligi ya Vodaco. Kwa maoni ya mtoa mada, huo ni ubabaishaji, na sitowashangaa wanaokubaliana naye. Ninaowangaa ni wanaotofautia naye huku wakijisema wenyewe kwenye hoja zao kwamba wanajua ukweli huo!
 

logical analysis
 
Rufaa ya yanga iliandalhwa getho kwa akilimali kwani ofisi imesombwa na mafuriko.
 
Pamba: Bingwa wa Muungano: 1 time

Tanganyika: -
Yanga: 24 times
Simba: 18 times
Mtibwa: 2 times
Coastal: 1time
Pan Africans: -ditto-
Tukuyu: -ditto-
Azam: -ditto-

Wapenzi wote wa Yanga tukubli matokeo, Azam ni bingwa halali. Nawatakia kila la heri.


Very true Mkuu, watu wanachanganya. Pamba imewahi kuchukua ubingwa wa "Muungano" na sio Tanganyika. Kwenye orodha yako ya mabingwa wa Tanganyika ongezea Cosmopolitan (1967) na Mseto (1975).
 
Simba, Yanga, Azam, wote ni wanunuzi wa mechi, kilichotokea mwaka huu ni mwenye kisu kikali ndo kapata.
 
Very true Mkuu, watu wanachanganya. Pamba imewahi kuchukua ubingwa wa "Muungano" na sio Tanganyika. Kwenye orodha yako ya mabingwa wa Tanganyika ongezea Cosmopolitan (1967) na Mseto (1975).

Asante sana Mkuu, marekebisho yamefanyika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…