Tatizo linaoonekana hapa ni hang over ambayo wengi wetu tunayo toka mfumo wa chama kimoja. Kwa kuwa CCM wana utaratibu fulani, basi tushakariri kuwa kila chama ni lazima kifuate utaratibu huo. Utaratibu wa vyama umo kwenye katiba za vyama, na sio kwenye katiba ya JMT. So usilazmishe Chadema wafanye kama walivyofanya wenzao wa CUF and CCM. Kwani mchungaji Mtikila aliteuliwa na nani, au Rungwe wa NCCR, je umepitia katiba zao ukaona zinasemaje?
Nadhani next time utahoji kwa nini Slaa hakusindikizwa kwa mbwembwe kwenda kuchukua fomu za uraisi NEC, au kwa nini hakumpa mwanae fomu amzungumshie mikoani kuomba udhamini?
Kusimamisha mgombea wa kupeperusha bendera ya chama ni kitu muhimu sana, huu mjadala hapa unafanyika kwa kuwa Chadema imemsimamisha mgombea makini. Mara nyingi watu wamelalama kuwa vyama vya upinzani haviko serious na makini, sasa Chadema imeamua kuwa serious this time, yet bado tunalalamika.
Hata kama katiba imepindishwa, since matokea ya kupindishwa huko ni kutuletea mwanaume Slaa anayekubalika, I have no problem at all with that. Mwenyekiti alisema walifanya utafiti, tukubaliane naye, na Dr Slaa hakuwa ameamua kugombea, ameombwa, kuna tetesi kuwa Prof Baregu alikuwa anazungumziwa, lakini si rahisi kumuuza Baregu kwa wananchi kwa kuwa hafahamiki na wananchi wa kawaida.
Huu mjadala sidhani kama una mantiki, kama kutakuwa na malalamiko ya uvunjaji katiba basi yataibuka tu kwenye vikao vya wiki hii, na ndipo tutaweza kujadili kwa upana zaidi.