Siyo Kila Kingaacho ni Dhahabu.

Siyo Kila Kingaacho ni Dhahabu.

joshydama yaani una bahati sana kuwa umekutana na haya.....kama ingekuwa ni mke wangu ungejuta maisha yako yote na mji ungeukimbia. Maana unajipanga ku-do na yeye, unakwenda sehemu husika huku umejiandaa unajikuta unainamishwa tena kwa ridhaa yako mwenyewe huku unampa mke wangu mzigo na anakupiga picha. Akimaliza kupakua kisamvu, chumba chote kinanuka na nakuja kubandika picha zako humu JF. Una bahati sana.
 
Heshima yako mwana MMU. Natumai mko salama na mnaendelea poa sana katika ujenzi wa taifa Letu.

Kama kichwa cha habari kinavyosomeka. Juzi nimedhihirisha na kutambua umhimu wa huu msemo wa kwamba siyo kila unachokiona kinag'aa basi ukasema ni dhahabu na kuvinga'ang'ania bali vitu vingine kubali tu vikupite mbali.

Ni kwamba miezi miwili liyopita kuna mdada nilikutana nae mitaa ya hapa Riverside-Dar es salaam karibu na kanisa la mzee Fulani hivi ni maarufu sana hapa mjini. Binti mzuri sana tena umbo namba nane matata na amejaaliwa vitu vingine vyote vinavyotuvutia na kutuhamasisha sisi wanaume.

Nilishindwa kuvumilia ikabidi nisimamishe ndinga na kumuita. Binti aliitikia wito na akawa amependa kwenye ndinga na ukizingatia mvua ilikuwa inanyesha hakuwa na namna zaidi ya kuingia kwenye gari na kuanza safari.

Baada ya kuingia kwenye gari nilimtania kimtindo..."Wewe ni mwanamke mzuri na umependeza sana natamani kama ungekuwa mama watoto...akajibu kwa sauti nyororo na kwa bashashi acha basi Tabia za kifataki basi na wewe.. bwanaa"

Tukacheka kidogo hahahahahh...hahahhh then safari ikaendeleaa kama kawaida. Katika kupiga story akesema anaelekea mwenge ingawa Mimi nilikuwa naenda kariakoo ilibidi nibadilishe safari wote tukaelekea huko mwenge.

Mara baada ya kufika sehemu aliyokuwa anaenda alishuka na tukaagana nami nikaanza safari ya kwenda nilikokuwa naelekea.

Baada ya siku tatu nikaanza kutengeneza mazingira ili mtoto ajae nifanye yangu. Kila nikiweka mtego mtoto anaupangua. Sikukata tamaa hata kidogo na sikutaka kuonesha kuwa nimeshindwa niliendelea kujipa matumaini kuwa lazima nitafanikisha lengo lango.

Nilipoona anazingua na kunirisha sana ikabidi niwe mkali zaidi ya mbogo aliyejeruhiwa na risasi wakuu. Mtoto akajishusha akasema anapenda sana siku moja anipe gemu sema kuna kitu ataniambi kwa nini anafanya hivyo.

Ilikuwa ngumu sana kuelewa anachomaanisha maana akili yangu yote ilikuwa inawaza lile umbo tamu nililoliona. Hivyo, nilimuona mzinguaji tu..shetani ana nguvu sana wakuu acheni tu. Baada ya kuona anazingua sana ikabidi nimpotezee.

Nashangaa juzi asubuhi akanicheki akilalamika kuwa nimempotezea japo aliongea kwa kiingilishi kuwa nimem-dump. Nikajitetea kwa kumpiga sound za hapa na pale basi akanielewa na akaomba tukutane mida ya kumi na moja.

Ilipofika muda uliopangwa tulikutana sehemu husika tukawa nikaagiza vinywaji na nyama choma tukala hapa na pale tukipiga story( yani nikiomba gemu)

Mtoto akaelewa nikachukua chumba. Baada ya kuingia ndani na ukizingatia tulikuwa tumependeza tayari tukaanza yale mazoezi ya kujindaa kuingia uwanjani.

Baada ya nusu hivi mtoto akaomba rasmi tuingie uwanjani yani kwa sauti nyororo na yenyewe maumivu ya kumisi chuma akiashiria kuwa yupo tayari kupokea chuma cha moto.

Ile najiandaa kuzamisha chuma nilijikuta narushwa chini mithili ya mtu aliyepigwa na shoti....ila baada ya dakika kadhaa nilirudi katika hali yangu ya kawaida na nikamshudia akiwa anahaingaika pale kitandani kama mtu anayekabwa ila baada ya muda kidogo alikuwa poa nikamuuliza akawa kimya hakunijibu chochote.

Nikajaribu tena nione kama itatokea tena hali kama iliyotokea. katika harakati za kuanza tukio kwa mara ya pili nilijikuta tena narushwa chini na kuanza kupigwa makofi na mtu nisiye muona na hayo makofi yalikuwa na maumivu makali sana nikawa naugulia maumivu kwa sababu sikutaka mtu ajue ingawa yeye alikuwa poa akishangaa kichotokea kwa hili tukio la pili.

Nilivyoona hali inakuwa ngumu zaidi ilibidi nitoke nduki hadi kwenye parking nikaingia kwenye gari nikasepa home...

Kufika home nikagundua nimeacha boksa na waleti yenye vitambulisho kule lodge. Kesho yake nikavifuatilia bahati nzuri mhudumu wa pale lodge tunafahamiana so akiwa anasafisha alivikuta na akawa amevitunza.

Wakuu ukiona unasumbuliwa na mdada usimuone kama mzinguaji huenda anafanya hivyo kukulinda wewe bila kujijua. Sema kwa sababu ya tamaa zetu unakuta unamuona mtoto wa watu kama ana nyodo, maringo na mzinguaji kumbe siyo.

Kiukweli, hili tukio limenifundisha mengi sana. Kwanza, usiparamie mtu usiyemjua. Pili, bora ukawashirikisha watu wanaomjua mhusika kuliko kwenda kichwa kichwa.
We rudia mchezo ila uende na kinyama au kimfupa cha mbuzi katoliki A.K.A noa A.K.A mdudu A.K.A kiti moto.hayo ni mapepo yatasepa then utakula vyako na baada ya kuachana nae baadae yatamchalaza yeye mwenyewe ili atie adabu asiyalee lee
 
Tunashukuru kwa taarifa kuwa "Unamiliki ndinga" ....HONGERA SANA kwa kujipromoti kwa warembo wa Jf wapenda wanaume wenye magari yao.
 
joshydama yaani una bahati sana kuwa umekutana na haya.....kama ingekuwa ni mke wangu ungejuta maisha yako yote na mji ungeukimbia. Maana unajipanga ku-do na yeye, unakwenda sehemu husika huku umejiandaa unajikuta unainamishwa tena kwa ridhaa yako mwenyewe huku unampa mke wangu mzigo na anakupiga picha. Akimaliza kupakua kisamvu, chumba chote kinanuka na nakuja kubandika picha zako humu JF. Una bahati sana.
Hahahah!

Mkuu una mikwara ya kitoto sana.
 
Tabia zetu hizo kuzindika wanawake.,, Tushee na wew kama nani labda..??
Na una bahati umepewa mikofi hiyo., Mi huwa naondoka na mbupu tu....!!
Naweka tu kengele ya chuma..!! tuone thatha nani mjanja.,,


Kila ukitembea ni ng'eng'ele ngelengele....!!
Ili kila mtaa ukipita watu wasali sala ya malaika wa bwana..!!
We kiboko
 
Tunashukuru kwa taarifa kuwa "Unamiliki ndinga" ....HONGERA SANA kwa kujipromoti kwa warembo wa Jf wapenda wanaume wenye magari yao.
Ndinga kawaida sana Mkuu.
Mwanaume wa kweli hawezi jivunia kuwa na ndinga mkuu.

Ingawa inakuongezea sifa na heshima kwa warembo wa type Fulani hivi.

Pia Hautochomwa na jua wala kuwa na mijasho ya hapa na pale Mkuu.
 
We rudia mchezo ila uende na kinyama au kimfupa cha mbuzi katoliki A.K.A noa A.K.A mdudu A.K.A kiti moto.hayo ni mapepo yatasepa then utakula vyako na baada ya kuachana nae baadae yatamuchalaza yeye mwenyewe ili atie asadabu aisiyalee lee
Nilikuwa sijui mkuu!
Ngoja nimcheki usiku huu!
 
Tabia zetu hizo kuzindika wanawake.,, Tushee na wew kama nani labda..??
Na una bahati umepewa mikofi hiyo., Mi huwa naondoka na mbupu tu....!!
Naweka tu kengele ya chuma..!! tuone thatha nani mjanja.,,


Kila ukitembea ni ng'eng'ele ngelengele....!!
Ili kila mtaa ukipita watu wasali sala ya malaika wa bwana..!!
Mwanaume wa kweli unamzindika vipi mwanamke?

Huko ni kutokujiamini.
 
Tabia zetu hizo kuzindika wanawake.,, Tushee na wew kama nani labda..??
Na una bahati umepewa mikofi hiyo., Mi huwa naondoka na mbupu tu....!!
Naweka tu kengele ya chuma..!! tuone thatha nani mjanja.,,


Kila ukitembea ni ng'eng'ele ngelengele....!!
Ili kila mtaa ukipita watu wasali sala ya malaika wa bwana..!!
yeuwiii msaada jamani mbavu zinatokaaaaaa..... khaa umeniacha hoi kwa kweli
 
Back
Top Bottom