Siwezi kuishi naye

Siwezi kuishi naye

kiwawira

Member
Joined
Aug 11, 2013
Posts
10
Reaction score
2
Mke wangu nimemfumania mara 2 na marafiki zangu, nilipomuuliza akaanza kunitukana na kunieleza kwamba nimelala na mama yake mzazi wakati simjui hata kwa sura kwani wakati tunaoana mwaka 2009 mama yake alishafariki mwaka 2003.

Nifanyeje nimyonge au nijinyonge au nimsamehe au niondoke nikaanze maisha yangu mapya yeye nimuache?

Naombeni ushauri wenu wana jf.
 
Ulipomfumania mara ya kwanza ulimsamehe kiongozi? Anajitoa ufahamu tu huyo, iweje ulalale na mama yake aliefariki 2003? Anyway choice is yours ila hakutaki huyo dada ndio jibu la haraka haraka
 
jitahidi umsamehe na uendelee na maisha yako mkuu...
 
Nionavyo mimi huyo Bi Dada anafanya makusudi kwa sababu alizo nazo, sio Bure hapo

Ushauri ni Jiulize MOYONI mwako kama unweza kumsamehe mkaendelea na maisha au vinginevyo, maana utakua unajua sababu za yeye kufanya hayo kwa kurudia
 
mke wangu nimemfumania mara 2 na marafiki zangu nilipomuuliya akaanza kunitukana na kunieleza kwamba nimelala na mama yake mzazi wakati simjui hata kwa sura kwani wakati tunaoana mwaka 2009 mama yake alishafariki mwaka 2003.nifanyeje nimyonge au nijinyonge au nimsamehe au niondoke nikaanze maisha yangu mapya yy nimuache?naombeni ushauri wenu wana jf

Pole sana kaka, hakuna kitu kibaya kama kuumia kisaikolojia , kama kafikia hatua hiyo na wewe ulimfumania live its beta ukaachana naye na kama mna watoto angalia ni mazingira gan wataishi endapo wewe na mkeo mtatengana maana wao ndiyo huwa waathirika wakubwa. Piga moyo konde yatapita tu
 
Akufukuzaye hakwambii toka....Huyo kaa naye chini achague moja.Kumsamehe pia ni option nzuri lakini kuna maradhi ndugu yangu....
 
Mke wangu nimemfumania mara 2 na marafiki zangu, nilipomuuliza akaanza kunitukana na kunieleza kwamba nimelala na mama yake mzazi wakati simjui hata kwa sura kwani wakati tunaoana mwaka 2009 mama yake alishafariki mwaka 2003.

Nifanyeje nimyonge au nijinyonge au nimsamehe au niondoke nikaanze maisha yangu mapya yeye nimuache?

Naombeni ushauri wenu wana jf.
Kuna wale wanaolewa kwasababu umri umeenda au pesa au sababu nyingenezo na nadhani huyo mkeo ni moja wao hakuingia kwenye ndoa na wewe kwasababu ana mapenzi ya dhati lahasha,Sasa kama ndoa imefikia hatua hio ni majanga matupu,utakuja kuletewa maradhi tu.We muache tu dunia itampa funzo kubwa sana malipo hapa hapa duniani "WHAT GOES AROUND COMES AROUND"
 
Too late, keshakupanda kichwani huyo. Cha msaada wee pima kuwa unamegewa daily au kusepa.
 
Mara nyingi humu JF tunaishia kujadili na kutoa ushauri kwa kubase kwenye taarifa za upande mmoja! this is too bad.
Mtoa mada angejieleza naye amewahi kumfanya nini mwenzake! Katika jamii zetu si kawaida kwa wanaume kumfumania mke tena na rafiki (even once) alafu hayo mahusiano yakaendelea.
Kama ameweza kufanya hivyo inawezekana (sina hakika), huyo bwana atakuwa amefanya mahasi makubwa sana so mwanamke ana equalize scores! kulala na mama inawezakuwa anahusiana na "Jimama Jikubwa" sawa na mzazi wake au wa binti.(ambako ni kudhalilishana kimsingi). kwa upande mwingine hao rafiki zako nao wa ajabu sana- pengine mna mazoea na siyo urafiki. wengi tumedhania MAZOEa kuwa ni URAFIKI. Rafiki atafanya kila liwezekanalo kukulinda na kukusaidia wewe na watu wako wa karibu kwa uwema kabisa.

Hebu tumtake mtoa mada naye atiririke vizuri (upande wake) ili tumpe mawaidha mazuri
 
Mkuu mie hata ushauri sina kama unampenda kumuacha huwezi. Mie wangu sijawah mfuma ila tunamaugomvi balaa yaani ni juzi tu nimetoka sero kwa ajili ya kumshushia kipigo cha mwana ukome. Ndoa balaa. Wanawake pasua kichwa babu acha tu. Msamehe zaidi sana mgegede bila mpangilio.
 
Mkuu mie hata ushauri sina kama unampenda kumuacha huwezi. Mie wangu sijawah mfuma ila tunamaugomvi balaa yaani ni juzi tu nimetoka sero kwa ajili ya kumshushia kipigo cha mwana ukome. Ndoa balaa. Wanawake pasua kichwa babu acha tu. Msamehe zaidi sana mgegede bila mpangilio.

Jf raha sana. Mgojwa aliyelazwa hospitalini aliyegongwa na starlet anamuonea huruma na kumfariji mgonjwa mwenzake aliyegongwa na Fuso kitanda cha pili.
 
Back
Top Bottom