Sitasahau simu yangu ya mobitel 2002

Sitasahau simu yangu ya mobitel 2002

Hute

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,537
Reaction score
6,479
sitasahau kituko hiki, nikikumbuka huwa nacheka peke yangu halafu najishangaa.

simu yangu ya kwanza kabisa katika maisha yangu ilikuwa siemens lakini kipindi kile simu ya mkononi tulikuwa tunaiita mobitel kwasababu ndio ulikuwa mtandao wa simu wakati huo kabla ya buzz na tigo. nilikuwa ndio nimemaliza form six na nimenunua simu hiyo, ilikuwa imara sana hata ukidondosha. niliwaringishia sana vijana wenzengu form six leaver si unajua kuwa na simu ya mkononi!

siku moja nikiwa miyomboni Iringa kuna mgahawa mzuriiii pale, niliingia nikala chakula changu safi. nikahisi kwenda msalani. choo ilikuwa ya kiarabu/asian yaani choo ya kibakuli sio ya kukaa ni ya kuchuchumaaa.

nikashusha suruali yangu, nikamaliza mambo yangu simu ilikuwa mfukoni. ile napandisha suruari baada ya kumaliza safari yangu, siemens yangu ikadondokea kwenye ile choo ikaserereka hadi ikaingia ikazama na kupotea kabisa. sikuamini macho yangu.

mle kwenye simu kulikuwa na namba ya msichana wangu wa muhimu sana ambayo bado nilikuwa sijaishika kichwani nimeisevu na ilikuwa nikiwa pale iringa nionane naye tusalimiane zilipendwa. huwezi amini.....niliangalia kama mlango nimeufunga vizuri...kilichoendelea hapo unakijua. ila simu yangu niliipata na choo ile ilikuwa na maji mengi ya bomba, nilinawa sabuni mara saba hivi, na wiki nzima sikuwa na hamu ya kula...hahahahahahaaaaaaaaaaaaaa

ungekuwa wewe ungefanyeje?
 
Duh! Kwamba ulivuruga mavi mpaka siemen ikapatikana. Tafuta kazi ya kuzibua vyoo upo juu sana
 
Duh! Kwamba ulivuruga mavi mpaka siemen ikapatikana. Tafuta kazi ya kuzibua vyoo upo juu sana
amini usiamini, nikikumbuka huwa naona kama sikuwa mimi. ila kipindi kile simu kilikuwa kitu cha ufahari sana kiasi kwamba ukipoteza na line tena yenye mchumba wako unawezafanya chochote. ila simu yangu niliipata nikaiosha fresh.
 
sitasahau kituko hiki, nikikumbuka huwa nacheka peke yangu halafu najishangaa.

simu yangu ya kwanza kabisa katika maisha yangu ilikuwa siemens lakini kipindi kile simu ya mkononi tulikuwa tunaiita mobitel kwasababu ndio ulikuwa mtandao wa simu wakati huo kabla ya buzz na tigo. nilikuwa ndio nimemaliza form six na nimenunua simu hiyo, ilikuwa imara sana hata ukidondosha. niliwaringishia sana vijana wenzengu form six leaver si unajua kuwa na simu ya mkononi!

siku moja nikiwa miyomboni Iringa kuna mgahawa mzuriiii pale, niliingia nikala chakula changu safi. nikahisi kwenda msalani. choo ilikuwa ya kiarabu/asian yaani choo ya kibakuli sio ya kukaa ni ya kuchuchumaaa.

nikashusha suruali yangu, nikamaliza mambo yangu simu ilikuwa mfukoni. ile napandisha suruari baada ya kumaliza safari yangu, siemens yangu ikadondokea kwenye ile choo ikaserereka hadi ikaingia ikazama na kupotea kabisa. sikuamini macho yangu.

mle kwenye simu kulikuwa na namba ya msichana wangu wa muhimu sana ambayo bado nilikuwa sijaishika kichwani nimeisevu na ilikuwa nikiwa pale iringa nionane naye tusalimiane zilipendwa. huwezi amini.....niliangalia kama mlango nimeufunga vizuri...kilichoendelea hapo unakijua. ila simu yangu niliipata na choo ile ilikuwa na maji mengi ya bomba, nilinawa sabuni mara saba hivi, na wiki nzima sikuwa na hamu ya kula...hahahahahahaaaaaaaaaaaaaa

ungekuwa wewe ungefanyeje?

Ningekuwa ni mimi ningetoka nje ya Choo kisha nikamwita mtu yeyote aliyekaribu ili asimame mlangoni ili mtu yeyote asiingie chooni,kisha fasta ningeenda kutafuta mfuko wa Nailoni nikauvaa mkononi na kuitoa Simu Kiulainiiiii..!!

Ulihatarisha maisha yako kutia mkono chooni sababu ya Simu tu,je ungekamata Wembe humo chooni na kukukata? Unajua kuna Bacteria wangapi na wa aina ngapi hapo ulipotia huo mkono wako? Kifupi Ulithamini Simu na kuyatia hatarini maisha yako na afya yako kwaajili ya Simu tu....!!!!
 
hahahahaaaaa!!! hute umetisha mbaba! hahaha
 
Sasa mkuu iliendelea kufanya kaz?...pole sana...
 
Back
Top Bottom