- Thread starter
- #81
Tatizo linaweza kuwa hapo nilipo bold na hayo maswali mengine uliojiuliza maana wakati mwingine labda approach unayotumia labda imepitwa na wakati maana kama kuna watu umewazidi kipato na kimtazamo wanakupiga bao, jipange ujue kinadada wanataka nini maana wakati mwingine kinakaka huwa tunadhani kinadada wanataka ela kumbe ela ni matokeo baada ya kukubaliwa. Kuwa real yaani kuwa kama wewe sio unamtokea mrembo alafu unajifanya babu kubwa au unajifanya una akili za darasani, wakati mwingine unatakiwa umpe assignment yule unaemtokea ili na yeye afanya kazi ya kuonyesha shauku ya kutaka kukufamu in course of your discussion sio unajinadi kama unagombea ubunge kiasi kwamba demu siku moja amekujua ukoje kwani atabaki huyu nae day one tu nimekutana nae mipango kibao. Alafu utumie vijisenti kidogo hata kutoka outing na kuongea other issues apart from relationship na ndio maana huwa tunaulizana hobby zetu katika maisha ya kawaida ili upate wigo mpana wa kuongea nae ili hata ukiagana nae kesho yake awe na ajenda ya kuongea na wewe au japo ukikaa kimya anapata shauku ya kuongea na wewe kwa simu. Pia usiwe king'ang;anizi nenda mdogo mdogo kwa kuheshimu kile anachokuambia
Nashukuru kwa mchango huu ntafanyia kazi ushauri wako kwa umakini,
Kiukweli kwa haya maumivu saa zingine najiona tofauti kabisaa " feelings of becoming mad" sitaki kukata tamaa lakini kwa vitu nilivyopitia sijioni kama kuna future katika mahusiano.Mbaya zaidi linapokuja swali "shemeji mzima ? Kila siku ni kujiuma uma tu , moyo uliopondeka. Kila ninachokiandika ni ukweli mtupu ,kama una njia pia ya ziada kunisaidia kuondoka katika janga hili unaweza kuni-pm