Sista
JF-Expert Member
- Sep 29, 2013
- 3,208
- 1,038
Jamani wanawake sio majamvi ya wageni. Hiki ni kilio cha wanawake wote duniani. Hebu ona mfano huu: Ni kwamba leo unatongozwa na Mentor unagundua ana vimada kibao nje unaachana nae. Mwezi unaofata unakuwa na CHAMVIGA 1 anaenda kwao anapewa mke na wazazi wake anakuacha. Unakutana tena na ddsmchau1712 anakuomba muwe wachumba mnakaa miaka kadhaa hakuna dalili ya ndoa unaamua kumuacha na mnakutana tena na mtoto wa mtumishi wa bwana Jamaa_Mbishi wazazi wake walokole wanagoma usiolewe naye mnaachana. Baada ya muda unakutana na Rutashubanyuma dada zake wanamzuia asikuoe kutokana na tofauti ya kabila. Sasa utafanyaje? Kama umeelewa kuanzia leo msituite malaya na pia hatubadili wanaume kwa kujitakia ni mazingira magumu yanachangia.