yusufummaka
Member
- Apr 7, 2012
- 30
- 20
Siku ni kitu cha kawaida kuzikuta siri nyeti za serikali mikononi mwa wasiokuwa serikalini. Zipo school of thought mbalimbali za namna ziri hizo zinavyofika mikononi mwa wasiohusika lakini nimeiamini ile falsafa ya "like desolve like". Inasemekana vyama vyetu vya siasa vya upinzani vimejikita kikanda, kikabila na kidini zaidi kuliko kiitikadi za kisiasa hasa kutokana na historia ya uwanzishwaji wake. mfano CUF imetokea Pemba, CDM kimetokea Kaskazini zaidi, NCCR kimetokea Kanda ya Ziwa na Kaskazini, n.k. Kwasababu hii wafanyakazi walio Serikalini waliotokea eneo na kanda moja kilipotokea chama fulani basi wanawajibika kukiunga mkono chama husika japo kwa kutoa siri nyeti zitakazosababisha kukipa nguvu na kukidhoofisha chama tawala kwa vile wao hawana cha kupoteza hata kama serikali itafanya vibaya wakati wa uchaguzi. Wanaamini kuwa chama kile kikishinda uchaguzi na wao watakuwemo tu kwenye system na kufaidika kwa namna moja au nyingine. Inasemekana mfanyakazi aliyetoka kanda moja na chama fulani bila kujali aina ya taaluma yake, cheo chake, na eneo analofanyia kazi lazima afanye kitu kukisaidia "chama chao". Hivyo wingi na aina ya siri zitakazovuja itategemea pia na wingi na position walizoshika wafanyakazi waliotokea eneo na kanda moja na chama husika. Njia hii inachangia asilimia 70 ya kuvuja kwa siri nyeti za Serikali. 10% inachangiwa na mashabiki wa vyama husika bila ya kujali dini na kanda ya waasisi wake. 19% ya kuvuja kwa siri za serikali inachangiwa na wanachama na mashabiki wa chama tawala wasioridhishwa na namna jambo fulani lilivyoendeshwa ndani ya chama na serikali. Kundi lingine (1%) ni la wafanyakazi wanaokomoana ama kugombea nafasi za juu na maslahi kazini. Ushauri wa bure kwa serikali ijaribu kubalance wafanyakazi katika section na position mbalimbali watoke kanda na dini mbalimbali nchini. Mfano iko wizara moja naijua ambayo wafanyakazi wake makao makuu 97% ni wa dini na wa kanda fulani tu, hivyo hata kwenye uteuzi wa nafasi, semina na training mbalimbali za kitaaluma utakuta wanaoalikwa ni wafanyakazi wa dini ile na wa kanda ile kwa 99% hata kama wengine hawana sifa ama walishastaafu.