Siri ya umaarufu na ushindi wa Lowassa

Siri ya umaarufu na ushindi wa Lowassa

tajirijasiri

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
2,863
Reaction score
3,854
Ushindi wa Kisiasa hujengwa na Umaarufu (Popularity). Umaarufu (Popularity) hujengwa kwa namna mbili:-

1. Famous:- Umaarufu kwa mema.

2. Notorious:- Umaarufu kwa mabaya.

Kitendo cha kurudia rudia (au kwa mema au kwa mabaya) kulitamka jina la mtu au kitu humfanya mtu huyo kujijengea umaarufu kwenye jamii.

Umaarufu kwa namna zote mbili humuwezesha mwanasiasa yeyote duniani kushinda kisiasa katika Uchaguzi wowote. Mfano Rais Kenyatta na Rais Zuma.

Mwisho, iwapo mwanasiasa akitamkwa tamkwa sana kwa mabaya (notorious) na akawa na umaarufu kwa namna hiyo, na likawepo kundi jingine linalofanya yale yale ambayo mwanasiasa huyo anatamkwa nayo, na mwanasiasa huyo akawa kimya basi jamii humuonea huruma (sympathy) na kumpa kura kama comfort (faraja) ya kumpigania.

AKILI KUBWA TU ITANIELEWA.
 
Mungu hadhihakiwi apandacho mtu ndicho atakachovuna. Kile kilofichikia Mungu atakiweka peupe wakati ukifika. Mungu akasema msiposamehe watu wanapowakosea Mungu naye hatawasamehe ninyi makosa yenu. Ni nani asiye na dhambi dunia hii mpaka kumuhumu Lowassa kwa chuki namna hiyo? Kwanini anachuki na Lowassa kiasi hicho? Kwanini unapenda kuhukumu watu wengine namna hiyo? Je wewe ni mtakatifu sana kuliko Mungu? Kwani kuna ubaya gani mwenye dhambi mmoja akitubu? Kwa nini mnapenda kujifanya watakatifu sana?

Lowassa ni binadamu kama binadamu wengine? Ni dhambi gani aliyefanya mpaka mshindwe kumsamehe? Yesu alisema, ikiwa kuna mtu yoyote asiye na dhambi basi na awe wa kwanza kutupa jiwe kwa mwezako. Kwa kweli, it was too personal, hotuba ile imejaa chuki na hakuna kingine. Lakini apandacho mtu ndicho atachovuna, Mungu hadhihakiwi kabisa.

Anyway Mungu huwa anatusamehe bure mara saba mara sabini na huwa hakumbuki makosa yetu ya kale, who are we to judge others? Mungu angehesabu makosa ni nani angesimama?. Saa inakuja Mungu mwenyewe atakwenda kuwahukumu wote mnajiohesabia haki na kuhukumu wengine? Why only Lowassa? Chuki hii inatoka wapi?. Mungu ameona kila kitu, hatuwezi kumficha chochote, wakati muafaka atafichua kila kitu. Siyo sawa kwa kweli, it was too personal.
 
Anatembea mwenyewe, hatukani mtu... kawaacha wabunge wa chadema wote wako majimboni yee anapiga kazi tuuu na umati anaopata unapelekea jasho liwatoke hukoooo
 
URA YANGU NI HALALI KWA MGOMBEA URAIS MWENYE SIFA ZIFUATAZO:
1.Lazima awe na tuhuma za wizi
2.Awe mchafu
3.Aliyehama Cycyem kwa kukatwa!
4.Awe aliwahi kuwa Waziri mkuu wa Kataifa Kangu.
5.Ni lazima atoke Monduli
6.Awe na Mvi
7.Mikutano yake ni lazima iwe katika mfumo wa mafuriko,tsunami n.k
8.Awe na PESA hata kama si za halali!
9.Awe na marafiki kibao wenye fedha kutoka mataifa yaliyokwisha endelea.
10.Awe na Mali isiyohamishika ndani na nje ya Tanzania
11.Ni lazima awe amehusishwa kwa kina na kashfa ya Richmond
12.Anayesingiziwa kuwa ni mgonjwa.
13.Hotuba yake ya ufunguzi wa kampeini ni LAZIMA niwe niliisoma Kwenye tovuti ya chadema
14.Awe anauchukia umaskini,kwa hiyo ni Lazima awe Tajiri kiasi chake!
15.Awe amehama majuzi katika chama dola
16.Awe si MTU wa kuongea sana majukwaani,dakika 8-11 zinatosha !
KURA YANGU YA AJABU SANA
17.Haijali kama maendeleo yatakuja ama laah!,ila sasa inamtaka mgombea urais ambaye hapendwi na chama dola kuliko wenzake wote!
SINA SHAKA MGOMBEA URAIS ANAEKIDHI BASHASHA NA MSHAWASHO WA KURA YANGU NI Rais E.N.Lowassa "THE HERO"
 
Lowasa kiboko yao ccm wote wanapambana na mtu mmoja,, eti fisadi nani msafi waliobaki ccm? Watanzania tumeamka hatudanganyiki haiwezekani umutuhumu mwenzeko wakati hata wewe sio msafi.. Lowasa juu
 
Duh natamani ningekuwa edo, jamaa kaisimamisha nchi, ccm wanajambajamba hovyo kwa ajili yake, mtu 1 anakitoa jasho chama chenye miaka 60!!!Lwaigwanan mkuu nakupenda sana, Mungu akulinde na maovu yote wanayopanga juu yako
 
Mimi ni sehemu tu ya wafuasi wengi wa Dr Wilbroad Slaa tuliokubali hoja zake toka akiwa mbunge na kuamua kumfuata na kumsupport yeye na Chadema.

Tuli-ignore umbumbu wa Mbowee tukiamini uwepo wa Dr Slaa ndani ya Chadema unaleta weledi ndani ya Chama.

Tulipata hamasa na hoja za Dr Slaa akiwa mbunge mpambanaji mwenye kujenga hoja ndani ya bunge lililojaa maccm na mafisadi.

Tulipata hamasa ya kuandamana au hata kukesha kwenye mikutano ya Chadema ili kumsikiliza Dr Slaa kwa kuwa alikuwa mkweli kwa kusema na kutenda.

Tuliiunha mkono Chadema kwa hali na mali kwa kumuamini Dr Slaa!

Tulikesha na Dr Slaa pale NMC Arusha na kupigwa mabomu kwa kuwa tuliamini anasimamia lile analolisema.

Tulikuwa mstari wa mbele kunzia philips na ile barabara ya Kupandisha Tanki la maji Arusha pamoja na mke wake josephine tukapigwa Mabomu na virungu kwa kuwa tulikuwa tunapambana na CCM na serikali yao yote tukiamini tunapambana na ufisadi.

Tulishuhudia mpambanaji wa kweli akivunjika mkono lakini akiwa mstari wa mbele wa mapambano kukabiliana na jeshi la mafisadi.

Tuliendelea kumuamini Slaa na kueneza chuki dhidi ya ufisadi katika vijiji na mitaa ili watanzania waelewe na kujiletea ukombozi dhidi ya ccm iliyokuwa inawabeba mafisadi.

Tuliendelea kuongozwa na Slaa pale ambapo baadhi yetu waliporubuniwa na mafisadi (ref madiwani wa chadema waliofukuzwa na Chadema Arusha)

Tulimkubali Slaa pale ambapo alipotuahidi katiba mpya ndani ya siku 100 na ccm wakaja kuikubali hoja yake na kuifanyia kazi lakini wakaivuruga.

Tulimpigia kura Slaa kwa kuwa alituahidi na kutuhakikishia kuwa elimu bure inawezekana ...baadaye ccm waliikubali hoja hii na kuanza kuitekeleza.

Tulimuamini Slaa kwa kututajia ile orodha ya mafisadi ambao baadhi yao wameathirika kisiasa mfano Rostam na Lowassa..

Ni Dr Slaa pekee aliyeweza kusimama na ile hoja muhimu kitaifa yaani ufisadi mpaka leo hii.

Ni Dr Slaa pekee anayeirudisha ajenda hii muhimu ya kupambana na ufisadi katika sura mbalimbali bila kumungunya maneno na huku akiwa na viambatanisho.

Ni Dr Slaa huyuhuyu anayekataa kusupport upande wowote uliokiuka msingi ya kupambana na ufisadi.

Ni Dr Slaa huyuhuyu anayekataa kuififisha hoja ya ufisadi na rushwa iliyoongelewa toka kipindi cha Nyerere.

Ni Slaa pekee aliyeifanya ccm ianzishe mchakato wa kujivua gamba.

Ni Slaa pekee anayebakia kuwa icon ya Mabadiliko ya kweli yanayoletwa na watu wasio na harufu ya yaleyale!

Najipambanua kuwa mimi ni mpinga ufisadi niliyekuwa inspired na Slaa then Chadema na kuamua kuisupport Chadema na kuikandamiza ccm.lakini sasa nitaanza rasmi kuishisha Chadema ili tu tuupate upinzani makini na mpya wa kuleta mabadikiko ya kweli Tanzania.

UWEZO UPO,NGUVU IPO NA NIA IPO!!!!!
 
meningitis

Ushindi wa Lowassa hauzuiliki Mkuu, Popularity na Sympathy ya jamii zinambeba sana! Kumbuka Uhuru Kenyatta na Jacob Zuma
 
Last edited by a moderator:
Nipo na Lowasa. Dr. Slaa asiumie sana kwa EL kuhamia CDM kwa kuwa hata yeye siyo mwanzilishi wa hiki chama. Alikikuta na akiache salama. Ulale kwa amani mwana mwema wa Tanganyika, Bob Makani
 
balogun

Amina ndugu, ikiwa Mungu amekusudia lowassa awe Rais hakuna mwanadamu hatakaye mzuia,

mimi namshauri lowassa awasamee maana hawajui walitendalo,
 
Last edited by a moderator:
URA YANGU NI HALALI KWA MGOMBEA URAIS MWENYE SIFA ZIFUATAZO:
1.Lazima awe na tuhuma za wizi
2.Awe mchafu
3.Aliyehama Cycyem kwa kukatwa!
4.Awe aliwahi kuwa Waziri mkuu wa Kataifa Kangu.
5.Ni lazima atoke Monduli
6.Awe na Mvi
7.Mikutano yake ni lazima iwe katika mfumo wa mafuriko,tsunami n.k
8.Awe na PESA hata kama si za halali!
9.Awe na marafiki kibao wenye fedha kutoka mataifa yaliyokwisha endelea.
10.Awe na Mali isiyohamishika ndani na nje ya Tanzania
11.Ni lazima awe amehusishwa kwa kina na kashfa ya Richmond
12.Anayesingiziwa kuwa ni mgonjwa.
13.Hotuba yake ya ufunguzi wa kampeini ni LAZIMA niwe niliisoma Kwenye tovuti ya chadema
14.Awe anauchukia umaskini,kwa hiyo ni Lazima awe Tajiri kiasi chake!
15.Awe amehama majuzi katika chama dola
16.Awe si MTU wa kuongea sana majukwaani,dakika 8-11 zinatosha !
KURA YANGU YA AJABU SANA
17.Haijali kama maendeleo yatakuja ama laah!,ila sasa inamtaka mgombea urais ambaye hapendwi na chama dola kuliko wenzake wote!
ENL pamoja
 
Lowasa hazuiliki. Mbinu za CCM zinakuwa chafu na watu watampigia kura Lowasa kwa kukataa uchafu wa CCM. Leo tukiangalia katika maneno yetu ni maneno yapi yametamkwa sana kati ya Magufuli na Lowasa. Hii ni advert kubwa kwa Lowasa.
Kesho Magazeti yote yatakuwa na neno Lowasa.
 
Ushindi wa Kisiasa hujengwa na Umaarufu (Popularity). Umaarufu (Popularity) hujengwa kwa namna mbili:-
1. Famous:- Umaarufu kwa mema.
2. Notorious:- Umaarufu kwa mabaya.
Kitendo cha kurudia rudia (au kwa mema au kwa mabaya) kulitamka jina la mtu au kitu humfanya mtu huyo kujijengea umaarufu kwenye jamii.

Umaarufu kwa namna zote mbili humuwezesha mwanasiasa yeyote duniani kushinda kisiasa katika Uchaguzi wowote. Mfano Rais Kenyatta na Rais Zuma.

Mwisho, iwapo mwanasiasa akitamkwa tamkwa sana kwa mabaya (notorious) na akawa na umaarufu kwa namna hiyo, na likawepo kundi jingine linalofanya yale yale ambayo mwanasiasa huyo anatamkwa nayo, na mwanasiasa huyo akawa kimya basi jamii humuonea huruma (sympathy) na kumpa kura kama comfort (faraja) ya kumpigania.

AKILI KUBWA TU ITANIELEWA.

Jamaa una akili sana
 
Back
Top Bottom