VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,870
Hakuna jambo jingine lolote zaidi ya Mwenyekiti Magufuli kutokuwa tayari kuongoza CCM. Mwenyekiti wetu mpya hakuwa tayari kukabidhiwa Uenyekiti sasa. Hata yeye na Mwenyekiti mstaafu wamesema.Ndiyo maana amewaachia uongozi 'kijanja' walewale.
Kiongozi mpya huingia na viongozi wapya. Tazameni na mshuhudie kilichotokea na kinachoendelea Serikalini. Imeshindikana vipi chamani? Utayari wa uongozi wa chama haukuwepo. Ndiyo maana waonambali tuling'amua. Tukashauri ima Kikwete aendelee au uchaguzi 'wa kweli' ufanyike.
Kumwacha Kinana na Sekretarieti nzima ni uthibitisho wa hoja zetu. Mazoea na kulazimisha yamejidhihiri kwa umahiri. Eti amepata kura zote za NDIYO! Mwenyekiti mpya akiwa tayari na wakati wake kufika,ataanza kuongoza. Kwasasa,'hajachukua' madaraka yake. Amewaachia 'wenyewe'!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa ZOTE-NDIYO Dodoma)
Kiongozi mpya huingia na viongozi wapya. Tazameni na mshuhudie kilichotokea na kinachoendelea Serikalini. Imeshindikana vipi chamani? Utayari wa uongozi wa chama haukuwepo. Ndiyo maana waonambali tuling'amua. Tukashauri ima Kikwete aendelee au uchaguzi 'wa kweli' ufanyike.
Kumwacha Kinana na Sekretarieti nzima ni uthibitisho wa hoja zetu. Mazoea na kulazimisha yamejidhihiri kwa umahiri. Eti amepata kura zote za NDIYO! Mwenyekiti mpya akiwa tayari na wakati wake kufika,ataanza kuongoza. Kwasasa,'hajachukua' madaraka yake. Amewaachia 'wenyewe'!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa ZOTE-NDIYO Dodoma)