Sipendi kuombwa hela na misaada nakereka

Sipendi kuombwa hela na misaada nakereka

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
11,127
Reaction score
24,429
Hakuna kitu kinanikera kama kuombwaombwa misaada yaani sasa hivi kila simu nayopokea kutoka kwa ndugu na jamaa ni za kunililia shida tu

Sijui watu huwa wananionaje mimi?Hapa nawazungumzia ndugu hawa wa ukoo mmoja na sio hawa nilozaliwa nao

Utapigiwa simu utaombwa hela na kila misaada hata kama ukijaribu kumuelewesha kuwa kuna mambo unapitia au hauna fedha kwa wakati huo au hela umepeleka kwenye miradi fulani ndo kwanza hawakuelewi

Mimi sijui watu huwa wanaonionaje wakuu, kila mtu nikikutana nae ni wa kunililia shida tu,

Cha ajabu huwa nina mengi sana na mambo yangu huwa napambana natatua mwenyewe bila kuomba msaada wao wanashindaje kutatua shida zao wenyewe?Kuombaomba ni ujinga labda iwe imekua too much na tatzo limekuzidi ngumu mtu ni nzima ana miguu na mikono haumwi wala nini yupo fiti anaombaomba kweli?

Wakuu mimi ni mtu wa tofauti kidogo mimi ni ngumu sana kumuomba mtu kitu yaani hata nyumbani wife tukipungukiwa na nini bora tukose tu kwa wakati huo hadi hela ipatikane sio kuomba...Kwenye maisha yangu sina utamaduni wa kuombaomba kabisa.

Niwaambie tu ukweli mimi huwa nawasaidia walowahi kunisaidia tu au watu baki wengine wenye uhitaji, Nimesoma darasa la kwanza hadi Chuo kikuu kuna kipindi nilikula msoto nyie acheni tu dadeki nilikonda nikawa kama uzi sio mjomba, sio shangazi, sio binam wala sio baba mkubwa alonisaidia walikua wananitazama tu kama uchafu leo nimepata simu ndo zinalia.

Mimi wazazi wangu na ndugu zangu na wote walowahi kunisaidia maishani nipo loyal kwao vibaya mno, huwa najitoa kwao kwa hali na mali, huwa naamini kuwa napaswa kula na wale walionisaidia tu, yaani kama kipindi cha nyuma nilikua nateseka nakuomba msaada au unapaswa unisaidie na uwezo ulikua nao lakini ukanipuuza usitegemee kukusaidia hata unakufa, nitakuacha ufe kwakweli.

Kiukweli naonekana nina kiburi, roho mbaya na majivuno kisa sitoagi hata senti kwa mtu, lakini mimi huwa nasema kabisa kuwa kama hukuwahi kunisaidia usitegemee msaada wowote kutoka kwangu...

Kwakweli nachukia kuombwa hela ile mbaya, mimi akiniomba hela mke wangu, wazazi wangu, mchepuko,watoto wangu, ndugu zangu na marafiki na jamaa ambao kwa shida na raha tunasaidianaga inatosha

Bora nimsaidie mtu baki kuliko kumsaidia ndugu nilozaliwe naye au wa ukoo au jamaa ambaye kipindi cha msoto hakunisaidia chochote zaidi ya kunicheka

Kwenye maisha yangu nimechekwa sana,nimebezwa sana nilishakatishwa tamaa sana wengine hadi nimezaliwa nao lakini nilisimama kiume na kufika hapa nilipofika

Waache waseme sana kwamba mimi nina roho mbaya au naringa ila wallah hawataona hata senti moja kutoka kwangu yaani ni kusema kuwa watasubiri sana nilivyokua nadharauliwa naonekana takataka na siwezi chochote halafu leo huyo mtu ananiomba hela haki nakumbuka nilipotoka huwa napata hasira sana nikikumbuka misoto niliyopitia machozi hunitoka kwahiyo hela yangu sio ya kuchezea kabisa na bado nitaendelea kuwatimulia vumbi tu.

Kila mtu abebe msalaba wake mwenyewe.
 
Hakuna kitu kinanikera kama kuombwaombwa misaada yaani sasa hivi kila simu nayopokea kutoka kwa ndugu na jamaa ni za kunililia shida tu

Sijui watu huwa wananionaje mimi?Hapa nawazungumzia ndugu hawa wa ukoo mmoja na sio hawa nilozaliwa nao

Utapigiwa simu utaombwa hela na kila misaada hata kama ukijaribu kumuelewesha kuwa kuna mambo unapitia au hauna fedha kwa wakati huo au hela umepeleka kwenye miradi fulani ndo kwanza hawakuelewi

Mimi sijui watu huwa wanaonionaje wakuu, kila mtu nikikutana nae ni wa kunililia shida tu,

Cha ajabu huwa nina mengi sana na mambo yangu huwa napambana natatua mwenyewe bila kuomba msaada wao wanashindaje kutatua shida zao wenyewe?Kuombaomba ni ujinga labda iwe imekua too much na tatzo limekuzidi ngumu mtu ni nzima ana miguu na mikono haumwi wala nini yupo fiti anaombaomba kweli?

Wakuu mimi ni mtu wa tofauti kidogo mimi ni ngumu sana kumuomba mtu kitu yaani hata nyumbani wife tukipungukiwa na nini bora tukose tu kwa wakati huo hadi hela ipatikane sio kuomba...Kwenye maisha yangu sina utamaduni wa kuombaomba kabisa.

Niwaambie tu ukweli mimi huwa nawasaidia walowahi kunisaidia tu au watu baki wengine wenye uhitaji, Nimesoma darasa la kwanza hadi Chuo kikuu kuna kipindi nilikula msoto nyie acheni tu dadeki nilikonda nikawa kama uzi sio mjomba, sio shangazi, sio binam wala sio baba mkubwa alonisaidia walikua wananitazama tu kama uchafu leo nimepata simu ndo zinalia.

Mimi wazazi wangu na ndugu zangu na wote walowahi kunisaidia maishani nipo loyal kwao vibaya mno, huwa najitoa kwao kwa hali na mali, huwa naamini kuwa napaswa kula na wale walionisaidia tu, yaani kama kipindi cha nyuma nilikua nateseka nakuomba msaada au unapaswa unisaidie na uwezo ulikua nao lakini ukanipuuza usitegemee kukusaidia hata unakufa, nitakuacha ufe kwakweli.

Kiukweli naonekana nina kiburi, roho mbaya na majivuno kisa sitoagi hata senti kwa mtu, lakini mimi huwa nasema kabisa kuwa kama hukuwahi kunisaidia usitegemee msaada wowote kutoka kwangu...

Kwakweli nachukia kuombwa hela ile mbaya, mimi akiniomba hela mke wangu, wazazi wangu, mchepuko,watoto wangu, ndugu zangu na marafiki na jamaa ambao kwa shida na raha tunasaidianaga inatosha

Bora nimsaidie mtu baki kuliko kumsaidia ndugu nilozaliwe naye au wa ukoo au jamaa ambaye kipindi cha msoto hakunisaidia chochote zaidi ya kunicheka

Kwenye maisha yangu nimechekwa sana,nimebezwa sana nilishakatishwa tamaa sana wengine hadi nimezaliwa nao lakini nilisimama kiume na kufika hapa nilipofika

Waache waseme sana kwamba mimi nina roho mbaya au naringa ila wallah hawataona hata senti moja kutoka kwangu yaani ni kusema kuwa watasubiri sana nilivyokua nadharauliwa naonekana takataka na siwezi chochote halafu leo huyo mtu ananiomba hela haki nakumbuka nilipotoka huwa napata hasira sana nikikumbuka misoto niliyopitia machozi hunitoka kwahiyo hela yangu sio ya kuchezea kabisa na bado nitaendelea kuwatimulia vumbi tu.

Kila mtu abebe msalaba wake mwenyewe.
Kumbe na nyie maskini mnaombwa pesa ,ungekuwa nazo kama mimi usingekeleka

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna kitu kinanikera kama kuombwaombwa misaada yaani sasa hivi kila simu nayopokea kutoka kwa ndugu na jamaa ni za kunililia shida tu

Sijui watu huwa wananionaje mimi?Hapa nawazungumzia ndugu hawa wa ukoo mmoja na sio hawa nilozaliwa nao

Utapigiwa simu utaombwa hela na kila misaada hata kama ukijaribu kumuelewesha kuwa kuna mambo unapitia au hauna fedha kwa wakati huo au hela umepeleka kwenye miradi fulani ndo kwanza hawakuelewi

Mimi sijui watu huwa wanaonionaje wakuu, kila mtu nikikutana nae ni wa kunililia shida tu,

Cha ajabu huwa nina mengi sana na mambo yangu huwa napambana natatua mwenyewe bila kuomba msaada wao wanashindaje kutatua shida zao wenyewe?Kuombaomba ni ujinga labda iwe imekua too much na tatzo limekuzidi ngumu mtu ni nzima ana miguu na mikono haumwi wala nini yupo fiti anaombaomba kweli?

Wakuu mimi ni mtu wa tofauti kidogo mimi ni ngumu sana kumuomba mtu kitu yaani hata nyumbani wife tukipungukiwa na nini bora tukose tu kwa wakati huo hadi hela ipatikane sio kuomba...Kwenye maisha yangu sina utamaduni wa kuombaomba kabisa.

Niwaambie tu ukweli mimi huwa nawasaidia walowahi kunisaidia tu au watu baki wengine wenye uhitaji, Nimesoma darasa la kwanza hadi Chuo kikuu kuna kipindi nilikula msoto nyie acheni tu dadeki nilikonda nikawa kama uzi sio mjomba, sio shangazi, sio binam wala sio baba mkubwa alonisaidia walikua wananitazama tu kama uchafu leo nimepata simu ndo zinalia.

Mimi wazazi wangu na ndugu zangu na wote walowahi kunisaidia maishani nipo loyal kwao vibaya mno, huwa najitoa kwao kwa hali na mali, huwa naamini kuwa napaswa kula na wale walionisaidia tu, yaani kama kipindi cha nyuma nilikua nateseka nakuomba msaada au unapaswa unisaidie na uwezo ulikua nao lakini ukanipuuza usitegemee kukusaidia hata unakufa, nitakuacha ufe kwakweli.

Kiukweli naonekana nina kiburi, roho mbaya na majivuno kisa sitoagi hata senti kwa mtu, lakini mimi huwa nasema kabisa kuwa kama hukuwahi kunisaidia usitegemee msaada wowote kutoka kwangu...

Kwakweli nachukia kuombwa hela ile mbaya, mimi akiniomba hela mke wangu, wazazi wangu, mchepuko,watoto wangu, ndugu zangu na marafiki na jamaa ambao kwa shida na raha tunasaidianaga inatosha

Bora nimsaidie mtu baki kuliko kumsaidia ndugu nilozaliwe naye au wa ukoo au jamaa ambaye kipindi cha msoto hakunisaidia chochote zaidi ya kunicheka

Kwenye maisha yangu nimechekwa sana,nimebezwa sana nilishakatishwa tamaa sana wengine hadi nimezaliwa nao lakini nilisimama kiume na kufika hapa nilipofika

Waache waseme sana kwamba mimi nina roho mbaya au naringa ila wallah hawataona hata senti moja kutoka kwangu yaani ni kusema kuwa watasubiri sana nilivyokua nadharauliwa naonekana takataka na siwezi chochote halafu leo huyo mtu ananiomba hela haki nakumbuka nilipotoka huwa napata hasira sana nikikumbuka misoto niliyopitia machozi hunitoka kwahiyo hela yangu sio ya kuchezea kabisa na bado nitaendelea kuwatimulia vumbi tu.

Kila mtu abebe msalaba wake mwenyewe.
Sawa tumekuelewa
 
Waambie wafuate maisha yao. Kwetu nazungukwa na baadhi ya watu ni matajiri ila sio mzee wala bimkubwa wana hela, sasa nikamaliza chuo nikawa nahitaji mtaji (mkopo) wa milioni 2 kwa mmoja niongezee na niliyonayo. Sikuwa nimemtajia nataka anipe hela ila nilikuwa na summary ya plan kwenye karatasi namuelezea maana nadhani aliniona mzembe mbona wenzio wanafanya hiki na kile wewe hufanyi. Kuona hivyo akawahi kusema "mtafute vya kwenu" na maelezo mengine jinsi Mungu alivyo mkubwa ambavyo amemuinua yeye na familia yake.

Akaanza nionyesha baadhi ya ukuu wa Mungu kwenye simu. Appartment ya kupanga anayojenga wanaweka madirisha, ana biashara kubwa moja jiji fulani kila mtu anaijua sitaki niitaje hapa. Ana biashara nyingine nje ya nchi na majumba mikoa tofauti kama minne.
Sikuonyesha kushtuka baadae akawa anasema moyo wangu unavuja damu nataka nimuombe hela ila nashindwa naanzaje. Leo usiku kanishtua nimsogeze airport kuna deal la kushtukiza anaenda saini nakadilia sio chini ya 300M, picha nimepiga kumuuliza mtu kisa hawa watu siwaelewi Waethiopia maana wameshushwa na Costa hawaelewi
LMC_15052023_010655.Version 1 not ready.jpg

Na sina shida nae, dunia haitaki makasiriko, shida zangu sio lazima uwe wajibu wake.

Nimeanzia mbali sana na kisa changu kukueleza jambo moja. Kama unaweza tengeneza wanaoweza ombwa msaada wengine kwenye ukoo, huo ukoo itakuwa una Vicious Cycle of poverty. Fanya wanaoweza kusaidia wawe wengi sio wewe tu, fanya kama Marekani ilivyofanya kwa Ulaya ilivyotoa Marshall plan baada ya WW2, iliona haiwezi zungukwa na maskini lazima waionee wivu na hawataisaidia kitu watainyonya. Fanya kama mabeberu walivyowekeza China na South Korea, inawanufaisha wao pia.

Badala ya kusubiri kutoa hela za sikukuu, shangazi anaumwa shingo, mjomba kameza shoka, binamu ana ujauzito. Scan watu kadhaa wenye upeo uwasaidie kidogo nao watainua wenzao, fanya kama Wayahudi, Wahindi, Waarabu wanafanya kwenye koo zao. Wabongo sisi kazi kuchangiana harusi.

Kama huwezi napo wasikunyonye fanya unachoweza
 
Waambie wafuate maisha yao. Kwetu nazungukwa na baadhi ya watu ni matajiri ila sio mzee wala bimkubwa wana hela, sasa nikamaliza chuo nikawa nahitaji mtaji (mkopo) wa milioni 2 kwa mmoja niongezee na niliyonayo. Sikuwa nimemtajia nataka anipe hela ila nilikuwa na summary ya plan kwenye karatasi namuelezea maana nadhani aliniona mzembe mbona wenzio wanafanya hiki na kile wewe hufanyi. Kuona hivyo akawahi kusema "mtafute vya kwenu" na maelezo mengine jinsi Mungu alivyo mkubwa ambavyo amemuinua yeye na familia yake.

Akaanza nionyesha baadhi ya ukuu wa Mungu kwenye simu. Appartment ya kupanga anayojenga wanaweka madirisha, ana biashara kubwa moja jiji fulani kila mtu anaijua sitaki niitaje hapa. Ana biashara nyingine nje ya nchi na majumba mikoa tofauti kama minne.
Sikuonyesha kushtuka baadae akawa anasema moyo wangu unavuja damu nataka nimuombe hela ila nashindwa naanzaje. Leo usiku kanishtua nimsogeze airport kuna deal la kushtukiza anaenda saini nakadilia sio chini ya 300M, picha nimepiga kumuuliza mtu kisa hawa watu siwaelewi Waethiopia maana wameshushwa na Costa hawaelewiView attachment 2622814
Na sina shida nae, dunia haitaki makasiriko, shida zangu sio lazima uwe wajibu wake.

Nimeanzia mbali sana na kisa changu kukueleza jambo moja. Kama unaweza tengeneza wanaoweza ombwa msaada wengine kwenye ukoo, huo ukoo itakuwa una Vicious Cycle of poverty. Fanya wanaoweza kusaidia wawe wengi sio wewe tu, fanya kama Marekani ilivyofanya kwa Ulaya ilivyotoa Marshall plan baada ya WW2, iliona haiwezi zungukwa na maskini lazima waionee wivu na hawataisaidia kitu watainyonya. Fanya kama mabeberu walivyowekeza China na South Korea, inawanufaisha wao pia.

Badala ya kusubiri kutoa hela za sikukuu, shangazi anaumwa shingo, mjomba kameza shoka, binamu ana ujauzito. Scan watu kadhaa wenye upeo uwasaidie kidogo nao watainua wenzao, fanya kama Wayahudi, Wahindi, Waarabu wanafanya kwenye koo zao. Wabongo sisi kazi kuchangiana harusi.

Kama huwezi napo wasikunyonye fanya unachoweza
Umeeleza vizuri sana ila kwa watu hawa sio kabisa....
 
Tisa kumi, ulivyosema namsaidia mchepuko, sawa kwakuwa mleta Uzi maamuzi yako, tusemeje Sasa, Ila kazi, madaraka vinamwisho, miili yetu inachoka huwezijua Nani atakunyanyua ukiwa mzee au mgonjwa.
 
Tisa kumi, ulivyosema namsaidia mchepuko, sawa kwakuwa mleta Uzi maamuzi yako, tusemeje Sasa, Ila kazi, madaraka vinamwisho, miili yetu inachoka huwezijua Nani atakunyanyua ukiwa mzee au mgonjwa.
Tafuta pesa ikupe heshima
 
Watz wenģi wamezoea kuombaomba2 tena bila yà aibu ni tofauti nà Kenya nilifika Dodoma ndo nilichoka watu waliopita pale nilikuwa napata supu ni wengi ajabu!
DOM miyeyusho sana Yaan kuna Dingu alinicheki niko kwa ATM ile natoka tu akanifata samahani unaweza kunisaidia 3000 nilichoka kabisa
 
Tafuta pesa ikupe heshima
Sawasawa dangote, mwenye pesa zake Africa, karibu Moro uje kuona umasikini wangu, na mi nije kwako kuona ufahari wako, alafu utakacho kiona kwangu uje kuleta Uzi humu, Kama hupo dom, nakuja likizo mwezi wa sita hapo nzuguni.
 
Back
Top Bottom