Sio synovate wala redet - mitandao inatosha

Sep 13, 2010
8
0
kwa muda wa week mbili sasa magazeti yamegubikwa na utata wa report za synovate and redet juu ya nani yuko juu katika uchaguzi 2010.

Ukweli ni kwamba wengine hatukujua wala kupata nafasi ya kushiriki kwani ninaimani hii kitu ilifanyika kimya kimya - bora mara mia nimeshiriki kwenye FJ, japo wasiofika kwenye FJ hawawezi shiriki.

Sasa nadhani njia iliyobakia kujaribiwa na kutolewa report yake ni njia ya mobile phone. kwani kunawatanzania zaidi ya 16 millioni wanaomiliki mobile phone.

Mitandao anzisheni huduma hii ya "election polling trend" hii haidanganyi kama njia zingine pia i wazi kwa walio wengi. ITV mna kipima joto, kwa nini msianzishe huduma ya polling trend 2010???

hii itatusaidia angalau - kwani zingine zote zinaonekana uzushi tu.
 
You have a point allp. Niliposikia kuwa Synovate na Redet wanafanya hiyo kazi nikafikiri kuwa wangetoka na suluhu ya poor sampling lakini haikuwa hivyo! Leo nimepiga kura yangu kwa polling ya MwanaHalis nikaona zaidi ya watu 2,000 walioshiriki, Dr Slaa amepata zaidi ya 80% wakati Jk akiwa 8%

Polling ya Jf wameshiriki watu zaidi ya 9,000 kiasi ni mara nne zaidi ya voters wa Redet na Synovate! Hapo Dr Slaa amepata 64% wakati Jk ana 21.91%

As far as statistics is concerned, matokeo ya jf yanaweza kutoa reflection nzuri ya hali ya siasa nchini!

By the way, kwa watu makini hawakutegemea kitu tofauti kutoka kwa Redet na Synovate! Synovate wameshindwa ku-match na the law of universe kuwa "ukitaka kuwa muongo hakikisha kuwa hauko msahaulifu, na kama we ni msahaulifu basi usiwe muongo". Ni wiki chache tu Synovate walijitokeza na kusema hawakufanya utafiti, je wamesahau au?
 
Back
Top Bottom