feyzal
JF-Expert Member
- Apr 20, 2016
- 6,805
- 12,668
Habari ya kuamka wadau.
Sijapenda kuandika huu uzi ila nimeona wacha niseme tu ili wengine wenye tabia kama hii muache mara moja. Leo asubuhi kabla sijafanya shughuli zangu nikaona nipite kwa mzee nimsalimu kisha nikahangaike na mkate wa kila siku.
Nimefika kwake saa 12 na dk kadhaa asubuhi alifurahi kuniona tukaongea mengi sana, lakini huku mwishoni alinikwaza kwa jambo ambalo karibu kila siku anarirudia nimemvumilia sana ila leo nikaona nimtolee uvivu Mwenyezi Mungu atanisamehe kama nimefanya dhambi.
Tuliongea mengi sana mazuri lakini aliharibu padogo tu na kuondoa maana ya mazungumzo yote. Haya ni baadhi ya mazungumzo yaliyonikera.
Baba: Mwanangu ujitahidi uoe mapema ni vizuri zaidi akili yako itatulia, mimi nilimuoa mama yako nikiwa nina miaka 21 kipindi ambacho hata sina maisha mazuri lakini nikahangaika na mke wangu nikafanikiwa ila vijana wa sasa mna visingizio vingi, kuoa hampendi kabisa.
Mimi: Sawa mzee nitaoa nikimpata mwanamke muadilifu.
Hapo tuliongea mengi ila alianza kunivuruga hapa
Baba: unajua mimi nilimuacha mama yako kwa sababu tu ya umalaya, nilimfumania na wanaume. Aliniaga anakwenda kwa mama yake kumuona Morogoro lakini nikawa nina mashaka nae mienendo yake ndipo nikaanza kumfuatilia...kweli siku aliyoniaga akaenda kwa huyo hawara yake na nilimkuta pale kwa hawara yake. Nilimpiga sana mwishowe nikaona nitaua nikamuacha. (Hili suala alikua akiliongea karibu kila mara tukionana)
Akaendelea "Usije ukaoa mwanamke wa kabila la mama yako,ni wahuni sana ndo maana tangu nimemuacha mpaka leo hana maisha ya kueleweka yupo anatanga tanga,ameolewa na mwanaume wa ajabu hana mbele wala nyuma kwa upumbavu wake..
zamani nilitaka kumrudia lakini nimeona bado ana tabia zile zile na amewaambukiza tabia yake hata kaka zako wakubwa wamezaa hovyo hovyo kwa umalaya,Ona kaka yako mmoja amepata na ukimwi muda wote ni upuuzi tu sasa na wewe usifuate tabia ya mama yako"..mengine sipendi niyaongee hapa ni mengi na mazito
Uvumilivu ukanishinda nikamuuliza
Mimi: Baba unajisikiaje moyoni mwako unavyoongea maneno ya namna hiyo kumuongelea vibaya mzazi mwenzako mbele ya mtoto wake, mbona una mdhalilisha mama, unanijengea picha gani pindi nikimuona? Niwe nadhani nimezaliwa na mama malaya? Kwanini usingemstiri mwenzio kwa watoto wake kutengana kwenu ikabaki stori yenu? Mbona una mvua nguo?
Wewe mangapi umemfanyia mama tena tukishuhudia na hakuna hata siku moja amewahi kukudhalilisha namna hii kwa watoto wake, mama leo ana maisha magumu kwa sababu yako mali zake za urithi umetapeli mbona hatusemi na anakuheshimu? Unamuongelea vibaya kila mahala ili iweje? Niliongea mengi kwa hasira sana (Mungu anisamehe)
Mzee alifyatuka na kusema kuwa ninamfokea kiufupi hali ya hewa ilichafuka nikaondoka kwa hasira sana. Niko kazini lakini moyo wangu umekosa amani sijawahi gombana na mzazi wangu kiasi hiki tangu nimezaliwa ila leo maji yalizidi unga.
Pengine siko sahihi kwa nilichofanya au nikawa sahihi pia...naomba wenye busara waniambie nini cha kufanya maana nahisi hata tukionana sasa hivi na mzee tutashikana mashati kwa hasira alizokua nazo na mimi sitaki tuwe na utofauti huo.
Lakini hii tabia si njema kabisa iwe kwa mzazi wa kike au wa kiume kumdhalilisha mwenzako kwa watoto hata kama kweli ana makosa kuachana kwenu kwanini isibaki siri yenu.
Sent using Jamii Forums mobile app
=====
Maoni
Sijapenda kuandika huu uzi ila nimeona wacha niseme tu ili wengine wenye tabia kama hii muache mara moja. Leo asubuhi kabla sijafanya shughuli zangu nikaona nipite kwa mzee nimsalimu kisha nikahangaike na mkate wa kila siku.
Nimefika kwake saa 12 na dk kadhaa asubuhi alifurahi kuniona tukaongea mengi sana, lakini huku mwishoni alinikwaza kwa jambo ambalo karibu kila siku anarirudia nimemvumilia sana ila leo nikaona nimtolee uvivu Mwenyezi Mungu atanisamehe kama nimefanya dhambi.
Tuliongea mengi sana mazuri lakini aliharibu padogo tu na kuondoa maana ya mazungumzo yote. Haya ni baadhi ya mazungumzo yaliyonikera.
Baba: Mwanangu ujitahidi uoe mapema ni vizuri zaidi akili yako itatulia, mimi nilimuoa mama yako nikiwa nina miaka 21 kipindi ambacho hata sina maisha mazuri lakini nikahangaika na mke wangu nikafanikiwa ila vijana wa sasa mna visingizio vingi, kuoa hampendi kabisa.
Mimi: Sawa mzee nitaoa nikimpata mwanamke muadilifu.
Hapo tuliongea mengi ila alianza kunivuruga hapa
Baba: unajua mimi nilimuacha mama yako kwa sababu tu ya umalaya, nilimfumania na wanaume. Aliniaga anakwenda kwa mama yake kumuona Morogoro lakini nikawa nina mashaka nae mienendo yake ndipo nikaanza kumfuatilia...kweli siku aliyoniaga akaenda kwa huyo hawara yake na nilimkuta pale kwa hawara yake. Nilimpiga sana mwishowe nikaona nitaua nikamuacha. (Hili suala alikua akiliongea karibu kila mara tukionana)
Akaendelea "Usije ukaoa mwanamke wa kabila la mama yako,ni wahuni sana ndo maana tangu nimemuacha mpaka leo hana maisha ya kueleweka yupo anatanga tanga,ameolewa na mwanaume wa ajabu hana mbele wala nyuma kwa upumbavu wake..
zamani nilitaka kumrudia lakini nimeona bado ana tabia zile zile na amewaambukiza tabia yake hata kaka zako wakubwa wamezaa hovyo hovyo kwa umalaya,Ona kaka yako mmoja amepata na ukimwi muda wote ni upuuzi tu sasa na wewe usifuate tabia ya mama yako"..mengine sipendi niyaongee hapa ni mengi na mazito
Uvumilivu ukanishinda nikamuuliza
Mimi: Baba unajisikiaje moyoni mwako unavyoongea maneno ya namna hiyo kumuongelea vibaya mzazi mwenzako mbele ya mtoto wake, mbona una mdhalilisha mama, unanijengea picha gani pindi nikimuona? Niwe nadhani nimezaliwa na mama malaya? Kwanini usingemstiri mwenzio kwa watoto wake kutengana kwenu ikabaki stori yenu? Mbona una mvua nguo?
Wewe mangapi umemfanyia mama tena tukishuhudia na hakuna hata siku moja amewahi kukudhalilisha namna hii kwa watoto wake, mama leo ana maisha magumu kwa sababu yako mali zake za urithi umetapeli mbona hatusemi na anakuheshimu? Unamuongelea vibaya kila mahala ili iweje? Niliongea mengi kwa hasira sana (Mungu anisamehe)
Mzee alifyatuka na kusema kuwa ninamfokea kiufupi hali ya hewa ilichafuka nikaondoka kwa hasira sana. Niko kazini lakini moyo wangu umekosa amani sijawahi gombana na mzazi wangu kiasi hiki tangu nimezaliwa ila leo maji yalizidi unga.
Pengine siko sahihi kwa nilichofanya au nikawa sahihi pia...naomba wenye busara waniambie nini cha kufanya maana nahisi hata tukionana sasa hivi na mzee tutashikana mashati kwa hasira alizokua nazo na mimi sitaki tuwe na utofauti huo.
Lakini hii tabia si njema kabisa iwe kwa mzazi wa kike au wa kiume kumdhalilisha mwenzako kwa watoto hata kama kweli ana makosa kuachana kwenu kwanini isibaki siri yenu.
Sent using Jamii Forums mobile app
=====
Maoni
Pole mkuu. Ila naona kama kwenye familia yenu kuna kitu hakipo sawa. Wewe mwenyewe umeshindwa kumsitiri mama yako, maana umeirudia story ya mzee kuthibitisha kuwa bibi mkubwa aliachwa kwa umalaya. INATHIBITISHA KUWA UNA KIFUA KIDOGO KAMA MWANAUME, au vinginevyo ungeiwasilisha mada kwa namna ya kuwafichia siri wazazi wako. Mzee nae kukaa chini na wewe na mkaanza kupiga story za umalaya wa mkewe ambaye pia ni mama yako, nalo ni a bit strange. Hamna mipaka ya kuongea kati ya wazazi na watoto?