MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 19,395
- 40,221
Nawasalimu katika jina la Chama Cha Mapinduzi. Najua kuna mambo mengi ya kitaifa yanaendelea ambayo mngependa niandike maoni yangu ila kwa leo nawasihi tuangalie hili suala dogo ambalo linataka kuleta taharuki kwenye jamii.
Chanzo cha huu uzi ni tukio la Komredi Will Smith kumtwanga kofi MC Chris Rock kwenye sherehe za utoaji tuzo za Oscar. Sababu ya lile kofi ni utani wa MC uliogusa maradhi yanayomsumbua mke wa komredi Will Smith. Binafsi namuunga mkono Will Smith kwa kitendo cha kishujaa alichokifanya maana Sababu alikuwa nayo, nia na uwezo. Yule MC hatarudia tena upuuzi wake na itakuwa fundisho kwa ma-MC wengine ambao pia ni Comedians.
Tukirudi hapa nchini ni kwamba kumetokea wimbi la vijana wachekeshaji (comedians) kujiaminisha wao wanauweza u-MC hivyo kujitangaza kama washereheshaji pia na kuanza kupata kazi za hapa na pale. Baadhi yao kweli wamefanya vizuri kama vile MC Pilipili na wengine wachache. Sio jambo baya kwasababu ni kazi ya halali kabisa ya kujipatia kipato. Tatizo ni pale wengi wao kutoweza kufuata miiko ya kazi ushereheshaji na kujikuta wanafanya comedy sehemu isiyotakiwa hivyo kuleta usumbufu usio wa lazima kama ilivyotokea kwa mpigwa kibao Chris Rock. Hapa Tanzania kuna washereheshaji ambao pia ni comedians wamekuwa wakilalamikiwa mno kuleta mizaha sehemu isiyotakiwa mizaha.
Ushauri wangu ni kwamba hawa comedians kama wanataka u-MC wajifunze baadhi ya mambo muhimu toka kwa manguli wa hiyo fani kama vile Taji Liundi, Cheni na MC GaraB ili kutojichanganya wanapokuwa kwenye majukumu yao. U-MC ni kitu kingine kabisa kinachojitegemea ndo maana hapa nchini ni comedians wachache sana wanaoweza kuingia kwenye top list ya ma-MC wanaoaminika na kulipwa pesa nyingi. Nampongeza sana comedian Joti kwa kuweza kusimama kwenye fani yake bila kuendekeza njaa za kutaka kuwa MC tena. Comedians jitahidini kutafuta namna nyingine ya kuongeza kipato ili kuepuka makofi kama ya Will Smith.
Chanzo cha huu uzi ni tukio la Komredi Will Smith kumtwanga kofi MC Chris Rock kwenye sherehe za utoaji tuzo za Oscar. Sababu ya lile kofi ni utani wa MC uliogusa maradhi yanayomsumbua mke wa komredi Will Smith. Binafsi namuunga mkono Will Smith kwa kitendo cha kishujaa alichokifanya maana Sababu alikuwa nayo, nia na uwezo. Yule MC hatarudia tena upuuzi wake na itakuwa fundisho kwa ma-MC wengine ambao pia ni Comedians.
Tukirudi hapa nchini ni kwamba kumetokea wimbi la vijana wachekeshaji (comedians) kujiaminisha wao wanauweza u-MC hivyo kujitangaza kama washereheshaji pia na kuanza kupata kazi za hapa na pale. Baadhi yao kweli wamefanya vizuri kama vile MC Pilipili na wengine wachache. Sio jambo baya kwasababu ni kazi ya halali kabisa ya kujipatia kipato. Tatizo ni pale wengi wao kutoweza kufuata miiko ya kazi ushereheshaji na kujikuta wanafanya comedy sehemu isiyotakiwa hivyo kuleta usumbufu usio wa lazima kama ilivyotokea kwa mpigwa kibao Chris Rock. Hapa Tanzania kuna washereheshaji ambao pia ni comedians wamekuwa wakilalamikiwa mno kuleta mizaha sehemu isiyotakiwa mizaha.
Ushauri wangu ni kwamba hawa comedians kama wanataka u-MC wajifunze baadhi ya mambo muhimu toka kwa manguli wa hiyo fani kama vile Taji Liundi, Cheni na MC GaraB ili kutojichanganya wanapokuwa kwenye majukumu yao. U-MC ni kitu kingine kabisa kinachojitegemea ndo maana hapa nchini ni comedians wachache sana wanaoweza kuingia kwenye top list ya ma-MC wanaoaminika na kulipwa pesa nyingi. Nampongeza sana comedian Joti kwa kuweza kusimama kwenye fani yake bila kuendekeza njaa za kutaka kuwa MC tena. Comedians jitahidini kutafuta namna nyingine ya kuongeza kipato ili kuepuka makofi kama ya Will Smith.