Bwana Bongo
Senior Member
- Dec 12, 2021
- 167
- 239
#Porojozabongo
"Sio kila anayekuuliza, anakujali—wengine wanakuscan."
"Unajua watu wa leo?" Anaongea Bw. Bongo huku macho yake yakivinjari usoni kwa Mgogo.
"Wana maswali mengi, lakini si ya kusaidia—ni ya kukuchunguza.
Anavuta pumzi,
"Eti una kazi?" akaigiza kwa sauti
"Una pesa?"
"Una mahusiano?" sasa akacheka. "Hili la mwisho si swali, ni uwanja wa mashindano."
Kisha akamtazama moja kwa moja. "Ukijibu vibaya, unakuwa kichekesho mtaani. Wataandika status juu yako.
Ukijibu vizuri, unakuwa chuki kwao. Wanajiuliza: kwa nini wewe na si wao?"
Akanyamaza. Maneno yale yalimuingia Mgogo Hapo akajua, kuna watu si marafiki, si maadui—ni skana za roho yako
"Sio kila anayekuuliza, anakujali—wengine wanakuscan."
"Unajua watu wa leo?" Anaongea Bw. Bongo huku macho yake yakivinjari usoni kwa Mgogo.
"Wana maswali mengi, lakini si ya kusaidia—ni ya kukuchunguza.
Anavuta pumzi,
"Eti una kazi?" akaigiza kwa sauti
"Una pesa?"
"Una mahusiano?" sasa akacheka. "Hili la mwisho si swali, ni uwanja wa mashindano."
Kisha akamtazama moja kwa moja. "Ukijibu vibaya, unakuwa kichekesho mtaani. Wataandika status juu yako.
Ukijibu vizuri, unakuwa chuki kwao. Wanajiuliza: kwa nini wewe na si wao?"
Akanyamaza. Maneno yale yalimuingia Mgogo Hapo akajua, kuna watu si marafiki, si maadui—ni skana za roho yako