Barieda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2018
- 1,811
- 2,483
Habarini wapendwa wa jukwa letu pendwa la MMU.
Bila kurundika maandishi yasiyo na maana niende moja kwa moja maada, wapendwa hapa tusiwazungumzie single mother waliofiwa wenza wao( wajane) pamoja na wale waliotalikiwa hawa wana kundi lao.
Kina Dada waliopewa ujauzito hali wakiwa nyumbani, masomoni, au katika harakati za kutafuta maisha huko wanakoishi, hili ndo kundi ninalotaka kulizungumzia.
Aina hii ya single mother ndiyo inayoonekana kuwa kikwazo kwa waoaji na ndiyo inayolalamikiwa katika jamii kutokana na mazingira ya upatikanaji wa mtoto huyo kuwa amepatikana kwa njia isiyo halali yaani zinaa, kiuhalisia ni kweli lakini naomba dhambi hii ichukuliwe kuwa ni kama dhambi zingine ambayo mtu anaweza akafanya toba ya kweli akasamehewa na kutakaswa.
Kumbuka aina hii ndiyo inayonyooshewa kidole na kila mtu kuwa hawafai kuolewa na hii kutokana na baadhi yao kuonekana wanarudiana na wazazi wenzao ( kukumbushia) kutokana na bond ya mtoto, jambo hili ndilo kikwazo kwa kila mwanaume anayetaka kumwoa hata kama anampenda kiasi gani, na ndiyo maana hata wazazi huwachukia vijana wao wanapooa mwanamke wa aina hii.
Ili mwanamke aweze kuolewa na aweze kudumu katika ndoa yake anatakiwa awe na sifa zifuatatazo;
1. Kutofanya mawasiliano ya aina yoyote na baba wa mtoto au ndugu wa mtoto.
2. Kutokuwa na sababu yoyote itakayoweza kuwakutanisha kati yake yeye na mzazi mwenzie au ndg wa mtoto siyo za ugonjwa au kifo.
3. Kutofanya mazungumzo yoyote na mwanaye yahusuyo upande wa pili, aishiye kujua tu kuwa anayemlea siyo baba yake mzazi, ila mzazi alimkataa tangu kuzaliwa kwake. Kama atamhitaji asubir mpaka atakapoanza kujitegemea amtafute yeye mwenyewe kwa muda wake.
4. Aruhusu mwanaye kutumia majina ya mzazi mlezi ili kuimarisha uhusiano kati yake na watoto wenzie.
5. Awe kama alikata kamba na kuirusha baharini ikazama nikimaanisha hawezi irudia tena.
Mwanamke wa aina hii atadumu kwenye ndoa mpaka kifo, na ndiye anayefaa kuolewa. Nakaribisha maoni ya wadau.
Bila kurundika maandishi yasiyo na maana niende moja kwa moja maada, wapendwa hapa tusiwazungumzie single mother waliofiwa wenza wao( wajane) pamoja na wale waliotalikiwa hawa wana kundi lao.
Kina Dada waliopewa ujauzito hali wakiwa nyumbani, masomoni, au katika harakati za kutafuta maisha huko wanakoishi, hili ndo kundi ninalotaka kulizungumzia.
Aina hii ya single mother ndiyo inayoonekana kuwa kikwazo kwa waoaji na ndiyo inayolalamikiwa katika jamii kutokana na mazingira ya upatikanaji wa mtoto huyo kuwa amepatikana kwa njia isiyo halali yaani zinaa, kiuhalisia ni kweli lakini naomba dhambi hii ichukuliwe kuwa ni kama dhambi zingine ambayo mtu anaweza akafanya toba ya kweli akasamehewa na kutakaswa.
Kumbuka aina hii ndiyo inayonyooshewa kidole na kila mtu kuwa hawafai kuolewa na hii kutokana na baadhi yao kuonekana wanarudiana na wazazi wenzao ( kukumbushia) kutokana na bond ya mtoto, jambo hili ndilo kikwazo kwa kila mwanaume anayetaka kumwoa hata kama anampenda kiasi gani, na ndiyo maana hata wazazi huwachukia vijana wao wanapooa mwanamke wa aina hii.
Ili mwanamke aweze kuolewa na aweze kudumu katika ndoa yake anatakiwa awe na sifa zifuatatazo;
1. Kutofanya mawasiliano ya aina yoyote na baba wa mtoto au ndugu wa mtoto.
2. Kutokuwa na sababu yoyote itakayoweza kuwakutanisha kati yake yeye na mzazi mwenzie au ndg wa mtoto siyo za ugonjwa au kifo.
3. Kutofanya mazungumzo yoyote na mwanaye yahusuyo upande wa pili, aishiye kujua tu kuwa anayemlea siyo baba yake mzazi, ila mzazi alimkataa tangu kuzaliwa kwake. Kama atamhitaji asubir mpaka atakapoanza kujitegemea amtafute yeye mwenyewe kwa muda wake.
4. Aruhusu mwanaye kutumia majina ya mzazi mlezi ili kuimarisha uhusiano kati yake na watoto wenzie.
5. Awe kama alikata kamba na kuirusha baharini ikazama nikimaanisha hawezi irudia tena.
Mwanamke wa aina hii atadumu kwenye ndoa mpaka kifo, na ndiye anayefaa kuolewa. Nakaribisha maoni ya wadau.