MAPUMA MIYOGA
JF-Expert Member
- Jan 30, 2013
- 3,792
- 2,362
Dodoma. Wakati dirisha la usajili likifungwa saa 6 usiku wa Ijumaa, Uongozi wa Singida United umethibitisha kuwasajili wachezaji sita wakiwemo nyota wa kikosi cha Serengeti Boys.
Wachezaji wa Serengeti Boy waliojifunga Singida United ni aliyekuwa nahodha wa timu hiyo Issa Abdi Makamba, Ally Ng'anzi, Asad Juma na Mohamed Abdallah wamesajiliwa kwa lengo la kuendeleza vipaji vyao.
Mbali na makinda hao pia Singida United imemsajili mshambuliaji wa Danny Lyanga kwa mkataba wa miaka mwili akiwa mchezaji huru akitokea Oman.
Katika kuhakikisha inaziba vyema pengo la washambuliaji Atupele Green na Pastory Athanas, timu hiyo imefanikiwa kunasa saini ya mshambuliaji Mkongo Kambale Salita au Papy Kambale kutoka Etincelles ya Rwandwa.
Maoni yangu: Mwananchi please taarifa yenu mjue inakuwa na maana ikiripotiwa toka SINGIDA na sio DODOMA
Wachezaji wa Serengeti Boy waliojifunga Singida United ni aliyekuwa nahodha wa timu hiyo Issa Abdi Makamba, Ally Ng'anzi, Asad Juma na Mohamed Abdallah wamesajiliwa kwa lengo la kuendeleza vipaji vyao.
Mbali na makinda hao pia Singida United imemsajili mshambuliaji wa Danny Lyanga kwa mkataba wa miaka mwili akiwa mchezaji huru akitokea Oman.
Katika kuhakikisha inaziba vyema pengo la washambuliaji Atupele Green na Pastory Athanas, timu hiyo imefanikiwa kunasa saini ya mshambuliaji Mkongo Kambale Salita au Papy Kambale kutoka Etincelles ya Rwandwa.
Maoni yangu: Mwananchi please taarifa yenu mjue inakuwa na maana ikiripotiwa toka SINGIDA na sio DODOMA