Sina mapenzi naye tena, ushauri wenu tafadhali

Sina mapenzi naye tena, ushauri wenu tafadhali

wanaume wote wamezaliwa na baba na mama mmoja,hawana tofauti hata kidogo,so have courage,samehe uolewe kama unahisi japo ana qualities unazozitaka....jiandae mdogo wangu kwny ndoa ndo balaa,utaacha mara1000 usipokua makini,ni shiiiiiiiiiiiider
 
Mimi ni binti nina mpenzi wangu ambaye tuna muda mrefu kwenye uhusiano wetu.

Tatizo ni kwamba wakati nampenda alinifanyia visa vingi sana aliniumiza mpaka nikaona dunia chungu ila sikuwa na uwezo wa kumuacha kutokana na jinsi nlivyompenda.

Sasa yale maumivu ya vitu alivyokua ananifanyia sasa hivi ndo yamekua makali kiasi kwamba hata ule upendo umepungua na yeye ndo kama amezidisha mapenzi na amenitambulisha kwa wazazi.

Ushaur wenu nifanyeje ili ule upendo urud mana nkikumbuka vile visa sitamani hata kumuona.

Ushauri tafadhali


Samehe my dia, nilazima tusameheane kwa sababu hakuna perfect relationship. Na kama wewe ni kule msalabani basi kusamehe ni lazima kwa sababu na wewe unamakosa ambayo unamuomba Mungu akusamehe, huwezi kusamehewa kama huwezi kusamehe. Kama mtu ameshatubu na kujirudi na kuamua kutulia kwa nini ufikirie mambo ya nyumba. Tengeneza future nzuri dia wangu kuanzia hapo.
 
maumivu niache......... yani alikuhumiza zamani halafu maumivu yamezidi muda huu? aya pole inaonekana akili yako inachelewa kurespond, subiri kwanza ikiisha hiyo hali ntakuja shauri.
 
bora hata huyo alijirud,
wapo ambo hajirud na visa vinaendelea, na kwenye ndoa hayo uliyoumizwa ni cha mtoto!

kwa hiyo set mind yako kuwa mtu akisema samahan LET IT GOOOO.....!

usiyakumbuke alayofanya, IKUMBUKE SIKU YA KWANZA ALIPOKWAMBIA NAKUPENDA NA UKASEMA NDIYO FURAHA ILIYOKUWEPO KATI YENU, blieve me utamwona mpya kila siku na hutokaa ukumbuke kama amewah kukukosea.
 
huna mapenzi nae tena halafu unasema amekupeleka kukutambulisha kwa wazazi!unawezaje kwenda kwa wazazi wa mtu unakubali kutambulishwa wakati mapenzi nae huna?!? si ungekataaa!
ukweli ni kwamba kilichokusukuma wewe kukubali kwenda kutambulishwa kwa wazazi wake ni unamtaka na kumpenda.palipo na upendo hapakosi msamaha!msamehe moyoni mwako mfungulie moyo wote upyaa!songa mbele!
 
kila siku huwa naamini akheri ya mwanaume umjuaye kasoro zake kuliko mpya aloficha makucha yake!
 
Mimi ni binti nina mpenzi wangu ambaye tuna muda mrefu kwenye uhusiano wetu.

Tatizo ni kwamba wakati nampenda alinifanyia visa vingi sana aliniumiza mpaka nikaona dunia chungu ila sikuwa na uwezo wa kumuacha kutokana na jinsi nlivyompenda.

Sasa yale maumivu ya vitu alivyokua ananifanyia sasa hivi ndo yamekua makali kiasi kwamba hata ule upendo umepungua na yeye ndo kama amezidisha mapenzi na amenitambulisha kwa wazazi.

Ushaur wenu nifanyeje ili ule upendo urud mana nkikumbuka vile visa sitamani hata kumuona.

Ushauri tafadhali

Hapo hamjawekana ndani yuko hivyo, subiri timbwili lake mkishaoana ndio utatia akili. #AchanaNae .
Usije kutulilia humu badae..You got a great life ahead of u, shida zote za nini wewe ??? Ungekua karibu yangu hapa ningekuzaba na makofi ujue namaanisha nachosema.
 
msamehe2 urudishemoyowako kwake coz utakokwenda utaanzamoja borauyo kaishakaakwenyemstari.think twic.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom