Simulizi ya mzigo wa bosi uliharibu maisha yangu

gilbert35

JF-Expert Member
Nov 20, 2021
247
474
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu.
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

SEHEMU YA 01

Kwa Majina Naitwa Gilbert Mwaitika, Nina umri wa miaka 25, Uzaliwapo mwanaume sharti upambane kwa jasho ili tu maisha yasikuendee kombo, umaweza kupambana kwa hisabati nzuri za kimaisha ama zile hisabati mbaya zinazopigwa vita. Niliamua kuzing'ang'ania hisabati mbaya lakini zilinigharimu. Amini Maisha si mteremko.
Anza Nayo
.... Ilikuwa ni jumatano tulivu yenye kiubaridi cha aina yake nikiwa stand ya mabasi Moshi Mkoani Kilimanjaro, nilikata tiketi yangu katika kampuni ya mabasi ya Kilimanjaro Expres tayari kwa safari ya kuelekea Dar es salaam. Ilikuwa ni safari ya kusafirisha mzigo nilioubeba katika tumbo langu. Hii ilikuwa ni moja kati ya misheni zangu za kusafirisha mizigo kama hii lakini kuusafirisha kupitia tumbo langu ilikuwa ni mara yangu ya kwanza katika misheni zangu.

Majira ya saa 12 alfajiri safari ilianza rasmi nami nilikuwa mmojawapo wa abiria. Nilipata siti ya mwisho kabisa tena dirishani, nilipenda kukaa karibu na dirisha ili nipate hewa safi kutokana na mzigo naousafirisha nilioubeba katika tumbo langu.

Wakati safari ikiendelea Majira ya saa 4 asubuhi nilishtuliwa na sauti ya Dada aliyeketi siti ya pembeni yangu,

"Kaka samahani, ni muda wa kwenda kupata kifungua kinywa maana naona umelala"

"ah ahsante,hapa ni wapi?". Nikakurupuka toka usingizini na kuuliza

" ni Korogwe tanga"
alijibu dada yule ambaye nilimfahamu kama abiria wangu.
Nilipotazama dirishani niligundua basi lilishafika Tanga na limepaki hoteli moja maarufu huku korogwe kwa ajili ya kuruhusu abiria kupata chai. Ndani ya basi abiria walianza kushuka kwaajili ya kwenda kupata chochote kitu.

"Hakikisha mdomo wako haugusi chochote hadi utakapofika"

Maneno haya yalipita katika kichwa changu. Nilikumbuka kauli ya bosi wangu juu ya kula au kunywa. Lilikuwa ni onyo kutokana na mzigo nilioubeba tumboni.

"kumbuka ukinywa au ukila chochote utajitafutia matatizo kwa afya yako na pia itakuwa ni rahisi kugundulika"

Nilizidi kukumbuka. Baada ya dakika 15 safari iliendelea,kila mtu alipata kifungua kinywa isipokuwa mimi.

"karibu tujumuike pamoja",

Abiria mwenzangu alinikaribisha. Nilipotupia macho nione anachokula ghafla mate yalijaa mdomoni, alikuwa akila Ndizi Roast na mishkaki ya Kuku.

Nilijikuta nameza mate lakini kabla ya kumeza nilikumbuka kitu.

"kumbuka kumeza mate ni sawa na kunywa maji. Jitahidi sana mate yakijaa mdomoni uyateme, hili ni kopo maalum utakalotemea"

Nilijikuta nazuia safari ya mate hadi kupelekea kupaliwa na mate, nilianza kukohoa kwa fujo baada ya Kipaliwa na mate.
Haraka jirani yangu alinipatia maji ninywe baada ya kuona nazidi kukohoa. Niliyakamata yale maji na kuyafungua kwa pupa. Nilianza kupeleka mdomoni na kuyafakamia, nikameza fundo la kwanza, nikakusanya fundo la pili tayari kwa kumeza lakini kabla sijameza la pili nilikumbuka tena maneno ya Bosi wangu,

"Endapo ikitokea umemeza mate jitahidi kwa haraka utafune vipande vitatu vya hizi biskuti. usizidishe wala kupunguza. maji usinywe kabisa"

"Mungu wangu nimekwisha.....nimevunja sharti ee Mungu nisaidie... "

Nilijikuta natamka maneno haya kwa sauti baada ya kutema maji yale nje. Niliyatupa maji yale chini bila kufunga chupa, kwa haraka nilifungua begi langu na kutoa pakiti ya biskuti.

"Hapa nakula vipande 6 kabisa ili vikanyonye haya maji".

Nilijisemea na kuvibugia mdomoni kisha kuanza kuvitafuna kwa pupa bila kujali macho ya watu waliokuwa wakinitazama, kila abiria ndani ya basi alinigeukia na kunitazama huku akiteta jambo.

"Una nini wewe kaka jamani"

Aliuliza dada huyu aliyenipa maji mda si mrefu, nilimtazama kwa hasira,

"kama si yeye nisingekunywa yale maji, ila uzembe ni wangu pia kwa kukurupuka. Haina haja ya kugombana nae"

Nilijisemea moyoni kisha nikakwepesha macho yangu kutoka kwa yule dada

"samahani, ni bahati mbaya si kusudi"

Nilimwambia yule dada kisha nikatazama mchezo wa kuigiza uliokuwa ukiendelea ndani ya basi kupitia tv iliyofungwa juu. Sikumbuki kama alijibu samahani yangu au lah.
Wakati natazama mchezo ule mara mlio wa ujumbe ukaita katika simu yangu, niliitoa na kufungua simu yangu aina ya Nokia Tochi

" Ukifika Dar usishukie Ubungo, Mwambie Dereva unashukia Mbezi. Pia ukishuka usipepese macho yako, utakaposhuka vua Kofia kisha Jikune kichwani Mara Mbili. Then Tazama angani kwa Sekunde Kumi. Hii itakuwa ni ishara ya Kumtaarifu atakayekupokea Umewasili Atakayekupokea amevaa Tisheti nyeupe na Track nyekundu, Miguuni atakuwa peku na atakupa salamu kwa kukuvalisha Kofia uliyokuwa umeivua. Vinginevyo ukiona kinyume Siye. Sawa?"

Ujumbe ulisomeka Hivyo. Taratibu nilivuta pumzi ndefu kisha kuitoa nje. Nilijibu ujumbe ule

"Sawa Bosi" kisha nikaendelea kutazama Mchezo uliokuwa ukiendelea Kwenye Basi kupitia TV.
Sasa ni Rasmi simulizi Hii imekamilika. Kwa malipo ya Tshs 1000/= unaweza kuipata yote kupitia Namba 0621249611
ITAENDELEA
1615743727808.jpg
 
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu.
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

SEHEMU YA 02
Tulipoishia.....
" Ukifika Dar usishukie Ubungo, Mwambie Dereva unashukia Mbezi. Pia ukishuka usipepese macho yako, utakaposhuka vua Kofia kisha Jikune kichwani Mara Mbili. Then Tazama angani kwa Sekunde Kumi. Hii itakuwa ni ishara ya Kumtaarifu atakayekupokea Umewasili Atakayekupokea amevaa Tisheti nyeupe na Track nyekundu, Miguuni atakuwa peku na atakupa salamu kwa kukuvalisha Kofia uliyokuwa umeivua. Vinginevyo Siye. Sawa?"

Ujumbe ulisomeka Hivyo. Taratibu nilivuta pumzi ndefu kisha kuitoa nje. Nilijibu ujumbe ule kwa neno "Sawa Bosi" kisha nikaendelea kutazama Mchezo uliokuwa ukiendelea Kwenye Basi kupitia TV.
Hatimaye ilitimu saa 9 Alasiri Basi Liliwasili Chalinze Bus Terminal, Nilitamani gari ifike haraka Mbezi ili nishuke maana Njaa nayo na kiu Viliniandama. Halikukaa sana na baada ya dakika 5 basi liliendelea na Safari.
Nilimtumia ujumbe Bosi Kumtaarifu ndio tunatoka Chalinze-Pwani. Baada ya muda mfupi ujumbe ulijibiwa

" Kutoka Chalinze hadi Mbezi sio Mbali sana. Ni dalili ya kwamba Unakaribia Kufika, Zingatia maelekezo na Kumbuka Ukifanikiwa kufika Salama kuna Donge lako nono"

"Sawa Bosi"

Nilijibu ujumbe ule, Nilianza kuweka begi langu sawa Ili nifikapo nishuke kwa haraka niendelee na ratiba nyingine, Niliangaza macho ndani ya basi kila mtu alikuwa Bize kutazama Mchezo wa kuigiza Muvi ya Kimarekani iitwayo Mission Impossible. Nami niliitazama japo Ilianza muda lakini Ilikuwa Nzuri sana na Ilinivutia.
Nikiwa Nazidi Kutazama Ghafla tumbo lilianza kuninyonga, kwakweli ilikuwa ni Maumivu Ya Aina yake, Nilitafakari cha kufanya nikakosa,
"Vipi upo sawa?"
Lilikuwa ni swali kutoka kwa dada mmoja aliyeketi karibu yangu, Kwa kujikaza nikamjibu
"Ndio niko sawa usijali"
Nilikumbuka Onyo kutoka kwa Bosi wangu endapo ikatokea hali ikiwa mbaya

"Kumbuka Mzigo ulioubeba ni Hatari, unapaswa kuwa makini,. Ikitokea hali inazidi kuwa mbaya Usimtaarifu yoyote zaidi yangu, ukigundulika mishe itakuwa imefeli Na utajiingiza matatizoni. Ikibadilika nijulishe nitakutaarifu cha kufanya"

Tumbo lilizidi kuuma vibaya mno nikashindwa kujikaza, taratibu nilijipinda mgongo huku nikishika tumbo langu.
"Nikicheza Hapa nitajisababishia matatizo". Nilijisemea moyoni

"Kaka una tatizo gani? Sema tukusaidie, "
"huyu itakuwa ni Njaa inamsumbua"
Yalikuwa ni maneno kutoka kwa Abiria waliokuwa jirani nami. Sikuyajai maneno yale, haraka nilikamata Simu yangu na Kutuma Ujumbe Kwa Bosi

"Naona Hali inakuwa mbaya Bosi"

Baada ya Dakika moja ujumbe ulijibiwa

" Ulikula Chochote"

"Hapana Bosi. Hali inazidi kuwa Mbaya tafadhali angalia cha kufanya Bosi"

"Hebu Uliza Hapo Basi limefika wapi?"

Nilimgeukia dada aliyeko jirani yangu na kumuuliza.
"Eti dada Samahani, hapa ni Wapi? "

" Ndio tunatoka Maili Sita"
Alijibu dada yule. Haraka nilimtumia Ujumbe bosi wangu na Kumtaarifu tupo Maili Sita

"Sasa hapo Bado kidogo tu Unafika Mbezi. Jitahidi kujikaza tena kidogo, wewe ni mwanaume Gilbert, Nakutegemea".

Ujumbe alionitumia Bosi ulisomeka Hivyo. Nilitafakari maneno Haya nikajiuliza Hivi kweli Bosi anaelewa haya maumivu au ni tamaa mzigo ufike? Baada ya Kutafakari kwa kina Nilikumbuka Umasikini Ulionitoa Mbeya na Kunipeleka Kilimanjaro Kutafuta, nako nimepigana na sasa Naelekea Dar es Salaam kupeleka mzigo nilioubeba Tumboni, tumbo ambalo halistaili kuubeba mzigo kama huu, tumbo ambalo halijapokea chochote tokea Jana zaidi ya Huu mzigo nilioubeba. Ningefanyaje? Niliamua kuubeba ujumbe ule wa Bosi. Maumivu yalizidi Sana Hadi Machozi yakaanza kunitoka, Nilinyanyuka Na kuanza koelekea mbele, mgongoni nimeweka begi langu, nikitembea kama nina Kibiongo. Nilimfikia Kondakta wa Basi na kumuuliza.

"Samahani Hapa hadi Mbezi ni Mbali?"

" Sio Mbali Kivile, ni mwendo wa kama Dakika 20"
Nilipata matumaini Kusikia hivyo, lakini Tumaini hilo halikudumu kwani Hali ilikuwa mbaya Zaidi. Jasho jingi lilianza kunitoka, nilikamata simu na kuelekea upande wa ujumbe mfupi. Nilikuta ujumbe was Bosi ukiuliza kama bado hali ni mbaya. Niiandika Ujumbe kwa haraka

"Bosi mimeshindwa please nisaidie hali mbaya"

"Sasa sikia, muulize Konda hapo ni wapi kisha niambie kwa haraka ili nimtaarifu mtu aje kukuchukua Hapo"

Nilimuuliza Konda Kisha nikaketi moja ya siti zilizokuwa wazi pale mbele.
"Hapa panaitwa Njia Panda ya Kimara"
Nilimtumia Ujumbe Haraka Bosi, hali ilizidi kuwa mbaya huku mapigo ya moyo yakienda kwa Kasi, jasho nalo halikukoma. Ujumbe uliingia

"Sasa kuna mtu Atakuja Hapo na Pikipiki kukuchukua nimemwagiza. Cha kufanya Toa Lain kwenye Simu yako kisha ivunje na kuitupa Nje. Ukishaitupa Toa betri ya Simu iweke mfukoni, simu tupa Nayo nje kabla haujashuka. Ukishashuka tu Utamwona Mwanamama amevaa Gauni la Njano mfwate atakupeleka na pikipiki"

Kwa Haraka nilitoa Lain Bila Kutafakari na Kuitupia Nje, Simu nayo Nilitupa nje Bila mtu kuona Kisha nikabakiwa na Betri. Nilinyanyuka na Kumwomba konda Anishushe Hapahapa ila akanigomea. Alipoiona Hali yangu inazidi kubadilika Haraka Dereva alisimamisha Basi Kisha Nikashuka,. Basi likaniacha na kuendelea na Safari, niliangaza macho kushoto na Kulia lakini sikuona Pikipiki wala Mwanamama wala Gauni la Njano. Nilichoka nikagundua Nimesalitiwa .
I T A E N D E L E A
 
SIMULIZI YA MAISHA ; Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu.
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

SEHEMU YA 03
Tulipoishia.....
Nilimtumia Ujumbe Haraka Bosi, hali ilizidi kuwa mbaya huku mapigo ya moyo yakienda kwa Kasi, jasho nalo halikukoma. Ujumbe uliingia

"Sasa kuna mtu Atakuja Hapo na Pikipiki kukuchukua nimemwagiza. Cha kufanya Toa Lain kwenye Simu yako kisha ivunje na kuitupa Nje. Ukishaitupa Toa betri ya Simu iweke mfukoni, simu tupa Nayo nje kabla haujashuka. Ukishashuka tu Utamwona Mwanamama amevaa Gauni la Njano mfwate atakupeleka na pikipiki"

Kwa Haraka nilitoa Lain Bila Kutafakari na Kuitupia Nje, Simu nayo Nilitupa nje Bila mtu kuona Kisha nikabakiwa na Betri. Nilinyanyuka na Kumwomba konda Anishushe Hapahapa ila akanigomea. Alipoiona Hali yangu inazidi kubadilika Haraka Dereva alisimamisha Basi Kisha Nikashuka,. Basi likaniacha na kuendelea na Safari, niliangaza macho kushoto na Kulia lakini sikuona Pikipiki wala Mwanamama wala Gauni la Njano. Nilichoka nikagundua Nimesalitiwa .
Nilipiga hesabu za haraka nini nifanye, wazo likanijia na kwa haraka nilijikongoja kuelekea Pale nilipotupa Simu pamoja Na lain,. Lahaula! Sikuambulia chochote, punde pikipiki ikapita nikaisimamisha na Kuuliza

"Habari, Hapa na Hadi mbezi Shilingi Ngapi?"

"Elfu 3,000 Kaka"

Kwa bahati nzuri nilikuwa na Tsh Elfu Arobaini (40,000/=) mfukoni, nilipanda huku nikijitahidi kujikaza. Baada ya Dakika 10 Nilifika pale Mbezi Bus terminal. Kwa Shida nilishuka na Kutoa Noti Ya Elfu Kumi kisha Nikaangaza macho huku na Kule wapi pa kwenda.
Kwa mbali Niliona Bajaji Ikisubiri abiria. Nilifwata uelekeo wa ile Bajaji

"Kaka chenchi yako"

Ilisikika Sauti ya Yule dereva wa pikipiki Ikinikumbusha Juu ya Chenchi, nadhani ilikuwa Ni Elfu Saba. Sikuwa na muda wa Kugeuka maana Akiki yangu Haikuwa Sawa. Nilitaka nielekee sehemu Yenye Maficho Ili Nifanye Utaratibu wa Kuutoa Mzigo niliokuwa nao Katika tumbo langu.
Niliifikia Ile Bajaji Na kupanda bila kuuliza uelekeo wake Dereva Akawasha Tukaondoka. Ndani ya Bajaji Hali ilikuwa Mbaya sana, mbali na jasho kunitoka kichwa nacho Kiliuma sana, tumbo nalo halikukoma, Dereva aliligundua hilo na Kuniuliza tatizo nini, Nilitoa Noti ya Shilingi elfu moja Nikampatia kisha Nikamwamuru anishushe. Bajaji ilisimama kisha nikashuka. Kutupa Macho mbele nikaoana Kichochoro kimoja Kikielekea Kichakani. Baada ya Bajaji kuondoka Nilitambaa kufwata Kile kichochoro. Sikufika mbali Hali Ilizidi Kuwa Mbaya, nilijisogeza Hadi kwenye kichaka Kimoja Na Kujipumzisha Huku Nikiugulia Maumivu

"Ee Nisamehe kwa yote Niliyoyatenda Baba, "

Nilijisemea moyoni Baada ya Hali kuzidi kuwa Mbaya
Taratibu macho Yalianza Kuona Giza Japo bado ilikuwa ni Majira Ya Saa 11 Jioni. Kwa mbali Nilisikia Sauti Ya Mwanamama Akiimba, nilijaribu kugeuza Macho yangu na Kufanikiwa kumwona akiokota kuni Huku akiimba, Nguvu Ziliniishia Na Kwa mbali nilisikia hatua zikija Uelekeo wangu

Nilianza kusikia sauti ya Mama akiimba, nikaanza kufungua macho taratibu, nikashangaa Kumwona yule mama akinikanda usoni kwa maji ya Uvuguvugu, Sikumbuki Nini kilitokea baada ya Pale kichakani lakini Nilipofumbua macho nilijikuta Ndani ya Jumba Moja, Moshi wa Kibatari ukiwa umetamalaki ndani ya Jumba lile

"Oh umeamka Baba? Ngoja nikuletee maji ya Kunywa kwanza"

Aliongea yule mama kisha akaelekea upande wa pili wa Jumba lile, niligundua yule ni mtu mzuri kwangu kutokana na Msaada wa kunitoa kule kichakani na Kunileta Pale , isitoshe hata nyimbo alizokuwa anaimba ni Za Kidini, nadhani alikuwa ni mlokole. Punde alirejea akiwa na Glasi yenye maji,

"Kumbuka Hupaswi kunywa Maji wala kumeza mate Kabla hujawasilisha Huo mzigo Gilbert"

Maneno haya Yalipita katika Kumbukumbu zangu na Kugundua Bado mzigo Wa Bosi upo katika tumbo Langu.

"Sipaswi kunywa Haya Maji kabla ya Kuutoa Huu mzigo"

Nilijisemea Moyoni na Kuyapokea Yale maji kisha nikayaweka chini kwani nilikuwa Nimelazwa Mkekani, tumbo lilipungua maumivu kidogo
"Samahani Mama, ahsante kwa Msaada wako ulionipa,"
"Usijali mwanangu, duniani Utatengwa na wengi lakini Daima Mungu Hatokutenga, unapaswa kusali sana Mungu akuepushe Na Maswaibu yote yanayokuandama, "

Niliona sasa Mama huyu anaanza kunihubiria Injili ambayo kwa Wakati huo Sikuihitaji Kwanza, nilihitaji Kula ili niweze Kutoa Mzigo Niliokuwa Nao Tumboni.
"Samahani mama naweza Kupata Chakula?"
"Usijali Kijana wangu ngoja nikuletee"

Alinyanyuka na kuelekea upande wa pili wa Ile nyumba. Nadhani ni Jikoni, punde aliwasili na Saani ya Ugali na Tembele; Nilitabasamu kwa Mbali baada Ya Kugundua Ugali utanisaidia Katika Harakati za Kuutoa Mzigo niliokuwa Nao tumboni. Nilianza kuufakamia kwa Pupa hadi nikaumaliza ndani ya dakika 3.

"Inaonekana Ulikuwa una Njaa sana, ila usijali Mungu yupo nawe wakati Wote, Unapaswa kumrudia Mungu na uwe mtu Safi"

Alianza kunihubiria Mama yule hadi nikapatwa na Hasira. Nadhani alihisi Mimi ni Teja kutokana na Mtindo nilioweka Kichwani Kwangu,. Nilikuwa nimesokota Rasta. Alihisi labda mimi ni teja nilizidisha madauwa hadi nikajiovadozi na kupelekea kulala Kichakani, Haikuwa hivyo lakini ndivyo alivyodhani, Nilimwomba Kupumzika Kidogo ili kuzuia Injili Aliyokuwa Ananipa.
Aliniacha pale na kuniahidi Atakuja Baadaye kunijulia Hali yangu, alienda Kurudishia Mlango kisha Akaingia Chumbani kwake.

Nilitazama Juu ya Dari na Kuutafakari mzigo huu nilioubeba. Nilianza kuwa na matumaini kutokana na Ugali niliokula Naamini Utanisaidia niweze kuutoa mzigo huu, Hapo ndipo Nilipoanza Kukumbuka Siku Mbili zilizopita Nikiwa Kilimanjaro ilikuwaje hadi Nikaubeba Mzigo Huu kupitia Tumbo Langu. Ilikuwa Hivi...
ITAENDELEA
 
SIMULIZI YA MAISHA; Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu.
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

SEHEMU YA 04

Tulipoishia.........
Nilitazama Juu ya Dari na Kuutafakari mzigo huu nilioubeba. Nilianza kuwa na matumaini kutokana na Ugali niliokula Naamini Utanisaidia niweze kuutoa mzigo huu, Hapo ndipo Nilipoanza Kukumbuka Siku Mbili zilizopita Nikiwa Kilimanjaro ilikuwaje hadi Nikaubeba Mzigo Huu kupitia Tumbo Langu. Ilikuwa Hivi...

Endelea nayo.......
SIKU MBILI ZILIZOPITA
Ilikuwa ni Jumatatu maeneo ya Pasua Mkoani Kilimanjaro majira ya Mchana na Kila mmoja wetu alikuwa Makini Kusikiliza Kile alichokuwa anakieleza Clara. Clara ni Mwanamama aliyekuwa anaendesha Genge la uuzaji wa Madawa ya Kulevya. Mimi nilikuwa ni mmojawapo kati ya Vijana wake waliokuwa wakitumiwa katika Usafirishaji wa Madawa ya Kulevya, Japokuwa sikuwahi pelea madawa mikoani au nje ya Nchi ila nilikuwa mzoefu wa Kuyasafirisha kutoka Wilaya moja hadi Nyingine ama mtaa huu hadi ule.
Siku hiyo ilikuwa ni maalum kwa ajili ya Kubadilishiwa majukumu kwetu Sote, Kuna ambao walipea jukumu la Kusafirisha kwenda China na Ulaya kwa Siku mbili Zijazo, wengine Ndani ya Afrika na Wengine ikiwemo mimi Kupeleka Katika Mkoa wa Dar es Salaam na Mwanza. Baada ya zoezi fupi kufanyika yalitoka Majina ya Wanaopaswa kusafirisha Mikoani, Jina langu lilitajwa Katika listi hiyo. Kati yawatu Kumi waume kwa wake Ni mimi tu nilibahatika Katika Safari ya Kupeleka Dar es Salaam. Wengineo walipaswa kusafirisha Kuelekea Mwanza na Zanzibar.
Zipo njia Nyingi zilizotumika katika kusafirisha Madawa hayo, njia kama kufanyiw upasuaji zilitumika na nyingine nyingi, kwa Upande wangu sikuwahi kusafirisha Kwa kufanyiwa upasuaji ama nyingine Zaidi ya kuweka ndani ya bidhaa maalum kama vile Maboga n.k.

Baada ya Kikao Kuisha Bosi Clara Alituita Mmoja mmoja ndani Ya ofisi yake Ili kumtaarifu kila mtu Njia bora ya Kusafirisha, Ilipofika zamu yangu Nilifahamishwa njia ya Kumeza pakiti ya Madawa na kusafirisha kupitia Tumbo langu, Njia hii Ilinipasa kutokan na Sehemu nayopeleka Madawa Ni hatari kiusalama.

"Utameza Pakiti Nne za Madawa haya, Kesho Saa 6 Usiku Jitahidi Umeze hadi Kufikia Jumatano Kesho kutwa alfajiri uwe umemeza Kwa Ajili ya kuanza Safari. Natambua Hujawahi kmeza Hapo kabla ndio maana nimekuambia Uanze kesho Saa 6 Usiku ili Hadi Alfajiri jumatano uwe Tayari"

Yalikuwa ni Maneno ya Bosi Clara kwenda kwangu, ilinipasa kufanya hivyo kwa kuwa nilitoka Mbeya na Kuja Kilimanjaro Kutafuta Pesa,. Nakumbuka Rafiki yangu aitwaye Chalamila alinionganisha na misheni kama hizi aliporudi Mbeya kwa likizo Fupi baada ya kuniona nataabika bila Kazi. Yeye alikuwa ni mbobezi wa usafirishaji kwenda Nchini China. Japokuwa Yeye alikamatwa na Kuhukumiwa kunyongwa Nchini China lakini haikuwa sababu ya mimi kuiacha Hii kazi kwani Ilinitoa katika Umasikini kwa Kiasi.
Nilitamani nami Siku moja Niwe kama Rafiki yangu Nisafirishe Madawa ya kulevya China lakini sikupata Bahati ya hata kusafirisha Mikoani,. Leo hii niliona Dalili ya Kufikia tamanio langu baada ya Kuambiwa napaswa kusafirisha kwenda Jijini Dar Es Saaam. Niliona dalili ya kwenda nje ya Nchi kwa siku za usoni.

"Hakikisha unakula Ugali wa Kushiba Ifikapo majira ya Saa 4 usiku hapo kesho, na ifikapo saa 6 uanze kumeza Pakiti moja moja hadi ukamilishe. Ukishazimeza zote hakikisha mdomo wako haugusi chochote kitu hadi utakapofika Dar Es Salaam"

"Sawa Bosi, Je ikitokea Nimemeza mate kuna Madhara?
Niliuliza!!

"kumbuka kumeza mate ni sawa na kunywa maji. Jitahidi sana mate yakijaa mdomoni uyateme, hili ni kopo maalum utakalotemea"

Kwa kweli hapa nilipatikana. Sikupaswa hata kumeza Mate, sikusita kuuliza kwanini kutokula ama kumeza mate nikiwa na Mzigo tumboni, Bosi Clara Hakusita kuniambia

"Endapo ikitokea umemeza mate jitahidi kwa haraka utafune vipande vitatu vya hizi biskuti. usizidishe wala kupunguza. Ukitafuna itakusaidia kufyonza kiasi cha mate uliyomeza. Ila kumbuka maji usinywe kabisa"

Aliendelea kunisisitiza

"Kumbuka Mzigo ulioubeba ni Hatari, unapaswa kuwa makini, utakapokunywa itapelekea mzigo kupata unyevu kiasi ikubwa na madawa yanaweza kuvuja katika utumbo. Na ikigusana na utumbo ni Hatari kwa Afya yako,. Pia Ikitokea Ukala kabla ya Kufika Utalazimisha choo ambacho kitaambatana na pakiti utakazomeza, hivyo unapaswa kula ukishafika,. Ila labda hali inabadilika kabla hujafika usisite kunitaarifu. Ikitokea hali inazidi kuwa mbaya Usimtaarifu yoyote zaidi yangu, ukigundulika mishe itakuwa imefeli Na utajiingiza matatizoni. Ikibadilika nijulishe nitakutaarifu cha kufanya"

"Sawa Bosi nimekuelewa"

Baada ya Hapo nilitoka ofisini Kwa bosi Na kuelekea Nilikopanga,
Ilikuwa ni Ngumu kwa Yeyote kugundua Kwa Ofisi kama ile inashughulika na Madawa kwani Eneo lile Lilikuwa limezungushiwa Ukuta na Madhari ya nyumba ile ilikuwa mithili ya Hoteli. Ilikuwa na wafanyakazi wasiopungua 130 Waume kwa Wake.

Ilipofika Jumanne majira ya Saa 6 usiku nilikuwa mbele ya Meza iliyobeba pakiti nne (4) za madawa ya Kulevya. Sikuwahi kumeza lakini ilikuwa ni oparesheni yangu ya kwanza kumeza. Nilikamata pakiti Moja na kuipeleka Mdomoni, Nilijikaza na kuimeza mithili ya kidonge cha dawa, nilifanikiwa kumeza kisha nikakamata na ya Pili, nayo nilifanikiwa kuimeza. Lakini Ghafla kichefuchefu kilianza kuniandama, nilitamani kunywa hata maji lakini sikupaswa kwani ningekosea Masharti, nilipumzika Kwanza hadi majira ya Saa 8 Usiku nilijihisi shwari ndipo nikaiendea Pakiti Ya tatu. Kabla sijaimeza Kichefuchefu kilinizidi, nilitaka kutapika lakini haikuwezekana, ilibidi niahirishe zoezi hadi Nusu saa Baadae nikafanikiwa kuimeza Pakiti ya Tatu kwa Tabu. Baada ya kuona kichefuchefu kinazidi niliahirisha pakiti Ya nne na Ya mwisho Hadi Hali ikikaa sawa. Nilipitiwa na Usingizi nkidogo

"Utameza Pakiti Nne za Madawa haya, Kesho Saa 6 Usiku Jitahidi Umeze hadi Kufikia Jumatano Kesho kutwa alfajiri uwe umemeza Kwa Ajili ya kuanza Safari. Natambua Hujawahi kmeza Hapo kabla ndio maana nimekuambia Uanze kesho Saa 6 Usiku ili Hadi Alfajiri jumatano uwe Tayari"
Nilishtuka Usingizini Baada ya kukumbuka maneno Haya, kutazama saa Ilikuwa ni Saa 11 Kasoro. Haraka niliamka na Kuelekea Mezani tayari kwa kumalizia Pakiti ya Nne iliyobakia, Mara simu Yangu Ikaita, kutazama alikuwa Bosi Clara..

"Hey Gilbert, Umefikia wapi"

"Bado pakiti Moja Bosi"

"Jitahidi ukamilishe kabla ya Saa 11:30 utakuja kuchukuliwa hapo kupelekwa Stendi kwa ajili ya Safari"

Simu ikakatwa, nilikamata pakiti ile Kicha nikaibugia Mdomoni na Kisha kuimeza Kabisa, haraka nilianza kupiga Mazoezi ya Push up ili kuzuia Kichefuchefu. Nilifanikiwa Kumeza Pakiti zote Nne na Ilipotimu saa 11:30 nilifwatwa na Dereva pikipiki kwa ajili ya Kuelekea Stand ya Mabasi Moshi Mkoani Kilimanjaro, nilikata tiketi yangu katika kampuni ya mabasi ya Kilimanjaro Expres tayari kwa safari ya kuelekea Dar es salaam. Nilipatiwa 40,000/= kama Dharura na Yule dereva pikipiki kwa maelezo Ya Bosi Clara.
Ilipotimu saa 12 alfajiri safari ilianza rasmi nami nilikuwa mmojawapo wa abiria. Nilipata siti ya mwisho kabisa tena dirishani, nilipenda kukaa karibu na dirisha ili nipate hewa safi kutokana na mzigo naousafirisha nilioubeba katika tumbo langu.

Hivi Ndivyo ilivyokuwa hadi kufikia Hapo nilipo katika Jumba Lile nililopatiwa msaada na Mama Mlokole, Nilitegemea Ugali niliokula lazima Haja kubwa Itoke ikiambatana Na Pakiti zile Za Madawa.
ITAENDELEA
 
SIMULIZI YA MAISHA: Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu.
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611
SEHEMU YA 05

Tulipoishia.........

Simu ikakatwa, nilikamata pakiti ile Kisha nikaibugia Mdomoni na Kisha kuimeza Kabisa, haraka nilianza kupiga Mazoezi ya Push up ili kuzuia Kichefuchefu. Nilifanikiwa Kumeza Pakiti zote Nne na Ilipotimu saa 11:30 nilifwatwa na Dereva pikipiki kwa ajili ya Kuelekea Stand ya Mabasi Moshi Mkoani Kilimanjaro, nilikata tiketi yangu katika kampuni ya mabasi ya Kilimanjaro Expres tayari kwa safari ya kuelekea Dar es salaam. Nilipatiwa 40,000/= kama Dharura na Yule dereva pikipiki kwa maelezo Ya Bosi Clara.
Ilipotimu saa 12 alfajiri safari ilianza rasmi nami nilikuwa mmojawapo wa abiria. Nilipata siti ya mwisho kabisa tena dirishani, nilipenda kukaa karibu na dirisha ili nipate hewa safi kutokana na mzigo naousafirisha nilioubeba katika tumbo langu.

Hivi Ndivyo ilivyokuwa hadi kufikia Hapo nilipo katika Jumba Lile nililopatiwa msaada na Mama Mlokole, Nilitegemea Ugali niliokula lazima Haja kubwa Itoke ikiambatana Na Pakiti zile Za Madawa.

Endelea nayo....

Nikiwa Pale mkekani usingizi ulinipitia na Baada ya muda kidogo nikashtuka, mwili ulikuwa umelowa Jasho jingi sana mithili ya mtu aliyemwagiwa maji, Nilihisi Haja kubwa Palepale na nilifungua Mlango ule ulioegeshwa,
"Vipi huko kuna Usalama"

Mama Yule aliuliza Baada ya kusikia Nafungua mlango

"Ndio, nahitaji kwenda msalani Mama yangu,."

Alinielekeza choo kilipo kisha Nikatoka, Kufika chooni Nilijisaidia Pembeni ya Tundu ili kama Pakiti ikitoka Niichukue kwani Mzigo kama ule kwa Hapa Dar ni dili, isitoshe Bosi wangu Alishanisaliti baada Ya kuniacha Kwenye Mataa bila hata ya Mawasiliano.
Nilifanikiwa Kujisaidia Lakini Nilipokichambua kile kinyesi kwa kutumia Kijiti niliona Tu pakiti Moja. Niliichukua Na kuifutafuta Kisha Nikaiweka Mfukoni nikitarajia Pakiti tatu zilizobakia tumboni Zitatoka tu muda Si mrefu. Nilirudi Ndani na kuendelea kupumzika

Siku inayofuata Asubuhi niliamshwa na Mama yule kwani Nililala sana kutokana na Uchovu wa Safari na Maumivu niliyopitia Siku Moja iliyopita. Nakumbuka ilikuwa Ni Siku ya Alhamisi, Mama yule alikuwa akijishughulisha na Kukaanga Mihogo kwa ajili ya Kwenda Kuuza, alinipatia Miogo Mitatu Pamoja na Chai niweze kufungua Kinywa, nilipokea japo Chai sikuinywa, nilitafuna Miogo Mikavu kwani bado pakiti Tatu zilikuwa ndani Ya Tumbo Langu. Baada ya Mama yule ninayependa kumwita mlokole alimaliza Kukaanga Mihogo na kuifunga kwa ajili ya Kwenda kuitembeza.

"Mimi natoka Kijana wangu, nitarudi Muda si Mrefu. Ukihisi njaa usisite Kuchukua Mihogo iko jikoni na Chai, usiwe na shaka maana Mungu bado hajakutenga kijana wangu"

"Sawa mama nashukuru, Nitakusubiri Hadi utakaporejea"

Alipoondoka tu Nilielekea Msalani kwani Haja kubwa ilikuwa Imenikamata. Nilitegemea Kutoa Pakiti tatu Zilizobakia Lakini haikuwa kama nilivyotajaria. Kinyesi kilikuwa Na Pakiti Moja Tu, hakika nilichoka kwani Kawaida huwa Kinyesi cha kwanza Hutoa Pakiti zote na ikikawai sana ni hadi Awamu ya Pili. Sasa Hii ni ya Pili lakini Imetoa Pakiti nyingine Moja, Nilihuzunika sana. Kinyesi kilikuwa na Rangi nyeusi lakini Sikutilia Maanani, niliweka pakiti ile mfukoni Kisha nikatoka.
"Sasa nina Pakiti mbili Mfukoni na mbili Tumboni"

Nilijisemea Peke yangu nikiwa chini ya Mti mmoja pale Kwa yule Mama mlokole. Nilijipa matumaini lazima Pakiti Hizi zilizobakia tumbini Lazima zitoke tu. Nikatafakari kisha Nikanyanyuka na Kuelekea ndani

"Hapa Lazima niondoke niingie Mtaani"

Nilijisemea. Nilikumbuka nilikuwa na Ile Elfu Ishirini Na tisa iliyobakia kwenye Shilingi Elfu Arobaini. Nikatoa Elfu 5 na Kuiweka Juu ya Mkeka kisha Nikaondokale nisijue Pa kwenda kuanzia

"utanisamehe maana naondoka bila Kukuaga japo umenitendea wema wa kutosha, Naamini Elfu tano Haitoshi lakini Itakusaidia kwa namna moja ama nyingine"
Nilijisemea Moyoni nikiwa Naondoka nikifwatisha barabara itokayo katika Nyumba ile.
Rasmi niliingia mtaani nikiwa sina Makazi maalum, mfukoni nina Tu shilingi Elfu Ishirini na nne, Pakiti mbili za Madawa ya kulevya aina ya Heroin na pakiti zingine mbili ndani ya tumbo langu. Nilitembea kwa muda mrefu hadi kiu kikaanza kuniandama kwa jazba. Nina takribani Siku ya pili sasa Sijanywa maji yanayotosha kukata kiu,.
"Liwalo na liwe"

Nilijisemea baada ya kiu kuzidi kuniandama, pakiti hazitoki tumboni, Haja hainishiki, iweje nivumilie nife kwa kiu?
"Ah kama yatavujia tumboni Yavujie tu bwana, nishachoka na kiu hiki bwana"

Nilijisemea huku nikiliendea Duka moja, nilitoa Elfu mbili na kuagiza Maji ya Kilimanjaro, niliyachukua na Kuelekea katika Barabara ya lami niliyoiona Kwa mbali, Niliona kijiwe cha Kahawa pembeni ya Barabara huku mjadala ukiendelea, ulikuwa ni Mjadala wa mpira wa Miguu Kufuatia Timu ya Yanga Kuifunga Simba Goli Moja kwa Bila, nilijikuta natabasam kwani nilikuwa ni mmoja wa mashabiki wa Yanga. Nilifungua chupa ya maji na Kuanza Kuyagugumia maji yale, Hadi nafikisha nusu chupa ndipo nilitosheka kisha nikafunika chupa yangu na Kusikiliza zaidi mjadala ule.

Tukiwa Pale alifika Bwana mmoja amevaa Pensi nyeusi, kichwani Kasokota Rasta, alimwendea muuza kahawa wakakonyezana kisha wakazungumza kwa ishara, Niliona muuza Kahawa akiingiza Mkono mfukoni na Kutoa Noti za shilingi elfu Kumi Na Kumpatia yule bwana. Nilipoona tukio lile niligundua Jambo, ndipo nilipokumbuka maneno ya rafiki yangu Chalamila akinieleza siku moja

"unajua mitaani ni Ngumu sana kugundua biashara ya Madawa ya Kulevya Ikiwa inafanyika"

"Kivipi Broo?"

"Hii biashara ni Ya siri sana, Maana ukigundulika Utapelekwa tu Jela na Kuhukumiwa, isitoshe unaweza kuuwawa maana biashara hii ina vigogo wengi, wanahofia kutajwa hivyo wanatuma mtu akumalizie mbali. Ukitaka kushuhudia biashara hii mitaani ama kuifanya we Fika kwa fundi Viatu ama vijiwe vya Kahawa, wauza Kahawa wengi Huwa wanauzia mateja unga, na Mawasiliano yao ni ya Siri sana."

Nilikumbuka maneno haya. Hakika sitamsahau Chalamala rafiki yangu, alinifundisha vitu vingi sana, yeye ndiye aliyenifundisha namna ya kujihami, nilikuwa sijui kupigana lakini yeye alinifunza. Alikuwa ni Mlinzi wa Bosi wetu kabla ya kutumwa China kusafirisha madawa. Na huko ndipo alipokamatwa na Kusadikika aliuwawa, palepale nilitabasamu kwa kuwa pakiti mbili nilizonazo naweza Kuziuza kirahisi. Palepale hali yangu ilibadilika Ghafla, tumbo lilininyonga kisawasawa

ITAENDELEA

SIMULIZI YA MAISHA: Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu.
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611
SEHEMU YA 06

Baada ya maumivu kuzidi nilinyanyuka na kujikongoja hadi katika gari bovu lililokuwa limeegeshwa pembeni ya kijiwe, nilijikaza kiume lakini haikusaidia chobhote,

"Itakuwa yale maji niliyokunywa ndio yameleta shida" Niliwaza. Lakini ningefanyeje ingali kiu ilinikamata? Nilijinyanyua na kuelekea hadi duka la dawa, niliagiza diclopa, nilipopewa nilibugia vidonge viwili bila maji, nilivitafuna kama sina akili zote, muhudumu alinishangaa lakini sikujali. Nilirudi pale kwenye gari bovu na kujilaza, kila apitaye alinichukulia kama teja kutokana na msokoto wa rasta pamoja na uchafu wa mavazi yangu.

Baada ya dakika 5 maumivu yalikata, zile dawa zilinisaidia kiasi, tumbo lilianza kudai haki yake, nilinyanyuka na kuelekea kwenye vibanda vya mama n'tilie, nilifika na kuagiza ugali maharage,

"Pesa kwanza" alidai mama muuza chakula, alihisi sikuwa na hela kutokana na mwonekano niliokuwa nao, kwa dharau nilizama mfukoni na kumtolea noti ya shilingi elfu kumi,

"Chenji kwanza naomba" nami niliamua kujibu mapigo, aliondoka kwa madoido na punde alirudi na chenji yangu. Alielekea jikoni na kupakua ugali maharage kisha aliuleta nami nikala.
Baada ya muda nilitoka pale na kuelekea kwenye mti mmoja wenye kivuli, nilijilaza hapo na punde usingizi ulinipitia.

Nilishtuka majira ya alasiri, nilijisachi kuhakiki kama kuna kasoro, vitu vyangu vilikuwa sawa, nilianza kuzurura mitaani hadi nikadikia kituo cha magari mbezi, katika angaza yangu niliona magari ya Temeke Buza.

"bila shaka huko ndiko kuna wahuni na mateja wenggi," nilijisemea. Haraka niliwahi gari iliyokuwa inaanza kuondoka,

"nauli unayo lakini? Tusije kushikana mashati". Alihoji konda
"Kamata kabisa na chenji yangu unipe". Nilimjibu baada ya kumtolea noti ya shilingi elfu moja

Baada ya dakika 45 tulifika Temeke, nilishuka na kunyoosha uelekeo wa sokoni, kwa mbali nilihisi haja kubwa, katika kuulizia nilifanikiwa kupata choo cha kulipia. Kama kawaida nilijisaidia pembeni ya tundu, kinyesi changu kilikuwa kinafuka moshi na rangi yake ilitisha, rangi nyeusi ya kuungua ilitamalaki. Kwangu mimi sikuwa na muda wa kudadisi moshi ama rangi, nilitaka kuona pakiti mbili zilizokuwa zimebaki tumboni zimetoka ama lah. Nilikichambua kinyesi lakini sikufanikiwa kuona pakiti hata moja ya madawa ya kulevya, kinyonge nilitoka bila hata ya kutoa kinyesi pale pembeni ya tundu la choo.

Giza lilipotanda nilielekea kwenye meza moja pale sokoni, niliingia uvunguni na kujilaza kusubiri kesho
Niliendelea kuwepo pale Tandika soko kwa takribani wiki mbili bila pakiti ya dawa kutoka, kila nikielekea msalani niliambulia patupu, hela nayo ilianza kuisha, niliingia mtaani rasmi kwa ajili ya kuuza pakiti mbili za madawa nilizokuwa nazo,

"Ngoja nikabahatishe kwa fundi viatu pale". Nilijishauri,

"oy jomba niaje" nilimsalimu fundi viatu.

"fresh mwana, karibu". Alijibu.
Baada ya dakika 3 za maongezi niligundua hafananii na biashara ya madawa. Nilielekea barabara ya mwmembe yanga, nilimwona fundi viatu mwingine, nilimwendea, huyu alikuwa tofauti na yule wa mwanzo.

"brother niaje". Nilisalimia.

"Fresh mwana. Baridi?"

"baridi mwamba. (nikaonyesha ishara fulani ambayo mateja wengi hupenda kuitumia) Vipi unachukua?". Niliuliza swali la kimtego. Aliangaza kulia na kushoto kisha akanitazama usoni kwa machale, nadhani alitaka kuthibitisha kama mimi si polisi.

"mzigo unao.?" bila kutegemea aliuliza.

"ni wewe tu mwamba. Mpunga unao?" nilihoji

"hebu tuone kwanza mzigo wenyewe."

Niliangalia kushoto na kulia kisha nikatoa pakiti moja na kumwonyesha. Alitabasamu nami nikatabasamu
Biashara Ilienda vizuri na nilimpatia pakiti zote mbili. Sasa nilikuwa na pesa tena kwa ajili ya kusogeza siku mbele, wakati huohuo pakiti nyingine mbili bado zipo tumboni japo maumivu hayakuniandama kama mwanzoni.
*******

Wiki ya pili ilikata tena nikiwa nalala tandika sokoni na wakati mwingine Majumba mabovu, uzuri ni kwamba nilikuwa sihofii vibaka kwakuwa sikuwa na utofauti na chokoraa ukinitazama, mapambano kidogo nayaweza hivyo hofu ilikuwa mbali nami,
Ilikuwa ni siku ya Jumanne nikiwa Chooni pakiti moja ilifanikiwa kunitoka, hii ilikuwa ni pakiti ya tatu kati ya zile nne nilizomeza nikiwa Moshi, japo nilishangaa pakiti kuchelewa kutoka lakini nilikubaliana na matokeo, Sasa ilibakia pakiti moja tu nikiisubiria itoke, majira ya Mchana nikiwa moja kati ya migahawa Tandika sokoni nilihisi kitu, kuna vijana walikuwa wakipeana ishara huku wakikisogelea kibanda kile, nilichukulia Labda ni vibaka lakini haikuwa hivyo, walikuja kwa ajili yangu, waliingia ndani na kuagiza chakula, walikuwa makini kunitazama muda wote, nilimwita mama n'tilie na kumlipa Hela yake kisha nikanyanyuka na kutoka, Nao walikiacha chakula na kunyanyuka kisha, wakaanza kunifuata taratibu kama vile hawakuwa wananifuata, nilikatiza uchochoro mmoja na kuwapotea, baada ya kwenda mbele kidogo alitokea mtu mbele yangu akiwa kafunika uso kwa kitambaa, nikageuka nyuma nikimbie lakini alitokea mwingine nyuma yangu. Sasa niliwekwa mtu kati.
"Nyinyi akina nani na mmetumwa na nani?" ...... Niliuliza lakini badala ya majibu niliambulia teke lililotua katika mbavu ya kulia, nilianguka, mmoja akaja kwa kasi kisha akapiga teke nikalikwepa, Nilinyanyuka na kujipanga upya , yule wa pili alitupa ngumi nikaikinga na mkonobwa kushoto, nikapeleka ngumi nzito iliyotua shingoni palepale akaanguka, yule mwingine alipoona mwenzake kaanguka alichomoa kisu, mara nikapigwa na kitu kizito kichwani na mtu aliyetokea nyuma yangu sikujua kilichoendelea.

Sikumbuki ni nini kilitokea ila nilijikuta nipo katikati ya chumba chenye giza, mikono na miguu imefungwa kwa katani, nilijaribu kujiinua lakini nilishindwa, hapo nilimsifu mfungaji kwani alinifunga vilivyo, nikaona nisubiri niñi kitatokea, baada ya muda kidogo mlango ulifunguliwa, taa ikawashwa na sasa nilikiona chumba kile vizuri, katikati ya chumba kile kulikuwa na viti viwili vilivyotenganishwa na meza katikati, juu ya meza ile kulikuwa na sahani pamoja na Faili kubwa, walinisogelea vijana wawili wenye misuli wakaniinua na kunikalisha katika moja ya kiti, mmoja akabonyeza kitufe kilichopo katika moja ya sikio lake kisha akautaarifu upande wa pili ujongee. Mlango ukafunguliwa...
"Aaaaaah Bosi ni wewe....!". sikutegemea kama ni yeye
 
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu.
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 07

Nilijikuta natamka baada ya macho yangu kugongana uso kwa uso na Clara, Mwanamama aliyenipatia pakiti Nne wiki chache zilizopita nizilete Dar es Salaam kwa kutumia tumbo langu, Hasira ilinipanda sana baada ya kumwona kwani nilimchukia baada ya kitendo cha kuniambia nitupe laini na simu akidhamiria kunipoteza Ndani ya Jiji.

" Ni bahati kukutana nawewe tena Gilbert....". Sasa aliongea, sikumjibu. Alisogea taratibu kisha akaketi. Alifungua Fail kisha akatoa picha moja na kunionesha. Nilishtuka sana baada ya kuitazama ile picha. Ilikuwa ni picha ikinionyesha mimi nikimkabidhi yule Fundi viatu pakiti mbili za Madawa ya kulevya. " Inamaana siku zote hizo nilikuwa nafwatiliwa bila kujua? Au yule fundi viatu anashirikiana na Clara...!" Nilijiuliza bila kupata jibu sahihi...
"Mbili uliuza, moja ndo hii, pakiti ya nne ipo wapi?" Niliulizwa na Bosi Clara baada ya kutoa pakiti moja na kuiweka juu ya meza, niliikumbuka ni ile pakiti ya tatu iliyotoka baada ya kupata haja kubwa, pakiti ya nne bado ilikuwa tumboni lakini nilikuwa na kiburi cha kutokujibu kwa wakati huo
"Mfundisheni kuzungumza huyu mshenzi...!". Aliagiza huku akisonya, sasa nilikung'utwa kwelikweli, yale maumivu ya tumbo yaliyoniacha takribani majuma mawili yaliyopita yalinirejea upya kwa kishindo kikali.
" nisipokuwa mpole wataniua hawa" . nilitafakari huku nikipigwa mateke ya tumbo. "Pakiti ya nne bado haijatoka....!". Niliropoka. Palepale bosi aliwaamrisha watoke nje, sasa tukabaki wawili ndani ya chumba kile.
" Siku ile uliposhuka kwenye basi nilikufwatilia kila nyendo, nilituma watu wakupeleleza kila hatua, lakini niligundua huwezi kutoboa siri juu ya biashara yangu. Ulichokosea ni kitendo cha Kuuza pakiti zile mbili kwa yule polisi"
Hapo nilishtuka kidogo, kumbe sikuhizi wanapolisi wanajifanya ni fundi viatu ili wapeleleze mienendo ya wauza madawa, Hakika nilijipeleka mkononi mwa polisi, lakini kwanini hakunikamata?. Nikiwa nawaza Bosi aliendelea kusema
"Baada ya kuuza pakiti zile ulianza kufwatiliwa na Wapelelezi ili kunasa wauzaji wenzako, bahati nzuri nimekupata kabla yao, Kuna machaguo mawili Gilbert mbele yako
"NIKUUE AMA NIKUGEUZE UWE SHOGA"
"Shoga...?? Kivipi yaani?..." niliuliza kwa mshtuko
"Kivyovyote". Nilijibiwa kwa mkato
" Nasubiri unipe jibu. Nina mengi ya kufanya, chagua Ufe ama nikugeuze uwe shoga na jamii ifahamu kwamba wewe ni shoga".... Sasa hapo nilimwelewa, nililia kama mtoto maana kufa mapema hivi mbona hapana? Na kugeuzwa shoga ndio sitaki kabisa kusikia ushetani huu. Sasa nichague lipi? Kweli niliingizwa kona mbaya sana. Kwakweli ikanibidi niwe mpole nikajikuta mwanaume mzima nalia kama mtoto

"Nipo chini ya miguu yako bosi wangu, naahidi nitafanya chochote utakachoniambia lakini usinifanye hivi wala usiniue, nitakusikiliza wewe tu" niliomba sana huku nikilia, laiti ungekuwa karibu ungenionea huruma, maumivu ya tumbo yalikuwa makali sana na kila nikitafakari lipi la kuchagua nazidi kuogopa

"Mh Mh...!". Bosi Clara alikohoa kidogo kisha akanipa sharti lililoniacha mdomo wazi pasipo kujibu
"Kwakuwa hutaki Kufa wala hutaki nikugeuze uwe shoga basi Kuna mzigo nitakupatia upeleke Mombasa Kenya Kesho kutwa, Mzigo nitakaokupa ni uleule, japo safari hii utasafirisha Pakiti 50.... Na kingine...! Au ngoja nitakupatia maelekezi yote Kesho, Wewe Samweli Njoo mumtoe mpatieni huduma ya kwanza kisha ale ashibe apate nguvu". Alitoka nje huku nikiwa mdomo wazi. Ina maana awamu hii nameza pakiti 50? Hapana..! Hapanaaaaa! Zile pakiti Nne tu zilinitoa jasho, hizi 50 si bora nichague kufa?. Nikiwa nawaza hayo aliingia Mlinzi mmoja, alinitazama kisha akanifungua kamba
"Nifuate"... Aliniamuru.
Bila kutafakari nami nilimtii na kumfuata kama tahira. "Huku itakuwa ni Posta"..... Nilijisemea baada ya kuiona madhari ya bahari ya Hindi kwa mbali, hii ni kutokana na kwamba tulikuwa Ghorofani, yaani nilitekwa nikiwa Tandika na sasa nipo Posta tena Ghorofani duh, niliendelea kumfuata hadi tukafika kwenye chumba kimoja, mlangoni Kimeandikwa namba 99, Niliamriwa niingie mle chumbani, niliingia kwa tahadhari huku nikiwa na woga, woga wa Kufanyiwa lile sharti la pili. Baada ya kuingia naye aliondoka, kilikuwa ni chumba kizuri chenye kuvutia, kitandani kulikuwa na suruali ya jinsi na tisheti nyeusi, nilizisogelea na kuzishika, niligundua kitu.
"Kumbe hakuwa na mpango wa kuniua wala nini, alitaka tu kunitisha ili nikubali kupeleka mzigo Kenya....!". Niliwaza,. Nilielekea bafuni na kujimwagia maji, nilikumbuka mara ya mwisho kuoga na sabuni nimajuma matatu yaliyopita, Siku moja kabla sijaanza safari ya kuja Dar,. Nilipomaliza kuoga nikaelekea sebuleni, nikakamata zile nguo na kuzivaa, punde mlango ukagongwa, nikaenda kwa tahadhari kufungua mlango, alikuwa ni yule Mlinzi akiambatana na Mwanadada mmoja, niliwakaribisha ndani, dada yule alikuwa ni Daktari, alianza kazi yake ya kunipatia huduma ya kwanza kwakuwa nilikuwa na majeraha baadhi miguuni na mgongoni, nikapatiwa dawa za kumeza lakini sikuzimeza kwa kuhofia pakiti moja iliyopo tumboni kama ikigusana na dawa itakuwa hatari kwa afya yangu.
Siku ikapita hivyo nikiwa nipo katika chumba kile huku huduma zote nazipata. Siku inayofuata nilipewa maelekezo yote na Bosi Clara juu ya Safari ya Kesho yake,
" Utakwenda kwa ndege, na kila kitu kipo tayari. Paspoti yako inaonyesha kama unaenda kwa ajili ya kwenda Kusoma chuo, Ila kuna begi pia utakwenda nalo, begi hilo ndipo mzigo ulipo, Begi lina Pedi za kike, hivyo polisi hata wakikagua hawatagundua maana pakiti zipo katikati ya Pedi hizo na zimefungwa kwa utaalamu mkubwa sana. Usionyeshe hofu yoyote ndani ya ndege na pindi ushukapo, ukikamatwa ujue umekwenda na maji maana wewe ndiye utakuwa umejikamatisha..... Endapo ukifanikiwa salama kufika, siku unayorudi Nitakukabidhi Milioni Mia Tano kama zawadi Gilbert."

"Kwahiyo mashine haziwezi kugundua?". Niliuliza huku nikiwa na mashaka.
"Usiwe na shaka maana kwa utaalamu tulio utumia hakuna mashine yoyote ya ukaguzi katika kiwanja chochote cha ndege itakayo weza kuona madawa tuliyo yaficha katika hizi pedi Gilbert. Endapo ikatokea umekatwa, hakikisha kwamba hutaji ni nani amekukabidhi huu mzigo endapo utafanya hivyo basi tambua Wazazi wako waliopo mbeya nitawaua kwa mikono yangu, " Hapo nilishtuka kusikia wazazi wangu watauwawa, nawapenda sana na Nimekimbia Mbeya kutafuta Pesa ili waishi maisha mazuri, wakifa nani atazifaidi sasa?


"Mwenyeji wangu atakuwa nani nikifika?..." Niliuliza swali
"Tazama hii picha, Hii ni picha yake na atavaa hivi hivi kama alivyovalia katika picha, Atabeba pia Bango lililoandikwa Jina lako. Anaitwa Chalamala"..... Palepale nilishtuka baada ya kuiona ile picha, Ni rafiki yangu niliyetoka naye Mbeya hadi Moshi katika harakati za kutafuta Pesa. Nilifurahi sana kusikia yeye ndiye atakayenipokea,. Kumbe hakufa siku ile alipopeleka Mzigo China.

Hatimaye siku ya Kupeleka Mzigo kenya ikawadia, Safari yangu ya kwanza Kwenda nje ya nchi, tena nikiwa na Mzigo hatari,
"Ee Mungu nisaidie nifike salama bila kugundulika"... Nilijisemea kila dakika tukiwa tunaelekea Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere. Ndege yetu ilikuwa ni ya Saa Tano Asubuhi. Hivyo tuliwahi kufika uwanjani huku nikisindikizwa na Walinzi wawili wa Bosi Clara. Hatimaye muda wa Kupanda ndege ukafika, mizigo yangu ni mabegi mawili tu, moja la Nguo na baadhi ya vyeti vya kuthibitisha naenda Kenya Kusoma, Begi lingine ni la Mzigo unaonipeleka Kenya.
" Madawa Ya Kulevya"
Mizigo ikapitishwa kwenye mashine maalumu ya Kukagua usalama wa mizigo, nilifurahi baada ya mabegi yangu kupita salama. Ilipotimu saa 5:00 asubuhi Ndege ilianza Kuundoka taratibu, Sauti nyororo ya muhudumu wa kike ilituamuru tuifunge mikanda yetu Kwani ndege ndio inaiacha ardhi ya Tanzania.
Nilitii agizo nami nikafunga mkanda vizuri kisha nikavuta pumzi ndefu huku nikimshukuru Mungu kwa kunisaidia kupanda Ndege salama bila kukamatwa. Macho yangu muda wote yapo katika mstari wa katikati wa siti hizi za ndege ya shirika la Air Tanzania tukitokea nchini Tanzania kuelekea nchini Kenya jijini Mombasa. Hofu yangu si kwamba ndio mara yangu ya kwanza kupanda ndege au Kwenda Nje ya nchi...!, la hasha ila ni mzigo ambao nimeubeba kwenye begi langu ulio katikati ya Pedi za Kike.

"Ee Baba Mungu ninakuomba unisaidie katika hili. Nifike tu salama huko Kenya bila Kukamatwa na huu mzigo"

Nilijisemea huku nikiendelea kupepesa macho bila kutulia . Wahudumu walianza kupita pita wakimuuliza kila abiria ni kitu gani anacho hikitaji kwa muda huu.

“Samahani Kaka utahitaji chochote?” Muhudumu huyu aliniuliza na kunifanya nitafakari cha Kusema kwa sekunde kadhaa.

“Naomba maji tu dada yangu" .....Nilizungumza kwa sauti ya upole ambayo kusema kweli inatia huruma japo mimi ni mwanaume tena ninayejua Kupambana na nyakati ngumu kama hizi. Nikatoa ile picha niliyopewa na Bosi Clara kwenye waleti ndogo, Nikageuza nyuma ya picha ile na kukutana na jina la Chalamala nililoliandika jana nilipopatiwa Hii picha, picha ya mtu nitakayekutana naye uwanja wa ndege wa Jomo Kenyata Airport huko Mombasa. Dada yule ambaye ni mhudumu akarejea na kunikabidhi chupa ya maji niliyoomba huku akitabasamu sana usoni mwake.

“Asante” Nilizungumza huku nikijitahidi kutabasamu na mimi ili kuondoa wasiwasi wangu nilio nao. Nikafungua mfuniko wa chupa hii taratibu huku nikiendelea kutazama abiria wa pembeni yangu kwa macho ya kuiba iba, nikapiga mafunda mawili ya maji haya kisha nikakifunga kichupa hichi na kuiweka katika sehemu maalumu.

ITAENDELEA

Simulizi Hii japo inakuja kwa kuchelewa lakini tutaenda nayo hadi mwisho wakuu. Ina Vipande 30, kama ukiihitaji kwa uharaka yote mcheki mwandishi atakutumia kwa Tshs 1000 tu, kama ofa. Namba yake ni HALOPESA NAMBA 0621249611 au Mpesa namba 0765824715
Jina Gilbert Evarist
Namba zote zipo whatsapp
 
SIMULIZI YA MAISHA : Mzigo wa Bosi uliharibu maisha yangu.
MWANDISHI: Gilbert Evarist Mushi
PHONE: +255621249611

Sehemu ya 08

‘Ohoo Mungu nisaidie’

Nilizidi kuongeza maombi katika safari hii kwani ninakumbuka bosi wangu, Clara amenialeza endapo nitacheza vibaya kwenye safari hii basi nitayaingiza maisha yangu matatani na endapo nitafanikiwa kufika salama, basi kimaisha nitakuwa nimetoka moja kwa moja na sinto kumbuka shida na matatizo niliyo nayo kwenye maisha yangu ya hivi sasa.
Baada ya Lisaa limoja na nusu tukawasili Uwanja wa ndege wa KIA (Kilimanjaro Internationaln Airport) na baadhi ya abiria waliteremka huku wengine wakipanda.
"Ndugu abiri, tunaomba mfunge mikanda iliyopo kwenye siti zenu kwani ndani ya dakika kumi zijazo ndege itatua katika kiwanja cha Jomo Kenyatta Mombasa Kenya, ndio itakuwa ni kituo chetu cha mwisho kwa safari hii. Asanteni sana kwa kutumia usafiri wa shirika letu la Air Tanzania, Karibuni sana kwa safari nyingine na tunawatakia wakati mwema mwendapo"

Sauti tamu ya mhudumu wa kike aliye zungumza kwa lugha ya Kiswahili, ilisikika kupitia vipaza sauti vilipo pembezoni mwa sehemu tulizo weka mabegi yetu, sauti ya dada huyu ilirudia tena huku awamu hii ikizungumza kwa Lugha ya kingereza. Taratibu nikaufunga mkanda wangu wa siti, huku nikimtazama Baba aliyeketi upande wangu wa pili, Nilipomtazama tu Alitabasamu

"Aaah"... Nilishtuka baada ya kumwona. Hakika niyeye, Nilimkumbuka

Alikuwa ni yule Baba Niliyemwona akishona viatu nikamchukulia kama fundi viatu

" Nimekwisha"
Nilijisemea baada ya kukumbuka maneno ya Bosi Clara aliponiambia zile pakiti mbili nilizoziuza kwa fundi viatu alikuwa ni Mpelelezi wa Siri.
"Kafwata nini huku sasa?". Nilijiuliza huku nikiwa na hofu baada ya kukwepesha macho yangu kwake.
" Kazi nzuri Kijana....! Umeahidiwa utapewa maisha mazurie...". Aliufungua mdomo wake sasa na kuniambia, jamani jamani, ina maana muda wote nimekaa nae sikumjua?

"Wewe nani na unataka nini?". Niliuliza

" Tulia Kijana. Come down. Nikutakie Bahati njema huko uendapo". Aliniambia huku akitabasamu na tararibu ndege ikaanza kutua kwenye uwanja huu wa Jomo Kenyatta, kwa bahati nikapata nafasi ya kuchungulia dirishani na nikaona jinsi palivyopendeza upande wa nje. Baada ya dakika kadhaa ndege ikatulia, milango mitatu ya ndege hii ikafunguliwa, Taratibu nikafungua mkanda wa siti yangu kisha nikanyanyuka huku nikiwa na hofu baada ya maneno ya huyu baba pembeni yangu, nikafungua sehemu ya juu na kulitoa begi langu lililojaa Pedi za wanawake pamoja na lingine likiwa na nguo zangu
"Chukua hii, utanitafuta ukijisikia Gilbert." Baba huyu alitamka huku akinikabidhi Karatasi iliyokunjwa. Loooh kumbe na jina langu analifahamu? Kweli polisi mtu mwingine kabisa.
"Hapa ni kujikausha na kujifanya sijui lolote". Nilijisemea baada ya kupokea karatasi ile. Alinyanyuka na kuelekea Msalani ndani ya ndege. Sikujishuhulisha kumfwatilia maana simjui na isitoshe nina hofu ya kukamatwa.

Nikatazama mlango nilio ingilia, taratibu nikaanza kutembea nyuma ya Babu mmoja mwembamba mweupe, Nikaanza kupiga hatua kwa mguu wangu wa kulia kuikanyaga ngazi hii ndefu kuelekea chini, macho yangu muda wote yanaangaza angaza kwenye hichi kiwanja kuangalia nani ni askari na nani si askari. Hadi ninaikanyaga ardhi ya nchi hii ya chini ikiwa ndio mara yangu ya kwanza kabisa tangu nitoke tumboni mwa marehemu mama yangu, sijaona askari yoyote. Tukaelekezwa kuingia kwenye basi moja refu sana, kama niliyo yaacha nchini Tanzania ambayo tunayaita mabasi ya mwendo kasi, ila huku Kenya ni mabasi ya kubebea abiria wanao shuka kwenye ndege zinazo tulia mbali kidogo na sehemu ya kutokea katika uwanja huu wa Jommo Kenyatta.

Nikashusha pumzi nyingi sana huku nikikaa siti moja na Dada Mweusi. Tukatazamana na kujikuta tukitabsamu tu kisha nikaufungua mdomo wangu kwa kutamka

"Hai"

"Hai mambo". Nikagundua kumbe mtanzania maana sijui kingereza mimi. Muda wote nimelishikilia begi langu kikamilifu pamoja na walleti yaangu yenye pesa, hati ya kusafiria, pamoja picha ya Chalamalana ambaye atakuja kunipokea hapa uwanja wa ndege.

‘Ehee Mungu nisaidie mimi’

Nilizungumza mara baada ya basi hili kusimama, abiria walio kaa kwenye siti wakaanza kusimama na kushuka na mimi ikanibidi kusimama taratibu na kuanza kushuka kwenye basi hili. Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio baada ya kuwaona askari walio valia nguo nyeusi wakiwa wameshika mbwa wakubwa mithili ya ndama wadogo.

‘Yesu wangu, nisaidie jamani’

Nilizungumza kwa woga huku nikijikaza sana mwili wangu kwani sheria moja wapo niliyo pewa katika kusafirisha mzigo huu, niliambiwa niwe jasiri na usoni mwangu nisionyeshe dalili yoyote itakayo waashiria askari kwamba nimebeba mzigo ambao ni wa hatari. Nikajiweka sawa na Dada yule niliyekaa naye kwenye siti ya basi, akanitazama tena na akatabasamu,. Tabasamu lake likaacha swali kichwani mwangu lakini sikutaka kulitilia maanani maana nitazidi kupandisha hofu. Tukaanza kuteremka kwa kutembea pamoja na Dada huyu mweusi tukafanikiwa kuwapita askari hawa watano walio simama wakiendelea kuimarisha ulinzi katika hili eneo.
Tukaanza kuelekea katika mashine maalumu ya kuweka mizigo inayo kaguliwa. Nikayaweka mabegi yangu nyuma ya begi la Dada huyu mweusi, nikasimama nyuma yake huku tukipita katika sehemu ya kugaguliwa na mashine maalumu. Nikafanikiwa kupita katika eneo hili, jambo ambalo lilinifanya nianze kumshukuru Mungu kimoyomoyo.

Usiwe na shaka maana kwa utaalamu tulio utumia hakuna mashine yoyote ya ukaguzi katika kiwanja chochote cha ndege itakayo weza kuona madawa tuliyo yaficha kwenye hizi pedi Gilbert...!"

Maneno ya bosi Clara yakanitia nguvu sana na kujikuta nikitazama sehemu inapo tokea mabegi yetu, likaanza begi la Dada huyu mweusi kisha yakafwatia mabegi yangu mawili. Nikayachukua na moja kwa moja nikaelekea sehemu ya kukaguliwa hati yangu ya kusafiria, nikamkabidhi dada mmoja mwenye asili ya Kijaluo. Akaitazama kwa muda hati yangu niliyomkabidhi.

“Gilbert Mwaitika. una miaka mingapi?"

Dada huyu aliniuliza kwa Kiswahili huku akinikazia macho.

“23 ” . Nikajibu kwa kujiamini.

“Umekuja Kenya kufanyaje?” ......... Aliuliza swali lingine tena,

“Kujiendeleza kimasomo”

Nilijibu kama vile visa yangu ilivyo jieleza kwamba nimekuja Kenya kujiendeleza kimasomo ya muda mfupi sana ya miezi sita. Dada huyu akaitazama hati yangu kwa mara nyingine, kisha akanitazama mimi tena. Nikatazama pembeni, nikawaona wanajeshi wawili walio shika mbwa wakubwa wakija katika eneo hili, mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio sana.

“Gilbert.....!”
Sauti ya dada huyu ikanistua sana na nikamtazama kwa macho ya wasiwasi mwingi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom