Ilikuwa ni majira ya jioni siku hiyo, Sarah alifika hapo kwenye bethdei pamoja na
Rahim ili kula, kunywa na kufurahi. Na alikuwa amekalia kwenye kochi huku kashika
kinywani mkononi,
pembeni yake walikaa wasichana wengine ambao nao walikuwa
wakiongea na kufurahi, pembeni yao kulikuwa na wavulana na wasichana wengine
waliosimama, waliokuwa wakiongea wengine wakicheza mziki uliokuwa ukisikika toka
kwenye spika za mahala hapo, huku wakinywa vinywaji, Rahim alikuwa amesimama na
kinywaji chake akipiga soga na baadhi ya rafiki zake, huku mziki mzuri ulisikika toka
kwenye spika za mahala hapo.
Usoni Sarah alionekana kuwa na furaha kuwa mahala
hapo, muda wote alimtumpia macho Rahim na watu wengine wote waliokuwapo hapo
wakifurahi.
Mara ghafla ikasikika sauti, “Joji, Joji mwanngu mwenyewe happy birthday bro”, ilikuwa sauti ya kiume ikitokea toka kwenye mlango wa mahala hapo, wote wakatupia
macho mlangoni, na kumuona jamaa mmoja mrefu mweusi mwenye makelele akiwa na
furaha akiingia ndani huku kaongozana na watu kadhaa, huyo alikuwa ni moja ya
marafiki waliokuwa wakiwasili kwenye hiyo bethdei.
Rahim na marafiki wengine wakawaka kwa furaha kumuona, nao wakayapokea
makelele yake kwa kelele, “Ayaa, mnyama umefika hahaha, mbona unachelewa wewe”, alisikika Joji ambaye hiyo ndio ilikuwa siku ya bethdei yake.
Basi, kukawa na kelele za
furaha tu mahala hapo, macho yote yakawa kwa huyo jamaa aliyeingia na watu
alioongozana nao, mmoja wa watu hao alikuwa ni wa kike.
Sarah alipomtazama huyo dada aliyeingia mahala hapo mara moja alimtambua, kuwa
alikuwa Cheusi, rafiki yake, waliyeishi wote huko mitaa ya mwananyamala. “Cheusi
amefuata nini hapa?”, alijiuliza Sarah.
Cheusi siku hiyo alikuwa kavalia kagauni kafupi, uso wake wake ulionesha dhahiri
kuwa tayari amekunywa kidogo.
Sarah hakutaka uwepo wa rafiki yake huyo mahala hapo, alikaa kwenye kochi na glasi
yake akimtazama Cheusi, huku akiomba rafiki yake huyo asimuone wala asimkaribie.
Sarah alimfahamu rafiki yake kwa tabia ya kuropoka, hakutaka Rahim amfahamu
Cheusi.
Asichokitaka kutokea ndio kikatokea Cheusi alimuona Sarah hapo kwenye kochi na
mara uso wake ukakenua kwa tabasamu na kuelekea hapo Sarah alipokuwa amekaa, alipofika akakaa pembeni yake kabisa, “Sarah unafanya nini huku?” aliuliza Cheusi, Sarah hakuwa na la kufanya , “ nikuulize wewe umefuata nini huku?”, alijibu Sarah kwa
kuuliza swali kama hilo hilo. “Umemuona yule jamaa niliyeingia nae, mteja wangu yule huwa anapitaga kwenye
kona zetu za kazi, anapenda ngono balaa, na ni wa kishua sana, halafu ni kama
nimemuelewa kimtindo na mimi nimemganda”, aliongea Cheusi akimwambia Sarah.
Sarah akaweka glasi kwenye meza, kisha akamgeukia Cheusi akiongea kwa usiriazi, “Cheusi, nakuomba eneo hili usiongelee masuala yahusianayo na kazi tunayofanya, niko hapa na rafiki yangu niliyekwambia anaitwa Rahim, sitaki ajue kuwa ninafanya kazi
ya kujiuza, naomba unyamaze, kama unaongea ongea kama mtu ambaye hatufahamiani sana”,
aliongea Sarah kwa hasira kidogo, alitamani ajifanye hamjui Cheusi kwa wakati
huo lengo likiwa ni Rahim asijetokea kufahamiana na Cheusi na kuja kujua ukweli wa
kazi yao wanayofanya.
Wakati wowote aliokuwa na Rahim, Sarah alifuta na
kujisahaulisha mambo yote yaliyohusu kazi na maisha yake binafsi hakutaka Rahim ajue
sehemu hiyo ya maisha yake.