VAN HEIST
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 1,434
- 617
George Iron Mosenya
SEHEMU YA KWANZA
Naitwa Lusubilo Mwaipaja, marafiki zangu wengi walizoea kuniita kwa ufupi. Waliniita Lusu! Niliyafurahia maisha sana nikiwa mjini Mbeya na familia yangu kwa takribani miaka ishirini na nne, mama yangu alikuwa akinieleza mara kwa mara
kuwa watu wengi wananipenda kwasababu ya upole na ukarimu wangu!
Lusu, angalia upole wako usizidi kipimo inaweza kukugharimu siku moja Mama aliwahi kunipa onyo ambalo sikujua kabisa alikuwa anamaanisha nini.Hakika! Sikujua anachomaanisha kwa wakati ule kwa sababu kila mtu katika jamii alinipenda na kuniheshimu kwa sababu ya huohuo upole. Kivipi mama ananieleza kuwa ipo siku upole wangu
utanigharimu?? Sikutilia maanani.
Giza likachukua nafasi, mchana ukaipokea nafasi hiyo. Ikawa usiku ikawa mchana siku zikazidi kusonga mbele.
Hatimaye ukakuchwa ule usiku ambao uliuleta mchana wa kukutana na Neema. Msichana ambaye na yeye kama ilivyokuwa kwa mama alinisifia kwa upole wangu na ukarimu. Lakini yeye aliendelea kunijaza sifa kila siku hatimaye jicho langu likamtazama katika namna ya pekee.
Mke mtarajiwa!
Sikujiuliza mara mbilimbili siku ambayo niliamua kumtamkia kuwa nahitaji kuwa naye katika mahusiano ya kimapenzi. Mahusiano ambayo yalidumu kwa muda mfupi kabla sijayapeleka katika uchumba, mama alikuwa wa kwanza kumfahamu Neema kisha baba.
Hatimaye nami nikajitambulisha kwao.Nikapokelewa kwa mikono miwili!! Wazazi wake wakanipenda!! Safari ya mapenzi yetu ikaongezeka kasi na hatimaye tukaoana.
Siku ile ya harusi mama yangu alinikumbatia kwa muda mrefu kupita ndugu zangu wote.Alidondokwa na chozi ambalo nilidhani kuwa lilikuwa la furaha lakini la! Nayakumbuka maneno ambayo alinieleza kwa sauti ya kunongona.
Lusu mwanangu, hakuna mwanamke anayekupenda duniani zaidi ya mimi mama yako, kama ingekuwa ndani ya uwezo wangu ungeishi nyumbani daima. Nyumba yenye mapenzi ya dhati kwako, ila nenda mwanangu, nenda umekuwa mtu mzima sasa..
Nikauacha rasmi mji wa Mbeya, mji ambao ulinipenda sana. Nikaondoka mimi na Neema. Tukahamia Morogoro, ambapo nilikuwa nimepata uhamisho wa kuhamia kule kama mwalimu!
****
Awali Neema alikuwa akinionyesha mapenzi ya dhati sana. Jambo ambalo halikuwa geni, nililitegemea vilivyo. Niliamini kuwa kama kweli mama ananipenda kuliko wanawake wote basi Neema ni wa pili katika orodha ile. Miezi mitatu pekee ya ndoa niliishi kwa amani ya moyo.
Mwezi wa nne ukaanza kwa mauzauza. Mauzauza ambayo hadi leo hii akitokea mtu ananiomba ushauri juu ya mwanamke gani wa kuoa. Sitakuwa na la kumjibu, zaidi atakuwa amenipandisha jazba tu!
Neema alianza kulalamika kuwa amechoka kukaa nyumbani. Anataka nimtafutie naye kazi ya kufanya ilimradi tu asiwe mtu wa kushindia nyumbani.
Nilishangazwa na ombi hili, wakati awali tulipanga vinginevyo. Nikaamua kuuvunja ukimya.Neema mke wangu, kwani mimi na wewe tulipanga nini mwanzo? Si tumekubaliana tupate mtoto kwanza ndo hayo yatafuata. Nilimuhoji. Akanitazama kwa jicho kali, kisha akasimama kwa ghadhabu akatoa msonyo mdogo wa kuonyesha kukereka, akaingia chumbani akaubamiza mlango. Looh! Ama kweli upole wangu, upole wangu lakini mama alinikanya!!
Nikasimama na kuelekea chumbani, nikamkuta amejifunika shuka gubigubi huku akitupa miguu huku na kule. Nikajongea kitandani nikaanza kumbembeleza. Nadhani ule ndo ulikuwa mwanzo wa Yule binti kuanza kuiendesha akili yangu. Nilimweleza kuwa kama kweli ana nia ya kufanya kazi basi ageuke tuzungumze. Neema akageuka huku akipekecha macho yake, ili kulazimisha machozi.
Mapenzi bwana! Ndicho nilichowaza kwa wakati ule kumbe yale hayakuwa mapenzi nilijidanganya tu!
Haya unataka kazi gani mke wangu!Neema akaachia tabasamu pana akanikumbatia na kunibusu, kisha akanieleza kuwa anataka kuwa anaenda dar kununua vitenge na nguop za wanawake kisha atakuwa anakuja navyo Morogoro
kuwauzia na kuwakopesha wanawake wa mtaani akianza na waalimu ambao naishi nao pale nyumba za shule.
Nikalifikiria wazo lake kisha nikamruhusu huku nikimkumbusha kuwa asisahau kuwa huku Morogoro ameacha mume anayempenda sana. Furaha ya Neema ikarejea. Akapiga mahesabu yake, nikampatia kiasi cha pesa akajipanga kwa
safari baada ya siku mbili! Nafsi yangu ilikuwa imemruhusu lakini kiukweli ni kwa shingo upande!!
Siku ikafika na mke wangu kipenzi akaondoka akiniachia manunguniko nafsini!! Akaenda jijini Dar es salaam!
Siku moja baada ya Neema kuondoka, mwalimu Jackson ambaye alikuwa ni mwalimu mkuu na yeye akaaga kuwa anaenda baraza la mitihani Dar. Nikamweleza kuwa akipata muda wa kuonana na Neema basi kuna zawadi nahitaji kumpa ampatie.
Mwalimu akanieleza kuwa hatapata muda kwa sababu anafika na kuondoka!! Lakini pia siku moja kabla Neema hajaondoka Mwalimu mkuu msaidizi naye aliondoka shuleni na sikujua wapi alielekea.Sikuwa na mashaka yoyote. Niliamini Neema ni wangu peke yangu!!
**Naam! Hii ni sehemu ya kwanza ya simulizi hii ya TONE LA MWISHO LA UVUMILIVU! Usikose kuwa nasi kesho tena muda na waktikama huu. Hapahapa!! Je? Ndoa hii itafikia katika kilele ama itakomea njiani nini maana ya TONE LA MWISHO LA UVUMILIVU?
SEHEMU YA KWANZA
Naitwa Lusubilo Mwaipaja, marafiki zangu wengi walizoea kuniita kwa ufupi. Waliniita Lusu! Niliyafurahia maisha sana nikiwa mjini Mbeya na familia yangu kwa takribani miaka ishirini na nne, mama yangu alikuwa akinieleza mara kwa mara
kuwa watu wengi wananipenda kwasababu ya upole na ukarimu wangu!
Lusu, angalia upole wako usizidi kipimo inaweza kukugharimu siku moja Mama aliwahi kunipa onyo ambalo sikujua kabisa alikuwa anamaanisha nini.Hakika! Sikujua anachomaanisha kwa wakati ule kwa sababu kila mtu katika jamii alinipenda na kuniheshimu kwa sababu ya huohuo upole. Kivipi mama ananieleza kuwa ipo siku upole wangu
utanigharimu?? Sikutilia maanani.
Giza likachukua nafasi, mchana ukaipokea nafasi hiyo. Ikawa usiku ikawa mchana siku zikazidi kusonga mbele.
Hatimaye ukakuchwa ule usiku ambao uliuleta mchana wa kukutana na Neema. Msichana ambaye na yeye kama ilivyokuwa kwa mama alinisifia kwa upole wangu na ukarimu. Lakini yeye aliendelea kunijaza sifa kila siku hatimaye jicho langu likamtazama katika namna ya pekee.
Mke mtarajiwa!
Sikujiuliza mara mbilimbili siku ambayo niliamua kumtamkia kuwa nahitaji kuwa naye katika mahusiano ya kimapenzi. Mahusiano ambayo yalidumu kwa muda mfupi kabla sijayapeleka katika uchumba, mama alikuwa wa kwanza kumfahamu Neema kisha baba.
Hatimaye nami nikajitambulisha kwao.Nikapokelewa kwa mikono miwili!! Wazazi wake wakanipenda!! Safari ya mapenzi yetu ikaongezeka kasi na hatimaye tukaoana.
Siku ile ya harusi mama yangu alinikumbatia kwa muda mrefu kupita ndugu zangu wote.Alidondokwa na chozi ambalo nilidhani kuwa lilikuwa la furaha lakini la! Nayakumbuka maneno ambayo alinieleza kwa sauti ya kunongona.
Lusu mwanangu, hakuna mwanamke anayekupenda duniani zaidi ya mimi mama yako, kama ingekuwa ndani ya uwezo wangu ungeishi nyumbani daima. Nyumba yenye mapenzi ya dhati kwako, ila nenda mwanangu, nenda umekuwa mtu mzima sasa..
Nikauacha rasmi mji wa Mbeya, mji ambao ulinipenda sana. Nikaondoka mimi na Neema. Tukahamia Morogoro, ambapo nilikuwa nimepata uhamisho wa kuhamia kule kama mwalimu!
****
Awali Neema alikuwa akinionyesha mapenzi ya dhati sana. Jambo ambalo halikuwa geni, nililitegemea vilivyo. Niliamini kuwa kama kweli mama ananipenda kuliko wanawake wote basi Neema ni wa pili katika orodha ile. Miezi mitatu pekee ya ndoa niliishi kwa amani ya moyo.
Mwezi wa nne ukaanza kwa mauzauza. Mauzauza ambayo hadi leo hii akitokea mtu ananiomba ushauri juu ya mwanamke gani wa kuoa. Sitakuwa na la kumjibu, zaidi atakuwa amenipandisha jazba tu!
Neema alianza kulalamika kuwa amechoka kukaa nyumbani. Anataka nimtafutie naye kazi ya kufanya ilimradi tu asiwe mtu wa kushindia nyumbani.
Nilishangazwa na ombi hili, wakati awali tulipanga vinginevyo. Nikaamua kuuvunja ukimya.Neema mke wangu, kwani mimi na wewe tulipanga nini mwanzo? Si tumekubaliana tupate mtoto kwanza ndo hayo yatafuata. Nilimuhoji. Akanitazama kwa jicho kali, kisha akasimama kwa ghadhabu akatoa msonyo mdogo wa kuonyesha kukereka, akaingia chumbani akaubamiza mlango. Looh! Ama kweli upole wangu, upole wangu lakini mama alinikanya!!
Nikasimama na kuelekea chumbani, nikamkuta amejifunika shuka gubigubi huku akitupa miguu huku na kule. Nikajongea kitandani nikaanza kumbembeleza. Nadhani ule ndo ulikuwa mwanzo wa Yule binti kuanza kuiendesha akili yangu. Nilimweleza kuwa kama kweli ana nia ya kufanya kazi basi ageuke tuzungumze. Neema akageuka huku akipekecha macho yake, ili kulazimisha machozi.
Mapenzi bwana! Ndicho nilichowaza kwa wakati ule kumbe yale hayakuwa mapenzi nilijidanganya tu!
Haya unataka kazi gani mke wangu!Neema akaachia tabasamu pana akanikumbatia na kunibusu, kisha akanieleza kuwa anataka kuwa anaenda dar kununua vitenge na nguop za wanawake kisha atakuwa anakuja navyo Morogoro
kuwauzia na kuwakopesha wanawake wa mtaani akianza na waalimu ambao naishi nao pale nyumba za shule.
Nikalifikiria wazo lake kisha nikamruhusu huku nikimkumbusha kuwa asisahau kuwa huku Morogoro ameacha mume anayempenda sana. Furaha ya Neema ikarejea. Akapiga mahesabu yake, nikampatia kiasi cha pesa akajipanga kwa
safari baada ya siku mbili! Nafsi yangu ilikuwa imemruhusu lakini kiukweli ni kwa shingo upande!!
Siku ikafika na mke wangu kipenzi akaondoka akiniachia manunguniko nafsini!! Akaenda jijini Dar es salaam!
Siku moja baada ya Neema kuondoka, mwalimu Jackson ambaye alikuwa ni mwalimu mkuu na yeye akaaga kuwa anaenda baraza la mitihani Dar. Nikamweleza kuwa akipata muda wa kuonana na Neema basi kuna zawadi nahitaji kumpa ampatie.
Mwalimu akanieleza kuwa hatapata muda kwa sababu anafika na kuondoka!! Lakini pia siku moja kabla Neema hajaondoka Mwalimu mkuu msaidizi naye aliondoka shuleni na sikujua wapi alielekea.Sikuwa na mashaka yoyote. Niliamini Neema ni wangu peke yangu!!
**Naam! Hii ni sehemu ya kwanza ya simulizi hii ya TONE LA MWISHO LA UVUMILIVU! Usikose kuwa nasi kesho tena muda na waktikama huu. Hapahapa!! Je? Ndoa hii itafikia katika kilele ama itakomea njiani nini maana ya TONE LA MWISHO LA UVUMILIVU?