Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,977
Mtunzi: Nyemo Chilongani
Treni ilisimama mwisho wa reli, mkoani Kigoma ambayo ilianza safari yake ya kuelekea huko siku mbili zilizopita kutoka jijini Dar es Salaam.
Wenyeji waliofika mahali hapo kwa lengo la kuwapokea wageni wao, wakaanza kusogea sehemu husika huku wakiangalia kwa makini abiria waliokuwa ndani ya treni hiyo ambapo wengine walikuwa wakichungulia dirishani.
Baada ya sekunde chache, treni ikasimama na haraka sana abiria kuanza kushusha mizigo yao huku wenyeji waliofika mahali hapo kwa lengo la kuwapokea wakianza kusaidiana nao, wafanye haraka na kuondoka stesheni.
Kila mmoja alionekana kuwa na haraka, wengine walipiga simu kwa ndugu zao waliokuwa nje ya jengo la stesheni na kuwaambia waweke magari tayari kwani wageni waliokuwa wamewafuata mahali hapo tayari waliwapata.
Vijana waliokuwa wakijihusisha na kubeba mizigo nao hawakuwa mbali, walikuwa na vitoroli vyao, walisogea karibu kabisa huku wakiwauliza wageni kama walikuwa tayari kusaidia kupeleka mizigo yao nje ya jengo la stesheni na kulipwa kidogo ama la.
“Mama nikusaidie? Utanipoza kidogo tu, hata hela ya maji mama naomba nikusaidie,” alisema kijana mmoja huku akiwa na kitoroli chake kidogo, na tayari alifika mahali hapo huku wenzake wakiwafuata wageni wengine.
Kipindi hicho hali ya hewa ilikuwa ni ya utulivu kabisa, hapakuwa na joto wala baridi, kwa kifupi ilitulia sana hasa mahali hapo ambapo kwa pembeni, kama hatua ishirini za miguu ya binadamu kulikuwa na Ziwa Tanganyika.
Watu wote walivalia nguo zao laini lakini kwa abiria wachache waliokuwa wameingia siku hiyo walikuwa na makoti makubwa, wengine masweta kutokana na hali ya baridi waliyokuwa wamekutana nayo huko njiani.
Wakati abiria wengine wakiendelea kutoka ndani ya eneo hilo, kijana mmoja ambaye kwa kumwangalia tu alionekana kuwa na miaka isiyozidi ishirini na tano akainuka kutoka katika kiti kimoja ndani ya behewa la treni lililotoka jijini Dar es Salaam na kwenda dirishani na kuanza kuchungulia.
Treni ilisimama mwisho wa reli, mkoani Kigoma ambayo ilianza safari yake ya kuelekea huko siku mbili zilizopita kutoka jijini Dar es Salaam.
Wenyeji waliofika mahali hapo kwa lengo la kuwapokea wageni wao, wakaanza kusogea sehemu husika huku wakiangalia kwa makini abiria waliokuwa ndani ya treni hiyo ambapo wengine walikuwa wakichungulia dirishani.
Baada ya sekunde chache, treni ikasimama na haraka sana abiria kuanza kushusha mizigo yao huku wenyeji waliofika mahali hapo kwa lengo la kuwapokea wakianza kusaidiana nao, wafanye haraka na kuondoka stesheni.
Kila mmoja alionekana kuwa na haraka, wengine walipiga simu kwa ndugu zao waliokuwa nje ya jengo la stesheni na kuwaambia waweke magari tayari kwani wageni waliokuwa wamewafuata mahali hapo tayari waliwapata.
Vijana waliokuwa wakijihusisha na kubeba mizigo nao hawakuwa mbali, walikuwa na vitoroli vyao, walisogea karibu kabisa huku wakiwauliza wageni kama walikuwa tayari kusaidia kupeleka mizigo yao nje ya jengo la stesheni na kulipwa kidogo ama la.
“Mama nikusaidie? Utanipoza kidogo tu, hata hela ya maji mama naomba nikusaidie,” alisema kijana mmoja huku akiwa na kitoroli chake kidogo, na tayari alifika mahali hapo huku wenzake wakiwafuata wageni wengine.
Kipindi hicho hali ya hewa ilikuwa ni ya utulivu kabisa, hapakuwa na joto wala baridi, kwa kifupi ilitulia sana hasa mahali hapo ambapo kwa pembeni, kama hatua ishirini za miguu ya binadamu kulikuwa na Ziwa Tanganyika.
Watu wote walivalia nguo zao laini lakini kwa abiria wachache waliokuwa wameingia siku hiyo walikuwa na makoti makubwa, wengine masweta kutokana na hali ya baridi waliyokuwa wamekutana nayo huko njiani.
Wakati abiria wengine wakiendelea kutoka ndani ya eneo hilo, kijana mmoja ambaye kwa kumwangalia tu alionekana kuwa na miaka isiyozidi ishirini na tano akainuka kutoka katika kiti kimoja ndani ya behewa la treni lililotoka jijini Dar es Salaam na kwenda dirishani na kuanza kuchungulia.