Sura ya 1270
Eliza karibu kusahau kama alikuwa mchumba wa Monte nyakati fulani.
Ni kwamba, Chaster alikuwa hajui kama huyo ni Charity, bali alijua ni Eliza.
"Pia alidhani mimi ni samaki mfu, hivyo akanitosa na kwenda kwa wengine."Eliza alijibu bila kufafanua mawazo yake.
Chester alitabasamu, lakini macho yake yalikuwa ya baridi isiyo ya kawaida. Ingawa Eliza hakuwa mwanamke wake wa kwanza, alichukizwa sana alipofikiria kuwa maeneo ambayo amegusa na Monte pia ameyagusa.
“Inaeleweka; sio watu wote wanachukizwa na samaki waliokufa kama mimi. Lakini.. any way, lazima nibadilishe shuka.” Chester alisema huku akiinama na kumbusu mdogo wake wa uso.
“Chester…” Eliza alikunja sura yake na kuinua kichwa chake.
“Kuna kitu kibaya?” Chester aliuliza huku akiinua nyusi zake huku macho yake yakiwa yamependeza.
“Nakuchukia.” Eliza alifoka kwa upole.
“Unanichukia kweli?” Chester aliikandamiza sigara kwenye sinia ya majivu, kisha akampindua na kumkandamiza tena.
"Chester, usiwe hivi, naogopa nikikaa na wewe kwa muda mrefu, nitakupenda." Eliza alisema huku akigeuza uso wake pembeni.
Chester alipigwa na butwaa kwa sekunde mbili kabla ya kugeuza uso wake na kusema, “Wewe ni Eliza, utanipendaje?”
“Niko serious; Nilikubali hatima yangu na nikafikiria jinsi ya kukabiliana nayo. Hata hivyo siwezi kukutoroka.” Eliza alisema kimya kimya. "Kwa kweli, huna cha kupoteza ikiwa utafikiria juu yake. Unaonekana mzuri, na mwenye nguvu. Ni wanawake wangapi katika tasnia ya burudani wanataka kuteleza na wewe kwenye kitanda chako? Unaona? Baada ya kuja kwa wafanyakazi wenzangu leo, Director aliniheshimu sana, na Gladys, ambaye alikuwa anashuti nami location, alionekana kunionea wivu na hakuna hata mmoja wa wafanyakazi aliyethubutu kunidharau."
Uso wa Chester haukuwa na hisia: “Je, hukupaswa kujua mambo haya mapema? Ulikuwa unanichukulia poa sana, na sasa una fahamu?”
“Naweza kukuhakikishia kuwa kubadilisha wanawake kwako ni sawa na kubadili nguo. Zaidi ya hayo, wewe na Cindy Tambwe mtafunga ndoa wakati huo. Mimi si mjinga kiasi cha kuwa hawara tu, hata nikiwa ni mjinga kiasi gani. Je, hilo si la muhimu? Sasa, ninakubali hatima yangu, lakini nataka utii baadhi ya maombi yangu.” Eliza alikumbatia shingo yake ghafla.
“Baadhi? Niambie kuhusu." Chester alisema kwa kumaanisha, akielewa jambo hilo.
"Kuwa na tabia ya usafi na huruhusiwi kutafuta wanawake wengine ninapokuwa na wewe. Pia, mimi ni mpenzi wako, kwa hivyo unapaswa kunipa rasilimali bora za filamu na televisheni." Eliza alisema kwa baridi.
“Mpenzi? Hujaelewa, ni lini nilikubali kuwa wewe ni mpenzi wangu?” Chester alitafakari.
Uso mzuri wa Eliza ulijawa na aibu, akamsukuma, akageuka ili aondoke.
"Unaenda wapi, eh?" Chester alimtania huku akimshika mkono na kumvuta mikononi mwake.
“Tafadhali niache niende.” Eliza alidhihaki, “Kwa hiyo mimi ni suluhu tu la mahitaji yako katika moyo wako? Kitu cha kuchezea?"
“Si kweli.” Chester alitania, “Nilikupa nafasi hapo awali, lakini hukuithamini, lakini usivunjike moyo, ngoja nilale kwa muda, labda nitabadili tena mawazo yangu.”
Eliza alikazia macho sura ya Chester ya kihuni.
Moyoni mwake hakuweza kujizuia. Kama angekuwa mkorofi mbele yake siku za nyuma, asingeweza kumwangukia.
“Sawa.” Eliza akauma mdomo. “Kwa kuwa sasa nina uhusiano na wewe, huwezi kulala na wanawake wengine.”
"Silali na wanawake wengine hata hivyo." Midomo ya Chester ilitetemeka. "Sina nguvu ya kuburudisha wanawake wengi."
“Mbali na hayo…”
"Bado una maombi mengine, huh?" Chester alianza kukosa subira.
Eliza alidhihaki, “Nimetaja maombi mengi, lakini umekubali moja tu. Lo, na ulikubali tu kwa sababu huna nguvu ya kuburudisha wanawake wengi. Chester, wewe nhuna akili kwangu. Ulisema sistahili kuwa mpenzi wako, na hujawahi kunipa marupurupu ambayo wapenzi wako wote wa awali walipata. Je, mimi ni mjinga ninayelala nawe bure?”
Kwa ulimi wake mkali, Chester alivutiwa naye zaidi. "Endelea."
“Nilipe.” Eliza akanyoosha mkono wake. “Nimekupa mwili wangu muda mrefu sana, lakini umewahi kunipa pesa? Nilipokuwa kwenye uhusiano na Monte, angalau alinipa pesa…”