Simulizi: Kisanga

Simulizi: Kisanga

Mr Acky

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2019
Posts
234
Reaction score
313
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi: Akida Siri Rambao
Contact: 0658328596
Email: akidasiri@gmail.com

MSIMU WA 1

NCHINI ZHONGO

SEHEMU YA 1A

KITONGOJI CHA NYAKWA-WILAYA YA CHOZI


Sauti yenye mchanganyiko, isiyoleweka uhasilia wake si me si ke iliendelea kupita masikioni mwake, ina himizo kuu! “Gotwaaaa! Gotwaaaaa! Gotwaaaa!” ikipambishwa kwa mtetemo wa mawimbi, dhahiri ya ushawishi kumvutia sana kiasi cha kutupilia mbali woga, ujasiri kifuani yu katikati ya mlango akijishauri kuingia au la! Macho akiyapeleka huku na kule, hatua mosi pili ikafata macho ya kutafuta . Chumba au ghala!?

Hakuwa na mpangonayo yu makini akitafuta amuitaye. Huyo kwa hamu ya kujua asiyoyajua tahadhari kiduchu tama kiloba mpaka kwenye kabati kubwa la kioo. Ni kama aliyekuwa akielekezwa cha kufanya! akachutama na kuvuta droo hapo hapo sauti ile ikakoma. Sasa macho yakawa juu ya karatasi iliyofubaa iliyokunjwa kunjwa.

Alibaki kuitazamakwa jicho la tama uzalendo ukamshinda akaishika na kuitoa. Kitendo cha kuitoa karatasa tu nyuma yake wakazuka watu wawili wanaume wazee wa makamo na mavazi yao ya kale kwa pamoja wakastaajabu sura zao zikionekana wazi kushangaa “Nani aliyetuita hapa tulikuwa kwenye mapumziko ya kadri!” mmoja alisema sasa akijinyoosha viungo ihali ni mtu aliye na uchovu mwenzake wakati wote yu kimya tuli lakini mwenye uduwanzi macho katumbua akimkodolea Gotwa, mtu huyo akaanza kupiga hatua akimfata kwa nyuma mwenzake akiwa nyuma yake akimtazama bila kusema neno .

Ni kama Gotwa alihisi kitu maana aligeuka na kutazama upande ule alipo bwana huyo aliye hatua chake toka kwake “Nimesikia kitu…” alijisemea akitazama huku na kule “Lakini nimesikia mtu akiongelea huku” alisema tena na kuwafanya watu wale waliozuka kutazamana kwa mshangao.

Gotwa akapuuza na kurudisha macho mikononi na kuanza kuikunjua, akamaliza, macho yakagandia karatasini yakizunguka kwa mtindo kukagua karatasi hiyo fifi-fii si nyeupe si manjano pau pau! ikiashiria mvua nyingi zilizowahi kupita tangu kucharazwa na kalamu ya wino. Ikiwa na hati ya kipekeee sana hati ya mlalo na maadishi yake ya bluu nyeusi iliyofubaa akatabasamu huku akiitazama vizuri karatasi hiyo ikimshawishi kuisoma “Mwandiko mzuri” alijisemea na kutabasamu.

Viumbe wale wawili wasiojulikana waliko toka mmoja akiwa na tabasamu lakini mwengine akiwa na jazba iliyosomeka machoni mwake waliungana kumtazma Gotwa kwa hamu ndipo Gotwa akaanza kuya soma maneno yale kwa sauti ya kunong’ona pasina Gotwa kuwaona hali ya kuwa walikuwa karibu yake, Ajabu!

“Huyu ndiye mama wa wote, ndiye anaye lisha kote-kote, anachoambulia ni mashuka kukuuu, vitamu-tamu, ving’ao-nga’o, na naniliu…!!! akiahidiwa hivi na vile baada ya kile na yale, eti Utandawazi! Kichwa dafu si nazi ya tui, hovyo kuliko kichwa panzi!!!. Mwenyewe anafurahiii akiimba, kucheza-cheza akiiota ndoto ya ngekewa isiyofika, isiyo na nyenzo! Mwee!

Mama huyu kapotea na hataki njia, ana macho haoni masikio yana ntap hasikii ya muhazini wala mkimu swala.

Anavaa na kula makombo, wakati jiko ni lake sufuria yake vyote vyake, asili yake ni kwake. Alishawapenda mahaba yake yote, kwetu ni kinyaa! Sijui ni kulogwa na sangoma!? Wakilia tu roho itampasuka huyo atahaha kanga kiunoni akienda akinung’una atabeba hiki na kile na kuwapa. Tazama! anawaabudu?! kana kwamba hajawalea na kuwahudumia mahitaji yao walipo kuwa watupu, yu kipofu. Huyu mama vipi!??

Tunajua ukweli wake si watoto wake ni wa kuwalea hawafanani mwendo, rangi wala pua hajulikani baba yao, ni wavamizi! Anawatoto wa kuwazaa walio wema sana kwake, watoto wa tumbo lake na ziwa lake! Uchungu wa mwana ni wa mlezi? Na si mzazi? Mhh ajabu ya karne?!
Loo! Sisi masikini ni mkia wa mbuzi tutafanyaje wakati tumboni hatufiki sembuse kifuani!!!!? Sasa katugawa tu wazuri tu makatili, tuwachoyo tu wahisani hatupendani kama zamani, katikati dosarini fitinani hasadini hatujuani mgeni yu thamani mwenyeji yu jikoni! ni zambi ya nani?! ya mama au ya wana au ya jirani!!? Huyu ndio mama yetu! Zumbukuku."

Alipo maliza kusoma mapigo ya moyo yakaongezeka kasi maradufu, hofu?!

Itaendeleaa.....
IMG-20220404-WA0018.jpg
 
KISANGA!!!

Mtunzi Akida Siri Rambao

Contact 0658328596

MSIMU WA 1

SEHEMU 1 B

Ilipoishia

Alipo maliza kusoma mapigo ya moyo yakaongezeka kasi maradufu, hofu?!


Tuendelee..

.....Maana si kwa kuhema kule, kutetemeka kukafata mkono umeganda ngaa!. Macho yamemtoka kama mjusi kafiri! akatazama pembeni, haelewi cha kufanya!? Airudishe aichukue aichane aiache. Akayanasisha tena kwenye karatasi sasa domo lipo wazi Mwaa!

“Gotwa bwana, kwa umri gani na akili ulizonazo kiasi cha kujishughulisha na mambo yaliyokuzidi umri, usiyoyajua asili yake!” aliongea bwana yule aliyeoneka kutokuvutiwa na Gotwa tangu kuzuka kwao chumbani humo, Ni kama alisikia vile Gotwa alitazama upande aliosimama bwana yule aliyemkebehi mwili kauegemeza kabatini wakatazamana kiasi cha kumshitua bwana huyo na kujitoka taratibu katika egemeo akirudi kwa hatua fupi fupi kwa mashangao, ajabu Gotwa alifatisha macho akimsindikiza. Kisha akarudisha macho kwenye karatasi.

“Unaona usidharau udogo wa choroko, weka tumaini juu yake, si rahisi kukuona bali anaongozwa na hisia kali” aliongea yule mwengine mwenye masharubu mengi akimtazama mwenzake aliyemrefu kumzidi mikono kaiweka kiunoni bado akimshangaa Gotwa “Ukimuona kama Mtu mzima na mipango madhubuti, sijaridhika kuweka karata yangu” alisema bwana huyo akijibu shambulizi akimtazama mwenzake kwa chini kwa kebehi na wote wakayarudisha macho kwa Gotwa.

Gotwa yupo mawazoni akijadili ujumbe mzito angalau ang’amue mbili tatu zimtoshe saizi ya bongo lake kutoka katika karatasi iliyo mikonononi lakini aliambulia kung’aaa ng’aa macho tu akibwenza bwenza huku akiyazungusha zungusha huku-huku ikawa ndio yale ya kutwanga maji kwenye kinu sawa na kuvaa suruali isiyo mtosha.

Gotwa!
Akiwa bado kakomaa kakaza kichwa akifanya mashauri, tabasamu likamjia akameza fundo la mate na kuikunja-kunja taratibu karatasi ile kama alivyo ikuta na kuisusia kwenye mfuko wa nyuma wa kibukta chake kifupi cha jinsi nyeusi.

Baada ya kuakikisha imekaa sawia akaridhika na kuutoa mkono wake safari hii moyo ulitua mahala pake, amani imepatikana. Sasa macho yametumbuka kwenye kioo kilichomfanya kumpa taswira nzima ya mwili wake ulivyo akajitazama kwa muda.

Akiangalia sura yake iliyo na midomo mipana na pua ya mchongoko pamoja na macho makubwa masikio kama upawa nyele za kipilipili, akakunja sura hakupendezwa macho juu ya taswira ya nywele kichwani mwake za kipilipili mfano wa mikutano ya nzi kwenye sukari au kidonda “Lazima nikanyoe leo” alijisemea domo akilivimbisha, huyo akachutama na kurudisha droo moja kati ya mbili zilizofanana kama watoto mapacha. Taratibu kwa madaha ilisaliti amri na kurudi pahala pake bira kupiga kelele hapo akatosheka na kutabasamu zaidi akajisimamisha na kutazama tazama kama kuna mtu aliyemchabo hapa kuwepo mtu, “Lakini mbona nahisi watu wakiongea humu mbona kama kua watu humu, au njaa?” Gotwa alijisemesha akijitazama kwenye kioo “Sielewi nywele zani sisimuka, Mhh!” alisema tena kisha kwa minyato akajitoa chumbani humo “Mhh Huyu mtoto ana hisia kali kashatushtukia” alisema Burushuti domo kaliacha wazi mwaa! “Tulia wewe fupi meli ndo kwanza iko feli” alisema Mti mkavu huku akiendelea kumtazama Gotwa akitoka.

“Haaa! Gotwaaa!... ulikuwa wapi mjukuu wangu nimekutafuta kila mahali” pandikizi la mama chinene! Chibonge haswaa! ngozi maji ya kunde mrefu wa haja sura yake pana mdomo ameachama, mshangazo! “…Ulikuwa wapi babu!?” aliuliza tena safari hii mikono yote akiiegesha kiunoni akipiga hatua fupi fupi macho ya nataka kujua! Gotwa wasiwasi mwingi kajituliza akitafuta cha kusema akijishauri ukweli au uongo akageuka kwa kuibia akitazama kile chumba na kurudisha kichwa haraka akameza fundo la mate macho wasiwasi mwing ghafla akabwatuka “Bibi! nilikuwa msalani” kwa aibu ya uongo akachimbia macho sakafuni,

“Ohh mjukuu wangu pole mlenda huo na maharagwe tumbo limevurugwa loo!...pole babuu!” simanzi usoni akasogea zaidi na kumnyakua juu-juu “Haya twende ukanywe chai babu” Hao wakatoka huku bibi akiachia sehemu zake za mwili zikitingishika kwa unene na vishindo vikifatia. Gotwa alibaki kuutazama mlango ule wa chumba alichokuwemo.

Itaendeleaa.....
 
KISANGA!!!

Mtunzi Akida Siri Rambao

MSIMU WA 1

Sehemu 1 C:

Tuendelee...

“Haaa! Gotwaaa!... ulikuwa wapi mjukuu wangu nimekutafuta kila mahali” pandikizi la mama chinene! Chibonge haswaa! ngozi maji ya kunde mrefu wa haja sura yake pana mdomo ameachama, mshangazo! “…Ulikuwa wapi babu!?” aliuliza tena safari hii mikono yote akiiegesha kiunoni akipiga hatua fupi fupi macho ya nataka kujua! Gotwa wasiwasi mwingi kajituliza akitafuta cha kusema akijishauri ukweli au uongo akageuka kwa kuibia akitazama kile chumba na kurudisha kichwa haraka akameza fundo la mate macho wasiwasi mwing ghafla akabwatuka “Bibi! nilikuwa msalani” kwa aibu ya uongo akachimbia macho sakafuni, “Ohh mjukuu wangu pole mlenda huo na maharagwe tumbo limevurugwa loo!...pole babuu!” simanzi usoni akasogea zaidi na kumnyakua juu-juu

“Haya twende ukanywe chai babu” Hao wakatoka huku bibi akiachia sehemu zake za mwili zikitingishika kwa unene na vishindo vikifatia. Gotwa alibaki kuutazama mlango ule wa chumba alichokuwemo.

****

“Unaseamje tuachane na wazo langu” Mzee yule mwenye masharubu mengi mfupi alisema na kumfanya mwenzake kumkodolea “Siliza Burushuti sitaki kutupa karata kama ilivyokuwa, nitakuwa nawe ila kwa sharti la kumuacha yeye mwenyewe akiongozwa na akili yake isije kuwa kama kwa Kileo, hili ni kwa muda Fulani, alafu…” akajikuna kidogo chini ya shingo yake ndefu na kuendelea “…Tumfate fate nyuma nyuma tu huenda lengo limebaki kwa Nkole, kumbuka tukiingia itatubidi tukubaliane nae kwa kila jambo kwa hiyo ni kheri tukapunguza papara nibado humuoni ni bado mdogo!?”

“Sizani, kila kitu umekiona bahati humfata mtu wala mtu haifati jaribu kujitoa upofu…hii ni bahati yake ndiye aliyechaguliwa na hiyo ya udogo sio sababu mi nauona uwezo wake mkubwa mchoni mwake tena wa kuzaliwa tofauti na babu yake pamoja na huyo unayemtegemea”
akaanza kusogea taratibu akimsogelea zaidi akimtazama kwa macho ya kumaanisha akisemacho “…nimekubaliana nawe wacha tuangalie uwezo wake sawa wewe Mti mkavu , lakini kwa sharti moja isichukue muda mrafu sana sitasubiri sana na kama hakunaishara tutakayo iapata tutabaki kumlinda Gotwa na si vinginevyo” aliongea Burushuti akimtazama Mtu mrefu akimmuangalia kwa juu “Wewe mtu mfupi una tabu king’ang’anizi na mbishi hukubali kushindwa teyari limepita Agano twende zetu” alisema Mti Mkavu.

******

“…mwenye kutaka mvua lazima avumilie jua pigo ulilolipiga lazima litupe faida Nkole, labda mimi sio Mzee Chogo wa milima ya Uzungwi sasa watu watakuona kama nabii watakuheshimu na kukupenda zaidi baada ya hapo tunaingiza karata nyingine na kulamba dume mchezo kwisha kisha hao taratiiibu hahahahh unabahati sana” alicheka mzee huyo na kujikuta akikhohoa mfululizo na mala macho yakaanza kumtoka akihema kwa kukoroma “KHOOH! KHOOOH! KHOOOO!” tabu imemshika kulikoni!? Mkono mmoja kifuani kalikunja shati lake jeupe akisugua kifua mwengine ukitafuta kitu jamvini, “Shika hiki hapa…” Mzee Chogo akakikwapua kichupa na kukiweka puani akivuta na kuvuta tena na tena,

“Ohhh… hhuuuh…kidogo nife wallah, asante Nkole ahueni Dah!” macho mekundu akamuangalia Nkole, macho yakakutana Nkole yukasimama kama mlingoti hofu tele Mzee Chogo yu Jamvini “Hebu kaa sitakufa” Mzee Chogo alisema na kuangua kicheko kiasi cha kumshangaza Nkole aliye baki akimtazama haelewi! “Sasa kunitolea macho hivyo vipi, kaa bwana sifi mpaka nione ushindi wako, za kwangu bado hazija fika”

Nkole akajikuta akitingisha kichwa kusikitika “Unajijua fika umgonjwa lakini wajiona mzima kila wakati ehh! kama nisinge kuwepo mahala hapa ingekuwaje baba?...kikopo umekiacha sebureni tena mezani badala ya kukiweka mfukoni, ahh! sijapenda hata kidogo” aliongea huku akiukunja mguu wake mmoja baada ya kukaa jamvini “Usingekuwepo angekuwepo mwengine kama hazijafika hazija fika…imetokea bahati mbaya tu” akayapeleka macho yake pembeni akiuma mdomo wake wa chini huku akizivuta vuta ndevu zake nyeupe miguu kainyoosha jamvini.

“Kifo bwana, kumbe kufa ni kugusa tu paap! mtu unakufa Dah!” alijsemea na kubaki akijiwazia wakati Nkole akibaki kumtazama tu. Vishindo ndivyo vilivyo watoa mzozoni wote wakageuza shingo zao kutazama kitu gani? Bibi akaingia mkono huu Chupa ya chai na ule bakuli la maji Gotwa nyuma yake na sahani kubwa ya mihogo, viazi vitamu, maboga pembeni bakuli la mbilimbi akavitua jamviini

Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

Mtunzi Akida Siri Rambao

MSIMU 1

Sehemu 1 D

Tuendelee...

...nyuma yake na sahani kubwa ya mihogo, viazi vitamu, maboga pembeni bakuli la mbilimbi akavitua jamvini.
Harufu ya diko diko la mbilimbili iliyoungwa barabara kwa viungo lukiki ikatapaa mahala hapo na kuzipa burudani pua zao wanaume midimo ikajaa mate macho bakulini kwa pamoja wakameza mate matabasamu yakisawili nyuso zao na kusahau yaliyotokea dakika chache nyuma “Haya wanaume chai hiyo kazi kwenu” Bibi alimalizia kumimina chai kwenye vikombe kisha huyooo akaenda zake “Ama! we vipi?”

Mzee Chogo alihamaki akimsindikiza kwa macho mkewe “Aaa nyie endeleeni nina kazi nitakula baadae” sauti tu ilisikika akiwa kesha potelea ndani “Haya mwenye macho haambiwi ona…” Mzee Chogo akakaa vizuri na kutowesa mkono katika bakuli la maji ya kunawa Nkole akammiminia maji kumsuuza, wote wakanawa na kuanza kula.

Muda wote Mzee Chogo alikuwa akimtazama Nkole kwa jicho la kuibia, wazi Nkole yupo mawazoni. ‘Ana nini huyu?’ alijisemea nafsini.
“Bwa mdogo hupaswi kukata tamaa, tamaa haikatwi hufatwa” aliongea Mzee Chogo huku akijitahidi kumeza kiazi mara ghafla akakifakamia kikombe cha chai ya moto “KHOO! KHOOH! KHOOH!” mkono wa shoto ukiziba mdomo, macho mekundu akibwenza bweza Nkole akimtazama kucheka anataka ila akijizuia kwa kutazama pembeni. “Mhh! Leo!...Khaa! Huyu mwanamke atatuua kwani sisi walevi?..pilipili kama sisi walevi” Mzee Chogo akabaki kulitumbulia macho bakuli la Mbilimbili sura kaikunja “Babu, usije chocha mbilimbli ya leo inapilipili sana” aliongea Mzee Chogo kisha akatabasamu huku akijitaharisha kuendelea kula. “Kuna mtu kakutaja ndio maana” aliongea Nkole na kuliacha tabasamu lake akicheka kimya kimya

“Mhh atakuwa nani habari zangu zisha zikwa…ila afadhari umetabasam” aliongea Mzee Chogo nae akitabasamu “Nikweli baba nina wasiwasi lolote linaweza tokea na tunafedha kichele” aliongea Nkole akitingisha kichwa kwa masikitiko.

“Nikweli watu tu vinyonga, bora maandalizi” aliongea Mzee Chogo simanzi ikamvaa akasitisha kipande cha muhogo mdomoni na kutazama pembeni kwa muda kisha akaongea “Cha msingi kuwa mpole na ufikirie kila hatua unayotaka kuipiga, unabahati mbaya akili yako iliyo kaza na kukataa shauri la wazee anagalau ungerekebisha palipo toboka na kuwa kinara” kisha akajiinamia akanyanyua kichwa kumtazama Nkole macho yakakutana kama majogoo yanayotarajia kupigana.

Gotwa alibaki tu akiwa tazama kwa makini na kupokea kila alisikilizalo tuli kama sio yeye, havumi! “Unaona niyasemayo Mti mkavu, Nkole si mtu wa kumuamini, mtazame Gotwa macho yake, utulivu wake jionee yani hapo hatuja pata amuzi la kuingia akilini mwake na kujua aliwazalo lakini pale alipo ni mtu mwenye tama yakudumisha haki na ukombozi, macho yake yanasema” aliongea Burushuti akiwa kando ya kuta akimtazama Mti Mkavu “Subiri na tuone kitu gani kitafata, chonde usivunje Agano” alisema Mti Mkavu na Burushuti akamtizama tu.

SAA LIKAKATA
“Babuu umeshamaliza?!” aliongea Bibi akimtazama Gotwa, Gotwa akatingisha kichwa kukubari , Bibi akatabasamu na kumsogelea karibu kwa macho ya upendo wa tosha “Kama tulivyoongea, pesa hii lakini usichelewe si unayaona mawingu?” “Sawa sitachelewa” aliongea Gotwa huku akipokea pesa kisha akampa mgongo akiuelekea mlango wa nje.

BARABARA YA BUKUSU, NYAKWA WILAYA YA CHOZI
Kipindi mwanga wa jua ukianza kuonekana na mawingu mazito kusambaratika, Upande wa Gotwa Tahadhari kubwa ilikuwa kichwani mwake akijijitahidi kukanyaga sehemu zenye afadhari huku mkono ukiziba tundu za pua kwa harufu kali ya uvundo iliyotapakaa eneo hilo la barabara.

Ndio! maganda ya viazi na mabaki ya vyakula vilionekana kumwagwa kuziba mashimo. Shangazo likaonekana machoni mwa Gotwa kipindi akijihimu kutokuchafuka na kuteleza topeni watoto warika lake walikuwa wakipita pekua bila kujali hali iliyomfanya awageukie na kuwatazama wakienda.

Wakati wote huo wazee wale waliozuka waliokuwa wakiandamana nae wakimtazama kwa makini huku wakijibizana, Gotwa ahana habari!
Ghafla Gotwa alishtuka na kumfanya ageuke nyuma kutazama kilichomshtua

“…unanishangaa nimevaa kinyago hebu nipishe mie Fyoooooo” Gotwa akajibana bana kumpisha msichana huyo aliyemshangaza kwa muonekano wake na ukali aliouonesha dhidi yake kipindi ameduaa akimtazama akasalimiwa na harufu ya manukato mazuri yaliyopenyeza kwenye tundu za pua yake mdomo wazi shingo ikageuka kumuangalia zaidi.

Hakuwa mwanamke tayari, ni kasichana tu ka umri wa kati miaka kumi na minne lakini vazi lililomwilini fupi la kumshika mwili likisadifu maungo yaliyo tuna tuna, yu kigoli yumbichi teketeke sehemu za kifua zikiwa wazi ngozi mwororoo kifua cha saa nne kilichongezwa na vigorori mduara wa kifuu cha nazi. Mpasuo ule kule kwa urefu uliopasua mioyo ya watizamaji mithili ya radi angani wakienda wakizivunja shingo zao Mhh! maana si kwa mchano ule ni kusudi na chokochoko. Binti anamambo ya vijimambo.

Viatu vile vya gharama na nywele za rasta zilizoshukia mgongoni ilikuwa tosha kutoa majibu ya maswali lukuki ya mtu amtizamae.

Gotwa akaachana nae na kuendelea na safari. Kweli dunia inamambo.

Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

Mtunzi Akida Siri Rambao

MSIMU wa 1

Sehemu 1E

Tuendelee..

Viatu vile vya gharama na nywele za rasta zilizoshukia mgongoni ilikuwa tosha kutoa majibu ya maswali lukuki ya mtu amtizamae. Gotwa akaachana nae na kuendelea na safari. Kweli dunia inamambo.
Hatua chache, “Ngere ngere ngere!….” taili la baiskeli hili Gotwa alishtushwa hamadi! akatowesa mguu katika tope topwaaa! na kumfanya kutoka mawazoni, sura akaikunja akajisogeza kando na kutoa upenyo.

Ndipo macho yake yakajionea Mzee wa makamo wa umri kati ya khamsini na kidogo akihangaika harufu ya jasho zito ikimtoka mwilini kama beberu, macho kayatoa akihema hovyo akipambania kujihimu. Mikono ikivuta na kuvuta baiskeli iliyojazwa madafu kila kona ya tenga miguu pekua ikilikabili tope na kuliacha na kulikabili tena mishipa ya shingo imemtoka huku baiskeli ikilalama kwa kuelemewa na uzito swiii swiiii!, lakini wala hakujali aliendelea kututumka akienda na kuenda akimuacha Gotwa akimshangaa huruma ikionekana dhahiri machoni mwake.

Alipoangaza angaza kwa mbali ndipo akamuona binti yule aliyepishana nae dakika kazaa zilizopita akipanda kwenye gari moja ya kifahari nakuondoka. Alijikuta akivuta pumzi nzito na kuzitoa kwa nguvu.
“Haya ndio maisha ya miji mingi hapa Zhongo, mjukuu wangu Gotwa si rahisi kwa mtu aliye kulia katika mazingira ya ustaarabu kuyaoana haya anaweza hisi ni maigizo” Sauti ya mwanaume mzee ilipita katika fikra za Gotwa akiwa kasimama akilitazama gari lile na mazingira yanayomzunguka kisha huyo akaanza kuharakisha.

Uso wake ukionekana kubeba mambo mengi yenye kumshughulisha.
Akaacha barabara na kufata uchochoro wa nyumba zilizo banana na kukosa ustaarabu wa kujengwa bila mpangilio huku mifereji ya maji taka yenye harufu ya kukureketa ikisheheni toka majumbani. Maji ya mabaki ya chakula na maji ya vyoo vilivyozibuka vilikuwa vikifata maporopoko hadi mtaroni, kichefu chefu! Gotwa akaziba pua, kuziba harufu mbaya ya maji ya mitaro iliyotuhama toka katika nyumba hizo. “Inabidi nifanye haraka” alijsemea Gotwa na kuanza mbio.

DAMPO LA KIVUMBI, NYAKWA; WILAYA YA CHOZI
Baada ya muda kidogo, Gotwa alikuwa mbele ya Dampo kuubwa, Idadi kubwa ya watu wa rika zote ikiwa machoni mwake. Watu hao walionekana wakiendelea na shughuli ya kuchakuwa kama kuku kwa mikono yao, bize wakitafuta wavitakavyo.

Sura zao zilizokosa tumaini la maisha wakisogezwa kwa nguvu ya pumzi ya bure, sura hazitamaniki kwa masinzi meusi yaliyoshikamana na ngozi kwa muda mrefu, nguo zao zikiwa hazitofautiani na dampo lenyewe. “Omba omba na machokoraa, mbona simuoni…yuko wapi?” alijisemea macho akiwa kayakaza akiwatazama kwa zamu huku kasimama sura kaikunja mkono ukiwa puani kuzuia harufu mbaya isiyoeleweka ya eneo hilo, hakuna mwenye habari nae.

Kipindi akiwa mawazoni akimtazama mtoto wa rika lake akiwa ameshikilia silesi ya mkate toka katika mfuko alishtushwa na makele ya ugomvi na kumfanya kupeleka shingo mahali itokako sauti hiyo. Alitahamaki kuona ugomvi, ugomvi kweli-kweli mama mmoja mwenye mtoto mgongoni alikuwa akigombaniana kipishori “Nimesema achiaaa…achieni nitawauaa!” mkono mmoja ameshikilia kipishori kilichoshikwa na wasichana wawili wengine wakimzuzua kumtisha kumtaka aaachie mara moja lakini hakuwa tayari akitishia kwa kisu ameshikilia kisu kuwakata akitaka ushindi. Mara sauti kali ya mtoto toka mgongoni mwake ikapazwa.

Mtoto alilia kwa kulaani kudhurumiwa haki yake ya burudisho la usingizi kwa kelele na pukurushani zilizomkumba, lakini mama yake yukaidi akipambana kumpambania tonge la siku hiyo, hakumjali.
Ilikuwa shoo kwelikweli wapita njia wengi walifurahishwa na tukio la watu hao lakini haikuwa bahati kwao maana sijui kijana yule alitokea wapi ilikuwa ghafla binvuu kipishori kikanyakuliwa Nyaku wakatahamaki mikono mitupu ni mishangao tu wakimsindikiza kwa macho kijana yule akitokomea upande wa pili. “Wamekosa wote” Gotwa alijikuta akiongea kwa huzuni. “…sasa mbona simuoni” akiangaza tena huku na kule kwa tumaini.
Dakika chache baadae, “Simuoni naondoka” huyo akashika njia hali yakuwa macho yakiranda randa kutafuta yakiwa hayajaridhika. “Vipi! Punguza ukaidi twajichelewesha buuuure” Burushuti alimsemesha Mti mkavu “Bwana wee usinilazimishe ume sahau agano letu” alimjibu na kuanza kumfata Gotwa aliyeshika njia akiondoka eneo hilo.

Itaendeleaa...
 
Kisanga!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao

Contact: 0658328596
Email : akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 1F

Tuendelee...

Dakika chache baadae, “Simuoni naondoka” huyo akashika njia hali yakuwa macho yakiranda randa kutafuta yakiwa hayajaridhika. “Vipi! Punguza ukaidi twajichelewesha buuuure” Burushuti alimsemesha Mti mkavu “Bwana wee usinilazimishe ume sahau agano letu” alimjibu na kuanza kumfata Gotwa aliyeshika njia akiondoka eneo hilo.

Aliluka vidimbwi vidogo vya maji huku akikwepa utelezi asianguke huyo kama tumbili, kwa tahadhari kubwa hatimaye akalimaliza Dampo la Kivumbi bila kupata akitakacho na kuingia katika makazi ya watu. Uchochoroni mbio mbio akiziacha nyumba nyuma yake mara akajikuta akipunguza mwendo na sasa akitembea taratibu moyo ukimuenda kasi macho kayatoa akilishika koo lake linalo muawasha kweli kweli “Kuna nini mbona nahisi kuogopa” alijiongelea peke yake huku akinyata kuvizia kitu kwenye kona ya nyumba ya matofali ya dongo bichi, kadri alivyosogea zaidi ndipo aliposikia mazungumzo vizuri, sauti hatarishi ya kiume nzito ikikemea “Nitakukata kichwa… toa kila kitu nakwambia la sivyoo…” Gotwa alimeza mate tamaa ya ushuhuda, akajibanza kwenye ukuta konani na kujionea vijana watatu wakiwa wamembana mwanamke katika ukuta akilia kimya kimya huku akivua vitu vyake vya thamani kwa hofu panga likiwa juu juu kumkata maungo yake.

Kipindi hicho Gotwa macho yamemtoka asijue la kufanya amejishikiza konani ukutani moyo ukimuenda mbiombio domo wazi kwa anachokiona kitu cha kumuogofya, mara Paaap! akateleza na kuanguka kama zigo Puuh! Kishindo chake kilifanya vijana wale watatu kupaparika hofu ikawapata wakaliacha zoezi lao na kutazama kunanii kwani?! lilikuwa kosa kubwa kwao kwa mwanamke chini ya maharamia wakabaji wezi majizi Dua zake zimejibiwa na sio siku za kufanya nyani miti kuteleza Upenyo wa nusra upo machoni mwake ni yeye juhudi ya miguu yake na mapafu kunusuru pumzi yake, hakuiacha bahati hiyo akachoropoka Shaa! Huo mshale mbele kwa mbele mbele yao akipiga mayowe “Jamani Weeeziiiii…weziiii wataniuaaa” waalishtuka kweupe mwanamke hayupo, hasira zao zikaongezeka maradufu baada ya kumuona Gotwa akiwa chini katoa macho akiwatazama “Shenzi mtoto mchawi wewe kuja hapaaa” mmoja wao akapiga hatua ndefu kumfata Gotwa “Sogea hapa baladhuri wewe nikutoe utumbo” Gotwa Hofu kubwa mwili ukapata ganzi mwili mzito asijue la kufanya akipepesa macho huku na kule akitamani msaada mapanga akinyooshewa.

Vizuka wale walikuwa mashahidi “Hapana Mti mkavu siwezi kuvumilia hili likatokea machoni mwangu si kwa hili tafadhari” alilalama Burushuti macho ya huruma yakimuelemea “Wewe tutajuaje kama ni jasiri na mwenye kujichunga hebu acha tuone” alisema Mti Mkavu macho kayakaza akitazama tukio la kuogofya mbele yake na kumuacha Burushuti akiwa njia panda na machaguo yenye kukinzana afanyaje?
‘Amka Gotwa na ukimbie hutakiwi kufa’ alisikia sauti ya ujasiri ikimuhimiza masikioni, Gotwa aligeuza shingo Ujasiri ukamuingia uchochoro upo pembeni yake hamadi binvuu akakurupuka na kuukimbilia kuufata Adui zake nao hawakulaza damu wakaunga nyororo nyuma yake kumfata kwa jazba mapanga juu juu.

Bila mapumziko alikimbia zaidi na zaidi, kila akitazama nyuma jicho la tumaini linamuishia ‘Ehh mungu nisaidie…ehhh mungu nisaidie!’ alijiongelea nafsini tamaa ikiwa moyoni kunusuru maisha. Njia ya vikwazo vya utelezi, uwembamba, vidimbwi vya maji visivyoisha huku akianguka mara kazaa kwa kuteleza uso ukidhihirisha majuto machozi haya yakimtoka.

Akiwa hana lile wala hili hoi-hoi! macho mbele akashtukia kuvutwa mkono Vuuuup! Mkono ukaziba mdomo wake asiujue ni wa nani na mwengine ukiwa umesmsika kisawa sawa kifuani asikurupuke kwa woga Akayafumba macho yake akiwa ni mwenye kusubiri yakumkuta, Hola! Akaanza kufumbua macho yake akiwa katulia kwa mkao aliyolazimishwa kukaa.

Itaendeleaa...

Hiki kweli KISANGA
 
Tuendelee bwana Acky
Sawa sawa nimeona nibadili ladha sio samaki wa kukaanga tu hata wa kuchemsha Ni mtamu ajabu

Lete maoni ndugu nijifunze mengi hata mtoto mwema hukuzwa na maneno ya hekima.

Kesho awe Bora kwa wa bora.
 
Sawa sawa nimeona nibadili ladha sio samaki wa kukaanga tu hata wa kuchemsha Ni mtamu ajabu

Lete maoni ndugu nijifunze mengi hata mtoto mwema hukuzwa na maneno ya hekima.

Kesho awe Bora kwa wa bora.
Una uandishi wa tofauti na waandishi wengi wa hiki kizazi cha sasa, kazi yako ni nzuri. Mi naona ungefanya mchakato hiki kitabu chako kipitiwe na kusomwa huko mashuleni, kwakupitia kusomwa kwa hiki kitabu wengi watapata hamasa ya kuandika simulizi kwa lugha inayofuata misingi yake
 
Hiyo picha kwenye avatar yako ni kitabu chako?, Je, nacho utaki'post' humu humu?
 
Hiyo picha kwenye avatar yako ni kitabu chako?, Je, nacho utaki'post' humu humu?
Ndio teyali mbona ipo humu inaendelea ipo MSIMU wa Tatu sehemu ya Tisa. Pia ipo kule pseudeusblog


Inaitwa The Hidden Truth ( Ukweli Uliofichika)

Inahusu Ujasusi itafute
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact : 0658328596
Email: akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 1G

Tuendelee...

kisawa sawa kifuani asikurupuke kwa woga Akayafumba macho yake akiwa ni mwenye kusubiri yakumkuta, Hola! Akaanza kufumbua macho yake akiwa katulia kwa mkao aliyolazimishwa kukaa.
“Unabahati sana…” sauti ilisikika nyuma yake na mkono ukatolewa. Hamu ya kutaka kumuona! akageuza shingo huku kaikunja sura yake kwa harufu nzito ya kukera pua!

“Haa Zora! Ni wewe!?” akatoa tabasamu akiwa ni mwenye kutoa amini akitazamacho, alikuwa kijana wa rika lake mrefu kumzidi mwenye macho madogo-dogo kichwa cha yai huku akibinua midomo yake ya wastani “Ulifata nini huku…hili eneo watu hawapiti hovyo hovyo ni hatari sana” aliongea kwa sauti yake ya kukauka akimshangaa Gotwa “…alafu…” aliongea tena yule kijana akimkazia macho Gotwa “…utakuja kutekwa ukauzwe” “Nini…nikauzwe?!” Gotwa alishtuka na kumtazama “Hujasikia au dharau, haya ulikuwa unaenda wapi?” “Soko la Mtungi” “Twende nikusindikize nazijua njia za huko vizuri…” aliongea nakuongoza njia.
Kipindi wakiendelea kutembea Gotwa alibaki akimtazama Zora kwa macho ya chunguzi alivumilia harufu isiyoeleweka inayotokana na mavazi aliyo nayo Zora, kaptula yake pana ya kitambaa, fulana ya mikono mirefu na mifupi iliyovaliwa kwa mara moja miguuni raba zake nyeusi zilizofubaa na kupoteza uzuri wake kwa kukosa matunzo stahiki “Navipenda sana viatu vyangu hivi ni vigumu, niliviiba mnadani kwa kuwa sikuwa na hela ya kutosha licha ya kutaka kupunguziwa lakini sikukubaliwa hivyo niliviiba” aliongea Zora baada ya kumuona Gotwa akivitazama viatu vyake.

Baada ya hatua kazaa, Gotwa akauvunja ukimya “Zora! kama vile nilikuona kule dampo!” Zora akasitisha mwendo akamtazama kwa muda nakusema “Ndio, nilikuwepo kule na niilikuona sana lakini nilikuwa na kazi yangu…niliona watu wakipoteza muda nikalipitia” Gotwa akaduaa “Haa! Kumbe ni kweli ulikuwa wewe!” akasimama akimtazama “Sikia, Nimekubali ombi lako ndio maana nipo hapa au niondoke zangu acaha kunishangaa kama kituko Fulani sipendi tabia yako” Zora akageuka akiwa na hasira akapandisha nyusi na kuyatoa macho nae kasimama mikono kiunoni miguu katanua akimtazama Gotwa kisha akapuuza na kukaa sawa baada ya kumuona Gotwa akiwa na huzuni “Ndio maisha yetu bahati tunaitafuta kwa gharama na sio kuisubiria kama wengi wanavyo dhani, nilazima nipole, niibe ndio niishi” aliongea akimtazama Gotwa ambaye alibaki tu kumtazama Zora “Unabahati ya mtende, ungekufa leo nishukuru nimekuokoa ulivyokuwa muoga na ulivyo muoga Haa! Haa! Haa!” Zora aliigiza na kutabasamu mwisho akaangua kicheko cha chinichini kilicho onesha muonekano mzuri wa sura yake ya asili kiasi cha Gotwa kumshangaa kwa muda.

Zora akakwepesha macho kwa aibu na kutazama pembeni akivunga huyo akaongoza njia akimuacha Gotwa
“Sipendi kuangaliwa usoni sawa dogo!?” aliongea Zora asijue kamuacha Gotwa mataani akishangaa vishangazo alivyonavyo akifikirisha bongo kwa kukuna sehemu ya upande wa kichwa kwa kucha sura kaikunja kiasi akimtazama Zora kwa kuibia “Naonekana kama wakiume eeh!? napenda kuwa hivi kwangu ni salama sana” akatabasamu na kuongea tena “Unajua nini Gotwa, nikiwa hivi wengi wanajua kuwa mi ni wakiume kifua changu kinaficha siri yangu, mbabe na najua kupambana wananiogopa” aliongea na kujitazama kifua chake kilichothibitisha maneno yake, Gotwa alibaki kumtizama tu.
“Leo nitakujibu maswali yako uliyoniuliza jana japo huwa sipendi kuongelea maisha yangu nayachukia uliza chap chap” aliongea tena Zora na kumuacha Gotwa nyuma yake akitabasamu.

“Kusema kweli jana usiku ulinifanya nilie sana nilikumbuka mbali sana ahh! lakini ni maisha yangu siwezi kuyakataa nilikuwa na ndoto zangu lakini haziwezi kutimia, mara kazaa huwa nakwenda kule ufukweni na kuwaona watu wakienda na kurudi na wazazi wao, furaha ikimea nyuosoni” aliongea Zora na kuanza kutembea kwa mwendo wa taratibu “…lakini hakuna cha kubadilisha watu wa mfano wangu ndio ndugu zangu japo huwa tuna koseana lakini ndio watu waina yangu nitafanyaje siwezi kuikataa hali yangu” aliongea Zora sasa machozi yakimlenga lenga akabwenza bwenza akijitahidi kuzuia kilio kilicho mlangoni

“Gotwa!” aliita Zora sauti ikikaribisha kilio akaendelea “..kila mtu unae muona kule dampo au mtaani au wale wakabaji wana hadithi za kuumiza sana kila mmoja anasababu iliyompeleka awe alipo, mfano mimi nilijiona ni mtu nisiye na chochote lakini nilipata moyo baada ya kuona kuna wenye hadithi chungu inayoumiza moyo kunizidi mimi yaani yangu ni cha mtoto” sasa kiganja cha mkono usoni kikifuta machozi yaliyozidi machoni na kuchuruza yeye akiyakausha “Sijui tamu ya baba mimi wala sijawahi muita mtu baba nafanya kusikia tu watu wakiita wakienda na baba zao” aliongea kwa unyonge kwa macho ya simanzi huku wakiendelea na safari Gotwa akimtazama tu kwa huzuni akitamani kusikia zaidi

“ ..na..na mama yangu alifukuzwa kwao kwa kushindwa kumtaja mtu aliyempa ujauzito akiwa shule, sijaijua akili ya mama mpaka hivi leo na amebaki kusema kuwa baba yangu ni mtu mwema sana, na atakuja kunichukua siku moja mpaka sasa nimekuwa sijawahi muona wala kusikia habari zake za uhai wala kifo mpaka mama yangu ameaga dunia” aliongea Zora na kutoa tabasamu feki, Gotwa alionekana kushtuka na huruma ikamuingia zaidi kiasi cha kuachia mdomo wake uwe wazi, alionekana kuhisi maumivu

Itaendeleaa...

Kweli Hiki Ni KISANGA!!!
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact: 0658328596
Email: akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 1 H

Tuendelee...

....lakini hakuna cha kubadilisha watu wa mfano wangu ndio ndugu zangu japo huwa tuna koseana lakini ndio watu waina yangu nitafanyaje siwezi kuikataa hali yangu” aliongea Zora sasa machozi yakimlenga lenga akabwenza bwenza akijitahidi kuzuia kilio kilicho mlangoni “Gotwa!” aliita Zora sauti ikikaribisha kilio akaendelea “..kila mtu unae muona kule dampo au mtaani au wale wakabaji wana hadithi za kuumiza sana kila mmoja anasababu iliyompeleka awe alipo, mfano mimi nilijiona ni mtu nisiye na chochote lakini nilipata moyo baada ya kuona kuna wenye hadithi chungu inayoumiza moyo kunizidi mimi yaani yangu ni cha mtoto” sasa kiganja cha mkono usoni kikifuta machozi yaliyozidi machoni na kuchuruza yeye akiyakausha “Sijui tamu ya baba mimi wala sijawahi muita mtu baba nafanya kusikia tu watu wakiita wakienda na baba zao” aliongea kwa unyonge kwa macho ya simanzi huku wakiendelea na safari Gotwa akimtazama tu kwa huzuni akitamani kusikia zaidi

“ ..na..na mama yangu alifukuzwa kwao kwa kushindwa kumtaja mtu aliyempa ujauzito akiwa shule, sijaijua akili ya mama mpaka hivi leo na amebaki kusema kuwa baba yangu ni mtu mwema sana, na atakuja kunichukua siku moja mpaka sasa nimekuwa sijawahi muona wala kusikia habari zake za uhai wala kifo mpaka mama yangu ameaga dunia” aliongea Zora na kutoa tabasamu feki, Gotwa alionekana kushtuka na huruma ikamuingia zaidi kiasi cha kuachia mdomo wake uwe wazi, alionekana kuhisi maumivu ndani kwa ndani yakiukabiri moyo wake kiasi cha kupeleka mkono kifuani “Walikuja bibi na babu kunichukua lakini sikuwa na furaha ya maisha yale ya unafiki vipi wanipende leo baada ya mama kufa na sio siku zote!? niliona hata mama atanichukia akisikia huko alipo nikaamua kutoroka na nipo hapa naishi nitakavyo” alisema tena Zora macho yakiwa mbele Gotwa akimuangalia tu kwa masikitiko “Pole, naona tumaini la baba yako siku moja” aliongea Gotwa kwa kujiamini, Zora alibaki kumtizama tu Gotwa wakienda zao. “Na siku hiyo nitakuwa na maswali ya kumuuliza ndipo nikubali kwenda nae tofauti na hapo…” alisema Zora akiishia njiani.

“Basi nitajaribu kuongea na bibi yangu maana ananipenda sana ili tuondoke wote tukaishi pamoja” alisema Gotwa huku akitabasamu kumaanisha, Zora akasimama na kumtazama Gotwa bado machozi yakimlenga lenga kisha akachimbia macho ardhini kwa sekunde “Basi na iwe hivyo, haya twende zetu” aliongea Zora na kimya kikaingia kila mtu akiwaza lake.
“Ohh tumeshafika soko lile pale” Zora kwa kidole akionyesha Gotwa akatazama kuthibitisha “Hii njia kweli fupi” aliongea Gotwa na kutabasamu kwa kuona idadi kubwa ya watu mbele ya macho yake wale wakienda na wale wakienda mikononi mifuko iliyotuna kwa bidhaa mbalimbali zilizo Languliwa toka kwa wakulima na kuchuuzwa kwa walanguzi kwenda uzwa magengeni wakizisunda bajaji, piki piki na wakupakia vichwani mwao walikuwepo.

Walikuwepo pia waliotandika viroba na kupanga mafungu ya nyanya, bamia, viazi vitamu, vitunguu na vinginevyo wakinadi bei zao kwa sauti kwa kila apitaye karibu yao pembeni ya soko hilo. Gotwa akaitupia macho ardhi Dongo jeusi la mfinyanzi lilikuwa kama uji uliotapikwa kila mahali na kuleta kichefuchefu kwa namna lilivyopondwa pondwa na wapitia njia na kuleta muonekano mbaya huku harufu ya matunda na viungo mbalimbali vilivyotupwa hovyo kukera pua za watu maana ni harufu mbaya ya uozo ulio tukuka, lakini hakuna aliye jali watu waliendelea na shughuli zao wakicheka kuongea huku wakila bila wasiwasi “Vipi mbona umekunja sura unahisi kichefu chefu” kauli hiyo toka kwa Zora ilimtoa Gotwa mawazoni “Ahh! Umesemaje!?” aliongea Gotwa akimtazama Zora kwa udadisi “Nasema Unahisi kichefuchefu?” aliongea tena Zora akimtazama Gotwa aliyebaki hisiani bila kificho pua kaikusanya “Mwanangu, njoo ntakuongoza…tano mia tatu” mama mmoja aliyepanga mafungu ya nyanya mshumaa aliashiria kumshika Gotwa aliyekuwa bize kuwatazama wanaume wa nguvu wakishusha magunia ya viazi, vitunguu na machungwa toka katika fuso zilizo egeshwa kando ya soko hilo kubwaa, walikuwa makuli.

“Hili lote ni soko la Mtungi mbona huku sijawahi fika?” aliongea Gotwa na kumtazama Zora kwa mshangao “Wee! huku ni nyuma ya soko wanakuita kwa kina kwangu pakavu tia mchuzi vitu bei cheee we umezoea kule juu barabarani kwa wadosi hahahaa” Zora aliangua kicheko akipiga na makofi na kutingisha kichwa “Kweli wewe mboga saba dah!” aliongea Zora na kumfanya Gotwa aushone mdomo wake na kutazama chini kwa aibu.

“..twende pale naviona nilivyotumwa” aliongea Gotwa na kutangulia mbele, dakika tatu tu alikuwa kasha hudumiwa mahitaji yake akamgeukia Zora “Sasa rafiki mimi nabadilisha njia kesho tutakutana si ndio wee nisogeze mpaka barabarani tu inatosha” aliongea Gotwa akishindilia alivyoagizwa nyuma ya mfuko wa kaptula yake ya jinsi akimtazama Zora “Nitakusindikiza tu mpaka kwenu wewe twende na mimi nina yangu ya kukuuliza” alioongea Zora na kumshika mkono Gotwa na kutabasamu.

Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao

Contact: 0658328596
Email: akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 1- i

Ilipoishiaa...

...ni soko la Mtungi mbona huku sijawahi fika?” aliongea Gotwa na kumtazama Zora kwa mshangao “Wee! huku ni nyuma ya soko wanakuita kwa kina kwangu pakavu tia mchuzi vitu bei cheee we umezoea kule juu barabarani kwa wadosi hahahaa” Zora aliangua kicheko akipiga na makofi na kutingisha kichwa “Kweli wewe mboga saba dah!” aliongea Zora na kumfanya Gotwa aushone mdomo wake na kutazama chini kwa aibu. “..twende pale naviona nilivyotumwa” aliongea Gotwa na kutangulia mbele, dakika tatu tu alikuwa kasha hudumiwa mahitaji yake akamgeukia Zora “Sasa rafiki mimi nabadilisha njia kesho tutakutana si ndio wee nisogeze mpaka barabarani tu inatosha” aliongea Gotwa akishindilia alivyoagizwa nyuma ya mfuko wa kaptula yake ya jinsi akimtazama Zora “Nitakusindikiza tu mpaka kwenu wewe twende na mimi nina yangu ya kukuuliza” alioongea Zora na kumshika mkono Gotwa na kutabasamu.

Tuendelee....

KITONGOJI CHA NYAKWA- WILAYA YA CHOZI

“Mjukuu wangu najua dhamira ya moyo wako japo humdogo lakini inaonekana ni mtu wa watu wewe utakuwa mtu wa watu siku za usoni, wala sitakuvunja moyo”

Mzee Chogo akaenda mihayo miwili mfululizo huku akijiziba mdomo kwa tumbo la kiganja cha mkono wa kuume mgongo umegema ukutani sasa akiiweka vizuri pua yake kwa kuivuta vuta “Lile eneo ni la walemavu lilitengwa na serikali kwa ajili ya kujengwa shule ya watu wenye mahitaji maalumu nafikiri unawajua” Gotwa alitingisha kichwa kukubali. “Palikuwa na fungu lililohefadhiwa na serikali dhidi ya watu hao, lakini katikati pakatokea bwana mmoja akidai eneo lile ameuziwa na serikali hiyo hiyo amabayo ilitenga eneo hilo kwa ajili ya walemavu upo?” Gotwa yu makini akitingisha kichwa kukubali

“Yule bwana alizamilia kujenga Zahanati akapeleka vitu vya ujenzi akiwaz hana hili wala lile viongozi wa walemavu wakafungua jarada la mashtka dhidi yake wakidai haki zao” Hamadi Mzee Chogo akaurusha mkono hadi katika shavu lake “Mhh! Kipindi hiki mbu nao huwa wengi kweli kweli…basi bwana ikawa vuta ni kuvute kesi ikadumaa” Mzee Chogo akaguna “Hivi unajua maana ya kudumaa” akamgeukia Mjukuu wake “Babu ndio si unamaana kesi haiku endelea?” alijibu kwa ujasiri kiasi cha kumshangaza Babu yake akabaki kutabasamu “Unaakili na maarifa sana wewe kama Babu yako Mzee Kileo” Gotwa akatabasamu

“…tuendelee, wananchi wa Kivumbi wakaanza kucheza mpira wa miguu ligi mbalimbali zilifanyika nani hakuujua uwanja wa Kivumbi wakati ule?!” aliongea na sasa akitabasamu akimuangalia mjukuu wake “Haikupita muda yule kijana aliyeuziwa na serikali alifariki kwa maradhi ya kikokhozi na mwenyekiti wa walemavu naye alipatwa na maradhi ya Utahira, serikali ikaingilia kati na mkono wake mrefu, ikapiga marufuku kufanyika shughuli yoyote ikidai inatafuta suluhisho” aliongea Mzee Chogo na kumuangalia tena Gotwa aliyemakinika na simulizi akionekana kuguswa sana.

“Unafikiri kilitokea nini...watu wenye pesa zao walianza kutupa taka usiku na badae mchana peupe mwisho ikawa kila mwenye taka anapeleka vitisho vikawekwa na mabango ya usitupe taka hapa! lakini wapi sheria iliwekwa li ivunjwe kibao kikang’olewa na kutupiliwa mbali ndo mpaka leo” alimaliza Mzee Chogo “Haya na leo nini umejifunza mjukuu wangu kutokana na simulizi hii” aliongea Mzee Chogo, Gotwa akafikiri kidogo kisha akanyanyua kichwa chake

“Mengi tu babu, moja ni Haki za binadamu toka somo la uraia serikali imewazurumu walemavu na Mfanyabiashara, na pili ni kuusu uchafu ulioanza kidogo na kuwa mwingi kwa hiyo ni kama ugonjwa unavyo anza na kusambaa pale tu usipochukuliwa hatua hiyo ni kutoka somo la biolojia na…” Mzee Chogo alishtuka na kumtazama vizuri Gotwa liyekuwa bize akiongea “Uchafu ule ulianza kutupwa na mmoja baadae wengine wakaiga, watu wanaweza iga kufanya jambo zuri au baya toka kwa mtu au watu wachache na pia babu..”
Gotwa akafinya macho yake akionekana kuendelea kufikiri, mara akaongea “Lakini babu, kwanini wale watu wanaweza kuishi maeneo yale”

Mzee Chogo akamtazama kwa muda na kuongea “Mjukuu wangu ni kwa sababu hakuna anaye jali, lawama zote zimetupiwa kwa wakazi wa Kivumbi yaani kwa kudai kuwa wao ndio chanzo cha umwagaji wa taka baada ya kukakazwa kuendesha michezo sasa hawana pa kwenda na hakuna anaye jali” Gotwaa aliguna na kuonekaan kutoridhika “Sasa kwani hawana viongozi babu?” aliuliza wakati huo Mzee Chogo akimtazama Nkole aliyesimama mbali kidogo muda akiwatazama “Vipi karibu naona umesimama ukitufatilia, umetoka wapi?” aliongea tena Mzee Chogo akimuangalia Nkole “Unamdekeza sana huyo mjukuu wako sizani kama yatamfaa si wakati wake huu kuambiwa mambo kama hayo, Gotwa haya twende ukalale kesho safari” Gotwa akashangaa na kumbukumbu ya ahadi yake na Zora ikampitia akilini mwake “Lakini baba si…” kabal hajamaliza Baba Gotwa akamkatisha “Hakuna cha lakini nimemaliza...” aliongea baba Gotwa hasira ikiwa machoni na kumshika mkono akimnyanyua hima hima hao wakaingia ndani “Mtoto wa nyoka ni nyoka tu hawezi kuwa Kenge!” aliongea mzee Chogo na kutabasamu. “Huyu mtoto!!..Mhh!” alisema tena huku macho kayatoa akitafakari mambo.

Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

Mtunzi Akida Siri Rambao
Contact: 0658328596
Email akidasiri@gmail.com

MSIMU 1

Sehemu 1 J

Ilipoishiaa....
Hakuna cha lakini nimemaliza...” aliongea baba Gotwa hasira ikiwa machoni na kumshika mkono akimnyanyua hima hima hao wakaingia ndani “Mtoto wa nyoka ni nyoka tu hawezi kuwa Kenge!” aliongea mzee Chogo na kutabasamu. “Huyu mtoto!!..Mhh!” alisema tena huku macho kayatoa akitafakari mambo.

Tuendelee...

UGHAIBUNIMASHARIKI YA NCHI YA CANON

“Unajua siamini macho yangu! yeye ni nani kiasi cha kutushika ndevu kiasi hiki, nani aliacha upenyo? Na ni nani anaye mpa kiburi kiasi hiki!?” aliongea bwana huyo mwenye miwani kubwa iliyoenea uso mzima vimacho vidogo dogo mashavu makubwa pua ya mchongoko domo kalikunja kwa juu akipitisha macho kama mshale wa saa, hasira nyingi! “Uhhhhhh!” alizishusha pumzi nzito zilizotetemesha karatasi karibu yake akainyoosha shingo yake nene huku akielegeza tai iliyokuwa ikimpa tabu.

Tai ya zambarau ikishereheshwa na mistari myepesi ya rangi ya maloni iliyokata ubavu wake na vidoti doti vyeupe vikipita katikati yake, Imeoshikizwa shingoni ndani ya suti ya gaharama rangi ya samawati michirizi meusi ikipita kwenye kola na mwishoni mwa mikono ikiongeza mvuto kweli kweli.

Watu kimya! Watu macho chini wazi wakiogopa kwa namna anavotisha bwana huyo aliyejawa na chuki akishambulia jukwaa huku sehemu za chini ya macho yake ikicheza cheza kwa hasira iliyotukuka “Nani anaweza kuniambia ilikuwaje! na amejuaje kama sio bwana Nasemwa katoboa ngarawa” aliongea tena bwana huyo kisha macho yake makali yakamgandia kijana wa makamo rangi mfanowe maji ya kunde katikati ya watu weupe “Balozi Ton unahusika kwenye hili?” alisema tena akimkazia macho,. Ton alisikia lakini alijiona kama si yeye azungumziwaye. Alianza pepeso huku na kule hakuwa na bahati aliishia kukutana na macho kumi na nane yakimtazama yakisema “tuambie Ton!” Aibu usoni mwake akavunga, akajiweka sawa kwa kuvuta kikoti chake kilicho mchonga mwili akanyanyuka “Samahani sana, ni makosa yangu Uniue ukitaka lakini kabla ya hayo kwaz hisani yako…” alitupia dubwasha lililoandikwa akalinyakua “…lakini sijakuja mikono mitupu Mac aliongea huku akitupia macho karabrasha iliyo mikononi mwake kwa sekunde kazaaa “Nikweli Nkole anamtu anamsaidia tena ni mtu mkubwa sana sizani kama mtaamini lakini naomba kuwasilisha” aliongea huku akigeuza kalabrasha. Sasa macho ya wajumbe wote yalikuwa kwa Mac J.
“Endelea Ton…” Mac J aliongea kwa sauti yake ndogo ya upole iliyopingana na sura yake chachu yenye hasira za wazi.

Ton akaanza kutoa makaratasi zilizo na Orodha kama si orodha mtiririko wa jambo Fulani akabaki kayashika. Haikuchukua muda mmoja kati ya watatu waliokuwa wamesimama muda wote masikioni wakiwa na vitu vya kupachikwa na miwani zao zilizo fanana na suti zao nyeusi alitoka aliposimama kama sanamu na kuchukua makaratasi hayo na kuyafikisha mezani mwa Mac J “Mac J! mazungumzo yote yaliyomo humo ni ya kimafumbo sana baina ya barua pepe ya Nkole pamoja na Rais wa Zhongo Dr. Mario Mataro lakini haikuwa rahisi sio rahisi haipo rahisi si maneno rahisi kabisa” aliongea Ton akimaanisha kwa kuyatoa macho kiasi cha watu wote kumgeukia Mac J akiendelea kukodolea makaratasi yake kung’amua kitu “…Ton unawezaje kusema Dr. Mario ni mshirika wa Nkole? Jaribu kutushawishi kabla hatuja ingia kwenye dhana ya moja kwa moja” aliongea Mac J.
Ton wazi swali likamkalia vibaya akatizama chini kwa sekunde akifinya finya macho yake, wazi mawazoni ajibu nini?! mara akatabasamu

“Mac J! si kawaida ya mtu kuwasiliana na mtu mwengine kwa njia kama hiyo bila ya kuwa na sababu ya siri, tena kwa muda wa aina moja tu!? wazi inaonekana ni watu walio kuwa na siri kati yao, wanafichiana Siri teyari namtilia mashaka Mh. Rais Dr. Mario Mataro kwanini awasiliane na Nkole kwa namna hiyo, na pia inatupa picha nyingine huwenda Nkole si mtu waz kawaida kama wengi wajuavyo inawezekana pia ni mtu mwenye kikundi Fulani kinachoendesha mikakati Fulani tusio ijua kama Mapinduzi hivi, nani anajua?!” aliongea Ton huku akiwatazama wajumbe wenzake wakiwa wametulia wakisikiliza kwa makini, akaendelea

“…ninaomba atafutwe mchambuzi hodari mwenye uwezo mkubwa wa kufumbua mafumbo ili atupe maana halisi ya mafumbo hayo yaliyotumika kuwasiliana baina yao” aliongea Nkole na kukaa, kimya kikatawala huku Mac J akiyatazama maneno yaliyomo katika makaratasi mkononi mwake. “Okay sawa, siwezi pinga lakini kwa hali ile Nkole awe na urafiki na Mataro sijui…sasa Ton kipindi tukiendelea kutafuta maana ya maneno hayo naomba kesho upande ndege na urudi Nchini Zhongo fika na utafute taarifa zote za Nkole na udhaifu wake kiasi cha pesa kitaingizwa kwenye akaunti yako mapema jioni hii, ni lazima tujue udhaifu wake upo wapi kumbuka hilo” Mac J akageuza shingo na kuwatazama watu wanao muangalia huku akikusanya viganja vya mikono yake na kuongea “…wajumbe tukutane kesho mapema asubuhi. January na Kennedy tuoanene tuongee kidogo”


Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

Mtunzi Akida Siri Rambao

Contact: 0658328596

Emailakidasiri@gmail.com

MSIMU 1

SEHEMU 2 A

Ilipoishia...

Mac J akageuza shingo na kuwatazama watu wanao muangalia huku akikusanya viganja vya mikono yake na kuongea “…wajumbe tukutane kesho mapema asubuhi. January na Kennedy tuoanene tuongee kidogo”

Tuendelee...

SEHEMU YA 2 A

NCHINI ZHONGO
KITUO CHA MABASI - KILIMANI - WILAYANI CHOZI
Mapema asubuhi vurumai zikiendelea kelele mtindo mmoja, heka heka pilika pilika, mziki mwingi, honi za magari yanayoingia na yanayotoka watu wakizoza na kuzozeana, wakisema na kusemana hakuna masikilizano kila mtu na lake katika mihangaiko ya riziki na usafiri. “Haya hakikisheni kila mmoja yumo katika siti iliyo katika tiketi yake, sasa hivi chuma kinaacha mji” bwana mmoja mwenye kitambi kilichomzidi alikuwa kasimama akiwatazama abiria wake mkononi ameshikilia kitabu kikubwa na kalamu akaanza kuandika andika kichwani balaghashia iliyochuja ubora kwa mstai wa nongo nyeusi kuzunguka kofia. Hakuchukua muda tangu kutia neno akiwa kajiiegemeza kwenye moja ya chuma, basi likatiwa funguo safari imewadia! dereva teyari kitini akivuta mafutaa na kuyaachia kwa sifaaa! Wapiga debe wauza mikate na juisi wakapokea kelele hizo kwa shangwe za makelele na miruzi.

Dereva nae hakuwa nyuma akaongeza sifa na utundu kunogesha kuzikonga nyoyo zao akabonyeza batani moja kushotoni mwa usukani mlio wa tumbuizo ukafatia “TALAA TALAA LILOOOO LILOOOOOOO OIIIIIIIIII!” ni kama ilikuwa ni kitu kinacho subiriwa na wapiga debe wakaziachia kelele za furahaaa “Oyyyyyooooo…weweeeee…chuma hichooo”

kweli zilikongwa roho zao abiria walibaki kucheka tu kwa namna ilivyokuwa, Raha mwenyewe! ilikuwa furaha miongoni mwao. Gari hilo likafata muelekeo kutoka katika kituo hicho cha mabasi ya mikoani na kuingia barabarani nyuma yake kwenye bamba kubwa yakisomeka maneno “Unaota we mdada! Unaota!” hiyoo safari ya Nyatumbu. Wakati wote huo Nkole alikuwa akiminyana kuweka vizuri begi lake lililokaa vibaya katika penyo iliyoshonana na mabegi ya abiria wengine akajihimu kwa kutumia nguvu nyingi kadri na kadri hatimaye akafanikiwa “Hhhh!!” akajituliza pahala pake bila kutia neno.

Kwa kuibia Gotwa alimtazama Babie aliyechuna chunu uso ukiwa mgumu kuashiria hasira za wazi na mchanganyiko wa mawazo. Muda uliendelea kuyoyoma huku basi likiacha mji wa Chozi kwa mwendo usiotamanika lakini hakuna aliye tia neno wengi wao walikuwa wakikodolea sinema ya Majuto toka nchi ya mashariki akiwavunja mbavu, wengine mazungumzoni, wengine usingizini na walio kuwa wapo wapo tu hawakukosekana.
Gotwa yeye alikuwa yupoyupo tu akipeleka shingo huku na kule mashaka yakiwa usoni, kama kuku mwenye kutaka kutaga, aliendelea kumtupia macho ya wizi wizi babie yu kimya! si kawaida ya baba yake! naye akitamani kumsemesha na kubaki kuyafinya finya macho yake.

Ataanzia wapi? Hilo ndilo swali lililoukabiri akili yake “Hivi nikwambie mara ngapi mtoto wewe unisikie?!…” sauti hiyo ilimtoa Gotwa mawazoni na kumtazama baba yake aliiye yatoa macho yake makubwa kumshambulia, Gotwa hakustahimili akaya kwepesha macho yake. “Nilishakwambia, lakini ni kama una baba mwengine…hutaki kuelewa kabisa” alijikuta Baba Gotwa akiongea kwa sauti hadi abiria wengine kumshanga. Kwa aibu akavunga na kujituliza akiangalia nje kupitia kioo bado akionekana yu mawazoni.
Mara basi ikapunguza mwendo na kusimama pembezoni mwa barabara. Wengi waliacha ya kuwahusu wakanyanyua shingo zao na kugeuza nyuso kutazama huku na kule. Watu wakaanza kuna nini… kuna nini? Mbona imesimama…. mbona hakuna abiria…au imeharibika?” kila aliyejaaliwa alisema


Itaendeleaa...
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

MSIMU 1

Sehemu 2 B

Tuendelee...

Mara basi ikapunguza mwendo na kusimama pembezoni mwa barabara.

Wengi waliacha ya kuwahusu wakanyanyua shingo zao na kugeuza nyuso kutazama huku na kule. Watu wakaanza kuna nini… kuna nini? Mbona imesimama…. mbona hakuna abiria…au imeharibika?” kila aliyejaaliwa alisema la kwake wengine wakibaki kunong’onezana huku shingo zikiwa ndefu kuchungulia madirishani. “Ni askari…” bwana mmoja alisikika akisema na watu kwa mkupuo wakatazama kumshuhudia sikioni simu malumu nyuma akifatiwa na mwanamama aliyezisuka nywele zake msuko wa kwenda kilioni nywele tatu. Konda akaonekana kushuka na mara Dereva nae akafatia.

Muda ukayoyoma, gari ikazimwa. “Mbona wanatuweka muda mrefu si awape tu hela wanayoitaka tuondoke zetu” mzee mmoja wa makamo kushotoni mwa Mkono wa Gotwa aliongea na kuonekana kumvutia sana Gotwa kiasi cha kumtazama kwa makini mzee huyo shingo akiinyanyua kutazama mbele “Ampe tu?! Bila kosa la maana unafikiri hela ni rahisi kiasi hicho, unazo zaz kutosha Babuu?...” akamtazama jirani yake huyo kwa jicho la shangazo “… kama sina kosa lenye kuthibitika sitoi na popote wanipeleke” mama huyo aliyatapikaz maneno tena akibinua mdomo juu akimaanisha alichokisema.

“Sasa vipi kuhusu sisi abiria zako ungetusubirisha mpaka saa ngapi? Hao watu huwajui vizuri na hawakosi sababu, ili usizue mengine ni bora uwape kiasi kidogo uokoe nyingi na muda wako kwa kujifanya mjinga” aliongea huku akimtazama, watu walikuwa kimya baadhi wakionekana kuvutiwa na hayo mazungumzo. Mara mzozo ukasikika nje ya gari, watu roho zikawapasuka na kuhamishia masikio nje wengine wakisimama kuchungulia kwa dirisha “He! Maafande tena” watu kazaa walisema kwa mshtuko mkuu na kuwafanya wasiojua kujua kuwa kuna cha kukijua wakajikuta wakiwa na hamu ya kujua zaidi. Teyari gari mbili za polisi zilikuwa zimepaki mbele na nyuma ya Basi hilo la abiria, baadhi yao wakiwa na bunduki mikononi.

Gotwa akajikuta akigeuka nyuma, na kukutanisha macho na bwana mmoja mwenye hofu kubwa wasiwasi mwingi mkononi ameshikilia begi jeusi asilotaka kuliachia kwa namna alivyolikumbatia barabara akamtazama Gotwa kwa macho ya Ole wako “Mhh” Gotwa aliguna na kugeuza shingo macho mbele akameza fundo la mate lililopita kwa tabu kooni. Akageuka kumtazama baba yake ambaye muda huo naye alionekana kuwa na wasiwasi kama abiria wengine. Wazi Gotwa alionekana akitamani kumwambia baba yake juu ya tukio hilo lakini akaishia kusitasita.
“Baba kuna mtu nyuma anaonekana kutisha sana”, Gotwa alijikuta akipenyeza sauti yake baada ya kumshtua baba yake na kiwiko cha mkono,

Nkole akamtazama Gotwa kwa muda akapuuza bila kutia neno. “Nafanyaje sasa…” alijisemea Gowa kwa sauti ya kunong’ona kabla hajapata jibu la swali lake. “Nawaomba kwa utulivu abiria wote mtoke ndani ya basi…” sauti hiyo ilimtoa Gotwa mawazoni na kupelekea yeye na abiria wengine kutega masikio huku wakinyanyua nyuso zao kumtazama mzungumzaji, alikuwa ni Polisi ofisa ndani ya mavazi ya kipolisi mbele yao “Afande Mbonde?!” Nkole alijikuta akitahamaki kwa sauti ya chini mdomo wazi akimshangaa macho yao yakakutana Afande Mbonde akatabasamu na kuendelea “…maana hili basi lenu ni bovu haliwezi maliza safari yake na hapo mbele kuna msitu mkubwa mtakosa msaada, kuhusu mizigo yenu msiwe na mashaka ipo timu maalumu itahusika na ushushaji kwa usalama na usumbufu” alimaliza kuongea akashuka sentensi hiyo ilikuwa tata kwa watu wengi hasa kwa Nkole “Kuna nini? ni kweli basi ni bovu?” mara moja zoezi likaanza huku watu wakionekana kutokupendezwa sura zikiwa na maswali.


Watu wakaendelea kutoka na kutoka mpaka wakakaribia kuisha, Nkole na mwanawe nao wakafata huku Nkole akipeleka macho huku na kule kabla hajapiga hatua zaidi, Afande Mbonde akamshika mkono na kumsogeza pembeni “Mbonde kuna nini mbona sio kawaida” aliongea Nkole mkono wake ukiwa umeshikwa na Mbonde “Mambo sio shwari kiongozi tupo hapa kuokoa maisha yako” “Maisha yangu?...” Nkole alishtuka jicho likamtoka akamtazama mwanawe ambaye alikuwa bize kanyanyua shingo akifatilia watu wanaoshuka kwenye basi, Nkole alionekana kuwaza kidogo akashika kiuno na kubana meno yake, kisha akamtazama Mbonde “Gari ipo tayari kukuchukua wewe na mwanao, nitawapeleka mimi mwenyewe hatuna muda"



Kunani Kwaniii???
 
KISANGA!!!

(Hisia za Mrithi)

MSIMU 1

Sehemu 2 B

Tuendelee...

Mara basi ikapunguza mwendo na kusimama pembezoni mwa barabara.

Wengi waliacha ya kuwahusu wakanyanyua shingo zao na kugeuza nyuso kutazama huku na kule. Watu wakaanza kuna nini… kuna nini? Mbona imesimama…. mbona hakuna abiria…au imeharibika?” kila aliyejaaliwa alisema la kwake wengine wakibaki kunong’onezana huku shingo zikiwa ndefu kuchungulia madirishani. “Ni askari…” bwana mmoja alisikika akisema na watu kwa mkupuo wakatazama kumshuhudia sikioni simu malumu nyuma akifatiwa na mwanamama aliyezisuka nywele zake msuko wa kwenda kilioni nywele tatu. Konda akaonekana kushuka na mara Dereva nae akafatia.

Muda ukayoyoma, gari ikazimwa. “Mbona wanatuweka muda mrefu si awape tu hela wanayoitaka tuondoke zetu” mzee mmoja wa makamo kushotoni mwa Mkono wa Gotwa aliongea na kuonekana kumvutia sana Gotwa kiasi cha kumtazama kwa makini mzee huyo shingo akiinyanyua kutazama mbele “Ampe tu?! Bila kosa la maana unafikiri hela ni rahisi kiasi hicho, unazo zaz kutosha Babuu?...” akamtazama jirani yake huyo kwa jicho la shangazo “… kama sina kosa lenye kuthibitika sitoi na popote wanipeleke” mama huyo aliyatapikaz maneno tena akibinua mdomo juu akimaanisha alichokisema.

“Sasa vipi kuhusu sisi abiria zako ungetusubirisha mpaka saa ngapi? Hao watu huwajui vizuri na hawakosi sababu, ili usizue mengine ni bora uwape kiasi kidogo uokoe nyingi na muda wako kwa kujifanya mjinga” aliongea huku akimtazama, watu walikuwa kimya baadhi wakionekana kuvutiwa na hayo mazungumzo. Mara mzozo ukasikika nje ya gari, watu roho zikawapasuka na kuhamishia masikio nje wengine wakisimama kuchungulia kwa dirisha “He! Maafande tena” watu kazaa walisema kwa mshtuko mkuu na kuwafanya wasiojua kujua kuwa kuna cha kukijua wakajikuta wakiwa na hamu ya kujua zaidi. Teyari gari mbili za polisi zilikuwa zimepaki mbele na nyuma ya Basi hilo la abiria, baadhi yao wakiwa na bunduki mikononi.

Gotwa akajikuta akigeuka nyuma, na kukutanisha macho na bwana mmoja mwenye hofu kubwa wasiwasi mwingi mkononi ameshikilia begi jeusi asilotaka kuliachia kwa namna alivyolikumbatia barabara akamtazama Gotwa kwa macho ya Ole wako “Mhh” Gotwa aliguna na kugeuza shingo macho mbele akameza fundo la mate lililopita kwa tabu kooni. Akageuka kumtazama baba yake ambaye muda huo naye alionekana kuwa na wasiwasi kama abiria wengine. Wazi Gotwa alionekana akitamani kumwambia baba yake juu ya tukio hilo lakini akaishia kusitasita.
“Baba kuna mtu nyuma anaonekana kutisha sana”, Gotwa alijikuta akipenyeza sauti yake baada ya kumshtua baba yake na kiwiko cha mkono,

Nkole akamtazama Gotwa kwa muda akapuuza bila kutia neno. “Nafanyaje sasa…” alijisemea Gowa kwa sauti ya kunong’ona kabla hajapata jibu la swali lake. “Nawaomba kwa utulivu abiria wote mtoke ndani ya basi…” sauti hiyo ilimtoa Gotwa mawazoni na kupelekea yeye na abiria wengine kutega masikio huku wakinyanyua nyuso zao kumtazama mzungumzaji, alikuwa ni Polisi ofisa ndani ya mavazi ya kipolisi mbele yao “Afande Mbonde?!” Nkole alijikuta akitahamaki kwa sauti ya chini mdomo wazi akimshangaa macho yao yakakutana Afande Mbonde akatabasamu na kuendelea “…maana hili basi lenu ni bovu haliwezi maliza safari yake na hapo mbele kuna msitu mkubwa mtakosa msaada, kuhusu mizigo yenu msiwe na mashaka ipo timu maalumu itahusika na ushushaji kwa usalama na usumbufu” alimaliza kuongea akashuka sentensi hiyo ilikuwa tata kwa watu wengi hasa kwa Nkole “Kuna nini? ni kweli basi ni bovu?” mara moja zoezi likaanza huku watu wakionekana kutokupendezwa sura zikiwa na maswali.


Watu wakaendelea kutoka na kutoka mpaka wakakaribia kuisha, Nkole na mwanawe nao wakafata huku Nkole akipeleka macho huku na kule kabla hajapiga hatua zaidi, Afande Mbonde akamshika mkono na kumsogeza pembeni “Mbonde kuna nini mbona sio kawaida” aliongea Nkole mkono wake ukiwa umeshikwa na Mbonde “Mambo sio shwari kiongozi tupo hapa kuokoa maisha yako” “Maisha yangu?...” Nkole alishtuka jicho likamtoka akamtazama mwanawe ambaye alikuwa bize kanyanyua shingo akifatilia watu wanaoshuka kwenye basi, Nkole alionekana kuwaza kidogo akashika kiuno na kubana meno yake, kisha akamtazama Mbonde “Gari ipo tayari kukuchukua wewe na mwanao, nitawapeleka mimi mwenyewe hatuna muda"



Kunani Kwaniii???
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom