Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Shunie

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2016
Posts
157,076
Reaction score
463,978
Mtunzi Ally Katalambula
Sehemu ya 1

“MWANAUME kutokwa na machozi, iwe kwa sababu ya maumivu au majonzi, si kitu kinachokubalika katika ukoo na kabila letu.

Ukiona mwanaume analia ujue ana roho ya kike. ukilia, huna sababu ya kuvaa kaptula ama surual,vaa gauni au sketi, machozi ya mwanaume yanatakiwa kuwa adimu sana, mwanaume kutokwa machozi ni udhaifu wa kiwango cha mwisho.

” Ni maneno ya marehemu baba yangu, niliyakumbuka nikiwa katika madhila makubwa sana, donge zito lilikuwa limenikaba kooni, uso wangu ulikuwa umechafuka kwa mikunjo iliyotokana na na hasira iliyochanganyikana na simanzi kubwa.

Nilikuwa nimejiinamia mkono ukiwa shavuni, maungo ya mwili wangu yalikuwa yakivuja jasho kama mgonjwa wa homa kali, macho yalikuwa mekundu kama mtu aliyeingiliwa na pilipili

machoni, kila wakati nilikuwa nikiachia msonyo mdogo, huku nafsi yangu ikijilaumu yenyewe. Kwa mara nyingine, nilinyakua simu yangu ya mkononi iliyokuwa kando na kupiga namba fulani. Namba niliyokuwa naipiga, nilikwisha ipiga kabla, zaidi ya mara kumi na moja bila mafanikio. Simu ilipokuwa sikioni, mapigo yangu ya moyo yalikuwa yakinienda kasi kuliko kawaida. japokuwa haikuwa mara yakwanza kuipiga ile namba, ila safari hii nilikuwa na presha kubwa.

Baada ya muda fulani kupita, majibu kupitia simu ile nikayapata: “…namba ya simu ya mteja unayempigia haipatikani kwa sasa...” Nilikata simu baada ya kupokea ujumbe ule.

Donge zito likaendelea kunikaba kooni, wivu na hasira vikaendelea kutanda moyoni mwangu, kwa mara nyingine nilijikuta nikisaliti ujasiri niliofundwa na baba yangu. Machozi yakanibubujika!.

“Kwanini unanifanyia hivi Nasra...kwa nini...Iweje jambo hili lifanywe na wewe!. haya ndio malipo ya pendo langu? Kosa langu ni kukupenda si ndivyo....nini maana yake hii sasa….Eeh!!..” nilinong’ona kwa fadhaa huku machozi yakinitoka.

Kwa mujibu wa saa yangu ya mkononi ilikuwa ni saa sita na nusu usiku, nilichukua pakiti ya sigara na kutoa mche mmoja na kuupachika mdomoni, nikawasha kwa kiberiti cha gesi ambacho kilitoa mlipuko mdogo wa moto, nikaunguza ile sehemu mbele ya sigara.
 
Sehemu ya 2

Nikavuta kwa mkupuo mmoja na kutoa moshi mwingi kupitia tundu za pua na mdomo, kisha nikatoa pumzi ndefu huku kifua changu kikipanda juu na kurudi chini..

Akili yangu ilinieleza wazi kuwa mke wangu Nasra hakuwa mtu sahihi kwangu, lakini moyo wangu ulinionya kutofanya kitendo chochote kitakacho pelekea kuwa mbali na kiumbe yule mrembo.

Haja ya moyo wangu ikazidi matwaka ya utashi wangu, hali ile ikanifanya nizidi kuangamia nafsini, nikawa mtu wa kujilaumu na kujipinga mimi mwenyewe.
Lakini pamoja na mgogoro huo wa ndani kwa ndani uliokuwa ukinivuruga hata afya ya mwili wangu bado nafsi yangu ilijiapiza kufa Kijerumani na tai shingoni!!!!. Mambo yalianza hivi:
 
Sehemu ya 3

Jina langu halisi naitwa Faraji Hussein Mpangalala, ni mzaliwa wa Kigoma kijiji cha Nguruka, ingawa kwa sasa naishi katika Jiji la Dar es Salam huko maeneo ya Kinondoni Studio, ni mtoto mwisho kati ya watatu kutoka kwa mzee Mpangalala, mbele yangu wakiwa ni dada zangu wawili Khadija na Shadia.

Dada zangu hao, wote walikwisha olewa miaka mingi iliyopita, baada tu ya kumaliza kidato cha nne na kupata matokeo ambayo hayakuwawezesha kuendelea na masomo. Naweza nikasema, katika familia yetu, ni mimi pekee ambaye wazazi wangu walikuwa na matumaini makubwa ya kuja kuwa kiongozi wa familia siku za usoni.

Hii ni kutokana na kwamba, kwanza nilikuwa mtoto wa kiume lakini pia nilikuwa ndiye mtu msomi na mwenye utashi mkubwa kuliko mwingine yeyote.

Nikiwa na umri wa miaka 27 baada ya kumaliza shahada yangu ya kwanza ya ualimu pale mlimani, niliajiliwa ofisi ya mkurugenzi wa manispaa ya Temeke Jiji Dar, kama mratibu wa elimu wa manispaa hiyo. Mwaka 2004 rasmi niliyaanza maisha ya kujitegemea, nikiwa kijana mwenye ndoto kubwa za mafanikio mbele yangu, mshahara mzuri pamoja na malupulupu ya hapa na pale yaliniweka katika daraja la juu sana kimaisha.

Nilikuwa nimeanzisha miladi mingi ya biashara hapa mjini ambayo iliniingizia kiasi cha kikubwa cha fedha, katika umri wa miaka 27 nilikuwa nina miliki gari zuri la kifahali, nyumba nzuri ya kisasa pamoja na viwanja kibao katika maeneo mbalimbali ndani ya jiji la Dar es Salam.

Kimsingi nilishi maisha ambayo kijana yeyote yule angapenda kuwa na maisha kama yale. Ni katika kipindi hicho cha ujana wangu, ndipo nilipoanza kupata shinikizo kubwa kutoka kwa wazazi wangu kuhusu kuoa.

Kwangu mimi wakati huo, ulikuwa ni wakati sahihi kabisa, hasa ukizingatia nilikuwa na kipato kikubwa, tena cha uhakika, lakini tatizo lilikuwa ni moja tu. Sikumwona mwanamke sahihi wa kuwa mke wangu.

Sio kwamba katika jiji la Dar nilikuwa sikutani na warembo. Lahasha!. Warembo niliwaona wengi, na baadhi yao nilishawahi kupata huduma ya penzi lao,
 
Sehemu ya 4

Na wengi walikuwa wakinitaka mimi. Si kwa kuwa labda nilikuwa mvulana mwenye mvuto, Laa!

Isipokuwa nilikuwa kijana mwenye fedha na mafanikio makubwa…Kwao fedha ilikuwa ni zaidi ya upendo, hata hao niliowahi kugalagala nao kitandani walishia kuniganda wakitaka ndoa, lakini kwa kuwa nilikuwa nikizitambua vema tabia zao.

Niliwapuuza. “Mwanangu kama tatizo ni hilo, tupe ruksa sisi tukutafutie mwanamke wa kuoa”

Siku moja mama yangu alinieleza, baada ya kumpa sababu za kwa nini nakawia kuoa. “Siyo jambo baya, wala sio jambo zuri, lakini Je?

Moyo wangu utamridhia mwanamke mtakaye nitafutia?” nilimuuliza. “Naamini hatuwezi kukuangusha.” Sikuwa na pingamizi juu ya ombi hilo, niliwakubalia wazazi wangu wanitafutie mchumba.

Hazikuzidi wiki mbili, nilipigiwa simu na baba na kunieleza kuwa wamekwisha mpata mchumba na kilichokuwa kimebakia ni kumposa.

“Jina lake?” niliuliza kwa kiherehere “Anaitwa Nasra Mfaume” “ Kabila gani?” “Ununataka kutambika?” baba naye aliniuliza kwa utani.

“Hapana nataka kujua tu.” “Ni mpemba, mchanganyiko wa Kiajemi na Kibantu, mzee wake ambaye ni marehemu sasa alikuwa mwenyeji wa huko Visiwani Pemba ila ndio hivyo, alilowea bara miaka mingi.

Kwahiyo ni wa huku huku kwetu” baba alisema. Nilishusha pumzi fupi huku taswira ya watoto wazuri wa Kipemba ikijengeka kichwani mwangu.

“Kwahiyo mipango iliyobakia ni kulipa mahari kisha ndoa tu,” baba akaendelea kueleza.

“Unaweza kunitumia picha yake kwa njia ya mtandao?” “Bila shaka mwanangu” “Basi nitumie picha ya huyo mchumba sasa hivi”nilisema kwa kiherehere huku nikikata simu kusubiri picha ya huyo mwanamke.

Nilitumiwa picha ya huyo mchumba kwa njia ya mtandao, haraka niliipakua kwenye simu huku shauku ikiwa kubwa.

Muda mfupi badaye, nilikuwa nikitizama picha ya mwanamwali mrembo. Niliachia tabasamu pana huku nikiendelea kusaili mwonekano wa kiumbe yule.

Alikuwa ni msichana wa kati ya miaka 20 ama 22, alikuwa kigori chotara aliyeumbwa akaumbika, katika ile picha, alikuwa kwenye mavazi ya heshima huku uso wake ukionesha kama mtu asiye na hatia yoyote maishani.

Nafsi yangu ilikiri nilikuwa natarajia kuwa na mke mrembo sana siku za usoni.
 
SEHEMU YA 5

Nafsi yangu ilikiri nilikuwa natarajia kuwa na mke mrembo sana siku za usoni. Kwa mara nyingine, nilijisikia furaha kwakuwa mvulana mwenye mika 27 tu, ambaye nilikuwa nakaribia kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha yangu.

Siku chache badaye, mahari ililipwa na mipango ya ndoa ikaanza kufanyika, kwakuwa nilikuwa bize sana na masuala ya kazi, niliwachia wazazi wangu pamoja na ndugu kuendelea na mchakato wote wa ndoa huku mimi nikingojea tu kuletewa mke.

Hatimaye siku iliwadia, ndoa ikafungiwa Kigoma, huku mimi nikiwalishwa na binamu yangu aitwaye Mrisho.

“Unatakiwa kumpokea mkeo stesheni” nilijulishwa baada ya mambo yote kukamilika. “Wanakuja kwa treni?” “Ndio” “Wanakuja wangapi?”

“Wapo watatu, mkeo Nasra, mjomba wako Majeed na mdogo wake na mkeo aitwaye Aisha.” “Kwanini msingesema niwatumie tiketi za ndege, usafiri wa treni ni tabu sana siku hizi…”

“Unahamu na mkeo baba eeh!” mama akaniuliza kwa utani. “Sana” “Basi usijali, kesho kutwa nenda ukampokee stesheni” mama alisema kisha akanipa usia mfupi wa namna nzuri ya kuishi na mke wangu.

Siku ya Ijumaa saa saa kumi na mbili jioni, nilikuwa posta eneo la stesheni nikingoja ugeni kutoka Kigoma.

Moyo wangu ulikuwa ukinidunda huku viganja vya mikono vikiloa jasho, sikujua kama hali hiyo ilitokana na hamu ya kuhitaji kumwona msichana yule chotara ama laa!.

Nusu saa badaye, treni iliwasiri, nikajiondoa katika gari langu nililokuwa nimelipaki katika kituo cha daladala cha stesheni na kusogea eneo la kutokea abiria katika jengo la Stesheni, macho yangu yalipepesa kwa kila abiria aliyetoka.

Nilisimama pale getini kwa muda mrefu hadi abiria wakaanza kupungua lakini sikuwaona wageni wangu. “watakuwa wapi?” nilijiuliza mkono mmoja ukiwa mfukoni huku mwingine nikiwa nimekamata lundo la funguo nililokuwa nikilitingishatigisha. “Faraji” sauti moja iliniita nyuma yangu.

Niligeuka haraka. Macho yangu yakakutana na watu watatu wakinitizama huku vinywa vyo vikiwa katika tabasamu pana.

“Wooh jamani ni ninyi!” nilisema kwa uchangamfu huku nikiwapokea mizigo wageni wale niliokuwa nikiwangojea. “Karibu sana jamani” “Ahsante Faraji za hapa?”
 
SEHEMU YA 6

“Hapa ni kwema, poleni na safari” “Tumekwisha poa shemeji” msichana mdogo aliyekuwa karibu na msichana mrembo na mtulivu alidakia huku uso wake ukiwa na tabasamu kubwa.

“Umejuaje kama huyu ndiye shemejio?” Mjomba Majeed akamuliza kwa sauti yenye kusuta katika hali ya maskhara. “Mke ataachaje kujua chake” binti yule mdogo akajibu kwa utani.

Wote tukacheka. “Huyu ndiye mkeo anaitwa Nasra Mfaume, na huyu ni mdogo wake, anaitwa Aisha…” Mjomba Majeed aliaanza kutoa utambulisho. “Nasra” mjomba aliita. “Abee mjomba” “Huyu ndiye mumeo, Faraji Hussein Mpangalala”

Mrembo yule alinikata jicho la wiziwizi kisha akanisalimia huku akinipa mkono. “Asalam aleykum” sauti itokeayo puani ikasikika ikapenya kwenye ubongo wangu na kuvuruga kabisa mwenendo ufanyaji kazi wa moyo wangu “Waleykum salama bibie hujambo?” nilimjibu huku nikiupokea ule mkono wake.

Picha ambayo nilitumiwa na baba yangu, haikuongopa hata kidogo. Urembo wa mke wangu ulikuwa vilevile.

Hata hivyo, baada ya kumtazama kwa makini zaidi nilibaini kuwa alikuwa na ziada moja juu ya urembo wake. Si kwa ile ngozi yake yake nyeupe, maana ile Ilikuwa ni ngozi ya kawaida ingawa ilimfanya imeremete na kushawishi kuigusa.

Wala Si lile tabasamu lake la mara kwa mara. Maaana hilo pia ni jambo la kawaida katika nyuso za wasichana wa kisasa na lingeweza kununuliwa kwa fedha tu iwapo mwenyewe angejali kujiunga na chuo kimojawapo cha usanii na kuhitimu.

Hali kadhalika, ziada hii haikutokana na macho yake maangavu, pua yake iliyochongoka, wala meno yake meupe yaliyojipanga kikamilifu kinywani mwake kama mistari miwili ya punje za mahindi kwenye kibunzi.

Alikuwa na ziada!

Lakini ziada hii ilikuwa ipi? nilijiuliza nikimtizama kwa hila Nasra Mfaume huku mkono nikiwa bado nimeukamata.

Nilimtekenya kwa siri kwenye kiganja chake nilichokuwa bado nimeking’anga’nia, tendo lile likamfanya anitizame, macho yetu yakagongana. Alishindwa kabisa kuhimili walau kwa sekunde mbili, alitizama chini lile tabasamu lake likigeuka kuwa katika sura nyingine.

Ni hapo nilipobaini ile ziada iliyonivuta katika sura na umbile la msichana huyu.

Aibu!

Alikuwa msichana mwenye aibu
 
SEHEMU YA 7

Nilimtekenya kwa siri kwenye kiganja chake nilichokuwa bado nimeking’anga’nia, tendo lile likamfanya anitizame, macho yetu yakagongana. Alishindwa kabisa kuhimili walau kwa sekunde mbili, alitizama chini lile tabasamu lake likigeuka kuwa katika sura nyingine.

Ni hapo nilipobaini ile ziada iliyonivuta katika sura na umbile la msichana huyu.

Aibu!

Alikuwa msichana mwenye aibu! Mmoja kati ya wasichana wachache kabisa duniani waliobakia na aibu. Wengi wao, toka walipoanza kuvaa suruali kama wanaume, kile kirusi kinachoitwa ‘aibu ’ kilitoroka zama za kale katika maumbile yao na hivyo kuwaacha wakavu kama wanaume.

Sifa zake hizo zikiwa zimepambwa kwa mavazi yenye heshima, sketi ndefu iliyovuka magoti na blauzi nyepesi iliyokifanya kifua chake kitoe picha ya uhai wa matiti yake. “Si…si..sija..sijambo,” alinijibu kwa kubabaika huku aibu yake ikiongezeka mara dufu.

“Karibuni sana,” nilisema huku nikiachia tabasamu. Tulielekea kwenye gari langu kisha safari ya kuelekea Kinondoni Studio ikaanza.

Lisaa limoja badaye, tuliwasili nyumbani kwangu, katika nyumba yangu kubwa ya kifahari, wageni wangu niliwapatia chumba kila mmoja na chake, ambapo niliwataka waoge na kubadilisha nguo ili kuchangamsha miili yao kabla ya kurudi mezani na kupata chakula cha usiku.
Mke wangu Nasra nilimwongoza hadi chumbani mwetu ambako pia nilimtaka aoge kabla ya kuungana na mjomba Majeed pamoja na shemeji Asha katika meza ya chakula.

“Faraji...” aliniita kwa sauti ya chini, uso wake ukionekana kuwa na jambo analotaka kunieleza. “Unasemaje mke wangu” akanitizama kisha akasema: “Nataka kuvua nguo” “Eeh, sawa vua tu.” “Unaweza kunipisha nibadili nguo?” mke wangu alisema huku uso wake ukionekana kujawa na haya.

Nilibaki nimeduwaa huku nikiwa sina jibu la kumpa, kwa mara nyingine nikabaini nilikuwa na mwanamke ambaye alikuwa na aibu nyingi.

Igawa awali nilivutiwa mno na hilo, lakini sikutaka tabia ya aibu kwa mke wangu ipite kiasi, kama ilivyokuwa wasaa ule. “Unanionea aibu?”nikamuuliza kwa sauti ya upole ilihali nikitambua hilo halikuwa swali bali jibu.
Alitikisa kichwa kukubali kwa
 
Sehemu ya 8

“Huna sababu ya kuwa na aibu, hasa unapokuwa mbele yangu, mimi ni mumeo upo kwenye maisha mapya, maisha ya kuwa kama ulivyozaliwa ukiwa ndani ya chumba hiki, maisha ya kuchezewa mwili wako vile nitakavyo jisikia.

Tegemea hayo kuanzia sasa,” nilizungumza nikiwa nimesimama sentimita chache mbele yake, wazungu wanasema ‘ziro distance’

Nasra alibaki ameinamisha kichwa chini, mikono akiwa ameikusanya pamoja na kusuguasugua viganja vyake.

Nilimtizama kiumbe yule kwa chati, nikaona uso wa mtu mshamba katika ulingo wa mapenzi, nikaendelea kujiuliza, Je? mrembo yule alikuwa bado mwanamwali, ambaye hajawahi kuguswa na mwanaume yeyote tangu azaliwe?

Kama ndivyo, basi nitakuwa nimelamba dume, nitakuwa nimepewa zawadi nzuri mno na wazee wangu nilijiwazia kimoyomoyo.

Nilipenyeza mikono kwa hila na kushika kiuno chake, akastuka kwa woga, hata hivyo hakuondoa mikono yangu! nikakipapasa kiuno chake chembamba, kiuno kilichoning’iniza makalio makubwa na mapaja yaliyonona, nikawa namwangalia chotara yule usoni huku nkitembeza viganja vyangu kwenye mzunguko wa kiuno chake.

Nasra alifumba macho yake, midomo yake akiwa ameiuma, aibu ilikuwa imevaa isivyo kifani. “Ngoja nikakoge,” akasema kwa kunong’ona. “Kuoga na nguo?”

“Nitavua.” “Acha nikuvue.” “Nitavua mwenyewe.” Alikwisha chelewa, kwani tayari nilikuwa nimekwisha fungua zipu ya sketi yake na kuivuta chini kwa nguvu. “Ayaaaa!!!” alibweka kwa fadhaa baada ya kubaki na kinguo cha ndani peke yake.

Nacho nikakishika kwa hila na kukiondoa mara moja.. “Aaagh!...aagh!!! oooii!! Jamani Faraji”akanung’unika
Akiwa amepandisha mguu mmoja kwa mwingine huku mkono wake mmoja ukiwa umeziba nyeti zake wakati ule wa pili akiwa amejiziba usoni kutoana na aibu, sasa alibaki ameduwaa kama sanamu.

Ile blauzi nyepesi aliyokuwa amevaa na kufanya kifua chake kitoe picha ya uhai wa matiti yake nayo nikaichojoa mauongoni, sasa nilikuwa nikimtizama mwanamke mrembo akiwa kama alivyozaliwa! Ndani ya chumba changu mwenyewe.

Nilianza kuhisi hali isiyo ya kawaida mwillini mwangu, mapigo ya moyo yakawa yanienda kasi, kitendo cha kuona maumbile ya mke wangu kwa kweli ilisababisha nipatwe na msukumo wa fulani usioelezeka
 
SEHEMU YA 9

Lisaa limoja badaye, shemeji yangu Asha alikuja kutuaga kuwa anajisikia usingizi hivyo anakwenda kupumzika.

Mimi na mjomba tukaendelea na mazungumzo, nusu saa badaye mjomba naye akahitaji kupumzika.

Tuliagana kisha naye akaelekea chumbani mwake, sikuwa na cha kusubiri pale sebuleni, nikajinyanyua na kwenda bwawani kwangu ili kumvua samaki wangu.

Nilipoigia tu chumbani, macho yangu yalitua kwa kiumbe aliyekuwa amejilaza kitandani huku akiwa amevalia ‘night dress’ nyepesi iliyoacha maungo yake yaharibu kabisa mfumo thabiti wa upumuaji wangu.

Alikuwa amezikusanya nywele zake ndefu na kuzifunga pamoja kwa kijibanio kidogo huku akiacha kamkia kadogo kuning’inia.

Sura nzuri ya kuvutia, iliniita. Kifua kilichobeba matiti mazuri, kilinisisimua. Na umbo lake la kuchora, lilinihamasisha.

Nilimsogelea pale kitandani huku nikiwa na nia moja tu.
KUFANYA mapenzi na mke wangu. lilikuwa ni hitaji langu kubwa wasaa ule.

Alikuwa amejilaza kifudifudi kanga nyepesi aliyokuwa ameivaa lubega ilikuwa ikitoa picha ya makalio yake yaliyokuwa yameumuka kama kichunguu.

Alipobaini kwamba nipo mbele yake, alijigeuza na kujikunyata kiubavu, aibu ya kisichana ikawa inajitengeneza machoni.

“Umeingia saa ngapi?” akaniuliza huku akiuma vidole.
“Muda tu.” “Safari ya treni ilinichochosha sana.”

“Pole.” “Ahsante, usingizi ulikuwa umenichukua.” “Pole mpenzi” nilimwambia, tabasamu likinitoka.
Nikawa nasaula nguo hadi nikawa mtupu, nikapanda kitandani, kisha nikajilaza kando yake.

“Huzimi taa?” Nasra aliniuliza kwa sauti ya chini.
“Unataka tufanye gizani?” nikamuuliza
“Sina maana hiyo Faraji?”
“Kumbe?”

“Siwezi kulala taa ikiwa inawaka,”mke wangu alisema, nikaendelea kumwona kama mgonjwa anayesumbuliwa mno na maradhi yaitwayo ‘haya’. “Mke wangu,” “Abee”

“Usiniogope”
Hakunijibu.
Nilishika waya wa swichi uliokuwa uking’inia kutokea darini, nikazima bulbu yenye mwanga mkali na kuwasha ile yenye mwanga hafifu wa rangi ya njano.

Nilipo yarejesha macho kwa mke wangu, nilimwona mithili ya malaika, kwa namna alivyokuwa akimeremeta katika mwanga wa rangi ya njano.

Mapigo ya moyo yalinienda kasi, nilishika kiuno chake nikatembeza kiganja changu polepole
 
SEHEMU 10

Joto lake likaongeza hisia za ajabu, wakati vidole vyangu vikihamia katikati ya mfereji wa uti wa mgongo na kutambaa kutokea juu hadi kwenye makalio ya chotara yule. Alishindwa kabisa kuizuia sauti isimtoke.

“Fa…Fa…Faraaahh…Jiiii!” Sikukoma. Vidole vyangu vikiwa vinafanya ziara pande zote za mwili wake, mdomo wangu niliusogeza kwenye matiti yake. Kisha nikawa nazimung’unya zile chuchu kama pipi.

Lilizuka balaa!. Nasra alikuwa akipiga kelele za ajabu sana. Ukubwa wa Kelele za mahaba, niliona zingeweza kumstua mjomba Majeed na shemeji Aisha.

Nilichofanya ni kufungulia redio sauti ya juu, ili sauti ya redio angalau imeza ukelele wa Nasra Mfaume.

“ Ngoja…ngoja kidogo,” Nasra alinisihi baada ya kuwa nimerudi kuendelea pale nilipoishia. “Kuna jambo ningependa nikueleze,”aliniambia “Jambo gani bibie?”
“Mwenzio sijawahi kufanya huu mchezo.”
“Acha masikhara.”

“Haki ya…..” “Tangu uzaliwe?”
“Ndio”
“Kwahiyo wewe ni bikira?”
“Kabisa.”

“Kama ni kweli nitakupenda maradufu,” nilimwambia. Uso wake ulikuwa umesawijika. “Kwahiyo unasemaje?” nikamuuliza.

“Naogopa…Utaniumiza!!!” “Huwezi kuumia”
“Kivipi?’
“…kwani unamiaka mingapi?”
“ 22” “Huwezi kuumia. Ushakuwa mkubwa, siwezi kukumiza mpenzi”
“Na ukiniumiza Je?”
“Nitandike kibao.”

Alitabasamu na mimi nikatabasamu. Nikamsogeza karibu, nikampa kinywa change, kisha tukaanza kunyonyana ndimi.

Mchuano ukaanza upya. Nilimwandaa kiasi cha haja. Sikutaka kabisa kumuumiza hasa ukizingatia siku hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kufanya tendo la ndoa maishani mwake.

Kwa kweli ndugu msomaji, usiku huo ni siku ambayo siwezi kuisahau maishani mwangu..

Penzi nililolipata kwa mke wangu ambaye mimi nilikuwa ndiye mwanaume wake wa kwanza, lilikuwa ni tamu pengine kuliko penzi nililowahi kupewa na mwanamke yeyote maishani.
*****
Asubuhi kulipokucha, nilikuwa wa kwanza kuamka, mionzi hafifu ya jua la asubuhi ambayo huwa inapenya chumbani kwangu kupitia dirishani. Iliniangazia .

Pembeni, mke wangu alikuwa bado akikoroma, saa ya ukutani ilionyesha ni saa mbili asubuhi, nilipiga miayo ya kivivu, nikajiondoa kitandani.

ITAENDELEA.
 
SEHEMU YA 11

Nilistushwa na mionzi hafifu ya jua la asubuhi ambalo huwa mara nyingi linapenya chumbani kwangu kupitia dirishani.

Pembeni , mke wangu alikuwa bado akikoroma, saa ilionyesha ilikuwa saa mbili asubuhi, nilipiga miayo ya kivivu, nikajiondoa kitandani.

Nilikuwa mtupu, taswira ya penzi la mwanamwali lilikuwa likijitengeneza upya akilini mwangu. Nilitabasamu na kujiona kidume mwenye bahati kubwa maishani.

Kuwa na mke ambaye hajawahi kuguswa na mwanaume ni ushindi mkubwa kwenye dunia ya leo, nilijiambia kimoyomoyo.

Nilisogea kwenye kioo na kusimama wima, nikaona ukoko wa damu ya Mwanamwali iliyogandana kwenye nyeti zangu, nikatabasamu tena huku moyo wangu ukiwa wenye faraja.

Nilipoyarudisha macho kitandani, Mwanamwali alikuwa bado akiuchapa usingizi.
Niliyatembeza macho pale kitandani, sikuwa nimeona kitu kingine nilichotarajia kukiona, nikasogea karibu zaidi.

Naam! hapo nikaona.

Damu ilikuwa imetapakaa kwenye mashuka meupe, nikajipongeza kimoyomoyo kwa kazi nzuri niliyoifanya usiku wa kuamkia siku hiyo.

Kazi ya kufungua bikira ya mwanamwali. ***** Maisha yangu na mke wangu, yalikuwa ni ya furaha, tulipendana na nilimwamini mno. Kama walivyo wanawake wengine wa Kipemba, Nasra alikuwa ni mwanamke mpole, msikivu na mchamungu.

Angalau hata ile aibu iliilipungua. Kwakweli alikuwa na kila kitu ambacho mwanaume yeyote angetaka mkewe awenacho. Wazungu wanasema ‘Wife material’

Ni miezi sita ilikuwa imepita, mjomba Majeed alikwisha rejea kijijini, katika mji wangu tulikuwa tumebakia watatu, yanii mimi, mke wangu, pamoja shemeji yangu Aisha. Huyu ni yule ndugu wa mke wangu.

Nakumbuka siku moja, baada ya kurudi kutoka kazini, kama kawaida yangu huwa napenda kujituliza nyumbani majira ya saa mbili kwa ajili ya kufuatilia taarifa ya habari katika vituo mbalimbali vya runinga.

Wakati huo mke wangu na nduguye walikuwa wakiendelea na matayarisho ya chakula cha usiku.

Nikiwa pale sebuleni, na rimoti mkononi, nikiwa nahamisha stesheni moja hadi nyingine, mara simu ya mke wangu ilianza kuita. Iliita muda mrefu hadi ikakatika.
 
Sehemu ya 12

Sikuijali. Mke wangu alikuwa mbali nayo, sikuthubutu kuipokea. Ikaendelea kuita hadi ikawa kero. “Kwa nini asikae na simu yake huko,” nilinong’ona. Kwa kuwa mke wangu alikuwa mbali na pale sebuleni, na wa muito wa simu ulikuwa ukioniondolea utulivu wa kutizima taarifa, niliinyakua ile simu ili niiweke ‘silence’

Wakati nafanya zoezi lile punde ujumbe wa maneno ukaingia, na katika kubofyabofya nikajikuta nimefungua ujumbe. “Mungu wangu!!” nilimaka kutokana na kile nilichokisoma! Mwili ulinitetemeka.

Ujumbe ulikuwa umetumwa na namba ile ile ambayo ilikuwa ikipimgia mke wangu muda mfupi uliopita.

Ujumbe ule ulikuwa umeambatana na meseji ya muamala wa fedha. . “Mbona hupokei simu mrembo? Nimekuingizia milioni tisa kwenye accont yako ya bank, nimekutumia na ujumbe wa muamala nilioufanya. Ukipata ujumbe huu nitafute”

Meseji ile ilisomeka hivyo. “Nani huyu!” nilinong’ona.

Nikafikiria mtu ambaye anaweza kumpa mke wangu kiasi kile cha fedha, bado sikuona ndugu yake yeyote mwenye uwezo huo.

“Huyu mtu sasa atakuwa ni nani, kwanini amtumie mke wangu fedha zote hizi, na mke wangu naye pesa hii ya nini?” Maswali yalikuwa mengi kichwani kuliko majibu, mwisho nikaona njia nzuri ya kupata majibu ni kuinakiri ile namba katika simu yangu, kisha nimpigie mfadhili yule na nimuulize yeye ni nani na alikuwa na biashara gani na mke wangu.

Nilinakiri haraka kisha nikaipiga, lakini kabla simu haijanza kuita nikakata simu, wazo jipya likanijia, niliona njia ile sio njia nzuri sana ambayo ingeweza kunipa ukweli wa jambo lile.

Kama kulikuwa na biashara isiyo ya kawaida kati ya mke wangu na mtu aliyemtumia fedha, kwa kutumia njia niliyotaka kuitumi, kamwe nisingeweza kubaini ukweli. Niliwaza kimoyomoyo Na wakati mawazo hayo yananijia kichwani, wivu wa mapenzi ukaanza kujitengeneza moyoni, fikra mbaya zikaanza kuniteka.

Hisia za mke wangu kuhongwa kiasi kile cha fedha na mwanaume mwingine mwenye uwezo mkubwa zaidi yangu zikavuruga kabisa mwenendo wa utashi wangu.

Waswahili wanasema, Subira yavuta heri, Nilichofanya ni kui-save’ namba ya mtu yule, halafu nikafuta simu zote zilizoingia kwenye simu ya mke wangu.
 
Sehemu ya 13

Nilifanya vile makusudi ili mke wangu asibaini chochote kama kuna mambo yasiyo ya kawaida nimeanza kuyashitukia.

Jambo la mwisho nililofanya katika simu ile nilifungau faili lililoandikwa ‘Play store’, nikafungua, kisha nikapakua ‘program’ iitwayo ‘Voice recoder, nikaiseti simu ile kuwa inajirekodi yenyewe simu yoyote itakayokuwa inaingia na kutoka.

Baada ya hapo, nilitulia tuli, moyoni nikiweka nadhiri ya kulifuatilia jambo lile kimyakimya.

Muda mfupi badaye, mke wangu na nduguye walimaliza kupika, aliniandalia chakula, tukala wote pamoja. Wakati wote nilimwonesha tabasamu, sikumwonesha kama kuna kitu kisicho cha kawaida nimekibaini dhidi yake.

Baada ya mlo wa usiku, tulielekea chumbani mwetu kulala huku mdogo wake, Aisha naye akielekea chumbani kwake.

Tukiwa chumbani, kama kawaida tulipeana mapenzi motomoto na kama nilivyokwisha eleza awali, katika kipindi cha miezi sita, tangu nifungue usichana wake, mke wangu alikuwa mjuzi mno kitandani. Tulipeana mapenzi mazito hadi miili yetu iliporidhika.

“Ahsante mume wangu.” “…kwa?” “Penzi tamu, unajua sana kunikuna,” mke wangu alinambia baada ya kumaliza mmenyano. “Kweli?” “Sikudanganyi mume wangu.” “Lakini hata wewe siku hizi umekuwa fundi sana kitandani.”

“Mwongo.” “Kweli mke wangu, sijui nani amekufundisha.” “Nimefundishwa na wewe mwenyewe au umesahau?” “Nikumbushe.”

“Umesahau ‘ningali’ mwanamwali ulichonieleza?” “Nilikueleza vingi, kipi unachokusudia?” Kuhusu aibu.” “Alaa! Kumbe somo hilo.” “Ndio, siku hizi ninalifaulu kwa kiwango kikubwa, ndio maana unaona nimekuwa fundi kitandani,” alisema.

Tulizungumza na kufanyiana utani wa hapa na pale kisha usingizi mzito ukatuchukua. **** Ni asubuhi ya siku mpya, wingu la mvua lilikuwa limetanda, ngurumo za radi zilidhirisha uwepo wa mvua kubwa ambayo ingenyesha asubuhi hiyo.

Magari yalikuwa mengi barabarani, watu walikuwa wakihaha huku na kule kuhakikisha wanakuwa sehemu salama ili kujiepusha na kadhia ya matone ya mvua.

Ngurumo za radi zilizokwenda sambamba na miale mikali, ilifanya asubuhi ya siku hiyo kuwa nzito kwa wakazi wengi wa jiji la Dare es salam.

Mvua kubwa iliyoambatana na upepo ilianza kunyesha, upepo ulikuwa ukizoa
 
SEHEMU YA 14


Dakika ishirini badaye niliwasili ofisini, akili yangu bado ilikuwa kwenye jina la mtumiaji wa namba iliyomtumia mke wangu pesa.

“Bosi naona leo uko mbali sana,” katibu muhtasi wangu aitwaye Debora aliniambia akiwa anamimina kahawa katika kikombe baada ya kuwa nimekwisha ingia ndani ya ofisi yangu.

“Kivipi?” nikamuuliza. “Umeingia ofisini ukionekana kuchanganyikiwa sana, hata salamu za baadhi ya staf hujajibu.”

“Kweli?” “Tangu lini nimekufanyia masikhara bosi?” “Kuna mambo fulani yananichanganya Debora,” nilimwambia. “Unaweza kunishirikisha, pengine naweza kuwa na msaada.” “Laaa! Si kitu, ni mambo binafsi,”nilimjibu, sikupenda mambo yangu nimshirikishe Debora ingawa tulikuwa tumeshibana mno na msichana yule.

Mimi na Debora ukiachilia mbali mimi kuwa bosi wake, lakini binti huyo mwenye umbo zuri na sura ya kushawishi tulikuwa ni maswahiba wa karibu sana, urafiki wetu ulitokana na kuendana tabia fulani fulani. nitaelezea wakati mwingine ni tabia gani tuliendana mimi na Debora, kwa sasa itoshe tu kufahamu kwamba mimi na binti yule, tulikuwa ni marafiki wa karibu.

Baada ya kuniandalia kahawa na kuondoka, nikawa na wakati mwingine wa kutafakari juu ya uhusiano ulipo kati ya mke wangu na mtu yule aliyemtumia pesa.

Baada ya kutafakari kwa kina nikawa nimepata majibu ni kitu gani natakiwa kufanya kama mwanaume ili niweze kutatua tatizo lile ambalo lilikuwa limekwishaanza kutia doa katika ndoa yangu. Nilifanya kazi zangu zote pale ofisini, saaa kumi jioni, nilikuwa ndani ya gari langu nikirejea nyumbani.

Baada ya kufika, kama ilivyo ada, mke wangu alinikaribisha kwa mapenzi na mahaba yote, nilikwenda kuoga, baada ya kutoka bafuni, nikakuta juisi nzito ya parachichi ipo mezani, akanikaribisha kinywaji kile.

Wakati napata kiburudisho ndipo nikaanzisha mazungumzo: “Mke wangu Nasra,” nilimwita kwa sauti tulivu. “Rabeka mume wangu,” akaitika. “Nina mazungumzo na wewe leo.” “Naona fikra zetu zilikuwa sambamba,” mke wangu naye akasema.

“Kwa nini?” “Hata mimi nilikuwa nahitaji kufanya mazungumzo na wewe, tena leo hii.” “Kweli fikra zetu zilikuwa zikisafiri katika ngalawa moja,” nikamjibu, akatabasamu.
 
SEHEMU YA 15

Tabasamu la mke wangu huwa ni sumu mbaya sana nafsini mwangu.

Tabasamu lile likaamsha maruhani yaliyokuwa yamelala kwa wakati huo. “Vipi tena?” akahoji, alipoona mikono yangu inazunguka kiunoni mwake. “Majini yamepanda.”

“Yatulize kwanza tuzungumze.” “We’ ndiye mganga wangu, tuliza tu haya mapepo,” nilimjibu kwa utani nikiwa napenyeza mkono wangu kwenye ikilu yake. “Weweeee!” mguno wa ajabu ukamtoka wakati kidole changu kikifanya ziara ya kushitukiza. “Si…si…ta…taa..ki,” akaendelea kuweweseka huku akinivutia kitandani.

Nikamchojoa nguo zake, kisha nikazama chumvini. Wakati namfanyia kitendo kile, mke wangu aliweweseka kama mgonjwa wa degedege, hazikuzidi dakika 20 tukajikuta tunashiriki tendo la ndoa.

Mchezo ule ulimalizika kwa sare ya bao moja kwa moja. Tulirudi bafuni, tukaoga huku tukifanyiana michezo ya kitoto, kwa kweli ulikuwa ni wakati mzuri mno maishani japokuwa kulikuwa na jambo zito lililonitesa.

Tuliporejea mezani ambopo kulikuwa na kile kinywaji laini cha juisi, mke wangu ndiye alikuwa wa kwanza kuanzisha mjadala kuhusu yale mazungumzo yetu.

“Unaonaje ukianza kuzungumza kile ulichodhamiria kunieleza kisha na mimi niseme kitu gani nataka kuzungumza na wewe” nilimwambia mke wangu. Wazungu wanasema ‘Lady is first’ “Sawa mume wangu.” “Nakusikiliza sasa,” nilimwambia “Jambo lenyewe ni hivi…” alianza kunieleza.

“Nimepata dili moja kwenye kampuni ya sky production ambayo ipo chini ya yule mwanamuziki maarufu aitwaye Abdul Ally.” alisema, akanyanyua glasi ya juisi na kupiga funda moja, kisha akaendelea.

“Kwa kweli nimekuwa njia panda kama natakiwa kukubaliana na ombi la hawa jamaa ama laa!

Hii ni kutokana na aina ya kazi ambayo natakiwa kufanya. Ndio maana kabla ya yote nikaona nikushilikishe wewe mume wangu,” alisema.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom