Simuelewi mtu huyu

kiki14

Member
Joined
Aug 28, 2014
Posts
6
Reaction score
3
Habarini kwanza, naombeni ushauri kwa hili.

Nina watoto 2 nimeishi na mwenazngu kwa miaka 5 ila bado hatujafunga ndoa mwenzangu ameanza tabia za ajabu ambazo hapo kabla sikuwahi kuzijua kabisa kawa mlevi wanawake ndo usiseme nilipokuja kugundua nilipewa kipigo nikaamua kurudi kwetu maana hatujafunga ndoa cha ajabu ndo kwanza alikuwa ananiambia we kaa huko huko me nitaishi peke angu mara me nitaoa mambo kibao ili ajue nitafanya nini ila mimi nikamjibu we fanya utakalo amua.

Ugomvi wetu ulikuwa mkubwa hadi kufikia kwa wazazi maana una mambo mengi imepita miezi kadhaa nilikuwa kimya tu saa ivi ananiambia anaomba yaishe nirudi wakati alishanikabidhi kwa wazazi wangu kuwa hanihitaji tena nami nikaamua kufanya yangu na nijipange tena upya kimaisha, na kule kwa wazazi wanajua ameshanikataa ila yeye moyon anakiri bado ananihitaji.

Niliacha kazi kwaajili yake maana tulikuwa tukaa mikoa tofauti ila sasa hivi nimerudi tena kazini ila yeye mpaka sasa hajui kama ninafanya kazi nimfanyaje mtu huyu.
 
Hilo nalo la kujiuliza????

Songa mbele....

U-girlfriend miaka 5 utadhani mwasomea sheria??????

Mkubaliane tu jinsi ya kutunza watoto.....

Unless unahitaji more drama unaweza mkubalia.... (aliamua kuwa na wanawake wengine kakutana na moto ndio anakumbuka shuka kumekucha??? Au kaona umesonga mbele na maisha yako yana msimamo anataka kukuridisha nyuma???)))

Na iwe funzo kwa wanawakw wote, unaachaje kazi kwa sababu ya boyfriend????

Tengeneza maisha yako for the sake of your kids
 
Achana nae mshamba tu huyo. Tena ikiwezekana chukua watoto wako achana nae ----- mtozen huyo
 
kwanza unaanzaje kuishi na mwanaume ambae hamjafunga nae ndoa?
La pili unaanzaje kuachishwa kazi na boyfriend?
kama umeshajua tabia zake hizo chafu kwanini uendelee kuwa nae huoni kama unajitengenezea bomu mwenyewe?
TAFAKARI CHUKUA HATUA
 
Labda amegundua makosa yake na amejirekebisha kweli, you never know....
 
mmhhh hapo itabidi uache tena kazi...mawee!!!
 
Hapana dada, kawazidi wanasheria. Huyu ni daktari. Na akirudi anapata speciality kabisa, tena ya udaktari wa moyo

ukiona mtu haumuelewi ujue haeleweki. Kazi kwako, kusuka ama kunyoa?
Hilo nalo la kujiuliza????

Songa mbele....

U-girlfriend miaka 5 utadhani mwasomea sheria??????
 
Hapana dada, kawazidi wanasheria. Huyu ni daktari. Na akirudi anapata speciality kabisa, tena ya udaktari wa moyo

ukiona mtu haumuelewi ujue haeleweki. Kazi kwako, kusuka ama kunyoa?

Kweli huyu ni daktari wa moyo....

Zaidi ya mahaba niue...

Unaacha hadi kazi ili ukamuvuzishwe na bf!!!!!!!!

Halafu anapoelekea kama kumrudia huyo mwanaume
 
Kuna kipindi wanaume tunahisi uliyenae anakubana hasa ukishamuweka ndani bila ya kumuoa kwa ndoa hakuna ina kuwa rahisi kumtamkia maneno ya ajabu kupelekea kutengana sasa tabu

inakuja pale ambapo umezoea kukuta mtu nyumbani hata saa tisa usiku utafunguliwa na mtu pia kuna mtu anakuwaza wewe ngoja nikwambie huwa najisikia raha sana kujua kwamba kwa muda huu kuna mtu ananiwaza.

ila kwa sasa anaona tabu anarudi nyumbani kimya sauti ni moja nyumbani kama watoto umeondoka nao ndio kabisa upweke ni kama ugonjwa mwenzio anaumwa.

Ushauri rudi nyumbani muishi kama zamani anajuta kwa maamuzi aliyochukua msamehe tu hakuna aliyekamili chini ya jua.

hebu sikiliza mwana fa ft mandojo &domokaya na Kama zamani
 

Posa na mahari keshatoa ilikuwa tufunge ndoa mwaka jana ila kukatokea dharula
 
Posa na mahari keshatoa ilikuwa tufunge ndoa mwaka jana ila kukatokea dharula

Ok...

Ukitazama miaka 10 baadae unaona kuna future????

Kama aliweza kukukataa sasa nini kitakachomzuia asikukatae baadae??

Shirikisha akili yako na si mahari wala posa....na
 
Posa na mahari keshatoa ilikuwa tufunge ndoa mwaka jana ila kukatokea dharula

yaani hapo kinachokuumiza ni hiyo ndoa.
Umenchekesha sana.
Haya rudi ukaolewe.
 
Hadi umekuja kuuliza huku inamaana kuna kasauti ndani kwako inakuambia still kuna chance.
Sikushauri usikilize ya humu, jipe muda sikiliza moyo wako unataka nini. Pia, kuna muda sio mbaya kufanya sacrifices kama unaona hatakusaidia mbeleni.
 
kwani we moyo wako unatakaje hasa....??? Maana kwa maelezo yako ni bora kusonga mbele na maisha maana uli sacrifice vitu kibao kwa ajili yake na bado alikutesa na akupiga teke ..... alafu unajishauri urudi kwamba bado yy anakuhitaji?? Yeah.. binadamu tunakosea ila sometimes kuwa na upendo kias na hasira kiasi... chukua maaumuz mazuri kwa ajili yako sio kwa ajili yake...
 
Ulifanya mistaje kubwa kujipeleka kwake na kuacha kaz kisa mwanaume...ndugu yangu angalia maisha yako.kwa sasa huyo.hafai ni.sawa na matapishi uliyoyatapika kamwe huwez kuyarudisha tumboni ukirud mchezo utakua ule ule akugeuze ngoma ake ulisha teleza bas sasa lea wanao.kwa kaz yako.uliyokua nayo hao ndo wakukupa faraja labda iwe unampenda bado
 

usirudiiiiiiiiii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…