Simuelewi kabisa Mbowe!

Simuelewi kabisa Mbowe!

William Mshumbusi

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2012
Posts
1,792
Reaction score
2,421
Kuwa bize kupinga matokeo ya urais pekee ndiko kunanifanya nimuone ama mamruki na anataka kutuyumbisha tu wapigania haki, naomba kuuliza.

1.Vipi hazungumzii kabisa wabunge wa ukawa na majimbo ambayo kunaviashiria vya ukawa wamefanyiwa fitina na kuporwa kwa fitina kama mbagala, nyamagana na kasulu, Rungwe, Kyela na kwingineko

2.Kwanini hazungumzii jinsi wabunge wa ukawa walivyotangazwa kwa mbinde na vuta nikuvute japo walishinda kama Kawe, Mtwala na Mikumi.

3.Vipi halipi uzito unaostahii swala la Zanzibar

Ni wakati wa wabunge wa ukawa kujisimamia na kuangalia ajenda za muhimu za kuanza kupigania la sivyo hali itakuwa mbaya mbeleni nilitegemea Mbowe angeyapa uzito maswala haya kuliko hilo la uraisi binafsi naona kama anatupotezea muda na kutuwaribia agenda.
Na kwa yanayotokea Sasa Nakumbuka movie ya wonders Love na Mbowe ndie JeJevidet, Msaliti mkuu na mpikuu na Jemedal mkuu wa CCM
 
Kuwa na subira wenyewe makamanda wanakuja mkuu
 
Kuwa bize kupinga matokeo ya urahisi pekee ndiko kunanifanya nimuone ama mamruki na anataka kutuyumbisha tu wapigania haki, naomba kuuliza
1.Vip hazungumzii kabisa wabunge wa ukawa na majimbo ambayo kunaviashiria vya ukawa wamefanyiwa fitina na kuporwa kwa fitina kama mbagala, nyamagana na kasulu, Rungwe, Kyela na kwingineko
2.,Kwanini hazungumzii jinsi wabunge wa ukawa walivyotangazwa kwa mbinde na vuta nikuvute japo walishinda kama Kawe, Mtwala na Mikumi.
3.,Vip halipi uzito unaostahii swala la zanzibar

Ni wakati wa wabunge wa ukawa kujisimamia na kuangalia ajenda za muhimu za kuanza kupigania la sivyo hali itakuwa mbaya mbeleni nilitegemea mbowe angeyapa uzito maswala haya kuliko hilo la uraisi binafsi naona kama anatupotezea muda na kutuwaribia agenda
Tatizo la watanzania wengi ni elimu,umeambiwa issue ya wabunge inaruhusiwa kupinga mahakamani kwa hiyo majimbo yenye utata mchakato unaendelea issue ya zanzibar waliisha toa statement na maalimu anaendelea na mapambano akiwa na support ya wanaukawa wote wewe ulichotaka afanye nini?
 
kimya cha upinzania ni kikubwa ni lazima kirudi na mshindo, kiwe na maana,na sio ku-buy time na kuwaacha watu wajishushe kasi wenyewe,maswali ni mengi kuliko majibu,pia hawajatoa tathmini za kura zilizotoka vituoni kwa upande wao,nini kinaendelea?
 
Tatizo la watanzania wengi ni elimu,umeambiwa issue ya wabunge inaruhusiwa kupinga mahakamani kwa hiyo majimbo yenye utata mchakato unaendelea issue ya zanzibar waliisha toa statement na maalimu anaendelea na mapambano akiwa na support ya wanaukawa wote wewe ulichotaka afanye nini?

ni ujinga kunyanganywa jimbo kirahisi na kuendelea kuziamini mahakama zetu hizi, Lazma wafanye kitu
 
Mbowe ni bora awe anapangilia kitu kikubwa,otherwise sitamuelewa kabisa.Wanaharakati wote wamekaa kimya; Lema yuko kimya,Lissu yuko kimya,Mdee yuko kimya,Mnyika yuko kimya~kitaa mimi natukanwaje??
Dhihaka kubwa tumefanyiwa watanzania na wanaharakati viongozi wapo kimya!

Sijui,Labda Lowassa anazamisha filosofia yake ya kupunguza kubweka na kuanza kung'ata,Labda kuna plan inafanyika maana Kingunge,Mwapachu,Lowassa,Sumaye,Masha na Apson haiingii akilini kwamba wameishiwa mbinu.This is the time that we need our star players to shine.They must really come good and help the team now.
 
Back
Top Bottom