Simuelewi hyu mr wangu.

Simuelewi hyu mr wangu.

yaani wewe utakuwa umekulia sehemu ambazo hazina utegemezi so nakushauri badilika na uanze kujua nini maana ya utegemezi..

Ina maana yeye (mdada) hana ndugu? Watoto unamwachia mkeo awatunze kisa unatunza wazazi? Hapo sijaielewa vizuri.
 
yaani wewe utakuwa umekulia sehemu ambazo hazina utegemezi so nakushauri badilika na uanze kujua nini maana ya utegemezi..

huyu jamaa aliingia choo cha kike. Yaani mama yangu amenisomesha akivaa ndala na kanga, nimepata kazi ashindwa hata kuvaa kitenge! Loh! Kweli ni afadhali nisioe kama wanawake ndo hawa!
 
Cha msingi kaa na mumeo mpange kwa pamoja matumizi,inavyoonekana na wewe dada una kipato chako na mumeo pia then kaeni pamoja mpange vipaumbele ikiwa pamoja na kusaidia extended family hizo africa hazikwepeki
 
Mimi ni mdada nimeolewa na nina watoto.tatizo ni mume wangu kabadilika sana.Anataka nimsaidie majukumu yake kwa asilimia kubwa na wakati ana kipato kikubwa.nimegundua kuwa hela anazopata kiasi kikubwa kinaenda kwao kwa mzazi wake na ukimuuliza anakuw mkali.sijakataa yeye kusaidia familia yke lakin aangalie na yeye ni baba sasa anahitaji kujenga familia yake.kma alijua kuwa anamajukum kwao asingeoa akamaliza majukum yake kwanza.nimejaribu kuongea nae lkn haelewi.ananipa makwazo sana .nimfanyeje jaman wana jf.


Bado anaweza akaacha ndowa akasubiri hadi awe tayari.
 
Hakikisha huyu mjamaa wako hana small house maana hizo ndizo zinamaliza fedha zote kwenye bajeti ya mwezi.

Iweje leo bajeti iwe ngumu kiasi hicho wakati hao wazazi alikuwa nao tangu hapo awali?
 
pole sana..sometimes ndoa ngumu..vumilia tu na kuwa na busara..punguza kununa nuna yatapita tuu...........
 
Tabia iliyojengwa kwa miaka 20 haiwezi kuondolewa kwa dakika 20. Wakati unataka abadilike jifunze kuwa na subira pia.
 
Wewe ndio mwenye matatizo, kwa sababu mtu kusaidia alikotoka ni muhimu. Wewe utakuwa na roho ya korosho...to trust a woman is not accepted!!!
 
Pole mami yawezekana wewe ni mchanga kwenye ndoa.mwanaume kuhudumia kwao ni lazima.naw wewe pata huduma zako na mumeo pia aendelee kuhudumia nduguze huwez jua.pia ushauri wa bure usioneshe kuumia sana anaposapot kwao la sivyo itakugharimu
 
Mimi ni mdada nimeolewa na nina watoto.tatizo ni mume wangu kabadilika sana.

Naona kiswahili kinazidi kutanuka. Kumbe mdada ni mwanamke aliyeolewa na mwenye watoto!!!
 
Kuna wanawake ambao hawapendi hata senti ya mume kusaidia ndugu wa mume lakini akisaidia mashemeji zake upande wa mke sawa. Sina uhakika sana na anachojaribu kuleta mtoa mada. Mwanaume ambaye ni mwanaume hawezi kusaidia ndugu hata kama ni wazazi kabla hajatimiza majukumu ya kifamilia.

Usime tu, kuna wakati kujibana kidogo ili na jamii nayo isaidiwe. Sasa kama ni kipindi cha kupunguza mambo fulani ya anasa ili wazazi wa mmeo wasaidiwe usione kama ni tatizo. Ndio hao waliokuzalia chema!

Hata hivyo, kwa jinsi ulivyoleta mada inaonekana na wewe unakipato fulani, maana umesema ..'Anataka nimsaidie majukumu yake kwa asilimia kubwa na wakati ana kipato kikubwa'. Sasa kuna tatizo gani ela yako kutumika wakati mmeo anatatua ugumu wa maisha ya wazazi wenu?

Kwenye familia yangu wazazi wa pande zote mbili kwangu ni sawa. Wakwangu na wa mke wangu. Kila tunapopata nafasi, tunawasaidia wote kwa kadiri Mungu anavyotubariki.

Ushauri:
  • Wapende wazazi wa mmeo kama wako.
  • Kama kweli unaona mmeo anapoteza ela basi weka mipango ya matumizi ili kabla hajafanya hivyo umwambie baba mbona jambo fulani hatujafanya?
  • Familia ni kusaidiana, sio jambo baya pesa yako kuingia katika matumizi ya familia. Kuna wanawake wengi nje wana pesa zao lakini wanajiona hawajakamilika kwa sababu hawana ndoa. Huwezi jua thamani ya kitu mpaka utakapokipoteza!
 
Wewe ndio mwenye matatizo, kwa sababu mtu kusaidia alikotoka ni muhimu. Wewe utakuwa na roho ya korosho...to trust a woman is not accepted!!!

tena hawa ndio wanawake njaa!halina hata haya aisee!eti 'nimegundua',maana yake mume hamshirikishi maana anajua roho yake mbaya!halafu mume anamsaidia 'mzazi',ingekuwa wazazi ama ukoo mzima je?
shida kwa ndugu haziishi,ukiona yamekushinda wewe kumsaidia hayo unayoyaita 'majukumu yake' fungasha virago vyako nenda kwenu!
hovyo!
 
Hilisio tatizo hata kidogo, ni wewe unafikiria kuwa ni tatizo. Mimi nitasema hivi:
1. Wewe unahitaji mafunzo ya haki na wajibu kwenye mahusiano na watu na katika hili, haki yako kwenye ndoa yako. Unaishi kwenye ndoa kwa assumptions. Futa assumptions zote na tafuta kujua reality ni nini.

2. Wewe umezoea mambo yaliyonyooka, na ikitokea jambo usilolipenda unaona kama dunia imeisha - una tabia ya kunyoosha yakwako. kama yako yanakwenda basi, mengine wewe hayakuhusu.

3.Jifunze namna nzuri ya kutatua matatizo yako kwa lengo la kufanya mahusiano yako na ndoa yako and indeed your whole welfare to be better than it was before. Matatizo ni opportunity yako ya kuonyesha uwezo wako wa kutatua na kujifunza. Acha kuishi kwenye ndoto. Karibu duniani. Hukuolewa kwenda beach, umeolewa kuongeza nguvu ya pamoja kutatua matatizo ili wewe pamoja na familia, jamaa,nchi na dunia iwe nzuri zaidi kupitia jitihada zako.

4.Ni kweli kuwa baadhi ya wazazi na ndugu au marafiki huwa wanahitaji msaada wetu wakati fulani. Ni wajibu wetu kujua tunategemewa.Hivyo tunapaswa kujijenga kielimu/kiuchumi ili tuwe msaada au tuweze wasaidia wale wanaohitaji msaada wetu. hii sio wazazi au ndugu peke yao bali hata marafiki au yatima,vikongwe.

5.Bora huyo anaepeleka pesa kusaidia wanadamu wenzio kuliko angekuwa anapeleka bar au kaoa au ana nyumba ndogo.

SOLUTION

Tatizo lako sio linaanza bali ni tatizo ambalo limekuwapo siku nyingi. You dont have a vision for your marriage. Wewe na mume wako mna shida ya :
1. Mawasiliano - hamuongei kupanga mipango ya familia/ fedha/ mipango ya raha zenu
*Nadhani hata sex huwa mnafanya usiku,mkiwa mmejifunika,mnakamatana ndani kwa ndani (shame)
*Nadhani hata watoto mlio nao hamkuulizana kama mpate mimba au la, mlishtukia hupati siku zako baaas! Mkaamua azaliwe. (Shame)
*Nadhani masuala ya pesa anaamua aliyeleta pesa hizo (zako za saloon na za baba za kujenga) (shame)

CHA KUFANYA
Renew your mind - anza kuvunja shida yenu ya kukosa ukweli na unyenyekevu (Acha mashindano)
*Jifunze mawasiliano na Upendo wa kweli
*Jifunze kupanga maisha (sio ya kuangalia kwenye TV - tafuta njia mpya kabla hujaisha!
 
Tatizo la wanawake wanaofanya kazi eti mshahara wa mumewe ndo utumike kuendesha familia kama mambo ya ada,kodi zote arafu mshahara wake yeye wa kununua vipuri,wigi,heleni,na mataka taka mengine hapo sasa kazi inakuja pale umeolewa na mkurya. makavu
 
Last edited by a moderator:
Weka malengo na mumeo na mtembee katika ratiba hiyo...
Usianze kujitutumua kama uji wa vitumbua kikaangoni, ndoa itakushinda hiyo.
 
mimi mwanamke anayeona shida mumewe kuwasaidia ndugu yeye mwenyewe namuona tatizo.
kinachotakiwa mnapswa kuwa na mipango ya pamoja kwa kila mnacho kifanya kwani kuwasaidia ndugu kwa famila zetu za kiafrika ni jambo lisilo epukika.

mimi sion shida yy kusaidia sema aniweke waz nijue.na wala simkataz sema isiwe too much mpk na ye ajisahau aishiwe hela ya nyumbani.na nilishamwambia kwamb ukisaidia niambie sio kwa ubaya ili nijue.
 
Mimi ni mdada nimeolewa na nina watoto.tatizo ni mume wangu kabadilika sana.Anataka nimsaidie majukumu yake kwa asilimia kubwa na wakati ana kipato kikubwa.nimegundua kuwa hela anazopata kiasi kikubwa kinaenda kwao kwa mzazi wake na ukimuuliza anakuw mkali.sijakataa yeye kusaidia familia yke lakin aangalie na yeye ni baba sasa anahitaji kujenga familia yake.kma alijua kuwa anamajukum kwao asingeoa akamaliza majukum yake kwanza.nimejaribu kuongea nae lkn haelewi.ananipa makwazo sana .nimfanyeje jaman wana jf.

wenzio wanafrahia kumlea mwanwaume kama mtoto mdogo wewe unaona anakukwaza
 
Mimi ni mdada nimeolewa na nina watoto.tatizo ni mume wangu kabadilika sana.Anataka nimsaidie majukumu yake kwa asilimia kubwa na wakati ana kipato kikubwa.nimegundua kuwa hela anazopata kiasi kikubwa kinaenda kwao kwa mzazi wake na ukimuuliza anakuw mkali.sijakataa yeye kusaidia familia yke lakin aangalie na yeye ni baba sasa anahitaji kujenga familia yake.kma alijua kuwa anamajukum kwao asingeoa akamaliza majukum yake kwanza.nimejaribu kuongea nae lkn haelewi.ananipa makwazo sana .nimfanyeje jaman wana jf.

Here we go again.
 
Back
Top Bottom