Simuelewi hyu mr wangu.

Simuelewi hyu mr wangu.

makavu

Member
Joined
Dec 10, 2012
Posts
13
Reaction score
4
Mimi ni mdada nimeolewa na nina watoto.tatizo ni mume wangu kabadilika sana.Anataka nimsaidie majukumu yake kwa asilimia kubwa na wakati ana kipato kikubwa.nimegundua kuwa hela anazopata kiasi kikubwa kinaenda kwao kwa mzazi wake na ukimuuliza anakuw mkali.sijakataa yeye kusaidia familia yke lakin aangalie na yeye ni baba sasa anahitaji kujenga familia yake.kma alijua kuwa anamajukum kwao asingeoa akamaliza majukum yake kwanza.nimejaribu kuongea nae lkn haelewi.ananipa makwazo sana .nimfanyeje jaman wana jf.
 
Njoo mie nikuoe mwaya, sina majukumu ka ndugu zangu...si umesema bado weye ni mdada? oooh what gud news (just kidding) on a serious note ni kwamba jaribu tu kumweleza na sio kutumia Lugha kama hii kuwa eti kama alijua ana majukumu mengine asingekuoa, hii lugha ya namna hii haijengi bali inabomoa. Thanks
 
pole my dear..matatizo ya ndoa yapo katika kila ndoa hata kama kwa nje ukiwaona wanandoa wataonekana wana furaha. jambo la msingi endelea kumpenda mmeo. unapoongea nae kuhusu yeye kuangalia majukumu ya nyumba tumia maneno ya hekima. usiongee naye maneno juu ya yeye kutoa pesa nyingi kwa ndugu zake wakati ndo tu amerudi home kutoka kazini au wakati hayuko ktk mood nzuri au hajala chakula. subiri muda ambao unamwona husb wako yuko happy. usiongee nae direct to the point na wala usitoe maneno kana kwamba unamkosoa au unamshutumu. wewe angalia katika nyumba kuna mambo yepi mnataka mfanye. je ni kujenga nyumba? kununua gari? kununua shamba?, nk. then mwambie 'mume wangu this time tufanye moja, mbili, tatu...kwa manufaa ya familia yetu'. kwa njia hiyo utambana mumeo pesa yake aielekeze kwenye majukumu/malengo ya maisha yenu!
 
yaani wewe utakuwa umekulia sehemu ambazo hazina utegemezi so nakushauri badilika na uanze kujua nini maana ya utegemezi..
 
DUUUUUUUh ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya firauni
Kila ndoa ni ndoano kwa namna yake. as it was well said all marriege start differently but ends the same.

pole mdada.
 
Suala la jamii zetu kutotegemewa hasa kama una kipato fulani, hilo haliepukiki kwa mtu mwenye moyo wa kusaidia. Lakini vilevile kumbuka kuwa jambo hili la ugomvi kati aya mwanamke na mumewe kwa mume kusaidia ndugu zake halipo kwako tu. Wanawake wengi wamekuwa na vinyongo sana na kutumia kauli hizo za jeuri kwa kumwambia mwanamume wake kuwa kama alikuwa hajamaliza shida za ndugu zake kwa nini alinioa? Shida za ndugu haziishi hata siku moja, hapa cha msingi fuata ushauri wa ndugu yangu KAMANDA KAZI.
 
kuna wanamme wengine unatakiwa uwa-let constant, afu u-differentiate. Ukipata jawabu ziro tu, mpotezee.

Ishi naye kwa huduma za usiku tu, maana hata ukiachana naye utagongwa na wengine bure wakupe magonjwa.

Bora huyu ni mwanamme suruali tu.

Vipi, chezo lake unalifurahia? Hapa ndo pa msingi.

Hasa kama familia haikuelemei, shida iko wapi? Fanya vya maana yeye anunue vitunguu, nyanya na chumvi.
 
Shosti hayo mambo ya kawaida afadhali hilo kuliko huyo mkwe angekua hapo na ma wifi tele,kaanae umueleze lakini tafuta wakati muafaka na nna hakika unajua wapi umshike ili atulie na umueleze yako....
 
Jaribu kuongea naye tena na tena naona wala sio issue ya kutisha....
Na yanatokea kwenye ndoa nyingi, hasa pale hela ya mama inapotumika ndani.
Ila kauli za kusema 'kwa nn alinioa wakati hajamaliza majukumu yake' hazijengi.
Tafuteni mfumo bora wa ku 'accomodate' matatizo ya ndugu kwa pande zote!
Nimemaliza!
 
Mimi ni mdada nimeolewa na nina watoto.tatizo ni mume wangu kabadilika sana.Anataka nimsaidie majukumu yake kwa asilimia kubwa na wakati ana kipato kikubwa.nimegundua kuwa hela anazopata kiasi kikubwa kinaenda kwao kwa mzazi wake na ukimuuliza anakuw mkali.sijakataa yeye kusaidia familia yke lakin aangalie na yeye ni baba sasa anahitaji kujenga familia yake.kma alijua kuwa anamajukum kwao asingeoa akamaliza majukum yake kwanza.nimejaribu kuongea nae lkn haelewi.ananipa makwazo sana .nimfanyeje jaman wana jf.

Maisha ya ndoa ni kama SERIKALI. Serikali yoyote bila mipango haiendi. Hakikisha kuna mawasiliano mazuri na mnakaa na kupanga mipango pamoja. Inaonekana kwenye ndoa yako hakuna mipango inayoainisha mapato na matumizi, wala hakuna maongezi ya nini kifanyike kujikwamua wenyewe na ndugu zenu. Wekeni kila kitu mezani na itakuwa rahisi kupanga nini kufanyike sio kila mtu anakurupuka tu na kupanga matumizi yake. Mshauri mumeo muanze kupanga mambo yenu, utafurahi na roho yako; ndoa tamu bana asikwambie mtu.
 
kuna wanamme wengine unatakiwa uwa-let constant, afu u-differentiate. Ukipata jawabu ziro tu, mpotezee.

Ishi naye kwa huduma za usiku tu, maana hata ukiachana naye utagongwa na wengine bure wakupe magonjwa.

Bora huyu ni mwanamme suruali tu.

Vipi, chezo lake unalifurahia? Hapa ndo pa msingi.

Hasa kama familia haikuelemei, shida iko wapi? Fanya vya maana yeye anunue vitunguu, nyanya na chumvi.

haaaa we kiboko. Kama ni hivyo kwa nini uolewe? bora ujikalie single!
 
Mimi ni mdada nimeolewa na nina watoto.tatizo ni mume wangu kabadilika sana.Anataka nimsaidie majukumu yake kwa asilimia kubwa na wakati ana kipato kikubwa.nimegundua kuwa hela anazopata kiasi kikubwa kinaenda kwao kwa mzazi wake na ukimuuliza anakuw mkali.sijakataa yeye kusaidia familia yke lakin aangalie na yeye ni baba sasa anahitaji kujenga familia yake.kma alijua kuwa anamajukum kwao asingeoa akamaliza majukum yake kwanza.nimejaribu kuongea nae lkn haelewi.ananipa makwazo sana .nimfanyeje jaman wana jf.

kwani mtu akiwowa ndio anasitisha huduma kwao?au kuna siku kwenu walishakua na uhitaji kama huo wa upande wa mume akakataa kuwasaidia au akakuzuia na wewe usisaidie kwenu?wanawake acheni roho mbaya
 
Mimi ni mdada nimeolewa na nina watoto.tatizo ni mume wangu kabadilika sana.Anataka nimsaidie majukumu yake kwa asilimia kubwa na wakati ana kipato kikubwa.nimegundua kuwa hela anazopata kiasi kikubwa kinaenda kwao kwa mzazi wake na ukimuuliza anakuw mkali.sijakataa yeye kusaidia familia yke lakin aangalie na yeye ni baba sasa anahitaji kujenga familia yake.kma alijua kuwa anamajukum kwao asingeoa akamaliza majukum yake kwanza.nimejaribu kuongea nae lkn haelewi.ananipa makwazo sana .nimfanyeje jaman wana jf.

Anasaidia nini kwao? How much per month anapeleka kwao?
 
Mleta mada na wewe unaonekana ni sehemu ya tatizo,maana lugha uliyotumia tu hapa ni ishara tosha.Huko ndani inaonekana balaa"......kama alijua ana majukumu asingeoa........"
 
Na ndugu zake ni sehemu ya familia yake dada, jaribu kumwambia taratibu ila hakikisha huna mentality asiwasaidie kwao, hivi wewe mtu akikwambia usimsaidie mdogo wako au mama yako si utamchukia? tatizo dogo hilo lishughulikie kiakili. na kwa taarifa yako kuoa si kuwa na kipato asingekuoa wewe angemua mwingine anayeweza kushirikiana naye kusaidia ndugu.
 
Pole rafiki... Usitumie nguvu mydia utaishia kuumia. Inategemea sana na mazoea aliyukuwa amejenga mumeo na wazazi wake.

La muhimu ni muwe na utaratibu wa kujadili mipango ya maendeleo ya familia yenu, lini mnaitekeleza, chanzo cha fedha n.k.

Mkiwa na utamaduni huu automatically baba atajitambua kwamba familia yake ina mahitaji gani muhimu na mchango wake unahitajika kwa kiasi gani.

Mawasiliano ni ufunguo mami .. Kama hamjadiliani kuhusu ishus, ada, ujenzi, hata jinsi ya kuwasaidia wazazi n.k na kila mtu akakaa kivyake na kujiamulia mwenyewe hapo ndo shida zinapoanzia

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mleta mada na wewe unaonekana ni sehemu ya tatizo,maana lugha uliyotumia tu hapa ni ishara tosha.Huko ndani inaonekana balaa"......kama alijua ana majukumu asingeoa........"

lugha za hovyo hovyo sana nazinazotia kinyaa,wanawake wao hela zao nikwa matumizi wanayoyajua wao sisi za kwetu ndio zakulea familia sio?siku hizi 50 50 hakuna cha m'ke wala m'ume wote lazima tubebanane kwa pamoja,lazima w'ke watoke kwenye hiyo dream land wanayoishi inayoamini m'ume ndio service provider wa kila kitu,hakuna anaefanya biashara hiyo tena ulimwengu huu,tuhudumiane tusaidiane period.
 
Binafsi sioni tatizo mtu akisaidia wazazi!!!!!!!!!!!!! Ingekuwa vipi kama angepeleka mshiko wote nyumba ndogo? SASA wazazi wajivuniae nini?
Kama familia unaimudu na mume unampenda endelea kwani hayo ni ya kawaida sana
 
mimi mwanamke anayeona shida mumewe kuwasaidia ndugu yeye mwenyewe namuona tatizo.
kinachotakiwa mnapswa kuwa na mipango ya pamoja kwa kila mnacho kifanya kwani kuwasaidia ndugu kwa famila zetu za kiafrika ni jambo lisilo epukika.
 
Back
Top Bottom