Simu zinazotumia android OS

Ramlis

JF-Expert Member
Aug 22, 2013
597
494
Wana JF ambao wametumia simu za android katika matumizi ambayo sio ya kupiga, kutuma sms na kuchati Whatsapp na FB tu, aliye tumia simu katika kazi mbalimbali kama kucheza game aina yoyote, kuchora ramani, ukiwasha data na kutumia internet kwa mda mrefu haichemki sana, ukipiga simu sauti inasikika vizuri, uimara wa betrii katika kutunza chaji nk. Tueleze ni simu ipi yenye sifa hizo ili hata mimi niweze kununua. Hapa tuzungumzie simu zenye kioo cha HD au full HD, Camera ya kupiga picha nzuri, ukubwa kuanzia nchi 4 hadi 6, internal memory kubwa, ram, OTA update nk.


Wengi tunalazimika kununua simu za tecno na itel na hizi huawei zenye uwezo mdogo maana ndo zimejaa madukani, kwenye maduka makubwa utakuta kuna zile Samsung, lg au htc zenye android 2.x.x os au matoleo ya zamani na bei yake inakuwa kubwa sana. Huku kwetu kuna duka moja tu linauza simu za Samsung galaxy kuanzia s2 hadi s4 na bei ni kuanzia million moja na kuendelea. Ukipata ya kuanzia laki tano unakuta ni clone.

Nimetumia simu za tecno sana na huawei hakuna hata moja yenye kuniridhisha, nyingi zina matatizo ambayo utayakuta kwenye simu zingine za matoleo husika.


Tecno H6.

- Inatabia ya kuchemka sana unapowasha data au unapoichaji ikiwa on.

- Ukifatilia vizuri kamera ya mbele inatoa picha nzuri kuliko ya nyuma (hii ni kwa simu nyingi za tecno)


Tecno C5/C8 ( na zenye android ya lollipop)

- Gps haifanyi kazi

- Kuna mda majina ya kwenye line yanapotea hadi uzime na uwashe tena

- Ukisave namba kwenye line inagoma au ikikubali baadae ukiitafuta huioni

- Message za whatsapp, emails, nk zinaingia pale unapofungua app husika, hii inafanya kutopokea message kwa wakati.

- Ukiwasha kamera au tochi ukatumia kwa mda kuanzia dk 10 chaji inapungua kwa asilimia kubwa sana kama ilikuwa asilimia 80 utakuta kati ya 20 hadi 35

- Kama unaichaji simu ina asilimia kuanzia 75 ukiizima na kuiwasha itakuandikia asilimia 100

- Haina factory recovery mode, akitokea mtu mwingine akaweka pattern kwenye simu yako itakulazimu kuiflash na njia hii hua inafuta IMEI namba.


Simu nyingi za tecno zenye bei kuanzia laki mbili kushuka vioo vyake havina quality nzuri. Tecno Boom J7 betrii yake inauwezo mdogo sana.


Kwa baadhi ya matoleo ya Huawei zinasumbua screen touch na kuganda ghafla, nyingi zinagoma sehemu ya Home, menyu, na back. Hata ukibadilisha screen touch unaweza ukatumia kama mwezi ikagoma.


Itel hakuna simu yenye ubora katika matoleo yao.

Kama unasimu eleza matatizo yake uliyokutana nayo ambayo ni common kwa toleo lote au ubora wake.
 
kwa simu zinazopatikana tanzania lg g2 ndio best value kwa sasa zinapatikana around 300,000 hadi 400,000 na zina specs kubwa kushinda Tecno za 700,000 kupanda.

kwa simu ambazo unahangaika na hazipatikani bongo xiaomi redmi note 3 ndio best kwa sasa ila itabidi uagizie nje au usubiri hadi kesi yao kenya iishe.

kuhusu kupata moto almost smartphone zote zinapata ila likizidi sana ndio mbaya.

na ukutafuta simu ambayo si nyembamba sana mara nyingi zinakuwa hazipati joto jingi sababu hewa hupita kwa wingi
 
69c62690e4865cb9f7031d15d9a42993.jpg


Simu hizo kwa mawasiliano zaidi piga simu namba 0652971495
 
kwa simu zinazopatikana tanzania lg g2 ndio best value kwa sasa zinapatikana around 300,000 hadi 400,000 na zina specs kubwa kushinda Tecno za 700,000 kupanda.

kwa simu ambazo unahangaika na hazipatikani bongo xiaomi redmi note 3 ndio best kwa sasa ila itabidi uagizie nje au usubiri hadi kesi yao kenya iishe.

kuhusu kupata moto almost smartphone zote zinapata ila likizidi sana ndio mbaya.

na ukutafuta simu ambayo si nyembamba sana mara nyingi zinakuwa hazipati joto jingi sababu hewa hupita kwa wingi

Asante Chief-mkwawa ngoja nitafute hiyo lg g2 hata kwa kuagiza dar au mwanza maana ndo maeneo ninayoyatumia sana kupata vitu visivyopatikana maeneo yangu.
 
kwa simu zinazopatikana tanzania lg g2 ndio best value kwa sasa zinapatikana around 300,000 hadi 400,000 na zina specs kubwa kushinda Tecno za 700,000 kupanda.

kwa simu ambazo unahangaika na hazipatikani bongo xiaomi redmi note 3 ndio best kwa sasa ila itabidi uagizie nje au usubiri hadi kesi yao kenya iishe.

kuhusu kupata moto almost smartphone zote zinapata ila likizidi sana ndio mbaya.

na ukutafuta simu ambayo si nyembamba sana mara nyingi zinakuwa hazipati joto jingi sababu hewa hupita kwa wingi

Oky mkuu. Vp lakini uwezekano wa copy( clone/fake) kwa lg upoje?
 
MimiTena it's your own fault to use TECNO devices, ndio maana hata hapa umewalenga Tecno.
TECNO sio wakulaumiwa kwuhusiana na ubora wa bidhaa zao, tena tusiwalaumu hata kidogo, maana walishasema wanataka wakupe experience ya smartphone at lower price, lower price goes with with crappy products.
Yaani wanataka wewe uhisi unatumia Samsung Galaxy S6 kumbe unatumia TECNO C8.

Lakini hao jamaa wanapotakiwa kulaumiwa ni kwenye bei tu, maana haziendani na ubora wa devices zenyewe kama walivyokuahidi muAfrica.
BTW
Nashindwa kukurecommend which smartphone you should pick, but wait for Samsung Galaxy S7 for entertainment, though if you're not a savy user, lakini kama una matumizi zaidi ya haya yakawaida kweli basi NEXUS series ndio the best zinakuja na pure android na unaweza fanya yote unayoyataka.
motorola-nexus-6-1.jpg


Hiyo Motorola Nexus ni nzuri tofauti na hii mpya ya Huawei Nexus 6P
huawei-nexus-6p-1.jpg


kwasababu nexus 6P haina wireless charging na ni teknolojia inayokuja juu nowdays.
 
Hapo chief unajuaje kama original kwa hiyo cpu z

cpu z inaonesha kilichomo ndani ya simu vitu kama soc (processor, gpu nk), battery, ram na vyenginevyo.

unachotakiwa ni kucompare specification unazoziona kwenye cpu z na zile ambazo ni halisi. specificatiob halisi zinapatikana site kama gsmarena, phonearena au website ya simu husika.

kama unashindwa kucompare just upload screenshot ya cpu z utasaidiwa kuangaliziwa kama ni original
 
cpu z inaonesha kilichomo ndani ya simu vitu kama soc (processor, gpu nk), battery, ram na vyenginevyo.

unachotakiwa ni kucompare specification unazoziona kwenye cpu z na zile ambazo ni halisi. specificatiob halisi zinapatikana site kama gsmarena, phonearena au website ya simu husika.

kama unashindwa kucompare just upload screenshot ya cpu z utasaidiwa kuangaliziwa kama ni original
Nakukubali chief asante kwa jibu zuri
 
Kwa ninavyoelewa( kuhusiana na simu kuchemka) sidhani kama ku-upgrade kutoka simu za kiwango cha chini utafute ya gharama zaidi kwamba ziko ambazo ukifanya hizo kazi hazichemki, sidhani kama ziko.

Mimi natumia Xperia z3 na kuchemka kwake ni kama kawa hasa nikiwa nimewasha data.

Kitu nilichogundua ni kwamba, Android phone apps zake zinaconsume ram sana. Simu kuchemka ni matokeo ya ram kutumika sana.

Nikawa nafuatilia review ya hii simu mpya SGS7 Edge, ambayo ram yake ni 4GB, na wengi wanasema haichemki km simu nyingine.

Sasa sijui km ni kweli. Ila kwa simu ambazo sijawahi kusikia malalamiko kwamba zinaoverheat, lumia is the best.
 
Back
Top Bottom