Simu zilizotingisha miaka ya 2000 - 2003 (Part 1)

Simu zilizotingisha miaka ya 2000 - 2003 (Part 1)

Kuna mzee mmoja,jirani yetu.Yeye alikuwa akiplay Ringtone muda wowote kwenye mkusanyiko wa watu,Hata hata akiwa peke yake lazima a play tuu.Basi ukiskia ring,tunasema mzee flan huyo anapita.

Mkuu mi nilikua nasubiria nikiwa naingia kwenye daladala naweka alarm dakika 2 mbele.. basi nikikaa ghafla simu inaanza kulia naichomoa naangalia angalia then nairudisha mfukoni.. Watu mimacho hiyoo!! Hahaaa.. dah..
 
Kwakweli ukiangalia jinsi teknolojia ya simu ilivyokimbia ndani ya miaka kumi iliyopita utashangaa sana.. Mimi simu yangu ya kwanza kabisa kununua mwaka 2002 ilikua hii hapa..
pic_3_39.jpg

dAh nilikuwa narekodi nyimbo kwenye kiredio changu cha tape afu naweka ringtone.weee full kujaza madenti geto kusikiliza mzki
 
Kumbe Usanii umeanza kitambo,Teh..Teh..Teh
thechoj
 
Last edited by a moderator:
Kumbe Usanii umeanza kitambo,Teh..Teh..Teh
thechoj

Hahaaa.. mkuu enzi zile kuwa na "mtandao" ilikua ni ishu nyingine kabisa.. Tena hasa enzi hizo ambazo simu zilikua chache yani simu ikiita kila mtu anashtuka na kugeuka kutaka kujua ni ya nani..?
 
nilianzia siemens dole gumba sijaiona then nokia jeneza;nokia toch;nk .kweli nilitamani ninunue kila toleo wakati ule
 
Philips savy sijaiona hapa.ndio ilikuwa yangu ya kwanza.
 
Maisha yanapita upesi sana..! Ukizungumzia C25 aka Twanga Pepeta unazungumzia CM yangu Enzi hizo pia C35 aka Dole Gumba daah....!! Nway kila zama na Kitabu chake...!!
 
enzi hizo tukipanda ktk vichuguu kutafuta mtandao siemen c35 ilikuwa na nguvu sana
 
Kwakweli ukiangalia jinsi teknolojia ya simu ilivyokimbia ndani ya miaka kumi iliyopita utashangaa sana.. Mimi simu yangu ya kwanza kabisa kununua mwaka 2002 ilikua hii hapa..
pic_3_39.jpg

Ni simu yangu ya pili kuimiliki Mwaka 2004 inaitwa Siemens A 50.
 
Mkuu umenikumbusha mbali sana. 2001 nikiwa f2 nilikuwa natumia siemens c25 then Nokia 3310 'jeneza'.
 
Umesahau kina motorolla x ndugu au hapa walikua bado!?cmu yangu ya kwanza kumiliki n nokia 1100 tena nilinunua kwa mtu elf 30,000 mwaka 2006 naenda advance Iringa
 
Daaah...umenikumbusha mbali sana, nimewahi kuopoa bonge la demu pale Mawela Pub mwaka 2000 nilikuwa na kitu Sony Ericsson. Si unajua mbwembwe za ile simu ikiwa na chaji kuna taa ya blue inawaka kama gari yenye alarm lock.

Simu ilikuwa kwenye mfuko wa shati, Demu alikuwa amekaa meza ya jirani na wenzake akaona mbwembwe zake. Akanisalimia then akaniomba aione nami bila hiyana nikampa, ikabidi akae meza yangu na huo ukawa mwanzo wa kuzoeana mpaka nikala mbunye. Nilifaidije....
 

Attachments

  • Simu-Sony T28 Ericsson.jpg
    Simu-Sony T28 Ericsson.jpg
    12.3 KB · Views: 190
Dah mmenikumbusha mbali sana aisee...nakumbuka hiyo 2002 nimenununa Siemens C 25 nikawa na jamaa yangu naye ana simu tulikuwa tunaambiza nipigie niko na watu ili nioshe
 
Haka kambilikimo nimekatumia mwaka 2005, kana kelele utafikiri King'ora cha gari ya polisi...
 

Attachments

  • Simu-Panasonic GD551.jpg
    Simu-Panasonic GD551.jpg
    9.9 KB · Views: 179
Dah mmenikumbusha mbali sana aisee...nakumbuka hiyo 2002 nimenununa Siemens C 25 nikawa na jamaa yangu naye ana simu tulikuwa tunaambiza nipigie niko na watu ili nioshe
Hahahahahaaaaaa...umenivunja mbavu mkuu.
 
Cm yangu ya kwanza kumiliki ni Siemens C25 al-maarufu kama twanga pepeta, 2001 hiyo halafu line tu 15,000 cm yenyewe inauzwa 180,000. Hlf nikanunua jeneza "Nokia 3310".... Nitaendelea tukiingia episode ya pili 2003-2006
 
Back
Top Bottom