TheChoji
JF-Expert Member
- Apr 14, 2009
- 6,551
- 20,260
Kama ilivyo kwa siku hizi ambapo kila mtu anataka awe na simu latest, hali ilikua hivyo hivyo miaka ya 2000 ambapo simu ndio kwaanza zilikua zinaingia. Zifuatazo ni simu ambazo zilikua maarufu kipindi kile na ukiwa nayo ulikua unajiona mtu wa maana sana..
1. NOKIA 1100 - Simu iliyouza zaidi katika historia ya simu duniani. Hadi sasa, imeuza nakala milioni 250! Pia ni kati ya simu ngumu sana kuwahi kutengenezwa. Miaka ile ilikua ni kawaida kukuta mtu anazo tatu au nne mfukoni..
2. NOKIA 3310 - Hii ndio simu inayoshikilia rekodi ya kuwa simu ngumu kuliko zote katika karne ya 21. Unaweza kuitumia kama mtwangio na bado ikaendelea kuchapa kazi.. Ndio simu ya kwanza kuja na game ya "Snake"
3. Sony Ericsson T28: Simu hii ndio iliyobadilisha muonekano wa simu kutoka kwenye maumbo makubwa na manene na kuleta umbo jembamba. Pia ilikua mwanzilishi wa "Flip phones" yaani simu zinazofunguka kwa mbele.. Ilikua kali sana.
4. SIEMENS C25: Huwezi ukawa ulikua na akili miaka ya 2000 halafu uwe hujawahi kuona simu hii.. Ilitesa sana enzi zile na kila mtu alitamani kuwa nayo.. Shuleni kwetu alikua nayo headmaster tu!
5. MOTOROLA C200: Haka kasimu kalikuwa maarufu sana miaka ya 2003 na wadada walikamatika sana hapa.. Kaliuza nakala milioni 60.
6. PANASONIC GD55: Haka kasimu kalikua ni kadogo mno.. yaani hadi ilikua sida kukabeba ila kalijizolea umaarufu sana hasa miongoni mwa wadada na masista duu wa enzi zile..
7. SAMSUNG Double-screen: Hivi visimu navyo viliibuka enzi zile na kusumbua sana.. Wadada ndio walivipenda zaidi visimu hivi vilivyokua kama yai..
8. BLACKBERRY 6230. Simu ya mwanzo kabisa kuwa na uwezo wa ku connect kwenye internet na kumuwezesha mtu kusome e-mails na mambo mengine.. Mtu wa kawaida enzi zile uliishia kuziona simu hizi kwenye muvi kwa jirani..
Kama uliwahi kumiliki mojawapo ya simu hizi gonga "like"
Itaendelea 2003 - 2005
1. NOKIA 1100 - Simu iliyouza zaidi katika historia ya simu duniani. Hadi sasa, imeuza nakala milioni 250! Pia ni kati ya simu ngumu sana kuwahi kutengenezwa. Miaka ile ilikua ni kawaida kukuta mtu anazo tatu au nne mfukoni..
2. NOKIA 3310 - Hii ndio simu inayoshikilia rekodi ya kuwa simu ngumu kuliko zote katika karne ya 21. Unaweza kuitumia kama mtwangio na bado ikaendelea kuchapa kazi.. Ndio simu ya kwanza kuja na game ya "Snake"
3. Sony Ericsson T28: Simu hii ndio iliyobadilisha muonekano wa simu kutoka kwenye maumbo makubwa na manene na kuleta umbo jembamba. Pia ilikua mwanzilishi wa "Flip phones" yaani simu zinazofunguka kwa mbele.. Ilikua kali sana.
4. SIEMENS C25: Huwezi ukawa ulikua na akili miaka ya 2000 halafu uwe hujawahi kuona simu hii.. Ilitesa sana enzi zile na kila mtu alitamani kuwa nayo.. Shuleni kwetu alikua nayo headmaster tu!
5. MOTOROLA C200: Haka kasimu kalikuwa maarufu sana miaka ya 2003 na wadada walikamatika sana hapa.. Kaliuza nakala milioni 60.
6. PANASONIC GD55: Haka kasimu kalikua ni kadogo mno.. yaani hadi ilikua sida kukabeba ila kalijizolea umaarufu sana hasa miongoni mwa wadada na masista duu wa enzi zile..
7. SAMSUNG Double-screen: Hivi visimu navyo viliibuka enzi zile na kusumbua sana.. Wadada ndio walivipenda zaidi visimu hivi vilivyokua kama yai..
8. BLACKBERRY 6230. Simu ya mwanzo kabisa kuwa na uwezo wa ku connect kwenye internet na kumuwezesha mtu kusome e-mails na mambo mengine.. Mtu wa kawaida enzi zile uliishia kuziona simu hizi kwenye muvi kwa jirani..
Kama uliwahi kumiliki mojawapo ya simu hizi gonga "like"
Itaendelea 2003 - 2005