Simu Inavunja Ndoa kama Utani ila ndo Inavunjika Kweli

Sodoku

JF-Expert Member
Feb 3, 2016
1,095
2,429
Kumekuwa na matumizi mabaya sana ya simu za mikononi hasa hizi smart phone kwa sasa. Unakuta mke na mume wamerudi kazini jioni baada ya kula wakapanda kitandani kila mtu yupo busy sana simu akichat na kuangalia nini kinaendelea kwenye insta n.k

Kama kawaida linapotokea jambo lolote la maendeleo waathirika wakubwa sana ni sisi waswahili au waafrika. Hatujui muda gani wa kutumia simu na wakati gani wa kutotumia. Si ajabu kwa sasa ukapanga appointment na mtu mkakae sehemu mpige story ukakuta mmeishia kunywa na kula ila muda mwingi wote au mhusika mmoja yupo busy na simu. Akichat, akisonya na wakati mwingine kutabasamu. Jambo hili limesababisha kukosekane upendo kwa kiasi kikubwa.

Kitandani kumekuwa balaa zaidi. Sasa mke au mume anatumia muda huu wa kuwa kitandani kujibu text zote ambazo alitumiwa asubuh na kuangalia kwenye pages za watu mbalimbali nini kimejiri na wakati mwingine ndIo hapo huanza kuchat na michepuko. Ukija kushtuka mtu anakoroma na usiku umeanza mkali. Siku imeisha.

Kuna wale wapuuzi ambao saa nne anakupigia simu anataka kukupa hi tu au wakati mwingine mtu anakupigia simu saa tano usiku unaamka unapokea anakwambia " mwanangu upo? Mbona kimya sana? Nipe story" huu ni ustaarabu mmbovu sana. Mimi binafsi mwisho kumpigia mtu simu ni saa mbili na nusu. Nami ifikapo saa tatu huwa sipokei simu isipokuwa kutoka kwa watu ambao nadhani pengine wana dharula.

Wenzangu lazima tuwe na heshima na ndoa au mahusiano. Simu zina wakati wake, si wakati wote mtu unapiga simu. Unanipigia simu asubuhi saa 12 au saa 1 na huku hauna jambo la maana. This isnt right. Kama tuna utaratibu flan its ok lakini kuna mida mizuri ya kumpigia mtu simu. Subiri weekend au lunch time kwa wafanyakazi. kama una dharura its ok. Ukipiga mara moja hajapokea tuma text. pia si akili kupiga simu mara 3 na kuendelea ikiwa mhusika hapokei.kawaida mara mbili inatosha sana ukiona hapokei unaacha unatuma text.

mida hiyo ya usiku ndo huwa wanaume na wanawake wengine wanajikuta wanaavyochat nawe wanaingia tamaa na kukutamkia maneno au kukuandikia maneno ya kimahaba...maana obvious mhusika anaona upo free sana hivyo utakuwa mpweke. mwenzako anapopata text au kusikia sauti kama hiyo tayari ni ugomv na hatimaye week mbili zilizopita mfanyakazi mwenzangu kamwacha mkewe baada ya kukuta texts nyingi zinazotumwa usiku kumtakia usiku mwema. kumbe mke anachat muda wote jamaa akiomba mke anajibu amechoka sana.jamaa aka conclude basi anayechat naye ndiye humchosha. wakaachana kwa ugomvi mkubwa sana.
 
Simu majanga sana, mnaweza panga kutana na washkaji mpige pombe. Mpo kwenye meza kila mtu busy na simu. Technolojia ina mazuri na mabaya yake.
 
Halafu kuna wale wafanyakazi wanao toa huduma kwa watu mfano: Ma'teller, kuna baadhi yao unakuta kuna foleni ya watu kabisa halafu unakuta mtu anachat. Kiukweli uvumilivu huwa unanishinda, ninawaondoleaga uvivu mie.
 
FB_IMG_1502913682973.jpg
 
Inasikitisha sana...

Simu hujaenga kama ikitumiwa vizuri...

Simu hubomoa na kuleta mtafaruku kama ikitumiwa vibaya...


cc: mahondaw
 
Mm na mke wangu ni watumiaji wazuri wa cm hizi lakini tumejiwekea utaratibu mzuri,kwanza hatutumii kwa kuchati ovyo na jinsia tofauti sanasana ni kwaajili ya kuzurura mitandaoni,ila ukifika wakati wa kula,kulala au kujadili mambo ya kimaendeleo huwa tunaweka simu pembeni. Wanandoa msipojadili namna ya kudhibiti nidhamu ya matumizi ya simu kweli mtafarakana. Mm mke wangu mpaka mabosi na marafiki zake wa kike ameshawakataza kumpigia cm usiku so mambo yanaenda vizur mkiweka utaratibu
 
Mkuu umenena coz mara nyingine unakuta jamaa kaenda na mchumba/mke wake sehemu kubarizi lakini mwisho wa siku ukijakuangalia unakuta kila mtu katulia na simu kama yupo internet cafe, na mwisho wa siku badala ya kuongea mambo ya maendeleo ya mahusiano yao na maendeo ya kiuchumi wanaishia tu kuondoka pasipo kutimiza lengo.

Kikubwa mimi ninachoona ni vyema tukawa na mipaka na haya masimu yetu nikimaanisha kwamba ukifika home pale kitandani kwako wewe na mke/mme wako ni sehemu takatifu hivyo inahitaji utulivu wa hali ya juu na hii iende sambamba na kuzima data.
 
Mimi binafsi mwisho kumpigia mtu simu ni saa mbili na nusu. Nami ifikapo saa tatu huwa sipokei simu isipokuwa kutoka kwa watu ambao nadhani pengine wana dharula.
Utaratibu mzuri mkuu.
 
Mimi binafsi mwisho kumpigia mtu simu ni saa mbili na nusu. Nami ifikapo saa tatu huwa sipokei simu isipokuwa kutoka kwa watu ambao nadhani pengine wana dharula.
Hii point sana mkuu japo wachache wanaweza kuielewa
 
Hawajielewi, mwenza wako akiwepo yakupasa kujibu message za muhimu tu na ukipiga upige simu za muhimu. Wakati hayupo waweza peruzi
 
kuna watu ni machiz simu sana....wanazithamini simu kuliko wenza wao...wanataman ata kungekuwa na apps za kusex waminyane online
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom