Simbachawene, una habari ya huu uozo?

Simbachawene, una habari ya huu uozo?

Zamazamani

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2008
Posts
1,903
Reaction score
828
Mkuu,

Salamu kwako,

Napenda kuleta malalamiko yangu kuhusu utendaji wa TANESCO. Ingawa najua siyo habari mpya ila hii inanishangaza sana! Pale mtaani tunapokaa, maeneo ya Victoria, mtaa wa Uporoto kuna tatizo la umeme ambalo limedumu zaidi ya mwaka sasa! Yaani huwa unakatika karibu kila siku na mafundi wakija wanabadilisha kifaa fulani kwenye transfoma then unawaka.

Lakini kesho yake au baada ya muda mfupi tatizo linajirudia. Hali hii imekuwa ikiendelea kila siku! Tumejaribu kuulizia wanasema load imeongezeka nk.

Sasa swali linakuja; ina maana kadhia hii haina mwisho? Mbona imechukua muda mrefu sana kupata ufumbuzi? Tukipgiga simu pale kitengo cha dharura, wanatuambia kwamba wakubwa wanajua na wamekuwa wakiwaeleza! Sasa tupo kwenye Dilemma kuu, hatujui hatma ya hii kitu manake vifaa vyetu vya umeme vimeungua mpaka basi, Inakatisha tamaa!

Naomba uweke siasa pembeni, sasa imekuwa ni ajabu ukiona umeme haujakatika kwa siku mbili, yaani tunashangaa!

Mheshimiwa Waziri, umeshaongea mengi kuhusu kuboresha utendaji tangu umeingia hapo wizarani, Hebu acha mambo ya Siasa. Hebu tunaomba ufanye kitu hapo TANESCO mkoa wa Kinondoni.

Mungu akuongoze!
 
Mkuu Salamu kwako,

Napenda kuleta malalamiko yangu kuhusu utendaji wa TANESCO ingawa najua siyo habari mpya ila hii inanishangaza sana!

Pale mtaani tunapokaa maeneo ya Victoria ,mtaa wa Uporoto kuna tatizo la umeme ambalo limedumu zaidi ya mwaka sasa,yani huwa unakatika karibu kila siku na mafundi wakija wanabadilisha kifaa fulani kwenye transfoma then unawaka lakini kesho yake au baada ya muda mfupi tatizo linajirudia.

Hali hii imekuwa ikiendelea kila siku! Tumejaribu kuulizia wanasema load imeongezeka nk.

Sasa swali linakuja, Ina maana kadhia hii haina mwisho ? Mbona imechukua muda mrefu sana kupata ufumbuzi?

Tukipgiga simu pale kitengo cha dharura ,wanatuambia kwamba wakubwa wanajua na wamekuwa wakiwaeleza!Sasa tupo kwenye dilemma kuu hatujui hatma ya hii kitu manake vifaa vyetu vya umeme vimeungua mpaka basi.

Inakatisha tamaa, naomba uweke siasa pembeni sasa imekuwa ni ajabu ukiona umeme haujakatika kwa siku mbili tunashangaa!

Mheshimiwa waziri, umeshaongea mengi kuhusu kuboresha utendaji tangu umeingia hapo wizarani..Hebu acha mambo ya siasa.

Tunaomba ufanye kitu hapo TANESCO mkoa wa Kinondoni.

Mungu akuongoze.
 
kama walijua itakuwa overloaded, waliongeza wateja wa nini...

Na ikiwa vifaa vinaharibika mara kwa mara hilo ni tatizo.
 
Hayo magumashi sio huko 2 ngoma TANESCO UKONGA toka mwezi 12 mwaka jana hawana nywaya mpaka sasa TANESCO ni moja ya idara zenye matizo kiutendaji, mfumo na kiubunifu naishauli selikali ifanye kama TTCL wakalibishe ushindani wa kiutendaji
 
Wadau kwa tunaoishi dar kwa siku za karibuni kumekuwa na tatizo kubwa la umeme, kuna mgao wa kimyakimya na kwingine umeme unawaka na kukatika hovyo tatizo ni nini? au hujma zimeanza?
 
Back
Top Bottom