Ukweli ni kwamba gap sio kubwa sana ndio maana Yanga kashinda mechi moja tu kapanda juu sana, wasiwasi wangu ni kwamba Simba inapoelekea ni pabaya zaidi kwa sababu wameshaanza kuangushia watu jumba bovu kwa maamuzi ya hasira na si busara, mchezaji kucheza hovyo kwa mechi moja ni jambo la kawaida sana hasa inapokuwa kwa mkongwe kama Kiemba ambaye hajapumzishwa iwe ni kwa klabu au timu ya Taifa hata hizo shutuma kwamba ile mechi ya starz alicheza vizuri nazo si za kitaalamu kwani timu nzima siku ile ilionekana NZURI kwa kushinda
Hali mbaya sana ni kwamba kuna njama zinapangwa za kumuangusha Aveva ambazo kama zitafanikiwa ni kwamba akina Aveva nao (Friends) watapanga njama za kuwaangusha watakaoshika timu..........(cycling) hatari zaidi hapo ni kwamba wao ndioa wamesajili kwa asilimia kubwa
NAIONA SIMBA IKIJIHATARISHA KUSHUKA DARAJA .............lol
Tulizoea timu zetu kushinda kimchekea sana (kwa kuhonga etc) ukweli ni kwamba kwanza wachezji wa timu hizi hawapishani sana viwango, wengi ni vijana wenye ari ya kucheza, soka la Tanzania limekua na hamasa kubwa (uwanja mzuri na mechi kuoneshwa LIVE) kila mchezji akitaka kung'aaa, hivyo upinzani wanaokabiliana nao Simba ni wa kawaida tu kimchezo sema hatujazoea hali hii...Hat timu yangu Liver huko UK inakamatwa sana na vitimu sasa hivi.
TUkubali ukweli kwamba timu zinasajili VIPAJI na si MAJINA siku hizi (UHAI CUP, COCACOLA etc) the CASE of Mtibwa Sugar etc