Simba vs Yanga: Oct 03, 2012

alafu ikumbukwe kwamba: Bahanuzi style yake ya kucheza mpira ni kukaa nyuma ya Beki akisubiri atanguliziwe mpira; kwa wachezaji wazoefu kama wa Simba style hiyo ilikua ngumu kuwa applicable na ndo maana muda wote alionekana anaotea.
 

La ball possesion siyo la kwangu Mkuu,mi nimenukuu tu kuota kituo cha radio na television ambacho kilionyesha mchezo huo jana,wame'compute vipi wanajua wenyewe...lkn coming back to Mwamuzi na Msaidizi wake sikatai inawezekana ikawa kweli kuna maamuzi yaliyokuwa yanai'favour Yanga lkn hayo hayawezi kuwa zaidi ya yale yaliyokuwa yanai'favour Simba,nitakuambia machache tu:-
Kaseja alikuwa anapoteza muda sana from 1st half baada ya Simba kupata goli la kuongoza lkn hakuchukua hatua yeyote zaidi ya kumuonya kwa mdomo kama mara 3 hv,angalia offsides walizokuwa wanaamua...unajua Bahanuzi si kweli kwamba huwa anakaa nyuma ya mabeki hapana Bahanuzi huwa anasimama mbele ya mabeki na inapopigwa pasi ya kutanguliza ndo huwa anachomoka kuwapita mabeki na kuipokea,matukio kama ma'2 ma'3 hv yalikuwa ya aina hiyo lkn wale Mabwege(am sorry to identify them in this way) walikuwa wanaona offsides..kuhusu card ya Edo angalia vizuri ni kweli wakati anamchomoka Canavaro alifanya kama kumvuta hivi kidogo akajishtukia akamwachia na kunyoosha mikono na Dogo akaendelea na move mbele kidogo alivyoona ameshaingia kwenye penalt area ndo akajiangusha ndo maana ikaonekana dhahiri amejiangusha,angekuwa smart sana wkt alipovutwa kidogo angejiachia palepale lkn mwenyewe dizaini aliona haina faida ksbb ilikuwa nje kidogo ya penalt area
 

Huyo best striker wa East Africa ameshindwa kuonesha makali yake kwa Mtibwa, mmekula tatu bila na yeye akiwemo. Mmeshindwa kuwafunga Prisons, mmeshindwa kuwafunga Simba jana wakiwa wamefixture Yosso.

I must admit defence ya Yanga inamuogopa Okwi kuliko unavyofikiri. Mchezaji yeyote ambaye ana go past defenders ni hatari usisikie. Waulize mabeki wa Yanga kwenye tano bila watakuambia Okwi ni nani, wewe huwezi kujua kwa sababu hukuwa unakabiliana nae.

Hebu jaribu kufikiria kabla ya game ya Simba na Yanga Simba alikuwa na record nzuri sana ya kutokufungwa hata mechi moja and yet Yanga ndio waliokuwa na confidence zaidi ya kushinda, the reason is simple, mtu wanaemhofia hakuwepo. Kumkaba Bahamuzi ni rahisi sana cos anasubiri apigiwe mpira na mabeki akimbie, it is not the case with Okwi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…