Simba vs Yanga michuano ya kimataifa

Las Mas Bobos

JF-Expert Member
Jun 15, 2012
991
326
Kuna hii tabia ya vyombo vya habari vya hapa nyumbani kupenda kuikweza Simba inapokwenda kuiwakilisha Tanzania nje ya nchi. Utasikia watangazaji wanavyoipamba na magazeti yanavyoiandika vizuri na kuibeza Yanga kabla haijaondoka.

Waandishi hawa wa kichaga wasiojua michezo sijui huwa wana rekodi gani ya Simba yenye kuonesha mafanikio nje ya Tanzania. "..simba ambayo imekuwa na rekodi nzuri katika kuiwakilisha Tanzania nje ya nchi inatarajiwa kuondoka kesho kwenda kukipiga na Haras Al Hadood ya Misri....."

Wakiwa ni Yanga ndio wanatoka, utaona wakianza kuzungumzwa vibaya hata kabla ya mechi yenyewe. Sasa mimi nauliza swali: KATI YA SIMBA NA YANGA, TIMU IPI IMEWAHI KUBEBA UBINGWA NJE YA NCHI NA KUULETA NYUMBANI?

Hapa sizungumzii kombe la Maulid linalochezwagwa Zanzibar, manake wengi wenu mnadhani Zanzibar ni nje ya nchi. Kwanza Yanga hawanaga interest na kakikombe ambako mshindi anapata laki 8 ilhali gharama za kuipeleka timu Zanzibar ni 8m.

Naomba majibu kutoka kwa waandishi uchwara na wapenzi wa hii timu ya kina 'Jumaa' (wafanyakazi wa ndani wa wahindi) yenye maskani sokoni bila uwanja hata wa kupigia dana dana.
 
Pole we Yanga. Kuwa makini na mapenzi ya hizo timu utaumia na kupata wazimu.
 
Vyombo vya habari vipo sahihi kutokama na ukweli kwamba simba huwa inatuwakilisha vizuri nje tatizo lenu mashabiki wa yanga mmeathiriwa na siasa mbovu za ccccm ie nape mnataka sifa wakati uwezo nothing acheni kufikilia kwa kutumia kucha
 
Simba alishafika fainali ya Confederation Cup mwaka 1993 na pia alishafika nusu fainali Champions League mwaka 1974 kama sijakosea. Na ni juzi 2 walikaribia kufika ktk hatua ya makundi (quarter finals) baada ya kutolewa na Al Ahly Shandy kwa penati 12_11. Nipe rekodi ya Yanga? Halafu jibu baki nalo mwenyewe..

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Simba alishafika fainali ya Confederation Cup mwaka 1993 na pia alishafika nusu fainali Champions League mwaka 1974 kama sijakosea. Na ni juzi 2 walikaribia kufika ktk hatua ya makundi (quarter finals) baada ya kutolewa na Al Ahly Shandy kwa penati 12_11. Nipe rekodi ya Yanga? Halafu jibu baki nalo mwenyewe..

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Hapo kwenye RED ndio panakuombea msamaha, otherwise ungekoga matusi yangu mkuu.

Kufika fainali si kuchukua kombe. Mimi niliuliza ikiwa mmeshawahi kubeba kitu chochote mkaja nacho nyumbani.

Na kwa taarifa yako, Yanga ndio timu ya kwanza ya Tanzania kufika Quarter Finals za Champions League. Ni baada ya kuifunga Coffeu ya Ethiopia bao 6-0. Mechi iliyofuata haikuwa nzuri kwetu kwani tulifungwa bao 8 na Raja Casablanca ya Morocco.

Mara 2 Yanga imekwenda ugenini na kuleta ubingwa wa Africa Mashariki na kati. Narejea swali langu, Simba ilishawahi kuja na medali toka nje?
 
Vyombo vya habari vipo sahihi kutokama na ukweli kwamba simba huwa inatuwakilisha vizuri nje tatizo lenu mashabiki wa yanga mmeathiriwa na siasa mbovu za ccccm ie nape mnataka sifa wakati uwezo nothing acheni kufikilia kwa kutumia kucha

Sijaona ulichoeleza, imetuwakilisha vizuri vipi?

Yanga ndio imewahi kupanda ndege na kombe, si Simba. Sasa nje wapi huko Simba ilikoenda kufanya ugomvi ikashinda, just tell me niwape saluti.

Huo ubishi wa kiswahili mimi siuwezi maana umeanza kunichefua na jina la Nape. Hayo ya kwako na Nape endeleeni Lumbumba mnakokutanaga, mimi nauliza hivi: SIMBA AMESHAWAHI KUBEBA NDOO UGENINI?
 
Pamoja na kwamba simba haijawahi kuleta kombe kubwa la afrika ukiacha afrika mashariki na kati lakini imekuwa na rekodi nzuri ya michuano ya kimataifa kulinganisha na yanga mara nyingi yanga imekuwa ikitolewa hatua za awali hata na zile timu zinazooneka dhaifu afrika
Jaribu kufatilia ushiriki wa yanga kwenye michuano ya kimataifa miaka 5 iliyopita na simba ndio utagundua ukweli
na hata kwenye ranking za vilabu afrika Simba iko juu
 
Kuna hii tabia ya vyombo vya habari vya hapa nyumbani kupenda kuikweza Simba inapokwenda kuiwakilisha Tanzania nje ya nchi. Utasikia watangazaji wanavyoipamba na magazeti yanavyoiandika vizuri na kuibeza Yanga kabla haijaondoka.

Waandishi hawa wa kichaga wasiojua michezo sijui huwa wana rekodi gani ya Simba yenye kuonesha mafanikio nje ya Tanzania. "..simba ambayo imekuwa na rekodi nzuri katika kuiwakilisha Tanzania nje ya nchi inatarajiwa kuondoka kesho kwenda kukipiga na Haras Al Hadood ya Misri....."

Wakiwa ni Yanga ndio wanatoka, utaona wakianza kuzungumzwa vibaya hata kabla ya mechi yenyewe. Sasa mimi nauliza swali: KATI YA SIMBA NA YANGA, TIMU IPI IMEWAHI KUBEBA UBINGWA NJE YA NCHI NA KUULETA NYUMBANI?

Hapa sizungumzii kombe la Maulid linalochezwagwa Zanzibar, manake wengi wenu mnadhani Zanzibar ni nje ya nchi. Kwanza Yanga hawanaga interest na kakikombe ambako mshindi anapata laki 8 ilhali gharama za kuipeleka timu Zanzibar ni 8m.

Naomba majibu kutoka kwa waandishi uchwara na wapenzi wa hii timu ya kina 'Jumaa' (wafanyakazi wa ndani wa wahindi) yenye maskani sokoni bila uwanja hata wa kupigia dana dana.


Mkuu unazungumzia rekodi nzuri ya jumla kwenye mechi za kimataifa au timu iliyowahi kuchukua kombe ugenini?
 
Back
Top Bottom