Simba na Yanga mpaka sasa kutokuwa na Viwanja vyao vyenye hadhi ya Kimataifa? Tatizo ni TFF, Sera au ?

Robert S Gulenga

JF-Expert Member
Jan 3, 2013
2,161
1,493
Simba na Yanga ni vilabu vikongwe na vikubwa si Africa Mashariki tu bali Afrika kwa ujumla.

Yanga na Simba zina historia kubwa pengine kuliko vilabu vingi Africa, historia zao zimejengwa katika lengo lililofanya vilabu hivi kuazishwa miaka zaidi ya 63 iliyopita.

Vilabu hivi unaweza kuviita ni vilabu vyenye mafanikio kwa maana ya ndani ya Uwanja lakini si nje ya Uwanja.

Miaka zaidi ya 60 toka kuazishwa kwake vilabu hivi havijaweza kuwa na viwanja vyao vyenye hadhi na ubora wa vilabu hivi.

Msingi wa timu yeyote ya mpira Duniani ni uwekezaji katika uwanja wa kisasa wa mpira, kwanini Yanga na Simba haviwekezi katika Viwanja vyao vya kisasa?

Shida ni Wasimamizi wa mpira ? Kwa maana ya TFF? Shida ni Sera za nchi? Shida ni uongozi wa vilabu hivi?

Wakati macho na maombi ya Watanzania yako kwa timu hizi mbili ziweze kuvuka hatua ya Robo. Ni vizuri Vilabu hivi vijiulize ni timu gani zimeingia hatua ya Robo hazina viwanja kama Simba na Yanga?

Tanzania sasa ni moja ya nchi ambayo mpira unakua kwa kasi kubwa sana, uwekezaji katika maslahi ya Wachezaji ni mkubwa kuliko nchi nyingi za Africa.

TFF wahimize, washirikiane, wawaongoze na kushauri kuhakikisha vilabu hivi vinakuwa na Viwanja vyenye hadhi ya Kimataifa

Pengine kwa mara ya kwanza tunaweza peleka timu mbili katika hatua ya nusu fainali katika moja ya michuano mikubwa zaidi kwa ngazi za vilabu Africa

Tuwaombee Simba na Yanga.

Tanzania kwanza.
Mungu ibariki Tanzania
 
Simba na Yanga ni vilabu vikongwe na vikubwa si Africa Mashariki tu bali Afrika kwa ujumla.

Yanga na Simba zina historia kubwa pengine kuliko vilabu vingi Africa, historia zao zimejengwa katika lengo lililofanya vilabu hivi kuazishwa miaka zaidi ya 63 iliyopita...
Kwa timu kutokuwa na viwanja sabb kubwa ni sera mbovu inayopelekea uwepo wa kodi na tozo zinazofanya timu zisiwe na viwanja vyao.

Kuna wakati kuliletwa majani bandia kwa ajili ya kiwanja fulani, hadi kutoka hapo bandarini kwenda sehem husika ilikuwa vuta nikuvute kwamba lazima kodi ilipwe.

Sasa majani tu, vipi kiwanja kizima..ujenzi, viti, vifaa vya mazoezi, tiba, nk itakuwaje..si bora kuacha, pengine wanajua Tanzania hakuna wachezaji kuna wababaishaji tu!
 
Kuwa na mashabiki wengi ni ndani ya uwanja au ni nje ya uwanja?
Mafanikio ya nje uwanja ni uwekezaji ambao vilabu vinafanya.
1. Wekeza kwenye viwanja
2. Wekeza timu za vijana
3. Kuwa na Mipango endelevu hata Mo na GSM watakapoondoka vilabu viweze lipa mishahara
4. Wekeza katika vifaa vya kisasa.
5.....

Vilabu vya Simba na Yanga kuwa na mashabiki wengi sio kwa sababu ya uwekezaji wa vilabu ila ni kwa sababu ya Watanzania wanapenda mpira, timu hizi mbili zimepata advantage ya kuwa vikongwe hivyo ina generational mashabiki
 
Kwa timu kutokuwa na viwanja sabb kubwa ni sera mbovu inayopelekea uwepo wa kodi na tozo zinazofanya timu zisiwe na viwanja vyao..kuna wakati kuliletwa majani bandia kwa ajili ya kiwanja fulani, hadi kutoka hapo bandarini kwenda sehem husika ilikuwa vuta nikuvute kwamba lazima kodi ilipwe..sasa majani tu, vipi kiwanja kizima..ujenzi, viti, vifaa vya mazoezi, tiba, nk itakuwaje..si bora kuacha, pengine wanajua Tanzania hakuna wachezaji kuna wababaishaji tu!
Mbona Azam wamejenga?

Mkuu TrueVoter unajua kama kuna msamaha wa kodi kwenye vifaa vya Uendelezaji viwanja vya michezo? Shida watu janja janja nyingi sanaa ..wanataka kutumia mwanya huo kujinufaisha. TRA lazima ijiridhishe
 
Ndugu viwanja vyenye international standards ni aghali sana.

Wewe mwenyewe si umesikia kiwanja kijacho cha arusha ni bilion 200+

Bajeti ya wote simba na yanga kwa mwaka haifiki Hata bilion 50.

Ni ulaya tu ndio vilabu vina viwaja kuanzia Manchester hadi akina luton.

africa si mamelodi si al ahly hawana viwanja
 
ni upigaji na kuchagua viongozi wasio na vision. hivi vilabu vimejaa viongozi matapeli na wezi sugu ndio maana mpaka sasa wameshindwa kuongeza majengo mapya.
 
Viongozi wengi wa hivi vilabu viwili wamekuwa na maneno mengi kuliko vitendo! Halafu wengi ni wajanja wajanja, na wamekuwa wakivitumia hivi vilabu kama daraja la kufikia malengo yao ya kisiasa, na pia kiuchumi.

Binafsi nimekaa pale 👉 😎 nasubiria Aprili ifike ili nishuhudie ule ujenzi wa uwanja wa Yanga tulioahidiwa, ukianza kujengwa.


Haiwezekani vilabu vilivyoanzishwa miaka ya 2000 vina viwanja vyao vizuri. Halafu Yanga na simba zilizoanzishwa miaka ya 1930's, eti mpaka leo hawana viwanja vyao binafsi! Huku ni kujiendekeza bila shaka.
 
Timu zimejaza mashabiki oya oya wasio na Msaada wa kiuchumi Kwa timu unategemea vilabu vitoe wapi Hela ya kujenga viwanja?.. lipeni kadi za uanachama bila shuruti uone kama hawatajenga pitch
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom