Simba SC kufungwa tena na Kaizer Chiefs

Simba SC kufungwa tena na Kaizer Chiefs

Sheikh23

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2016
Posts
1,202
Reaction score
2,001
Habari wana jamvi,leo jioni itakua siku nyingine chungu kwa mashabiki wa Simba SC,Kaizer anaenda kutoa kipigo kingine kama sio kinachofanana na kilichopita (4G) basi chini kidogo ya kipigo kilichopita (Kaizer3_Simba SC1) au (Kaizer5_Simba SC 2)

*kocha hana game plan zaidi ya biriani[emoji1787][emoji1787]

*hajui muda amfanyie sub nani,hana timing nzuri ya substitution

*beki ya simba inaaminiwa ni Beki bora ilhali ni beki mbovu,Mo Husein siyo yule wa zamani,kwasasa ni uchochoro,Kapombe ni homa za vipindi,performance yake haitabiriki.

*Forward ni butu,specifically Mugalu ni galasa,kuanzishwa kwa Mugalu ni red card kwa timu.Inafaa aanzishwe Bocco au Kegere kutegemea au wote kwa pamoja itategemea na mfumo/game plan ya kocha.

*Kiungo cha Mkude,Injinia Thadeo hakina ubunifu,kinacheza kizamani sana,waige kwa Mukoko na Feisal wa Yanga SC[emoji123]

*Miquisone na Chama ni watu[emoji109][emoji122][emoji122][emoji122],na hawa ndio engine ya timu ya Simba kwa sasa,shida ni pale timu inapozidiwa hata kikubwa wanachofanya hakionekani (refer last game)

*Bwalya ni homa za vipindi,performance yake haitabiriki.

*Manura ni kipa mbovu kucheza mipira iliyokufa,ni kipa anayepotea anapotunguliwa magoli ya mapema,kama unaanza kushabikia soka leo hili huwezi kulijua...

■Nakiona kipigo kingine kwa Simba leo,tujiandae kisaikolojia...

Sheikh23View attachment 1793629
20210516_143349.jpg
 
Sawa mkeka tumeuona subiri matokeo sasa
 
Hawa ndo wachawi wenyewe pumbavu
Ndg napenda Simba ishinde ili izidi kulitangaza soka letu kimataifa but analytically kwa uwezo wa player mmoja mmoja wa simba vs kaizer,na zile spidi za Simba ikiwa taifa,pasi nyingi (biriani) zisizo na maamuzi ya mchezo ninaiona kaizer ikienda kutoa kipigo tena,tujiandae..
 
Umenajisi sana jina/cheo cha Sheikh23 .

Hivi Manura ni kifaa gani katika vyanzo vya nishati nchini?

Unasema kocha hana plan nzuri wakati huo huo unasema kagere au Bocco wakicheza Pamoja ni bora kuliko Mugalu kama plan za kocha zikiwa hivyo.
 
Back
Top Bottom