Congo
JF-Expert Member
- Mar 13, 2008
- 2,079
- 2,333
Leo 25.7.2022 ni siku ya mashujaa. Tarehe hii imechaguliwa kwa sababu ndio tarehe zilipofanyika sherehe za kwapokea askari wetu walioenda kukomboa Kagera na baadaye kupigana Uganda. 25.7.1979.
Jana na leo TV zimetumia muda wao kuonyesha sinema ya vita hiyo ya Uganda.
Mie natofautiana sana na wazo la kuifanya siku hii kuwa siku ya mashujaa.
Kwanza, niwape mfano hivi unaweza kusherehekea kupigana na nduguyo hata kama amekuchokoza? Natumaini inatakiwa baada ya kukuchokoza mkapigana hata kama umeshinda ukae na kuanza kusikitika kwa nini nduguyo alikuvamia au alikuchokoza na hatimaye mkapigana. Mnatakiwa kujutia ugomvi wenu badala ya mmoja kusherehekea ushindi wa kumpiga nduguye. Waganda nawaona kama ndugu zetu. Hata kama tulipigana ilikuwa kumuondoa Idi Amini wala sio kushinda vita. Tunatakiwa kusikitika kwa nini ndugu zetu watuvamie, hatimaye wasababishe tupigame vita. Siku hii ingekuwa siku ya kutukuza amani na kusema isitokee tena kupigana na ndugu zetu.
Pili, hivi kwa siasa za Uganda kesho na kesho kutwa wakibadili sera yao na kumuona Amini kama shujaa wao, na kuamua kumuenzi sisi tutasemaje.
Tujitafakari sana kuviona vita ya Uganda kama ndio vita pekee vya ushujaa.
Kwangu mie MASHUJAA ni hawa.
1. Mkwawa, Kinjekitile, Bushiri na viongozi na wapiganaji wote waliopigana dhidi ya wavamizi wa kikoloni.
2. Wazazibar walioshiriki mapinduzi ya Zanziba 12.1 1964.
3. Wapiganaji wote walioshiriki vita ya ukombozi wa bara la Africa. Walikuwa wanaondoa ukoloni.
4. Viongozi walioshiriki kuanzisha vuguvugu la kupigania uhuru wa Tanganyika. Watambuliwe kwa ushujaa wao huo.
Tarehe 25.7.2022 ibadilishwe kuwa siku ya JWTZ ambayo wataitumia kutuinyeshq shughuli wanazozifanya.
N.B. Waliopigana vita kuu kwangu mie sio mashujaa kwa sababu walikuwa wanatumikia ukoloni. Wana siku yao ya kumbukumbu za vita hizo.
Jana na leo TV zimetumia muda wao kuonyesha sinema ya vita hiyo ya Uganda.
Mie natofautiana sana na wazo la kuifanya siku hii kuwa siku ya mashujaa.
Kwanza, niwape mfano hivi unaweza kusherehekea kupigana na nduguyo hata kama amekuchokoza? Natumaini inatakiwa baada ya kukuchokoza mkapigana hata kama umeshinda ukae na kuanza kusikitika kwa nini nduguyo alikuvamia au alikuchokoza na hatimaye mkapigana. Mnatakiwa kujutia ugomvi wenu badala ya mmoja kusherehekea ushindi wa kumpiga nduguye. Waganda nawaona kama ndugu zetu. Hata kama tulipigana ilikuwa kumuondoa Idi Amini wala sio kushinda vita. Tunatakiwa kusikitika kwa nini ndugu zetu watuvamie, hatimaye wasababishe tupigame vita. Siku hii ingekuwa siku ya kutukuza amani na kusema isitokee tena kupigana na ndugu zetu.
Pili, hivi kwa siasa za Uganda kesho na kesho kutwa wakibadili sera yao na kumuona Amini kama shujaa wao, na kuamua kumuenzi sisi tutasemaje.
Tujitafakari sana kuviona vita ya Uganda kama ndio vita pekee vya ushujaa.
Kwangu mie MASHUJAA ni hawa.
1. Mkwawa, Kinjekitile, Bushiri na viongozi na wapiganaji wote waliopigana dhidi ya wavamizi wa kikoloni.
2. Wazazibar walioshiriki mapinduzi ya Zanziba 12.1 1964.
3. Wapiganaji wote walioshiriki vita ya ukombozi wa bara la Africa. Walikuwa wanaondoa ukoloni.
4. Viongozi walioshiriki kuanzisha vuguvugu la kupigania uhuru wa Tanganyika. Watambuliwe kwa ushujaa wao huo.
Tarehe 25.7.2022 ibadilishwe kuwa siku ya JWTZ ambayo wataitumia kutuinyeshq shughuli wanazozifanya.
N.B. Waliopigana vita kuu kwangu mie sio mashujaa kwa sababu walikuwa wanatumikia ukoloni. Wana siku yao ya kumbukumbu za vita hizo.