Elections 2015 Siku tano za kampeni: Chokochoko za CCM, serikali yake na vyombo vya ulinzi

Jun 20, 2009
45
225
SIKU TANO ZA KAMPENI: YAFUATAYO YANAONESHA DHAHIRI KUWA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA NA MAMLAKA ZA SERIKALI ZINASHIRIKIANA NA CCM KUJARIBU KUHARIBU UCHAGUZI HUU;


Na. Julius Mtatiro.


1. Kumzuia mgombea urais wa CHADEMA/UKAWA kuhudhuria msibani eti kwa sababu amesindikizwa na watu, kana kwamba watu walewale kwa idadi ileile wangekwenda wenyewe wangeleta madhara yoyote. Najiuliza tu, ingekuwaje mgombea na watu wale wangelazimisha kwenda msibani; JIBU: Mapambano na Polisi, mgombea kukamatwa na kufunguliwa kesi, wafuasi kujeruhiwa kwa risasi, kuuawa ama kukamatwa.


2. Kupiga Marufuku maandamano na mbwembwe za kuwasindikiza wagombea kurejesha fomu. Hili lilifanywa mara baada ya Magufuli na Lowassa kwenda kwa maandamano lakini yale ya Lowassa yakionekana kuwa na maelfu mengi ya watu zaidi kuliko ya magufuli. Lakini pamoja na marufuku hiyo majuzi nimejionea wafuasi wa CCM wakiandamana kutoka Manzese hadi Jangwani wakiwa na MASABURI, bila polisi kuwazuia.


3. Kuzuia mgombea wa UKAWA/CHADEMA kufanya ziara maalum za kushtukiza kuwatembelea wananchi wa kawaida. Hizi zinapigwa marufuku kwa mgombea huyu wakati wale wa CCM wakifanya watakavyo. Mfano ni Bi. Samia Suluhu alivyoonekana Moshi akiacha ratiba ya ziara na kutembelea raia mtaani bila kukatazwa na Polisi.


4. Kuzuia UKAWA kufanya mkutano wake wa uzinduzi Uwanja wa Taifa na hata UKAWA ilipoamua kufanyia mkutano huo katika viwanja wa JANGWANI umezuiwa na Manispaa ya Ilala nadhani kwa shinikizo la CCM chini ya sababu dhaifu sana kwamba kuna watu wameshaukodi, Ni halmshauri ipi hivi sasa ambayo ina-PRIORITIZE shughuli zingine kwenye viwanja vikubwa wakati vyama vya siasa viko kwenye uchaguzi mkuu jambo ambalo ni kipaumbele cha taifa kwa sasa?


5. CCM kufanya mkutano wake wa uzinduzi hadi saa 12.38 jioni tena mbele ya Mkuu wa nchi na viongozi wote wa serikali wakati wanajua fika kuwa sheria inawataka kufunga mkutano saa 12.00 jioni. Kwamba CCM na inavionesha vyama vingine kuwa iko juu ya sheria na kwamba wengine wakiiga watajiju. Na baada ya kupitisha muda huo CCM inamshinikiza Mkurugenzi wa manispaa ya ILALA aandike barua NEC kuijulisha kuwa ni yeye ndiye alielekeza mkutano uendelee hadi muda huo (very illogical reason).


6. Rais mstaafu wa awamu ya 3 Benjamin William Mkapa kusimama hadharani na kuwatukana wapinzani kuwa ni "MALOFA na WAPUMBAFU". Mpumbavu ni neno kali na lina maana ya "juha", "zuzu", "mtu asiyejielewa", "-----", "----", n.k. Wakati Mkapa akitukana hivyo hadharani na kuachwa juu ya Sheria, Lawrence Masha ambaye ni mwana UKAWA (hivi sasa) lakini zamani akiwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Tanzania, yeye amekamatwa na kuwekwa rumande na kunyimwa dhamana (inacheleweshwa kimakusudi) kwa "kosa" la kumtukana askari polisi (wengi kama sikosei) kwamba ni "washenzi", "wasio na shukrani na wasio na dini". Kwamba kwa tafsiri ya CCM na serikali yake pamoja na vyombo vinavyosimamia sheria (POLISI), neno "Upumbavu na Ulofa" siyo tusi lakini neno "Ushenzi na Kutokuwa na shukrani" ni tusi baya sana.


Hayo mambo sita niliyoyataja na mengine kadhaa ni dalili tosha kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka huu unaweza kuishia mahali pabaya. Hadi sasa sijaona CHOKOCHOKO kutoka upande wa UKAWA, hii ina maana kwamba hizi za CCM, VYOMBO VYA DOLA NA MAMLAKA ZA SERIKALI zikiendelea na zikawa zinahujumu kwa dhahiri maslahi ya UPINZANI na UKAWA, lolote lile linaweza kutokea.


Julius Sunday Mtatiro,
Dar Es Salaam.
 
Niliwahi kusema hapa 'i smell blood' katika uchaguzi Mkuu Tanzania Oktoba 25.

Pamoja na hayo, zoezi la uandikishwaji wapiga kura kisha kutohakiki majina yao,watu walioamka usiku na kushinda katika vituo vya uandikishwaji hadi jioni wakisubiri kuandikishwa. Leo hii mnawaambia majina yao hayapo? Viongozi wa CCM kuputa mitaani kuandikisha tena kadi za kupiga kura na kuchukua namba za simu..

Nakumbuka rafiki wangu(mwanajeshi mwenye cheo kikubwa tu), aliwahi kuniambia wakati tukijadili mambo ya kisiasa nchini, kwamba "mwaka huu 2015 ukishapiga kura wewe rudi utulie kwako usitake kujua mengine na ninakueleza kama rafiki".

Kuna wakati fulani tunasema 'mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni', kila mtu ana threshold ya uvumilivu, na uonevu wa wazi nchi hii unaonekana CCM kudhani "wapinzani wataleta uvunjifu wa amani" wananchi wanaona mchokozi ni nani.

MUNGU wao(wa wanyonge hawa wanaoonewa, kutukanwa na kudhihakiwa) atawatetea vinginevyo tutegemee alot of assassination attempts.
 
dalili za mvua ni mawingu....

The end ( oct , 25) will come to justify the commencement
of the given general election.
 
Kiufupi CCM wameshaona dalili zote za kushindwa, sasa wanafanya kila liwezekanalo ili kuhujumu uchaguzi na wajichukulie ushindi kwa ubabe, ama uchaguzi ushindikane na kufanya dola iliyo chini ya CCM na hivyo wataendelea kutawala.
 
Mkuu[MENTION]Julius Mtatiro[/MENTION] hizi ni "the last minutes of a dying horse"
Wacha waweweseke tu
 
Julius Mtatiro
Nimegundua kwa nini kuna binadamu huwa wanajitoa muhanga na kuua wenzao wasio na hatia. -Issues kama hizi zinazofanywa na serikali kama hii ndiyo huwa chanzo.

Huwezi amini nipo Kilimanjaro hii habari inawaumiza sana watz walio hapa na ndiyo maana wanasubiri siku.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo lenu UKAWA mnafikiria mambo ni rahisi tu kwamba mpite mnadanganya watu kuwa mnataka kuwaletea mabadiliko wakati hamuwezi halafu serikali iwaache tu mfanye mnavyotaka. Haiwezekani.
 
Chadema imeshauzwa. Kuna kila dalili kuwa mnunuzi wa Chadema anataka kuibadilisha iwe kikundi cha sanaa...

mwanasheria zuzu kikwete amebakiza siku 44 tu sijui utalamba viatu vya nani miaka mitano unakenua JF nchi imeendelea kuungua na kubaki masikini wa kutupwa
 
Tuliombee Taifa linapita kwenye kipindi kigumu, ni hatari sana kuamua jambo litakalo egemea upande wowote wakati huu,
 
Najiuliza sana huyu Lofa siku akiamua kuweka kando Ulofa wake itakuaje? Atakufa kwa risasi na mabomu lakini wanawe wataishi kwa furaha! Ndio wanayoyataka
 
Tatizo lenu UKAWA mnafikiria mambo ni rahisi tu kwamba mpite mnadanganya watu kuwa mnataka kuwaletea mabadiliko wakati hamuwezi halafu serikali iwaache tu mfanye mnavyotaka. Haiwezekani.
serikali ipi hii ya raisi wake anahongwa suti pair tano kwa kubadilishana na loliondo hii ya kumaliza asilimia sitini tembo kwi kwi itaipata safari hii na nguvu ya umma
 
Najiuliza sana huyu Lofa siku akiamua kuweka kando Ulofa wake itakuaje? Atakufa kwa risasi na mabomu lakini wanawe wataishi kwa furaha! Ndio wanayoyataka

Mkuu, they should not underestimate the power of 'stupid' people in large groups!
 
Back
Top Bottom