only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
Nimekuwa nikifuatilia mwelekeo wa hii kamati kuu mpya ya CCM tangu iingie madarakani, kwa sasa ina muda kama wa siku saba hivi, na kwa upande wangu nimeona yafuatayo.
- Uropokaji na kuongea bila kufikiria madhara yake ni kukubwa mno, hawana tofauti na akina Makamba na Tambwe, ukifuatilia kauli za Nape Nnauye na Katibu wake wakiwa Dom, Manzese DSM, Chalinze, Kibaha nk.
- Hawajui wanapambana na nani, na kama wanajua wanatupumbaza watanzania, kwa hiyo wanatapatapa kila kona bila mwelekeo.
- Bado ni waoga, wanachama mafisadi wanawajua, badala ya kuwachukulia hatua wanaropokaropoka kwa umma. Sasa tuwaelewe je?