Siku moja na Sir Andy Chande

Asante kaka kwa simulizi,Andy Chande,Rajani,Kassum ,Amir Jamal ni wazalendo hasa kuliko hata sisi Wamatumbi tunaojifanya ndio wenye nchi na hawa pamoja na utajiri wao kutaifishwa wakabaki marafiki wa Mwalimu JK Nyerere,hawakukimbia wakabaki hapahapa ingawa wengine wamezikwa Canada lakini bado historia ya nchi hii haitawasahau-Pia uandishi wako ni murua unavutia kwa mtiririko ni kama Mohamed Ganzel yule mwandishi maarufu wa riwaya wa miaka ile.Asante mkuu kwa kutoa darasa kuhusu Sir Andy
 
Tunaomba utueleze kuhusu hiyo club
Hiyo club ipo miaka mingi makao yake yapo opp na Kilimanjaro Hotel na ni siku hizi tu ambapo watu wanaiona Freemason kama inahususiana na mambo ya kichawi na utajirisho ,na kuonekana kama club ya siri,nijuavyo mimi nilianza kuijua Freemason miaka mingi na huyu Sir Andy Chande alikuwa mara nyingi yeye na wenzake wakitoa hata misaada kwa vikundi mbalimbali kama vile ilivyo Msalaba Mwekundu,katika miaka ile hatukusikia hayo mabaya yanyosemwa kuhusu FM hivi sasa na hiki ni exclusive club utamkuta mume wa Malkia wa Uingereza,maraisi na ni miaka mingi huko nyuma,siku hizi eti hutangazwa na waganga kwa kubandika matangazo kuwa watawaingiza watu kwenye FM ,huo ni upotoshaji na dhana nzima juu ya Freemason,hapa Tanzania wapo wengi wanachama wa hiyo club ni matajiri kama ilivyo kwa club nyingine exclusive kama Msalaba Mwekundu,Red Crescent n.k
 
Mkuu huyu Amir Jamal naye mzalendo?,nikisikia alivyokuwa wizara ya fedha aliiba mifedha mingi na kwenda kujificha Canada?..
 
Sijaelewa hii story maudhui yake nini ?
Kwani unadhani Daud Bashite alipenda kupata division zero wakati same class kuna vipanga vimepiga division one point seven?

Wewe ni Bashite tu, sasa machapisho aliyoandika Mzee Mohamed Said kwa kingereza si ndio utatoka kapa kabisa?

Kwanza kama wewe ni mtu wa mashambani, humjui Mzee Janguo wala humjui Dr Ramadhani Dau kwa hakika thread hii kaa pembeni hutoelewa kitu.
 
Jenguo huyu alikuwa mbunge wa Kisarawe kwa miaka makumi kadhaa??
Sasa nimeelewa "urafiki' wa Mzee Said na Dau ulisarujiwa wapi haswaa
Leo ndio siri imefichuka, ni wazi Dr Dau amewabeba sana ndugu zake katika imaani hasa huyu Mzee Mohammed Said, karani ambaye alikuwa na access ya kuingia hadi board meeting.
 
Si utani wale watoto walianza kula bata long time, ninakumbuka miaka ile ya awamu ya kwanza holiday walikuwa wanakwenda London.
Kwa kifupi those days bandari ilikuwa ni mali ya Mzee Janguo na kabla wapemba hawajatuharibia kujilipuwa tulikuwa tukienda UK kama unavyokwenda South Africa tu kwa sasa bila kuomba viza ubalozini, sasa kama manoti unayo ni kwa nini weekend usilikwee BA to Heathrow London? Mambo yamebadirika sana.
 
Mkuu huyu Amir Jamal naye mzalendo?,nikisikia alivyokuwa wizara ya fedha aliiba mifedha mingi na kwenda kujificha Canada?..

..Amir Jamal aliteuliwa kuwa Balozi wa Tz Geneva (mashirika ya UN) kati ya 1988 mpaka 1993.

..akiwa huko aliugua na kuamua kwenda Canada kujiuguza chini ya uangalizi wa wanawe.

..mauti yalimkuta akiwa Canada na akazikwa hukohuko.

..nilitaka kuweka taarifa kwa Amir Jamal hakutoroka nchini.

..Serikali ilimfanyia kumbukumbu baada ya kifo chake na kama sijakosea Benjamin Mkapa wakati huo akiwa Waziri alimuwakilisha Waziri Mkuu Cleopa Msuya ktk tukio hilo.
 
Ile pale nyuma ya Kilimanjaro hotel ni Temple tu kamwe wenyewe huwezi kuwaona hata siku moja wakiingia jengo lile.

Kuna watu kichwani wamejaa fungus, Freemason ndio wenye Rotary club na Lions club.

Kwa mtu ambaye yupo hapa mjini kitambo anajuwa vyema charity zilizofanywa na club hizi.

Tatizo kubwa la Watanzania ni poor IQ na slow learners.
 
Mkuu huyu Amir Jamal naye mzalendo?,nikisikia alivyokuwa wizara ya fedha aliiba mifedha mingi na kwenda kujificha Canada?..
Amir Jamal ni mmoja wa Wazalendo wa nchi yetu.

Ametumikia nafasi mbali mbali na aliaminiwa sana na Mwalimu

Baada ya kustaafu alihamia Canada ambako umri wake uliishia hapo

Mwalimu Nyerere na Benjamin Mkapa walikutana chuo cha IFM katika kuomboleza na ndiyo siku Mwalimu alianza kumshawishi Ben kuhusu Urais

Kuhamia Canada si kwasababu ya kuiba kama watu wanavyozusha. Si kweli hata kidogo

Pumzika kwa Amani Amir Jamal, Mzalendo na Mwananchi

JokaKuu
 
Mfianchi,
Ahsante kaka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…