Siku 100 Za Rais Magufuli Zinavyojadiliwa na Wadau

Kibo10

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
11,277
8,859
MKWAMO wa kisiasa visiwani Zanzibar umetia najisi sifa na mafanikio ya Rais John Magufuli katika siku 100 alizokuwepo madarakani zinazofikia kesho tangu aapishwe tarehe 5 Novemba mwaka jana, anaandika Faki Sosi.

Waliotoa maoni yao kwa MwanaHALISI Online wametofautiana mtazamo kuhusu siku 100 za Rais Magufuli madarakani huku wengine wakisema ameshindwa kufikia maratajio ya wengi hususani utatuzi wa mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzibar.

Alhad Mussa, Sheikh Mkuu wa MKoa wa Dar es Salaam amesema kuwa siku 100 za Rais Magufuli ni za baraka na neema kwa Watanzania na kwamba zimetoa nuru na heshima kubwa kwenye serikali yake.

Amesema, ameokoa kiasi kikubwa cha fedha na kwamba Watanzania watafurahia keki ya Taifa ambapo ameshauri wananchi kushikamana na kauli mbiu yake ya ‘Hapa Kazi Tu.’

“Kauli mbiu hii imeridhiwa na Mungu kwani Mungu aliumba mbingu na ardhi kwa kuashiria kuwa kazi ni wajibu,” amesema Sheikh Alhad.

Dk. Benso Bana ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) amesema, siku 100 za uongozi wa Rais Magufuli amevunja rekodi ya kuwa rais pekee Afrika mwenye utendaji wa kasi lakini pia ametofautiana na watangulizi wake kiutendaji.

“Rais Magufuli amekuwa ni tumaini kwa Watanzania, ndani ya siku 100 amewawajibisha watumishi waandamiza zaidi ya 190,” amesema Dk. Bana.
Hata hivyo, kuhusu mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzibar Dk. Bana amesema, Rais Magufuli hapaswi kulaumiwa kutokana na kwamba yeye anajua kuwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) ndio iliyo na mamlaka na uchaguzi huo.

Amedai kwamba ZEC inaweza kusimamia suala hilo na kwamba anazitaka nchi za Ulaya zisipewe nafasi kuingilia mgogoro huo kwa kuwa zinaweza kuuzidisha.
Profesa Abdall Sharrif ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Katiba Zanzibar (BAKIZA) amesema, katika siku 100 za Rais Magufuli hakufanya cha ajabu.
Amesema siku hizo 100 za Rais Magufuli ni kama amekuja kusalimu na kusimamisha watu kazi huku akikwepa nafasi yake ya kutatua mgogoro wa Zanzibar kwa kudai hana mamlaka wakati vurugu zitakapozuka, atatumia majeshi yake kwenda kuzizima.
“Majeshi ya Jamhuri ya Muungano ndio yaliyoua Wazanzibari mwaka 2001 na hayo hayo yanaweza kutumika tena kufanya kile kilichofanywa mwaka huo,” amesema.

Prof. Sharifu amemsifu Ibrahimu Kaduma ambaye ni kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwa mkweli na kujitokeza mbele ya umma.
Amesema kuwa, hatua ya Kaduma kusema kwamba chama chake (CCM) kimeshindwa na kiwaachie walioshinda ni ujasiri ambao alipaswa kuwa nao Rais Magufuli na ingeleta tija kwa taifa.

Sheikh Ponda Issa Ponda ambaye ni Katibu Mkuu wa Jumuiya na Taasisi za Kislamu nchini amesema kuwa, Rais Magufuli ameonesha nia ya kutaka uwajibikaji kwa watumishi wa umma.
Amesema, pamoja na hivyo lakini ameshindwa kusimamia utatuzi wa mgogoro wa kisiasa unaondelea Zanzibar na kwamba, visiwani humo kumetokea uvunjifu wa katiba uliofanywa na Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa ZEC.
Sheikh Ponda amesema kuwa, kiongozi huyo ameunda Baraza la Mawaziri bila kuzingatia usawa wa dini na kwamba, kwenye baraza hilo kuna mawaziri wanane tu ambao ni Waislamu.

Amesema kuwa, Rais Magufuli hatakiwi kusikiliza ushauri wenye ukada ndani yake kwani wanaCCM wengi hawana uzalendo na nchi.

Sheikh Ponda amemtaja Benard Membe ambaye alikuwa Waziri Mambo ya Nje katika Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kuwa, alimshauri Rais Magufuli njia sahihi ya kutatua mgogoro wa Zanzibar.

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe mkoani Kagera, Benson Bagonza amesema kuwa, Rais Magufuli anafukia shimo kwa kuchimba shimo lingine kutokana na kushindwa kupata ufumbuzi wa mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzaibar.

Amesema kwamba, mgogoro huo hauwezi kutatuliwa kwa kutumia majeshi wala silaha za moto pia kurudia uchaguzi isipokuwa maafikiano.

“Kuvurukiga kwa uchaguzi wa Zanzibar sio suala geni na kwamba kwanini chaguzi za nyuma hazijarudiwa,”amehoji Askofu Bagonza huku akionesha kushangazwa na Rais Magufuli kushindwa kupata ufumbuzi wa mgogoro huo mpaka sasa.

Akitoa maoni yake juu ya utendaji wa siku 100 za Rais,Tundu Lissu amesema Rais Magufuli amevuruga bunge na kamati zote muhimu na wala kamati hazikuvurugwa na spika wa bunge kama ambavyo wengi wanavyoaminishwa.

Nianze kwa kusisitiza kuwa ni siku 100 kati ya takribani zaidi ya siku 1825 za miaka mitano(5).
Aidha nami nianze kwanza kukupongeza Mheshimiwa rais Dr. John Pombe Magufuli, siku 100 ofisi umefanya mambo makubwa na mazuri. Nchi ilikuwa imefikia pabaya siyo rahisi uwafurahishe wote lakini katika mazingira hayo, wengi watakuwa wamefurahia hizi siku 100 na katika mazingira hayo hayo siku zote wachache lazima waumie kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Tembea kifua mbele rais wetu, umepongezwa na hata wale ambao kumpongesa mtu huwa ni miujiza. Pamoja na pongezi zao kama kawaida yao neno LAKINI halikosekani vinywani mwao.
Baadhi ya wachache wasio na mazoea ya kumpongeza mtu hata akifanya vizuri vipi na maneno yao ni pamoja na:

1. Zitto Zuberi Kabwe(Kiongozi Mkuu wa ACT-WAZALENDO na Mbunge wa Kigoma mjini.)

Anasemaje: "Nilitarajia Mgufuli angekuwa Kiongozi atakayeweza kubadili mfumo wa nchi yetu katika maeneo muhimu lakini hadi sasa nilichokiona ni KUBANA matumizi , kufukukuza watumishi na kuongeza juhudi za kukusanya mapato lakini bila kufanya mabdiliko ya vyombo husika kimkakati. Siku 100 ni chache kumhukumu kiongozi ambaye amepewa miaka mitano ya kutawala, ingawa zinaweza kuonyesha picha ya aina gani ya kiongozi ambaye taifa linaweza kuwa naye katika kipindi hicho.*

Tafakuri: Kwanza ni jambo jema Zitto kutambua kuwa rais anabana matumizi, kufukuza watumishi wahujumu uchumi na kuweka juhudi katika kukusanya mapato na kwamba siku 100 ni chake kumhukumu rais. Kwa upande mwingine, Zitto ambaye kati ya Wabunge wa Upinzania waliobaki Bungeni wakati Rais analihutubia Bunge ni yeye, lakini zake zinatokana na mambo makuu mawili ambayo hayana tija kwa taifa. Moja ni kutaka kukubalika ndani ya UKAWA, dalili ambazo zilianza kuonekana wakati kiongozi wa Upinzani Bungeni akijiandaa kutangaza bazara kivuli. Jambo la pili ni kinyongo tu kwa sababu rais ameona faida kubwa kuliko hasara za kumrejesha Waziri Muhongo katika Wizara ya Nishati na Madini pamoja na kwamba aliiongoza Wizara hiyo wakati wa ESCROW. swali la msingi tu ambalo ningependa kumuuliza Zitto ni je ndani ya siku 100 za uongozi wa rais kipi kilitakiwa kutangulia kati kuwatimua wahujumu uchumi na kubadili mifumo katika vyombo ambavyo wahujumu hao walihudumu?

2. Prof. Kitila Mkumbo(Mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es Salaam na mshauri wa mambo ya siasa ndani ya ACT-WAZALENDO)
Anasemaje: "Rais Magufuli amejipambanua vizuri kama Kiongozi atakayepambana vizuri na kero za kijamii kama vile rushwa na ufisadi. Hata hivyo rais bado hajajipambanua katika maeneo mengine matatu muhimu ya Kiongozi , ambayo ni falsafa, dira na ulinzi wa tunu za kitaifa.

Kipimo cha siku 100 kinachowekwa kwa marais wapya, kilianza kutumika nchini Marekani kutokana na mafanikio ya Rais Franklin Delano Roosevelt aliyeapishwa Machi 4, mwaka 1933 na ndani ya siku 100 alikuwa amepitisha sheria mpya 15 zilizosaidia kufufua uchumi wa Marekani.*

Tafakuri: Bado Prof. Anacheza ndani ya aliyotangulia kuyasema Kiongozi wake wa chama au inawezekana yeye ndiye ametembea ndani ya maneno ya Prof. Kutolea mfano wa Rais wa Marekani eti alitumia siku 100 kufanya mageuzi ndano ya Taifa hilo bila kusema aliikuta nchi ikiwa na hali gani, watu gani walikuwa wanamzunguka ni kutomtendea haki rais.

3. Shekh Ponda Issa Ponda(Katibu Mkuu wa jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini).
Anasemaje: Rais Magufuli anaonesha nia ya kutaka uwajibikaji kwa watumishi wa Umma. Pamoja na hayo ameshindwa kusimamia utatuzi wa mgogoro wa Zanzibar.
Tafakuri: Rais anatengenezewa mazingira ya kauli za wabaya wake kuwa ni DIKTETA zihalalishwe. Rais aingilie mgogoro wa Zanzibar kwa kipengele gani cha Katiba au kipengele gani cha sheria ya Uchaguzi? Kuingilia ZEC kuna tofauti na kuingilia Maamuzi ya Mahakama, Bunge n.k?
4. Benson Bagonza(Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT), Dayosisi ya Karagwe Mkoani Kagera.
Anasema: -Rais Mgufuli anafunika shimo kwa kuchimba shimo lingine kutokana na kushingwa kupata ufumguzi wa mgogoro wa kisiasa visiwani Zanzibar.
Tafakuri: Itashangaza sana kuona Kiongozi yeyote wa KKKT nchini akisifia uongozi wa awamu ya tano chini ya rais Dr. John Pombe Magufuli. Kufanya hivyo ni kumsaliti LOWASSA ambaye amewekeza nguvu na mali zake nyingi kwenye kanisa hilo. Nisharti WALUTHERI waendelee kuamini rais wao ni LOWASSA na si vinginevyo. Wanayoyasema viongozi wake yanaakisi ukweli huo.

5. Prof. Abdall Sharrif(Mwenyekiti wa Baraza la Katiba Zanzibar(BAKIZA)).
Anasema: Katika siku 100 za rais Magufuli hakufanya cha ajabu. Ni kama amekuja kusalimu na kusimamia watu kazi huku akikwepa nafasi ya kutatua mgogoro wa Zanzibar kwa kudai hana mamlaka wakati vurugu zitakapozuka , atatumia majeshi yake kwenda kuzizima.
Tafakuri: Matumizi ya vyombo vya ulinzi kwenye vurugu ni haki ya kikatiba ya rais(yeye ndo Amri jeshi mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama wa nchi). Rais hawezi kuingilia vyombo vingine kama Mahakama, Bunge na tume za uchaguzi. Kufanya hivyo ni UDIKTETA ambao watu wasio wajua dikteta ni nani wanamuita rais wetu hivyo. Polisi, jeshi na vyombo vongine vya ulinzi wataingia hata ikulu endapo rais ataanzisha vurugu . Ndiyo maana wanaingia Bungeni, Mahakamanin.k. huko ndiko mahali pao pa kujidai.

NARUDIA TENA: RAIS USIKATISHWE TAMAA NA HIZI LAKINI zao, Watanzania wasa wanyonge tuna imani nawe.
 
Mengi mazuri yamefanyika ila kwangu mimi kuna mawili hayajafanyiwa kazi kabisa. La kwanza ni tatizo la umeme bado tatizo limeendelea kuwa kubwa na hakuna sababu zinatolewa za kukatikakatika umeme, naongolea Arusha.

Eneo lingine ni la afya, kwa upande DDH hali imekuwa mbaya kabisa kwani zile huduma za bure kwa watoto chini ya miaka mitano, wamama wajawazito na wazee hospitali hizo zimeelemewa kwa kutokupewa pesa za kutosha hapa narehea St. Elizabeth Hospital.

Hayo maeneo mawili yakifanyiwa kazi wanyonge wataona faida za kukua kwa makusanyo ya serikali
 
Jamani nipo naangalia malumbano ya hoja ITV yaani nashindwa kuelewa... Watu wanajadiri kama mada ilivisema ILA cha ajabu mtu akimkosoa magufuli wale waandishi WA habari wanaosimamia mjadala wanampinga na kumkatisha na kumjibia magufuli... Hahaaaa imenshangaza kidogo... If hawaruhusu kumkosoa eti kisa cku 100 Ni chache Sana kumkosoa so why mada imeletwa??
BACK TO MY TOPIC
Maoni yangu Mimi Ni kwamba naenda tofauti kidogo na watu... Sitaweza kumsifia magufuli hata kwa jambo moja na naona amefanya nothing (kwa nionavyo Mimi)
point zangu zifuatazo zinathibitisha Hilo....

(1) MAISHA YAPO VILE VILE JAPO ALIKUWA NA UWEZO WA KUBADILISHA WALAU KIDGO KWA SKU HIZO 100
bidhaa bado ziko juu, pato la mwananchi WA kawaida Ni kilekile, bidhaa zngne ndo zimezdi kupanda bei, mishahara ya wafanyakazi ndo ileile, jamni majibu Ni ishara ya kwamba ndani ya mwili Kuna tatizo.. Sasa yeye badala ya kushughulika na ugonjwa ye anashughulika na matokeo ya ugonjwa...jamani mi Tampa credit nitapoanza kuona kuwa Kuna kitu kimebadilika kwa wananchi kuanzia kwenye pato la mwananchi mmoja mmoja na familia.. Nionavyo magufuli anahangaika Tu ili kupata sifa na ili watu warudishe imani na chama.... Jamani mi mtaniuta hater au mpinzani (yes Ni mpinzan nisie na chama na kwenye kukosoa nakosoa na kwenye kusifia nasifia)

(2) MEDIAS/VYOMBO VYA HABARI
nikianza na TBC kuzuiwa kuonesha bunge, jamani ebu acheni unafki. Tena ameniudhi yule mwandishi aliesma ooh tunataka kuwapima wabnge kwa maendeleo jimbni sio kuwaona, hivi unaakili wewe?? Serikali ndo inayotoa pesa na ndo inamiliki kodi zetu.. Na wabnge kazi Yao Ni kuwasilisha natatizo ya wananchi bungeni then sisi kama wananchi tunatakiwa sisi wananchi tuone Ni jinsi gani mbunge wetu anawasilisha matatizo yetu bungeni na jinsi gani mawaziri wanajibu kuhusiana na hoja za wabunge wetu ili lolote litalotokea asilaumiwe mbunge... Shule isipojengwa, maji yaspopelekwa, barabara zispojengwa nk asilaumiwe mbunge ilaumiwe serikali... Lakini amachofanya magufuli anataka awabebeshe mzigo wabunge, anataka asifiwe sku zote na asitokee mtu akamlaumu... Hahahaaa very interesting... Anaogopa media.. Yes becaz anajua movie anayotuchezea...

(3) PROPAGANDA ZA CCM NDO ZNAFANYA KAZI
jamani Nia ya ccm Ni kuona inarudsha imani kwa wananchi.. Kubali au kataa but that's the truth.Jamani kama kweli magufuli yupo upande WA wananchi then arudishe katiba ya walioba (rasimu) jambo ambalo Hawezz kulifanya hahahaaa.....
Nina mengi but ngoja niwaachie na nyie mtoe maoni yenu katika hili.... We unamuonaje Rais magu
 
Huna point wewe, ugumu wa maisha yako usiisingizie serikali wewe unayona yaliyofanyika kwa muda mfupi ni madogo??
Mishahara iongezwe budget imesomwa lini??
Bora ungekaa kimya kuficha mapungufu yako
 
Siku 100 za mambo meengi ambayo mwisho wa siku nothing has changed..

Bado IPTL inalipwa bilioni 8 kila mwezi licha ya mahakama kuwahi kusema ifilisiwe

Bado Konyagi wanalipa kodi kuliko vodacom

bado kibuku wanalipa kodi kuliko kampuni zote zinazoiuzia TANESCO umeme

Bado miji mingi michafu

bado wagonjwa wanalala chini mahospitalini nchi nzima

bado wanafunzi wanakaa chini shule nyingi nchi nzima

bado katiba mpya rasimu ya Warioba hakuna mabadiliko

bado mawaziri hadi wakuu wa wilaya wanaendesha mashangingi

Seating allowance kwa wabunge bado ipo

Andrew Chenge ni mwenyekiti wa bunge

Mwakyemba na Muhongo ni mawaziri katika baraza la mawaziri
 
Hii ni jana....



Hapa chini ni alipofanya ziara ya kushtukiza hapo hapo Muhimbili miezi mitatu na ushee iliyopita!





Mimi nadhani ana nia njema kwani sina sababu za kwa nini asiwe na nia njema.

Ila sina hakika na njia atumiazo kufanya hayo mema aliyonayo.
 
Kweli watz wajuzi wa vigelegele wakusepa kasepa wageni kazi yake ni kushtukiza tu Zanzibar imemshinda
 
Hii ni jana....



Hapa chini ni alipofanya ziara ya kushtukiza hapo hapo Muhimbili miezi mitatu na ushee iliyopita!





Mimi nadhani ana nia njema kwani sina sababu za kwa nini asiwe na nia njema.

Ila sina hakika na njia atumiazo kufanya hayo mema aliyonayo.

Cha msingi jamaa yenu sio rais wa nchi hii maana mambo yangekuwa mabaya muda huu.
 
Siku 100 za mambo meengi ambayo mwisho wa siku nothing has changed..

Bado IPTL inalipwa bilioni 8 kila mwezi licha ya mahakama kuwahi kusema ifilisiwe

Bado Konyagi wanalipa kodi kuliko vodacom

bado kibuku wanalipa kodi kuliko kampuni zote zinazoiuzia TANESCO umeme

Bado miji mingi michafu

bado wagonjwa wanalala chini mahospitalini nchi nzima

bado wanafunzi wanakaa chini shule nyingi nchi nzima

bado katiba mpya rasimu ya Warioba hakuna mabadiliko

bado mawaziri hadi wakuu wa wilaya wanaendesha mashangingi

Seating allowance kwa wabunge bado ipo

Andrew Chenge ni mwenyekiti wa bunge

Mwakyemba na Muhongo ni mawaziri katika baraza la mawaziri
List ya matatizo hayo yalitakiwa yawe yametatuliwa within 100 days???
 
List ya matatizo hayo yalitakiwa yawe yametatuliwa within 100 days???


We unaonaje?
kuna ugumu gani kuhakikisha makampuni makubwa yanalipa kodi?
inahitaji siku ngapi kwa hilo?

la IPTL linahitaji miaka mingapi?

seating allowance na mashangingi lahitaji miaka mingapi?

la Andrew Chenge?

kama alisema mapato yaliiyokusanywa bilioni 100 yaameenda kusimamia elimu bure
nini kimemzuia kuweka na pesa ya madawati?

au linahitaji miaka hilo pia?
 
We unaonaje?
kuna ugumu gani kuhakikisha makampuni makubwa yanalipa kodi?
inahitaji siku ngapi kwa hilo?

la IPTL linahitaji miaka mingapi?

seating allowance na mashangingi lahitaji miaka mingapi?

la Andrew Chenge?

kama alisema mapato yaliiyokusanywa bilioni 100 yaameenda kusimamia elimu bure
nini kimemzuia kuweka na pesa ya madawati?

au linahitaji miaka hilo pia?
Hivi Magufuli ndio alimteua Chenge kuwa Mwenyekiti wa Bunge ?
Miji ni michafu still unamlaumu Raisi ?
Fanya assessment kwenye mambo ambayo Raisi anafanya maamuzi moja kwa moja

Magufuli hawezi kumaliza matatizo yote ya Watanzania hata akitawala miaka 20
 
Binafsi namshukuru kwa barabara ya Mwenge-Moroko kwa upanuzi nachukia foleni
 
ktk hizi siku mia tumeshuhudia
  • sana sana amekuwa akiitawala Tanganyika tu (.. matatatizo ya ZNZ anadai eti ni ya ZEC & akina Shein na Maalim)
  • mamia ya watz wenzetu wamepoteza makazi na mali zao pale mkwajuni na kwingine
  • separation of powers is under threat (wanafanya vitu vingi kwa decree /amri, fukuzafukuza, wamefuta mfumo wa gpa kwa decree bila mchakato wowote, n.k.)
  • kumekuwa na maswali kuhusu uhuru wa mahakama kuingiliwa ...
  • 'amekimbia' mabalozi ...
  • bei ya vitu haishikiki ...
  • upatikanaji wa habari unaminywa (e.g., kuminya matangazo ya TBC live toka bungeni, kufungiwa kwa gazeti, )
  • amefanya teuzi ambazo zimelalamikiwa na jamii kadhaa za watz (mfano akina Sheik Ponda hapo juu)
  • etc.
lakini pia amejitahidi ... tumeshuhudia
  • makusanyo ya kodi yameongezeka (ingawa bado tofauti ya maisha mitaani haionekani)
  • nidhamu ya watendaji (ingawa inaonekana wazi ni nidhamu ya woga ..)
  • ...
 
Naomba watu wa CCM wanisaidie katika hili, hivi yule rais aliyevuliwa madaraka na Nyerere kule zanzibar ilikuwaje vile.
Je Nyerere alivuka mipaka na kwa faida ya nani.
Sasa kama Nyerere aliweza Magu anashindwa nini.
 
Back
Top Bottom